Menu



jamii muongozo

Haja ya Mwongozo kutoka kwa Allah (s.

Haja ya Mwongozo kutoka kwa Allah (s.w)

Haja ya Mwongozo kutoka kwa Allah (s.w)


Mwanaadamu pamoja na elimu aliyotunukiwa, hana uwezo pasina msaada wa muumba wake, kupata majibu sahihi ya maswali ya msingi ya maisha yake hapa duniani na huko akhera. Maswali haya ya msingi ni:



1 Nani chanzo cha maumbile yote?



2 Ni lipi lengo la mwanaadamu hapa ulimwenguni?



3 Atalifikiaje lengo hilo?



4 Ni ipi nafasi halisi ya mwanaadamu hapa ulimwenguni?



5 Ni ipi hatma yake baada ya kufa, je kufa ndio mwisho wa maisha yake?
Mwanaadamu bila ya mwongozo kutoka kwa muumba wake hana uwezo wa kutoa majibu sahihi ya maswali haya. Elimu ya mazingira aliyonayo mwanaadamu ni finyu mno kiasi kwamba haimuwezeshi hata kuijua roho yake kama tunavyokumbushwa katika Qur-an:
“Na w anakuuliza habari ya roho. Sema: “Roho ni jambo lililohusika na Mola wangu. Nanyi hamkupewa katika elim u ila kidogo ka b isa.” (17:85)
Maana ya Kuamini Vitabu vya Allah
Imani ya kweli katika Uislamu haishii moyoni tu bali ni lazima idhihirishwe katika matendo ya kila siku. Hivyo, waumini 162wa kweli wa vitabu vya Allah (s.w) ni wale wanaoendesha maisha yao ya kila siku katika kila kipengele kwa kufuata bara bara maongozi ya vitabu vya Allah (s.w). Kabla ya Qur-an kushushwa, waumini wa kweli wa vitabu vya Allah vilivyotangulia, vikiwemo Taurat, Injili, Zaburi, n.k. ni wale walioishi kwa mujibu wa maongozi ya vitabu hivyo kama tunavyojifunza katika aya zifuatazo:


“Hakika tuliteremsha Taurati yenye uw ongozi na nuru; ambayo kwayo Manabii waliojisalimisha (kwa Allah) waliwahukumu Mayahudi; Watawa na Maulamaa pia (walihukumu kwa hiyo Taurat); kwa sababu walitakiwa kuhifadhi kitabu hicho cha Allah; Nao walikuwa mashahidi juu yake. Basi, msiwaogope w atu, bali niogopeni (Mimi). Wala msibadilishe Aya zangu kwa thamani chache (ya maslahi ya dunia).Na wasiohukumu kwa yale aliyoteremsha Allah, basi Hao ndio m akafiri.” (5:44)


“Watu wa Injili wahukumu kwa yale aliyoteremsha Allah ndani yake. Na wasiohukumu kwa (kufuata) yale aliyoteremsha Allah, basi hao ndio mafasiki (maasi)” (5:47)


Baada ya Qur-an kushushwa kupitia kwa Mtume Muhammad (s.a.w) kwa ajili ya walimwengu wote, Waumini wa kweli wa vitabu vya Allah (s.w) ni wale wanaoishi kwa kufuata maongozi ya Qur-an na Sunnah ya Mtume Muhammad (s.a.w) katika maisha yao yote. Si muumini yule anayeikataa Qur-an na Mtume aliyeshushiwa hatakama anadai kuwa anaiamini Taurat, Zabur, Injili, n.k. na Mitume walioshushiwa vitabu hivyo kwa mujibu wa aya ifuatayo:


“Enyi mlioamini! Mwaminini Allah na Mtume wake na kitabu alichokiteremsha juu ya Mtume wake,na vitabu alivyoviteremsha zamani. Na mwenye kumkanusha Allah na Malaika wake na vitabu vyake, na Mitume wake na siku ya mwisho, basi bila shaka amepotea upotofu uliombali (na haki)” (4:136)
Hivi sasa, katika vitabu vya Allah (s.w) vilivyoshushwa hapa ulimwenguni, ni Qur-an pekee iliyobakia katika lugha yake ya asili (Kiarabu fasaha) na katika usahihi wake wa asili. Vitabu vilivyoitangulia Qur-an vinakabiliwa na matatizo makubwa mawili yafu atayo:
1. Lugha zilizotumika katika vitabu hivyo zimekufa (zimetoweka). Kwa mujibu wa Qur-an kila Mtume aliletewa wahay kwa lugha ya watu wake



