Haki ya ElimuKatika Uislamu kujielimisha ni faradhi inayowahusu Waislamu wote, wanaume na wanawake: "Soma kwa jina ?
Haki ya Elimu
Katika Uislamu kujielimisha ni faradhi inayowahusu Waislamu wote, wanaume na wanawake: "Soma kwa jina ?a Mola wako aliyeumba" (96: 1). Aya hii na nyingi nyinginezo zinazosisitiza elimu katika Uislamu hazikumbagua mwanamke. Pia Mtume (s.a.w) katika kusisitiza elimu amesema: "Kutafuta elimu ni faradhi kwa kila Muislam mwanamume na kila Muilsm mwanamke ".
Bali kutokana na tabia ya jamii nyingine ulimwenguni ya kuwanyanyasa wan awake na kuwaona kuwa ni nuksi, wasiostahiki kulelewa vizuri na kuelimishwa, Uislamu umetoa motisha mkubwa wa ahadi ya kupata malipo makubwa kutoka kwa Allah (s.w) kwa kuwalelea watoto wa kike vizuri na kuwaelimisha ipasavyo. Katika Hadith iliyosimuliwa na Imam Ahmed, Mtume (s.a.w) amesema:
Yeyote atakayewalea mabinti wawili hadi wakakua, yeye na mimi Siku ya Kiyama tutakuwa kama hivi. (Akaonesha vidole vyake viwili iii kupigia mfano watakavyokuwa karibu sana huko Peponi). (Ahmad)
Lengo Ia mafundisho haya ya Mtume (s.a.w) ni kuwaondosha watu katika zile fikra dhaifu za kuwaona watoto wa kike kama kwamba si watu. Na katika Hadith nyingine iliyosimuliwa pia na Ahmed, Mtume (s.a.w) amesema: Yeyote ambaye amemzaa binti, na hakumzika yungali hai, na hakumtukana au kumkashfu, na hakumpendelea mtoto wake wa kiume zaidi kuliko huyo wa kike, Allah atamuingiza Peponi. (Ahmad)
Zaidi ya mafundisho haya Mtume (s.a.w) alionesha mfano katika maisha yake mwenyewe, kwa kuwaheshimu na kuwatendea vizuri binti zake, kiasi ambacho aliwahi kusema juu ya binti yake, Fatma; "Fatma ni sehemu yangu mimi, furaha yake ni yangu, na ghadhabu zake ni uchungu wangu ".
Umuhimu wa kuwaelimisha watoto wa kike uko wazi. Tumeona kuwa katika jamii ya Kiislamu hapana budi kuwepo wanawake madaktari, wauguzi, walimu n.k. Ni dhahiri kuwa itabidi waelimishwe kwanza ndio waweze kupata ujuzi wa kufanya kazi hizo.
Wanawake wajifunze fani zipi za Elimu? Qur'an haijaweka mipaka yoyote inayowakataza wanawake fani fulani fulani za elimu. Kama kuna fani ya elimu ambayo ni haramu kwa wanawake basi fani hiyo itakuwa pia haramu kwa wanaume. Kwa mfano kujifundisha uchawi ni haramu kwa Waislamu wote (wanaume na wanawake),Qur'an (2: 102).
Ingawa kila mtu anayohaki ya kujipatia elimu, katika fani na kiwango chochote anachoweza, kipo kiwango fulani cha elimu ambacho ni lazima kila mtu awe nacho. Elimu ya lazima ni pamoja na kujua misingi ya Uislamu - Imani na Nguzo za Uislamu, namna ya kutekeleza Kwa ukamilifu Ibada maalum kama vile, kusimamisha swala, zakati, funga, hija, n.k., kujua wajibu katika familia na katika jamii, kujua katika maisha yetu ya kila siku lipi ni halali kulitenda na lipi ni haramu kwa mujibu wa Qur'an na Sunnah. Kwa ujumla elimu juu ya mambo haya ya msingi, tunaiita elimu ya mwongozo". Elimu hii ni faradh am kwa kila muislamu mwanamume na mwanamke.
Ingawa wanawake hawajazuiliwa kusomea fani yoyote ya elimu, bado tunaweza kusema kuwa zipo baadhi ya fani za elimu ambazo .ni vizuri sana wanawake wakizisomea kwani zitawafaa sana katika kutimiza jukumu Ia uzazi na malezi ya jamii, kama vile elimu ya tiba (medicine) uuguzi (nursing), ualimu, uendeshaji wa nyumba (home management), saikolojia, n.k. Fani nyingine za elimu zinabakia kuwa ni halali kwao kama zilivyo halali kwa wanaume.
Kutokana na mifano hii michache katika maeneo haya ya haki tuliyojaribu kuyabainsiha humu, Uislam kama ulivyo Dini ya haki, humpa kila mtu haki yake bila ya ubaguzi wa ama yoyote.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download
Download NowJe! umeipenda hii post?
Ndio Hapana Save post
Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Tawhid Main: Post File: Download PDF Share On Facebook or Whatsapp Views 552
Sponsored links
👉1
kitabu cha Simulizi
👉2
Madrasa kiganjani
👉3
Kitabu cha Afya
👉4
Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
👉5
Kitau cha Fiqh
👉6
Simulizi za Hadithi Audio
Sifa za Wanafiki zilizotajwa katika Surat ahzab
Na waliposema wanafiki na wale wenye maradhi nyoyoni mwao, "Mwenyezi Mungu na Mtume wake hawakutuahidi ila udanganyifu tu. Soma Zaidi...
Maswali juu ya nguzo za Imani
Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...
Kujiepusha na Kibri na Majivuno
Soma Zaidi...
Lengo la maisha ya mwanadamu
Soma Zaidi...
Lengo la kuletwa mitume
Mitume wameletwa kuwa Waalimu na viongozi wa kuwafundisha watu Uislamu na kuwaelekeza kuusimamisha Uislamu katika jamii kinadharia na kimatendo kama tunavyojifunza katika Qur-an:“Kwa hakika Tuliwapeleka Mitume wetu kwa dalili wazi wazi na Tukavitere.. Soma Zaidi...
Makemeo juu ya Zinaa na Hukumu kwa Wazinifu.
Tendo la zinaa ni tendo chafu kimaadili na Allah (s. Soma Zaidi...
Mitume waliosimuliwa katika Qur-an ni hawa ishirini na tano (25) wafuatao:
Adam (a. Soma Zaidi...
Maamrisho ya kushikamana nayo
Yale tunayoamrishwa kushikamana nayo ni haya yafuatayo: (i)Kumuabudu Allah (s. Soma Zaidi...
Maswali juu ya dini anayostahiki kufuata mwanadamu
Dini anayostahiki kufuata mwanadamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...
Mgawanyo wa elimu usiokubalika katika uislamu unasababishwa na sababu zifuatazo
Mgawanyo wa elimu usiokubalika katika uislamu unasababishwa na nini?
(EDK form 1: mgawanyo wa elimu usiokubalika katika uislamu unasababishwa na sababu zifuatazo) Soma Zaidi...