image

jamii muongozo

Haja ya Mwongozo kutoka kwa Allah (s.

Haja ya Mwongozo kutoka kwa Allah (s.w)

Haja ya Mwongozo kutoka kwa Allah (s.w)


Mwanaadamu pamoja na elimu aliyotunukiwa, hana uwezo pasina msaada wa muumba wake, kupata majibu sahihi ya maswali ya msingi ya maisha yake hapa duniani na huko akhera. Maswali haya ya msingi ni:



1 Nani chanzo cha maumbile yote?



2 Ni lipi lengo la mwanaadamu hapa ulimwenguni?



3 Atalifikiaje lengo hilo?



4 Ni ipi nafasi halisi ya mwanaadamu hapa ulimwenguni?



5 Ni ipi hatma yake baada ya kufa, je kufa ndio mwisho wa maisha yake?
Mwanaadamu bila ya mwongozo kutoka kwa muumba wake hana uwezo wa kutoa majibu sahihi ya maswali haya. Elimu ya mazingira aliyonayo mwanaadamu ni finyu mno kiasi kwamba haimuwezeshi hata kuijua roho yake kama tunavyokumbushwa katika Qur-an:
“Na w anakuuliza habari ya roho. Sema: “Roho ni jambo lililohusika na Mola wangu. Nanyi hamkupewa katika elim u ila kidogo ka b isa.” (17:85)
Maana ya Kuamini Vitabu vya Allah
Imani ya kweli katika Uislamu haishii moyoni tu bali ni lazima idhihirishwe katika matendo ya kila siku. Hivyo, waumini 162wa kweli wa vitabu vya Allah (s.w) ni wale wanaoendesha maisha yao ya kila siku katika kila kipengele kwa kufuata bara bara maongozi ya vitabu vya Allah (s.w). Kabla ya Qur-an kushushwa, waumini wa kweli wa vitabu vya Allah vilivyotangulia, vikiwemo Taurat, Injili, Zaburi, n.k. ni wale walioishi kwa mujibu wa maongozi ya vitabu hivyo kama tunavyojifunza katika aya zifuatazo:


“Hakika tuliteremsha Taurati yenye uw ongozi na nuru; ambayo kwayo Manabii waliojisalimisha (kwa Allah) waliwahukumu Mayahudi; Watawa na Maulamaa pia (walihukumu kwa hiyo Taurat); kwa sababu walitakiwa kuhifadhi kitabu hicho cha Allah; Nao walikuwa mashahidi juu yake. Basi, msiwaogope w atu, bali niogopeni (Mimi). Wala msibadilishe Aya zangu kwa thamani chache (ya maslahi ya dunia).Na wasiohukumu kwa yale aliyoteremsha Allah, basi Hao ndio m akafiri.” (5:44)


“Watu wa Injili wahukumu kwa yale aliyoteremsha Allah ndani yake. Na wasiohukumu kwa (kufuata) yale aliyoteremsha Allah, basi hao ndio mafasiki (maasi)” (5:47)


Baada ya Qur-an kushushwa kupitia kwa Mtume Muhammad (s.a.w) kwa ajili ya walimwengu wote, Waumini wa kweli wa vitabu vya Allah (s.w) ni wale wanaoishi kwa kufuata maongozi ya Qur-an na Sunnah ya Mtume Muhammad (s.a.w) katika maisha yao yote. Si muumini yule anayeikataa Qur-an na Mtume aliyeshushiwa hatakama anadai kuwa anaiamini Taurat, Zabur, Injili, n.k. na Mitume walioshushiwa vitabu hivyo kwa mujibu wa aya ifuatayo:


“Enyi mlioamini! Mwaminini Allah na Mtume wake na kitabu alichokiteremsha juu ya Mtume wake,na vitabu alivyoviteremsha zamani. Na mwenye kumkanusha Allah na Malaika wake na vitabu vyake, na Mitume wake na siku ya mwisho, basi bila shaka amepotea upotofu uliombali (na haki)” (4:136)
Hivi sasa, katika vitabu vya Allah (s.w) vilivyoshushwa hapa ulimwenguni, ni Qur-an pekee iliyobakia katika lugha yake ya asili (Kiarabu fasaha) na katika usahihi wake wa asili. Vitabu vilivyoitangulia Qur-an vinakabiliwa na matatizo makubwa mawili yafu atayo:
1. Lugha zilizotumika katika vitabu hivyo zimekufa (zimetoweka). Kwa mujibu wa Qur-an kila Mtume aliletewa wahay kwa lugha ya watu wake



