Ingawa hakuna ajuaye Kiyama kitakuwa lini, kupitia Aya mbali mbali za Qur’an na Hadith kadhaa za Mtume (s.a.w) zinabainisha kwa uwazi juu ya dalili mbali mbali za kusimama kwa kiyama. Ziko Dalili kubwa na Dalili ndogo, na zipo ambazo tayari zimekwishadhihiri nyingine zinaendelea na ambazo bado kudhihiri kwake; Kama Allah Aliyetukuka anavyotubainishia:
“Kwani wanangoja jingine ila kiyama kiwajie kwa ghafla? Basi alama zake(hicho kiyama) zimekw ishakuja. Kutaw afaa w api kukumbuka wakati kitakapow ajia ? ” (47:18)
Pia anasema“Saa ya Kiyama imekaribia; na mwezi umepasuka” (54 :1)
Dalili Ndogo za Kiyama:
(i)Watu kumiliki mali na hali ya kuwa ni madhalimu wasio na uadilifu
(ii)Kuenea mno kwa riba kiasi cha kila mtu kuathiriwa nayo
(iii)Kuenea kwa kila aina ya Ulevi
(iv)Wanawake kukithiri katika kuvaa nguozinazochochea zinaa (nguo nyepesi za kuangaza , fupi na za kubana)
(v)Wanawake watawaiga wanaume katika mavazi kadhalika wanaume watawaiga wanawake katika mavazi. Leo wanaume wanavaa hereni, shanga, bangili, na mengineyo yanayojulikana kuwa mapambo ya kike.
(vi)Kuenea kwa Liwati (kujimai baina ya jinsia moja-wanaume kuwaendea wanaume wenzao na wanawake kuwaendea wanawake wenzao) Homosexuality and Lesbiansm. Jambo hili leo limehalalishwa na watu wa Magharibi, pia hapa kwetu Afrika na hasa Kenya na Afrika kusini ni halali Mwanaume kuolewa na mwanamume mwenzake! Subhaanallah!
(vii)Kuenea sana kwa zinaa na itafanyika hadharani.
(viii)Watu hawatawajali tena wazazi wao, ndugu zao najamaa zao badala yake watawathamini nakuwasaidia rafiki zao.
(ix)Watu watachukia sana kulea watoto.
(x)Unafiki utaenea sana.
(xi)Mauaji yataenea sana, kwa kutoka Taifa mojakwenda kulivamia Taifa jingine na watu baadhikuwaua wengine kwa maslahi yao binafsi
(xii)Watu wataona uzito sana kutoa sadaka
xiii)Watawala watakuwa wengi sana lakini hakuna atakayekuwa mkweli na mwadilifu
xiv)Mtu ataheshimiwa kwa shari yake na si kwa uadilifu na wema wake.
xv)Kujifaharisha kwa misikiti
xvi)Pamoja na haya yote, bado kutakuwepo na kundi dogo tu la waislamu ambalo litadumu katika njia iliyonyooka na halitatetereka kwa lolote.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya hapa chini kuipakua sasa!
Umeionaje Makala hii.. ?
"Na (wazazi wako) wakikushurutisha kunishirikisha na (yale) ambayo huna ilimu nayo, usiwatii; lakini kaa nao kwa wema hapa duniani (Maadamu ni wazee wako, ila usiwafuate tu mwenendo wao mbaya); Shika mwenendo wa wale wanaoelekea kwangu, kisha marejeo yenu
Soma Zaidi...Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu mtazamo wa uislamu juu ya dini (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Mwanadamu hawezi kuishi bila dini, kwani dini imekusanya mfumo mzima wa maisha yake.
Soma Zaidi...Kuamini Malaika ni imani ambayo pindi ikithibiti vema moyoni, huleta taathira kubwa sana katika maisha ya kila siku na hivyo kubadili kabisa tabia na mwenendo wa Muumini.
Soma Zaidi...Nguzo za Imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Si zinaa tu iliyoharamishwa bali hata yale yote yanayotengeneza mazingira na kuchochea kufanyika kwa zinaa nayo pia yameharamishwa.
Soma Zaidi...