Maadili katika surat luqman

Maadili katika surat luqman

Maadili katika surat luqman


Na kwa yakini Tulimpa Luqmani hikima, tukamwambia Mshukuru Mwenyezi Mungu; na atakayeshukuru, kwa yakini anashukuru kwa ajili ya nafsi yake; na atakaye kufuru,


Mwenyezi Mungu ni Mkwasi, Asifiwaye, (hahitaji kushukuriwa na yeye). (31:12)


Na (wakumbushe), Luqmani alipomwambia Mwanawe; na hali ya kuwa anampa nasaha.Ewe mwanangu! Usimshirikishe Mwenyezi Mungu, maana kushirikisha ndiyo dhulma kubwa. (31:13)


Na tumemuusia mwanaadamu (kuwafanyia ihsani) wazazi wake - mama yake ameichukuwa mimba yake kwa udhaifu juu ya udhaifu, na (kumnyonyesha na kuja) kumwachisha kunyonya katika miaka miwili - ya kwamba unishukuru Mimi na wazazi wako; marejeo yenu ni Kwangu. (3 1:14)


Na (wazazi wako) wakikushurutisha kunishirikisha na (yale) ambayo huna ilimu nayo, usiwatii; lakini kaa nao kwa wema hapa duniani (maadamu ni wazee wako, ila usiwafuate tu mwendo wao mbaya); shika njia ya wale wanaoelekea Kwangu, kisha marejeo yenu ni Kwangu, hapo Nitakuambieni mliyokuwa mkiyatenda. (31:15)



Ewe mwanangu! Kwa hakika jambo lolote lijapokuwa na uzito wa chembe ya hardali, likawa ndani ya jabali au mbinguni au katika ardhi, Mwenyezi Mungu Atalileta (amlipe aliyefanya); bila shaka Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa mambo yaliyofichikana, (na) Mjuzi wa mambo yaliyo dhahiri. (31:16)


Ewe mwanangu! Simamisha Sala, na uamrishe mema, na ukataze mabaya, usubiri juu ya yale yatakayokusibu (kwani mwenye kuamrisha mema na kukataza mabaya lazima zitamfika tu taabu); Hakika hayo ni katika mambo yanayostahiki kuazimiwa (na kila mtu). (31:17)


Wala usiwatazame (usiwafanyie watu jeuri), kwa upande mmoja wa uso, wala usende katika nchi kwa maringo; hakika Mwenyezi Mungu Hampendi kila ajivunae, ajifahirishaye. (31:18)


Na ushike mwendo wa katikati, na uteremshe sauti yako; bila shaka sauti ya punda ni mbaya kuliko sauti zote (kwa makelele yake ya bure). (31:19)
Mzazi wa Kiislamu mwenye hekima ni yule atakayekuwa mstari wa mbele kutenda mema na kuwalea watoto wake wafuate nyayo zake pamoja na kuwausia na kujiusia yeye mwenyewe kufanya yafuatayo:




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 790

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 Madrasa kiganjani    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Dua za Mitume na Manabii   

Post zinazofanana:

Kujiepusha na kufuata mambo kwa kibubusa

Waislamu wanakatazwa kufanya na kufuata mambo kwa kibubusa (kwa mkumbo) bila ya kuwa na ujuzi unaostahiki.

Soma Zaidi...
Kujiepusha na Shirk

Shirki ni kitendo chochote cha kukipa kiumbe nafasi ya Allah (s.

Soma Zaidi...
Mgawanyiko wa elimu usiokubalika katika uislamu

Ni mgawanyo upi wa elimu haukubaliki. Ni ipi elimul akhera na elimu dunia? (Edk form 1 Dhana ya elimu)

Soma Zaidi...
Humtegemea Mwenyezi Mungu peke yake

Hawamuogopi au kumtegemea yeyote kinyume na Mwenyezi Mungu.

Soma Zaidi...
Kuwa wenye shukurani mbele ya Allah (s.w)

Mwanaadamu ametunukiwa neema mbali mbali na Mola wake kuliko viumbe wengine wote kama tuanvyojifunza katika aya mbali mbali za Qur'an.

Soma Zaidi...
Sifa za Wanafiki zilizotajwa katika Surat ahzab

Na waliposema wanafiki na wale wenye maradhi nyoyoni mwao, "Mwenyezi Mungu na Mtume wake hawakutuahidi ila udanganyifu tu.

Soma Zaidi...
Kuamini Qadar ya Mwenyezi Mungu

Nguzo za imani (EDK form 2:dhana ya elimu ya uislamu

Soma Zaidi...
Maana ya muislamu.

Kwenye kipengele hichi tutajifunza ni nani muislamu.

Soma Zaidi...
Mtazamo wa kikafiri juu ya maana ya dini.

Maana ya dini kwa mujibu wa makafiri ina utofauti mkubwa na vile ambavyo uislamu unaamini kuhusu dini.

Soma Zaidi...