Mtazamo wa kikafiri juu ya maana ya dini.

Maana ya dini kwa mujibu wa makafiri ina utofauti mkubwa na vile ambavyo uislamu unaamini kuhusu dini.

MTAZAMO WA KIKAFIRI JUU YA DINI

 

Maana ya Dini kwa Mtazamo wa Makafiri
Makafiri wanatafsiri dini kuwa ni:

(i)“Imani inayohusiana na mambo ya kiroho baina ya binaadamu na Mwenyezi Mungu au njia ya kuhusiana na Mwenyezi Mungu” (Kamusi ya Kiswahili sanifu)


(ii)“Imani juu ya kuwepo Mungu Muumba aliye muweza na mwenye nguvu juu ya kila kitu, Mmiliki wa ulimwengu, ambaye amempa binaadamu roho ambayo huendelea kuishi baada ya kifo cha mwili” (Oxford Advanced Learner’s Dictionary of Current English).

 


Kutokana na tafsiri hii ya dini iliyonukuliwa kutoka kwenye kamusi ya Kiswahili na ya Kiingereza, tunajifunza mambo makubwa mawili:
Kwanza, kwa mtazamo wa makafiri dini inahusiana na imani ya kuwepo Allah (s.w).

 

Hivyo wenye dini ni wale tu wanaoamini kuwepo kwa Allah (s.w), na wale was ioamini kuwepo kwake hawana dini. Ni katika mtazamo huu V. I. Lenin katika kitabu chake “Socialism and Religion (Ujamaa na Dini) amedai:


“Everybody must be absolutely free to profess any religion he pleases or no religion whatever; i.e. to be an atheist which every socialist is as a rule...”


Tafsiri:
“Kila mtu hanabudi kuwa huru kabisa kufuata dini yoyote anayotaka au asiwe na dini kabisa, yaani awe kafiri, jambo ambalo inambidi kila mjamaa awe kama sheria...”


Pili, kwa mtazamo wa makafiri, dini inahusiana na mambo ya kiroho au ulimwengu wa kiroho tu, na haihusiani kabisa na

 

ulimwengu wa kimaada (wa vitu). Ni kwa mtazamo huu kwa makafiri, matendo ya wafuasi wa dini yamegawanywa katika sehemu mbili, matendo ya dini na matendo ya dunia. Katika mtazamo huu pia Waislamu hulaumiwa na makafiri kuwa wanachanganya dini na siasa, dini na uchumi; dini na utamaduni, na kadhalika.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 2244

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi    👉2 Bongolite - Game zone - Play free game    👉3 web hosting    👉4 Dua za Mitume na Manabii    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

SHIRK

Jifunze tawhid yaani kumpwekesha Allah subhaanah wata'aala

Soma Zaidi...
Mtazamo wa uislamu juu ya Elimu, nini maana ya elimu na nani aliye elimika.

Ni nini maana ya Elimu na ni nani aliye elimika? Uislamu una mtazamo gani juu ya Elimu?

Soma Zaidi...
Elimu Yenye Manufaa

Kwenye kipengele hiki tutajifunza elimu yenye manufaa kwenye jamii na pia tutajifunza sifa za elimu yenye manufaa.

Soma Zaidi...
Mtazamo wa uislamu juu ya dini

Kwenye kipengele hichi tutajifunza mitazamo ya kikafiri juu ya dini.

Soma Zaidi...
Mwanadamu hawezi kuishi bila ya dini kutokana na maumbile yake

Kuwa ni kwa nini mwanadamu hawezi kuishi bila ya dini kutokana na umbile la mwanadamu.

Soma Zaidi...
Kwa nini hakuna haja ya Mtume mwingine baada ya Muhammad

Na tukiutafiti Uislamu kwa makini kama mfumo kamili wa maisha tunaona unadhihiri ukweli wa aya hii ya Qur-an.

Soma Zaidi...
Kujiepusha na kukaribia zinaa

Si zinaa tu iliyoharamishwa bali hata yale yote yanayotengeneza mazingira na kuchochea kufanyika kwa zinaa nayo pia yameharamishwa.

Soma Zaidi...