picha

Kuwa wenye shukurani mbele ya Allah (s.w)

Mwanaadamu ametunukiwa neema mbali mbali na Mola wake kuliko viumbe wengine wote kama tuanvyojifunza katika aya mbali mbali za Qur'an.

Kuwa wenye shukurani mbele ya Allah (s.w)

(a) Kuwa wenye shukurani mbele ya Allah (s.w)



Mwanaadamu ametunukiwa neema mbali mbali na Mola wake kuliko viumbe wengine wote kama tuanvyojifunza katika aya mbali mbali za Qur'an.


"Na hakika tumewatukuza wanaadamu na tumewapa vya kupanda barani na baharini, na tumewaruzuku vitu vizuri vizuri, na tumewatukuza kuliko wengi katika wale tuliowaumba, kwa utukufu ulio mkubwa (kabisa)." (17: 70)


β€œBila shaka tumemuumba mwanaadamu kwa umbo lililo bora kabisa." (95:4) Pamoja na neema zilizoainishwa kwa upeo mpana katika aya (17:70),


Mwanaadamu ameboreshwa kuliko viumbe wengine kwa kutunukiwa vipawa vya ziada vifuatavyo:



1. Akili inayomuwezesha kufikiri na kutafakari
2. Utambuzi wa ubinafsi unaomuwezesha kujitambua, kuyatambua mazingira yake na mahusiano yake na muumba na vile vyote Alivyoviumba
3. Kipawa cha elimu - uwezo wa kujielimisha na kuelimisha wengine.
4. Uhuru wa kuamua na kutenda.



Neema zote hizi ametunukiwa binaadamu ili aweze kufikia lengo la kuumbwa kwake ambalo ni kumuabudu Allah (s.w) katika kila kipengele cha maisha yake (Qur'an 51:56) na kisha kuwa Khalifa katika jamii. Hivyo, binaadamu atakuwa ni mwenye kumshukuru Allah (s.w) iwapo atamuabudu Allah (s.w) ipasavyo katika kila kipengele cha maisha yake na atakuwa ni mwizi wa fadhila endapo atatakabari na kuwaabudu wengine kinyume na Allah (s.w).



Anaye shukuru kwa kumuabudu Allah (s.w) ipasavyo anafanya hivyo kwa faida ya nafsi yake ya kuishi kwa furaha na amani katika maisha ya hapa duniani na kupata maisha bora zaidi huko akhera. Anayekufuru kwa kuacha kumuabudu Allah (s.w) iipasavyo, anaitia khasarani nafsi yake mwenyewe kwa kuishi maisha ya mashaka na khofu hapa duniani na kustahiki adhabu kali isiyo na mfano wake katika maisha ya akhera. Allah (s.w) hafaidiki kwa chochote kutokana na kushukuru kwetu na pia hapungu kiwi na chochote kutokana na kukufuru kwetu. Allah (s.w) ameliweka hili wazi mara tu baada ya kutufahamisha lengo la kuumbwa kwetu.


"Sikuwaumba majini na watu ila wapate kuniabudu. Sitaki kwao riziki wala Sitaki wanilishe. Kwa yakini Mwenyezi Mungu ndiye Mtoaji wa riziki, Mwenye nguvu, Madhubuti". (51:56-58).




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 1127

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
πŸ‘‰1 kitabu cha Simulizi    πŸ‘‰2 web hosting    πŸ‘‰3 Kitabu cha Afya    πŸ‘‰4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    πŸ‘‰5 Madrasa kiganjani    πŸ‘‰6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu

Faradhi kwa maiti ya muislamu (edk form 2:dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Maswali juu ya dini anayostahiki kufuata mwanadamu

Dini anayostahiki kufuata mwanadamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Nguzo za imani

Zifuatazo ni nguzo za imani (EDK form 2: elimu ya dini ya kiislamu)

Soma Zaidi...
Kwa nini mwanadamu hawezi kuishi bila dini?

Mwanadamu hawezi kuishi bila dini, kwani dini imekusanya mfumo mzima wa maisha yake.

Soma Zaidi...
Mwanadamu hawezi kuishi bila ya dini kutokana na maumbile yake

Kuwa ni kwa nini mwanadamu hawezi kuishi bila ya dini kutokana na umbile la mwanadamu.

Soma Zaidi...
Mtazamo wa Uislamu juu ya maana ya dini

Uislamu unaitazama dini katika nyanja zote za maisha ya mwanadamu. Hii ni tofauti na mtazamo wa kikafiri juu ya dini.

Soma Zaidi...
Kwa namna gani Allah huwasiliana na wanadamu kwa kupitia ndoto.

Ndoto za kweli ni moja kati ya njia ambazo Allah huwasiliana na wanadamu.

Soma Zaidi...
Kujiepusha na kula mali ya Yatima

Waumini wanawajibika kuwatunzia mayatima mali zao na kuwakabidhi wanapofikia baleghe yao baada ya kuwajaribu na kuthibitisha kuwa wanao uwezo wa kutunza mali zao - Rejea Qur-an (4:5-6).

Soma Zaidi...
Kina Cha uovu wa shirk

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...