Mtazamo wa kikafiri juu ya maana ya dini.

Maana ya dini kwa mujibu wa makafiri ina utofauti mkubwa na vile ambavyo uislamu unaamini kuhusu dini.

MTAZAMO WA KIKAFIRI JUU YA DINI

 

Maana ya Dini kwa Mtazamo wa Makafiri
Makafiri wanatafsiri dini kuwa ni:

(i)“Imani inayohusiana na mambo ya kiroho baina ya binaadamu na Mwenyezi Mungu au njia ya kuhusiana na Mwenyezi Mungu” (Kamusi ya Kiswahili sanifu)


(ii)“Imani juu ya kuwepo Mungu Muumba aliye muweza na mwenye nguvu juu ya kila kitu, Mmiliki wa ulimwengu, ambaye amempa binaadamu roho ambayo huendelea kuishi baada ya kifo cha mwili” (Oxford Advanced Learner’s Dictionary of Current English).

 


Kutokana na tafsiri hii ya dini iliyonukuliwa kutoka kwenye kamusi ya Kiswahili na ya Kiingereza, tunajifunza mambo makubwa mawili:
Kwanza, kwa mtazamo wa makafiri dini inahusiana na imani ya kuwepo Allah (s.w).

 

Hivyo wenye dini ni wale tu wanaoamini kuwepo kwa Allah (s.w), na wale was ioamini kuwepo kwake hawana dini. Ni katika mtazamo huu V. I. Lenin katika kitabu chake “Socialism and Religion (Ujamaa na Dini) amedai:


“Everybody must be absolutely free to profess any religion he pleases or no religion whatever; i.e. to be an atheist which every socialist is as a rule...”


Tafsiri:
“Kila mtu hanabudi kuwa huru kabisa kufuata dini yoyote anayotaka au asiwe na dini kabisa, yaani awe kafiri, jambo ambalo inambidi kila mjamaa awe kama sheria...”


Pili, kwa mtazamo wa makafiri, dini inahusiana na mambo ya kiroho au ulimwengu wa kiroho tu, na haihusiani kabisa na

 

ulimwengu wa kimaada (wa vitu). Ni kwa mtazamo huu kwa makafiri, matendo ya wafuasi wa dini yamegawanywa katika sehemu mbili, matendo ya dini na matendo ya dunia. Katika mtazamo huu pia Waislamu hulaumiwa na makafiri kuwa wanachanganya dini na siasa, dini na uchumi; dini na utamaduni, na kadhalika.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 2402

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
πŸ‘‰1 Kitau cha Fiqh    πŸ‘‰2 Bongolite - Game zone - Play free game    πŸ‘‰3 Dua za Mitume na Manabii    πŸ‘‰4 kitabu cha Simulizi    πŸ‘‰5 web hosting    πŸ‘‰6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

UMBILE LA MBINGU NA ARDHI

β€œKatika kuumbwa mbingu na ardhi na mfuatano wa usiku na mchana,ziko alama (hoja) za kuonyesha kuwepo Allah (s.

Soma Zaidi...
Shahada mbili

Kwenye mada hii tutajifunza shahada mbili,tafsiri ya shahada kstika maisha ya kila siku.

Soma Zaidi...
KUAMINI MITUME WA ALLAH (S.W)

Mtu hawi Muumini wa kweli mpaka awe na yakini juu ya Mitume wa Allah (s.

Soma Zaidi...
Mtazamo wa uislamu juu ya Elimu, nini maana ya elimu na nani aliye elimika.

Ni nini maana ya Elimu na ni nani aliye elimika? Uislamu una mtazamo gani juu ya Elimu?

Soma Zaidi...
Kumuamini mwenyezi Mungu..

Nguzo za Imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Uchambuzi wa Neema Alizopewa Nabii Sulaiman(a.s)

(i) Kutiishiwa Upepo Qur'an inatufahamisha kuwa Nabii Sulaiman alitiishiwa upepo akaweza kuutumia apendavyo kwa amri yake.

Soma Zaidi...
Ni ipi maana ya Imani katika Uislamu, na ni zipi sifa za muumini.

Katika Uislamu imani inanguzo kuu 6.Pia muumini anatakiwa ajipambe na sifa za waumini. Posti hii itakufundisha kuhusu imani katika Uislamu.

Soma Zaidi...
Kuamini siku ya mwisho

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu

Soma Zaidi...
Kwa namna gani nabii Musa na Bi Mariam waliweza kuzungumza na Allah nyuma ya pazia

Nabii Musa na Mama yake nabii Isa bi Mariam waliweza kuwasiliana na Allah nyuma ya pazia.

Soma Zaidi...