Kuwa wenye shukurani mbele ya Allah (s.w)

Kuwa wenye shukurani mbele ya Allah (s.w)

Mwanaadamu ametunukiwa neema mbali mbali na Mola wake kuliko viumbe wengine wote kama tuanvyojifunza katika aya mbali mbali za Qur'an.

Download Post hii hapa

Kuwa wenye shukurani mbele ya Allah (s.w)

(a) Kuwa wenye shukurani mbele ya Allah (s.w)



Mwanaadamu ametunukiwa neema mbali mbali na Mola wake kuliko viumbe wengine wote kama tuanvyojifunza katika aya mbali mbali za Qur'an.


"Na hakika tumewatukuza wanaadamu na tumewapa vya kupanda barani na baharini, na tumewaruzuku vitu vizuri vizuri, na tumewatukuza kuliko wengi katika wale tuliowaumba, kwa utukufu ulio mkubwa (kabisa)." (17: 70)


“Bila shaka tumemuumba mwanaadamu kwa umbo lililo bora kabisa." (95:4) Pamoja na neema zilizoainishwa kwa upeo mpana katika aya (17:70),


Mwanaadamu ameboreshwa kuliko viumbe wengine kwa kutunukiwa vipawa vya ziada vifuatavyo:



1. Akili inayomuwezesha kufikiri na kutafakari
2. Utambuzi wa ubinafsi unaomuwezesha kujitambua, kuyatambua mazingira yake na mahusiano yake na muumba na vile vyote Alivyoviumba
3. Kipawa cha elimu - uwezo wa kujielimisha na kuelimisha wengine.
4. Uhuru wa kuamua na kutenda.



Neema zote hizi ametunukiwa binaadamu ili aweze kufikia lengo la kuumbwa kwake ambalo ni kumuabudu Allah (s.w) katika kila kipengele cha maisha yake (Qur'an 51:56) na kisha kuwa Khalifa katika jamii. Hivyo, binaadamu atakuwa ni mwenye kumshukuru Allah (s.w) iwapo atamuabudu Allah (s.w) ipasavyo katika kila kipengele cha maisha yake na atakuwa ni mwizi wa fadhila endapo atatakabari na kuwaabudu wengine kinyume na Allah (s.w).



Anaye shukuru kwa kumuabudu Allah (s.w) ipasavyo anafanya hivyo kwa faida ya nafsi yake ya kuishi kwa furaha na amani katika maisha ya hapa duniani na kupata maisha bora zaidi huko akhera. Anayekufuru kwa kuacha kumuabudu Allah (s.w) iipasavyo, anaitia khasarani nafsi yake mwenyewe kwa kuishi maisha ya mashaka na khofu hapa duniani na kustahiki adhabu kali isiyo na mfano wake katika maisha ya akhera. Allah (s.w) hafaidiki kwa chochote kutokana na kushukuru kwetu na pia hapungu kiwi na chochote kutokana na kukufuru kwetu. Allah (s.w) ameliweka hili wazi mara tu baada ya kutufahamisha lengo la kuumbwa kwetu.


"Sikuwaumba majini na watu ila wapate kuniabudu. Sitaki kwao riziki wala Sitaki wanilishe. Kwa yakini Mwenyezi Mungu ndiye Mtoaji wa riziki, Mwenye nguvu, Madhubuti". (51:56-58).




                   


Download Post hii hapa

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 775

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

Elimu Yenye Manufaa
Elimu Yenye Manufaa

Kwenye kipengele hiki tutajifunza elimu yenye manufaa kwenye jamii na pia tutajifunza sifa za elimu yenye manufaa.

Soma Zaidi...
Maana ya kumuamini mwenyezi Mungu (s.w) katika maisha ya kila siku
Maana ya kumuamini mwenyezi Mungu (s.w) katika maisha ya kila siku

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Lengo la kushushwa vitabu vya mwenyezi Mungu (s.w)
Lengo la kushushwa vitabu vya mwenyezi Mungu (s.w)

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Muhtasari wa sifa za waumini
Muhtasari wa sifa za waumini

Lengo tarajiwa la Muhtasari huu ni kutuwezesha kuzibaini fika sifa za Waumini zilizoainishwa katika Qur'an, kisha kujipamba nazo ili tuwe waja wema watakaorehemewa na kuridhiwa na Allah (s.

Soma Zaidi...
 ALAMA YA MUUMINI WA UKWELI KATIKA UISLAMU
ALAMA YA MUUMINI WA UKWELI KATIKA UISLAMU

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه و سلم قَالَ: "مَنْ كَانَ يُؤْمِنُ بِاَللَّهِ وَالْيَوْمِ...

Soma Zaidi...
Sifa za wuamini zilizotajwa katika surat Al-ma'aarij
Sifa za wuamini zilizotajwa katika surat Al-ma'aarij

Kwa hakika binaadamu ameumbwa, hali ya kuwa mwenye pap atiko.

Soma Zaidi...