Ushahidi juu ya kosa la Uzinifu

Ushahidi juu ya kosa la Uzinifu

Ushahidi wa kuthibitisha kutendeka kwa kosa la uzinifu unapatikana kwa namna tatu zifuatzo: (i)Kushuhudia tendo hilo likifanyika kwa wakati mmoja watu wanne Mukalafu (Walio baleghe na wenye akili timamu), wakiwa ni Waislamu waadilifu.

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Ushahidi juu ya kosa la Uzinifu

(c) Ushahidi juu ya kosa la Uzinifu



Ushahidi wa kuthibitisha kutendeka kwa kosa la uzinifu unapatikana kwa namna tatu zifuatzo:
(i)Kushuhudia tendo hilo likifanyika kwa wakati mmoja watu wanne Mukalafu (Walio baleghe na wenye akili timamu), wakiwa ni Waislamu waadilifu.
(ii)Muhusika au wahusika kukiri kwa hiari yake/yao bila ya shinikizo au mazingira yanayopelekea shinikizo lolote.
(iii)Mwanamke kupata ujauzito nje ya ndoa.



Nje ya ushahidi huu, mtu hatahukumiwa kwa kosa la uzinifu au ubasha pamoja na kuwepo mazingira ya kutatanisha. Sana sana atahukimiwa kukurubia zinaa na kupewa nasaha na maonyo stahiki. Ila ikitokea kwa mwanandoa kumkamata mwenziwe ugoni, bila ya mashahidi wanne au muhusika kukiri kosa kwa hiari yake, wanandoa hawa watalazimika kula kiapo mbele ya kadhi kama ilivyoelekezwa katika aya zifuatazo:


Na wale wanaowasingizia wake zao (kuwa wamezini) na hawana mashahidi ila nafsi zao, basi ushahidi wa mmoja wao utakuwa kushuhudilia mara nne kwa kiapo cha Mwenyezi Mungu: ya kwamba bila shaka yeye ni mmoja wa wanaosema kweli. Na mara ya tano (aape) kwamba laana ya Mwenyezi Mungu iwe juu yake ikiwa ni miongoni mwa waongo.Na (mke) itamuondokea adhabu kwa kutoa shahada mara nne kwa kiapo cha Mwenyezi Mungu ya kwamba (huyu mume) ni miongoni mwa waongo.
Na mara ya tano (aape) ya kwamba hasira ya Mwenyezi Mungu iwe juu yake kama (mumewe) yu miongoni mwa wanaosema kweli, (na yeye mke ndiye muongo)." (24:6-9)




                   


Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 1086

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 Bongolite - Game zone - Play free game    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 Madrasa kiganjani    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

Mazingatio kabla ya kuosha maiti
Mazingatio kabla ya kuosha maiti

Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2:dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
KUAMINI VITABU VYA ALLAH (S.W)
KUAMINI VITABU VYA ALLAH (S.W)

Mtu hawi Muumini wa kweli mpaka awe na yakini juu ya vitabu vya Allah (s.

Soma Zaidi...
Sifa za Waumini zilizotajwa katika surat Ahzab
Sifa za Waumini zilizotajwa katika surat Ahzab

Bila shaka wanaume wenye kufuata vizuri nguzo za Uislamu, na wanawake wanaozifuata vizuri nguzo za Uislamu, na wanaume wanaoamini vizuri nguzo za Imani, na wanawake wanaoamini vizuri nguzo za Imani, na wanaume wanaotii, na wanawake wanaotii, na wanaume wa

Soma Zaidi...
Ni nini maana ya Ilhamu katika uislamu?
Ni nini maana ya Ilhamu katika uislamu?

Ilhamu ni moja katika njia ambazo Allah huwasiliana na wanadamu na kuwafundisha mambo mablimbali.

Soma Zaidi...