Na kwa yakini Tulimpa Luqmani hikima, tukamwambia Mshukuru Mwenyezi Mungu; na atakayeshukuru, kwa yakini anashukuru kwa ajili ya nafsi yake; na atakaye kufuru,
Mwenyezi Mungu ni Mkwasi, Asifiwaye, (hahitaji kushukuriwa na yeye). (31:12)
Na (wakumbushe), Luqmani alipomwambia Mwanawe; na hali ya kuwa anampa nasaha.Ewe mwanangu! Usimshirikishe Mwenyezi Mungu, maana kushirikisha ndiyo dhulma kubwa. (31:13)
Na tumemuusia mwanaadamu (kuwafanyia ihsani) wazazi wake - mama yake ameichukuwa mimba yake kwa udhaifu juu ya udhaifu, na (kumnyonyesha na kuja) kumwachisha kunyonya katika miaka miwili - ya kwamba unishukuru Mimi na wazazi wako; marejeo yenu ni Kwangu. (3 1:14)
Na (wazazi wako) wakikushurutisha kunishirikisha na (yale) ambayo huna ilimu nayo, usiwatii; lakini kaa nao kwa wema hapa duniani (maadamu ni wazee wako, ila usiwafuate tu mwendo wao mbaya); shika njia ya wale wanaoelekea Kwangu, kisha marejeo yenu ni Kwangu, hapo Nitakuambieni mliyokuwa mkiyatenda. (31:15)
Ewe mwanangu! Kwa hakika jambo lolote lijapokuwa na uzito wa chembe ya hardali, likawa ndani ya jabali au mbinguni au katika ardhi, Mwenyezi Mungu Atalileta (amlipe aliyefanya); bila shaka Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa mambo yaliyofichikana, (na) Mjuzi wa mambo yaliyo dhahiri. (31:16)
Ewe mwanangu! Simamisha Sala, na uamrishe mema, na ukataze mabaya, usubiri juu ya yale yatakayokusibu (kwani mwenye kuamrisha mema na kukataza mabaya lazima zitamfika tu taabu); Hakika hayo ni katika mambo yanayostahiki kuazimiwa (na kila mtu). (31:17)
Wala usiwatazame (usiwafanyie watu jeuri), kwa upande mmoja wa uso, wala usende katika nchi kwa maringo; hakika Mwenyezi Mungu Hampendi kila ajivunae, ajifahirishaye. (31:18)
Na ushike mwendo wa katikati, na uteremshe sauti yako; bila shaka sauti ya punda ni mbaya kuliko sauti zote (kwa makelele yake ya bure). (31:19)
Mzazi wa Kiislamu mwenye hekima ni yule atakayekuwa mstari wa mbele kutenda mema na kuwalea watoto wake wafuate nyayo zake pamoja na kuwausia na kujiusia yeye mwenyewe kufanya yafuatayo:
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Kwa nini uislamu ndio dini pekee ya haki ambayo watu wanatakiwa waifuate.
Soma Zaidi...Ni nini maana ya Elimu na ni nani aliye elimika? Uislamu una mtazamo gani juu ya Elimu?
Soma Zaidi...Je ni kwa nini mwanadamu hawezi kuishi bila ya kuwa na dini?. Vipawa alivyopewa na Allahni jibu tosha juu ya swali jilo
Soma Zaidi...Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Katika Qur'an tunakumbushwa neema mbali mbali walizotunukiwa Bani Israil (Mayahudi) na Mola wao ili kuwawezesha kusimamisha Ufalme wa Allah(s.
Soma Zaidi...Maringo, majivuno, majigambo, dharau ni vipengele vya kibri.
Soma Zaidi...