“Na hatukumpeleka Mtume yeyote isipokuwa kwa lu gha ya watu wake ili ap ate kuwaba in is hia...” (14:4).
Tunajua kutokana na historia kuwa lugha hukua na kufa. Hivi sasa kwa mfano Allah (s.w) akituletea kitabu alichoshushiwa Nabii Adam (a.s) katika lugha aliyozungumza Adam (a.s) na wanawe wa karibu wa wakati ule, hatuwezi kupata ujumbe wake.2. Vitabu vilivyoitangulia Qur-an viliingizwa mikono ya watu, vikabadilishwa na kupotoshwa ili kukidhi matashi ya watu waliodai kufuata vitabu hivyo kinyume na Allah (s.w). Taurat, Zabur, Injili, n.k. Vilikumbwa na tatizo hili.
Qur-an imeepukana na matatizo haya kwani hivi leo, Lugha ya Kiarabu, ni miongoni mwa lugha kubwa zinazokua kwa kasi; pia Kiarabu ni lugha fasaha na tajiri kwa maneno kuliko lugha zote duniani. Pia Qur-an tofauti na vitabu vingine vya Allah (s.w), haitaingiliwa na mkono wa mtu, kwani imepewa hifadhi na Allah (s.w) mwenyewe:Hakika sisi ndio tulioteremsha mawaidha haya (hii Qur-an) na hakika Sisi ndio tutakao yalinda” (15:9).


“Haitakifikia batili mbele yake wala nyuma yake; kimeteremshwa na Mwenye Hikma ” (41:42).Hivyo hivi sasa, Muumini wa kweli wa vitabu vya Allah (s.w) ni yule:



1. Anayeamini pasi na tone la shaka kuwa Qur-an yote kama msahafu ulivyo kuanzia sura ya kwanza (Al-Faatiha) mpaka sura ya mwisho (An-Naas) ni maneno kutoka kwa Allah (s.w). Muumini anayakinisha kuwa:“Hiki ni kitabu kisichokuwa na shaka ndani yake, ni uwongozi kwa wamchao Allah” (2:2).



2. Anayaongoza maisha yake ya kila siku kwa kufuata Qur’an na mwenendo au sunnah ya mfasiri wa Qur-an, Mtume Muhammad (s.a.w). Qur-an yenyewe inasisitiza:


“Haiwi kwa mwanamume aliyeamini wala kwa mwanamke aliyeamini, Mwenyezi Mungu na Mtume wake wanapokata shauri, wawe na hiari katika shauri lao. Na mwenyekumuasi Mwenyezi Mungu na Mtume wake, hakika amepotea upotofu ulio wazi (kabisa).” (33:36)“... Na wasiohukumu kwa yale aliyoteremsha Mw enyezi Mungu, basi hao ndio m akafiri”. (5:44)“... Na wasiohukumu kwa yale aliyoteremsha Mwenyezi Mungu, basi hao ndio madhalimu” (5:45)“... Na wasiohukumu kwa yale aliyoteremsha Mwenyezi Mungu, basi hao ndio mafasiki (maasi) “ (5:47)




                   






           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 176


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

KUAMINI MITUME WA ALLAH (S.W)
Mtu hawi Muumini wa kweli mpaka awe na yakini juu ya Mitume wa Allah (s. Soma Zaidi...

Sifa za waumini zilizotajwa katika surat Al-Mu’uminuun (23:1-11)
Soma Zaidi...

UMBILE LA MBINGU NA ARDHI
“Katika kuumbwa mbingu na ardhi na mfuatano wa usiku na mchana,ziko alama (hoja) za kuonyesha kuwepo Allah (s. Soma Zaidi...

Mitume wa uongo
Wafuatao ni baadhi ya wale waliodai utume wakati Mtume (s. Soma Zaidi...

Sifa za waumini zilizotajwa katika surat ash-Shuura
“Basi vyote hivi mlivyopewa ni starehe ya maisha ya dunia tu, lakini kilicho kwa Mwenyezi Mungu ni bora na cha kudumu (milele). Soma Zaidi...

Maana ya uislamu.
Kwenye kipengele hichi titajifunza maana ya uislamu,na maana nyingine tofauti. Soma Zaidi...

Mambo anayofanyiwa maiti baada ya kufa
Dhana ya faradh kwa muislamu (EDK form 2:dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Kujiepusha na kufuata mambo kwa kibubusa
Waislamu wanakatazwa kufanya na kufuata mambo kwa kibubusa (kwa mkumbo) bila ya kuwa na ujuzi unaostahiki. Soma Zaidi...

mtazamo wa uislamu juu ya dini
Soma Zaidi...

Sifa za Wanafiki zilizotajwa katika surat Al-Munaafiqun
Wanapokujia wanafiki, husema: "Tunashuhudia ya kuwa kwa yakini wewe ni Mtume wa Mwenyezi Mungu. Soma Zaidi...

Lengo la ibada maalumu
Lengo la ibada maalumu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Umbile la mbingu na ardhi linavyothibitisha uwepo wa Allah
Allah anatutaka kuchunguza umbile na mbingu na ardhi ili kupata mazingatio. Soma Zaidi...