picha

Kujiepusha na Shirk

Shirki ni kitendo chochote cha kukipa kiumbe nafasi ya Allah (s.

Kujiepusha na Shirk

(b) Kujiepusha na Shirk



Shirki ni kitendo chochote cha kukipa kiumbe nafasi ya Allah (s.w) katika dhati yake, Sifa zake, Mamlaka yake na Hukumu zake.
Allah (s.w) aliyemuumba binaadamu na viumbe vyote vilivyo mzunguka kwa lengo, ndiye mwenye Haki na Uwezo pekee wa kumuwekea mwanaadamu mwongozo wa maisha utakao muwezesha kuishi kwa furaha na amani katika maisha ya hapa duniani na maisha ya baadaye huko akhera.


Yeyote yule katika viumbe atakayechukua au kupewa nafasi ya Allah (s.w) katika kutoa kanuni, sheria na mwongozo wa maisha ya binaadamu katika jamii, atakuwa amechukua au amepewa mamlaka ambayo hana uwezo nayo na kwa vyovyote vile atakuwa ameitumbukiza jamii katika Kiza cha Khofu na Huzuni kinachosababishwa na dhuluma za aina mbalimbali. Allah (s.w) analiweka hili wazi katika aya zifuatazo:


"Hakuna kulazimishwa (mtu kuingia) katika dini. Uongofu umekwisha pambanuka na upotofu. Basi anayemkataa shetani na akamwamini Mwenyezi Mungu, bila shaka yeye ameshika kishiko chenye nguvu kisichokuwa na kuvunjika. Na Mwenyezi Mungu ni mwenye kusikia mwenye kujua.."



"Mwenyezi Mungu ni mlinzi wa wale walioamini. Huwatoa katika giza na kuwaingiza katika nuru. Lakini waliokufuru, walinzi wao ni matwaghuti. Huwatoa katika nuru na kuwaingiza katika giza. Hao ndio watu wa Motoni, humo watakaa milele." (2:256-25 7).



Hivyo kwa mnasaba wa maelezo haya na aya tulizozirejea, tunajifunza kuwa chanzo cha dhuluma zote anazofanyiwa binaadamu na binaadamu mwenziwe zimetokana na kumshirikisha Allah (s.w) ama katika Dhati yake, Sifa zake, Mamlaka yake au katika Hukumu zake.




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Tawhid Main: Post File: Download PDF Views 2261

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Kitabu cha Afya     👉5 Bongolite - Game zone - Play free game     👉6 Dua za Mitume na Manabii    

Post zinazofanana:

Humtegemea Mwenyezi Mungu peke yake

Hawamuogopi au kumtegemea yeyote kinyume na Mwenyezi Mungu.

Soma Zaidi...
Mwanadamu hawezi kuishi bila ya dini kutokana na maumbile yake

Kuwa ni kwa nini mwanadamu hawezi kuishi bila ya dini kutokana na umbile la mwanadamu.

Soma Zaidi...
KUAMINI MITUME WA ALLAH (S.W)

Mtu hawi Muumini wa kweli mpaka awe na yakini juu ya Mitume wa Allah (s.

Soma Zaidi...
Kuamini vitabu vya mwenyezi Mungu (s.w)..

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Mtazamo wa uislamh juu ya ibada

Katika kipengele hich tutajifunza dhana ya ibada katika uislamu,maana ua ibada

Soma Zaidi...