“Na hatukumpeleka Mtume yeyote isipokuwa kwa lu gha ya watu wake ili ap ate kuwaba in is hia...” (14:4).
Tunajua kutokana na historia kuwa lugha hukua na kufa. Hivi sasa kwa mfano Allah (s.w) akituletea kitabu alichoshushiwa Nabii Adam (a.s) katika lugha aliyozungumza Adam (a.s) na wanawe wa karibu wa wakati ule, hatuwezi kupata ujumbe wake.2. Vitabu vilivyoitangulia Qur-an viliingizwa mikono ya watu, vikabadilishwa na kupotoshwa ili kukidhi matashi ya watu waliodai kufuata vitabu hivyo kinyume na Allah (s.w). Taurat, Zabur, Injili, n.k. Vilikumbwa na tatizo hili.
Qur-an imeepukana na matatizo haya kwani hivi leo, Lugha ya Kiarabu, ni miongoni mwa lugha kubwa zinazokua kwa kasi; pia Kiarabu ni lugha fasaha na tajiri kwa maneno kuliko lugha zote duniani. Pia Qur-an tofauti na vitabu vingine vya Allah (s.w), haitaingiliwa na mkono wa mtu, kwani imepewa hifadhi na Allah (s.w) mwenyewe:Hakika sisi ndio tulioteremsha mawaidha haya (hii Qur-an) na hakika Sisi ndio tutakao yalinda” (15:9).


“Haitakifikia batili mbele yake wala nyuma yake; kimeteremshwa na Mwenye Hikma ” (41:42).Hivyo hivi sasa, Muumini wa kweli wa vitabu vya Allah (s.w) ni yule:



1. Anayeamini pasi na tone la shaka kuwa Qur-an yote kama msahafu ulivyo kuanzia sura ya kwanza (Al-Faatiha) mpaka sura ya mwisho (An-Naas) ni maneno kutoka kwa Allah (s.w). Muumini anayakinisha kuwa:“Hiki ni kitabu kisichokuwa na shaka ndani yake, ni uwongozi kwa wamchao Allah” (2:2).



2. Anayaongoza maisha yake ya kila siku kwa kufuata Qur’an na mwenendo au sunnah ya mfasiri wa Qur-an, Mtume Muhammad (s.a.w). Qur-an yenyewe inasisitiza:


“Haiwi kwa mwanamume aliyeamini wala kwa mwanamke aliyeamini, Mwenyezi Mungu na Mtume wake wanapokata shauri, wawe na hiari katika shauri lao. Na mwenyekumuasi Mwenyezi Mungu na Mtume wake, hakika amepotea upotofu ulio wazi (kabisa).” (33:36)“... Na wasiohukumu kwa yale aliyoteremsha Mw enyezi Mungu, basi hao ndio m akafiri”. (5:44)“... Na wasiohukumu kwa yale aliyoteremsha Mwenyezi Mungu, basi hao ndio madhalimu” (5:45)“... Na wasiohukumu kwa yale aliyoteremsha Mwenyezi Mungu, basi hao ndio mafasiki (maasi) “ (5:47)




                   


Download app yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download

Download Now Bongoclass

           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu image Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Tawhid Main: Post File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Views 261


Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉3 Simulizi za Hadithi Audio     👉4 Kitau cha Fiqh     👉5 Madrasa kiganjani     👉6 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

Adabu ya kuingia katika nyumba za watu
Enyi mlioamini! Soma Zaidi...

Kubisha hodi katika nyakati za faragha katika familia
“Enyi mlioamini! Soma Zaidi...

Sifa za wanafiki zilizotajwa katika surat at-Tawbah
Mwenyezi Mungu amekuwia radhi (amekusamehe). Soma Zaidi...

KUAMINI SIKU YA MALIPO
Soma Zaidi...

Mwanadamu hawezi kuishi bila dini kutokana na vipawa alivyooewa na Allah
Je ni kwa nini mwanadamu hawezi kuishi bila ya kuwa na dini?. Vipawa alivyopewa na Allahni jibu tosha juu ya swali jilo Soma Zaidi...

Kuwa wenye shukurani mbele ya Allah (s.w)
Mwanaadamu ametunukiwa neema mbali mbali na Mola wake kuliko viumbe wengine wote kama tuanvyojifunza katika aya mbali mbali za Qur'an. Soma Zaidi...

Kumuamini mwenyezi Mungu..
Nguzo za Imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Nguzo za Imani kwa mujibu wa mafunzo ya kiislami.
Makala hii inakwenda kukufundisha kuhusu nguzo sita za imani katika Uislamu. Soma Zaidi...

Sifa za Waumini zilizotajwa katika surat Ahzab
Bila shaka wanaume wenye kufuata vizuri nguzo za Uislamu, na wanawake wanaozifuata vizuri nguzo za Uislamu, na wanaume wanaoamini vizuri nguzo za Imani, na wanawake wanaoamini vizuri nguzo za Imani, na wanaume wanaotii, na wanawake wanaotii, na wanaume wa Soma Zaidi...

Sifa za malaika
Soma Zaidi...