picha

Maadili katika surat luqman

Maadili katika surat luqman

Maadili katika surat luqman


Na kwa yakini Tulimpa Luqmani hikima, tukamwambia Mshukuru Mwenyezi Mungu; na atakayeshukuru, kwa yakini anashukuru kwa ajili ya nafsi yake; na atakaye kufuru,


Mwenyezi Mungu ni Mkwasi, Asifiwaye, (hahitaji kushukuriwa na yeye). (31:12)


Na (wakumbushe), Luqmani alipomwambia Mwanawe; na hali ya kuwa anampa nasaha.Ewe mwanangu! Usimshirikishe Mwenyezi Mungu, maana kushirikisha ndiyo dhulma kubwa. (31:13)


Na tumemuusia mwanaadamu (kuwafanyia ihsani) wazazi wake - mama yake ameichukuwa mimba yake kwa udhaifu juu ya udhaifu, na (kumnyonyesha na kuja) kumwachisha kunyonya katika miaka miwili - ya kwamba unishukuru Mimi na wazazi wako; marejeo yenu ni Kwangu. (3 1:14)


Na (wazazi wako) wakikushurutisha kunishirikisha na (yale) ambayo huna ilimu nayo, usiwatii; lakini kaa nao kwa wema hapa duniani (maadamu ni wazee wako, ila usiwafuate tu mwendo wao mbaya); shika njia ya wale wanaoelekea Kwangu, kisha marejeo yenu ni Kwangu, hapo Nitakuambieni mliyokuwa mkiyatenda. (31:15)



Ewe mwanangu! Kwa hakika jambo lolote lijapokuwa na uzito wa chembe ya hardali, likawa ndani ya jabali au mbinguni au katika ardhi, Mwenyezi Mungu Atalileta (amlipe aliyefanya); bila shaka Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa mambo yaliyofichikana, (na) Mjuzi wa mambo yaliyo dhahiri. (31:16)


Ewe mwanangu! Simamisha Sala, na uamrishe mema, na ukataze mabaya, usubiri juu ya yale yatakayokusibu (kwani mwenye kuamrisha mema na kukataza mabaya lazima zitamfika tu taabu); Hakika hayo ni katika mambo yanayostahiki kuazimiwa (na kila mtu). (31:17)


Wala usiwatazame (usiwafanyie watu jeuri), kwa upande mmoja wa uso, wala usende katika nchi kwa maringo; hakika Mwenyezi Mungu Hampendi kila ajivunae, ajifahirishaye. (31:18)


Na ushike mwendo wa katikati, na uteremshe sauti yako; bila shaka sauti ya punda ni mbaya kuliko sauti zote (kwa makelele yake ya bure). (31:19)
Mzazi wa Kiislamu mwenye hekima ni yule atakayekuwa mstari wa mbele kutenda mema na kuwalea watoto wake wafuate nyayo zake pamoja na kuwausia na kujiusia yeye mwenyewe kufanya yafuatayo:




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2018-08-01 Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 951

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 Dua za Mitume na Manabii    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Kujielimisha kwa Ajili ya Allah (s.w).

Elimu ndiyo zana aliyotunukiwa mwanadamu ili aitumie kutekeleza majukumu yake kama Khalifa wa Allah (s.

Soma Zaidi...
Tawhiid

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
NJIA ZA KUMJUA MWENYEZI MUNGU (S.W)

Zifuatazo ni njia nyingi za kumjua Mwenyezi Mungu (EDK form 2:dhana ya elimu katika uislamu)

Soma Zaidi...
Maamrisho ya kushikamana nayo

Yale tunayoamrishwa kushikamana nayo ni haya yafuatayo: (i)Kumuabudu Allah (s.

Soma Zaidi...
Nafasi ya Elimu katika uislamu

Elimu imepewa kipaumbele kikubwa kwenye uislamu. Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu nafasi ya Elimu katika uislamu.

Soma Zaidi...
Shahada mbili

Kwenye mada hii tutajifunza shahada mbili,tafsiri ya shahada kstika maisha ya kila siku.

Soma Zaidi...
Lengo la ibada maalumu

Lengo la ibada maalumu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...