picha

Haki za kielimu za mwanamke katika uislamu

Haki ya ElimuKatika Uislamu kujielimisha ni faradhi inayowahusu Waislamu wote, wanaume na wanawake: "Soma kwa jina ?

Haki za kielimu za mwanamke katika uislamu

Haki ya Elimu
Katika Uislamu kujielimisha ni faradhi inayowahusu Waislamu wote, wanaume na wanawake: "Soma kwa jina ?a Mola wako aliyeumba" (96: 1). Aya hii na nyingi nyinginezo zinazosisitiza elimu katika Uislamu hazikumbagua mwanamke. Pia Mtume (s.a.w) katika kusisitiza elimu amesema: "Kutafuta elimu ni faradhi kwa kila Muislam mwanamume na kila Muilsm mwanamke ".


Bali kutokana na tabia ya jamii nyingine ulimwenguni ya kuwanyanyasa wan awake na kuwaona kuwa ni nuksi, wasiostahiki kulelewa vizuri na kuelimishwa, Uislamu umetoa motisha mkubwa wa ahadi ya kupata malipo makubwa kutoka kwa Allah (s.w) kwa kuwalelea watoto wa kike vizuri na kuwaelimisha ipasavyo. Katika Hadith iliyosimuliwa na Imam Ahmed, Mtume (s.a.w) amesema:



Yeyote atakayewalea mabinti wawili hadi wakakua, yeye na mimi Siku ya Kiyama tutakuwa kama hivi. (Akaonesha vidole vyake viwili iii kupigia mfano watakavyokuwa karibu sana huko Peponi). (Ahmad)



Lengo Ia mafundisho haya ya Mtume (s.a.w) ni kuwaondosha watu katika zile fikra dhaifu za kuwaona watoto wa kike kama kwamba si watu. Na katika Hadith nyingine iliyosimuliwa pia na Ahmed, Mtume (s.a.w) amesema: Yeyote ambaye amemzaa binti, na hakumzika yungali hai, na hakumtukana au kumkashfu, na hakumpendelea mtoto wake wa kiume zaidi kuliko huyo wa kike, Allah atamuingiza Peponi. (Ahmad)



Zaidi ya mafundisho haya Mtume (s.a.w) alionesha mfano katika maisha yake mwenyewe, kwa kuwaheshimu na kuwatendea vizuri binti zake, kiasi ambacho aliwahi kusema juu ya binti yake, Fatma; "Fatma ni sehemu yangu mimi, furaha yake ni yangu, na ghadhabu zake ni uchungu wangu ".



Umuhimu wa kuwaelimisha watoto wa kike uko wazi. Tumeona kuwa katika jamii ya Kiislamu hapana budi kuwepo wanawake madaktari, wauguzi, walimu n.k. Ni dhahiri kuwa itabidi waelimishwe kwanza ndio waweze kupata ujuzi wa kufanya kazi hizo.



Wanawake wajifunze fani zipi za Elimu? Qur'an haijaweka mipaka yoyote inayowakataza wanawake fani fulani fulani za elimu. Kama kuna fani ya elimu ambayo ni haramu kwa wanawake basi fani hiyo itakuwa pia haramu kwa wanaume. Kwa mfano kujifundisha uchawi ni haramu kwa Waislamu wote (wanaume na wanawake),Qur'an (2: 102).
Ingawa kila mtu anayohaki ya kujipatia elimu, katika fani na kiwango chochote anachoweza, kipo kiwango fulani cha elimu ambacho ni lazima kila mtu awe nacho. Elimu ya lazima ni pamoja na kujua misingi ya Uislamu - Imani na Nguzo za Uislamu, namna ya kutekeleza Kwa ukamilifu Ibada maalum kama vile, kusimamisha swala, zakati, funga, hija, n.k., kujua wajibu katika familia na katika jamii, kujua katika maisha yetu ya kila siku lipi ni halali kulitenda na lipi ni haramu kwa mujibu wa Qur'an na Sunnah. Kwa ujumla elimu juu ya mambo haya ya msingi, tunaiita elimu ya mwongozo". Elimu hii ni faradh am kwa kila muislamu mwanamume na mwanamke.



Ingawa wanawake hawajazuiliwa kusomea fani yoyote ya elimu, bado tunaweza kusema kuwa zipo baadhi ya fani za elimu ambazo .ni vizuri sana wanawake wakizisomea kwani zitawafaa sana katika kutimiza jukumu Ia uzazi na malezi ya jamii, kama vile elimu ya tiba (medicine) uuguzi (nursing), ualimu, uendeshaji wa nyumba (home management), saikolojia, n.k. Fani nyingine za elimu zinabakia kuwa ni halali kwao kama zilivyo halali kwa wanaume.



Kutokana na mifano hii michache katika maeneo haya ya haki tuliyojaribu kuyabainsiha humu, Uislam kama ulivyo Dini ya haki, humpa kila mtu haki yake bila ya ubaguzi wa ama yoyote.




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 1197

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 Dua za Mitume na Manabii    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

Kuangamizwa Waovu na Kuokolewa Waumini

Baada ya kuonywa wasionyeke, Allah(s.

Soma Zaidi...
mitume

Labda itaulizwa: Kwanini Mtume Muhammad (s.

Soma Zaidi...
Muumini ni yule ambaye anazungumza ukweli

Ukweli ni katika sifa za waumini. Siku zote hakuna hasara katika kusema ukweli. Kinyume chake uongo ni katika madhambi makubwa sana.

Soma Zaidi...
Shahada mbili

Kwenye mada hii tutajifunza shahada mbili,tafsiri ya shahada kstika maisha ya kila siku.

Soma Zaidi...
Sifa za wanafiki zilizotajwa katika surat al-Baqarah

Na katika watu, wako (wanafiki) wasemao: "Tumemwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho"; na hali ya kuwa wao si wenye kuamini.

Soma Zaidi...
Maswali juu ya nguzo za Imani

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Mtazamo wa makafiri juu ya dini

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu mtazamo wa uislamu juu ya dini (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Nguzo za imani

Zifuatazo ni nguzo za imani (EDK form 2: elimu ya dini ya kiislamu)

Soma Zaidi...
Mafundisho yao kutoathiriwa na mazingira ya jamii zao

Takriban Mitume wote walitokea katika jamii zilizozama katika ujahili, lakini kamwe ujumbe wao haukuathiriwa na mitazamo ya ujahili kwa ujumla, walahawakuingizautamaduni wa kijahili katika dini ya Allah (s.

Soma Zaidi...