Mwanaadamu ametunukiwa neema mbali mbali na Mola wake kuliko viumbe wengine wote kama tuanvyojifunza katika aya mbali mbali za Qur'an.
Mwanaadamu ametunukiwa neema mbali mbali na Mola wake kuliko viumbe wengine wote kama tuanvyojifunza katika aya mbali mbali za Qur'an.
"Na hakika tumewatukuza wanaadamu na tumewapa vya kupanda barani na baharini, na tumewaruzuku vitu vizuri vizuri, na tumewatukuza kuliko wengi katika wale tuliowaumba, kwa utukufu ulio mkubwa (kabisa)." (17: 70)
βBila shaka tumemuumba mwanaadamu kwa umbo lililo bora kabisa." (95:4) Pamoja na neema zilizoainishwa kwa upeo mpana katika aya (17:70),
Mwanaadamu ameboreshwa kuliko viumbe wengine kwa kutunukiwa vipawa vya ziada vifuatavyo:
1. Akili inayomuwezesha kufikiri na kutafakari
2. Utambuzi wa ubinafsi unaomuwezesha kujitambua, kuyatambua mazingira yake na mahusiano yake na muumba na vile vyote Alivyoviumba
3. Kipawa cha elimu - uwezo wa kujielimisha na kuelimisha wengine.
4. Uhuru wa kuamua na kutenda.
Neema zote hizi ametunukiwa binaadamu ili aweze kufikia lengo la kuumbwa kwake ambalo ni kumuabudu Allah (s.w) katika kila kipengele cha maisha yake (Qur'an 51:56) na kisha kuwa Khalifa katika jamii. Hivyo, binaadamu atakuwa ni mwenye kumshukuru Allah (s.w) iwapo atamuabudu Allah (s.w) ipasavyo katika kila kipengele cha maisha yake na atakuwa ni mwizi wa fadhila endapo atatakabari na kuwaabudu wengine kinyume na Allah (s.w).
Anaye shukuru kwa kumuabudu Allah (s.w) ipasavyo anafanya hivyo kwa faida ya nafsi yake ya kuishi kwa furaha na amani katika maisha ya hapa duniani na kupata maisha bora zaidi huko akhera. Anayekufuru kwa kuacha kumuabudu Allah (s.w) iipasavyo, anaitia khasarani nafsi yake mwenyewe kwa kuishi maisha ya mashaka na khofu hapa duniani na kustahiki adhabu kali isiyo na mfano wake katika maisha ya akhera. Allah (s.w) hafaidiki kwa chochote kutokana na kushukuru kwetu na pia hapungu kiwi na chochote kutokana na kukufuru kwetu. Allah (s.w) ameliweka hili wazi mara tu baada ya kutufahamisha lengo la kuumbwa kwetu.
"Sikuwaumba majini na watu ila wapate kuniabudu. Sitaki kwao riziki wala Sitaki wanilishe. Kwa yakini Mwenyezi Mungu ndiye Mtoaji wa riziki, Mwenye nguvu, Madhubuti". (51:56-58).
Umeionaje Makala hii.. ?
(v)Kuwaombea dua wazazi.
Soma Zaidi...Dini anayostahiki kufuata mwanadamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Ni nini maana ya Elimu na ni nani aliye elimika? Uislamu una mtazamo gani juu ya Elimu?
Soma Zaidi...Kwa nini uislamu ndio dini pekee ya haki ambayo watu wanatakiwa waifuate.
Soma Zaidi...Posti hii inaonyesha dalili,sababu na mbinu za kutoa huduma ya kwanza kwa aliyepata jeraha kwenye ngozi kwa kuingiliwa na kitu Kama mwiba,Pini,sindano n.k
Soma Zaidi...Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2:dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Allah hutumia maandishi kuwafundisha wanadamu. Mfano mzuri ni nabii Musa ambaye alipewa vibao vya maandishi.
Soma Zaidi...