Kumuamini malaika wa mwenyezi Mungu...
Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
- Kuamini Malaika wa Mwenyezi Mungu (s.w).
- Maana: Malaika ni viumbe walioumbwa kutokana na nuru.
- Sifa za Malaika:
- Ni viumbe wa kiroho wenye mabawa.
- Ni viumbe wasio na matashi ya kimwili (kula, kunywa, kulala, n.k.)
- Hawana hiari katika kumuabudu Mwenyezi Mungu (s.w).
- Ni vimbe wasio na jinsia.
- Ni viumbe walioumbwa kutokana na Nuru.
- Kazi za Malaika.
Zifuatazo ni baadhi tu ya kazi za baadhi ya Malaika.
- Kuleta Wahyi (ujumbe) kwa wanaadamu kutoka kwa Mwenyezi Mungu (s.w).
Malaika Jibril ndiye mhusika mkuu wa kupeleka wahyi kwa mitume na manabii.
Rejea Qur’an (81:19-20), (16:2) na (11:69-73).
- Kumchunga na Kumlinda kila mtu na kuandika amali zake nzuri na mbaya.
Kila mtu anakundi la malaika nyuma na mbele yake kumlinda na mambo yaliyo nje na uwezo wake. Pia kuna malaika wa kulia anayeandika mema na wa kushoto anayeandika maovu ya mtu.
Rejea Qur’an (82:1-12), (50:17-18) na (13:11).
- Kuwaombea Waumini maghufira kwa Mwenyezi Mungu (s.w).
Hawa ni malaika ambao huzunguka katika makundi ya waumini anapotajwa ndani yake Mwenyezi Mungu (s.w) au kusomwa Qur’an Tukufu.
Rejea Qur’an (40:7), (42:5) na (17:78).
- Kuwasaidia waumini katika vita vya kupambana na maadui wa Allah (s.w).
Pindi waumini wanapopigana katika kusimamisha haki, Mwenyezi Mungu (s.w) huteremsha malaika kuwasaidia.
Rejea Qur’an (3:123-126) na (8:12).
- Kuwaangamiza watu waovu waliopindukia mipaka.
Watu waovu waliopindukia mipaka ya Mwenyezi Mungu (s.w) wakaonywa muda mrefu na wasionyeke huangamizwa na malaika maalum.
Rejea Qur’an (11:81-83).
- Kutoa roho za viumbe.
Malakul-Maut ndiye mhusika mkuu na wengineo katika kutoa roho za viumbe.
Rejea Qur’an (32:11).
- Kuzihoji, kuzistarehesha au kuziadhibu roho za wafu kaburini.
Malaika wanaohusika na kazi hii ni Munkar na Nakir.
- Kupuliza Parapanda siku ya Qiyama.
Mipulizo ya Parapanda katika kufisha na kufufua viumbe siku ya Qiyama itafanywa na malaika Israfil.
Rejea Qur’an (39:68).
- Kuwaliwaza na kuwakaribisha watu wema peponi.
Hili kundi jingine la malaika watakaofanya kazi hiyo siku ya Qiyama.
Rejea Qur’an (41:30-32) na (39:73).
- Kuwasimanga na kuwaadhibu watu waovu motoni.
Kuna kundi la malaika watakaokuwa wanaadhibu watu waovu motoni. Mlinzi mkuu wa milango ya moto ni Malaika Maalik.
Rejea Qur’an (25:22), (74:26-30) na (43:77).
- Kumtukuza na kumsifu Mwenyezi Mungu (s.w).
Kuna kundi la malaika maalum kwa kazi hii tu.
Rejea Qur’an (40:7).
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉2 Kitabu cha Afya 👉3 Bongolite - Game zone - Play free game 👉4 Madrasa kiganjani 👉5 ai web app 👉6 Dua za Mitume na Manabii
Post zinazofanana:
Maamrisho ya kushikamana nayo
Yale tunayoamrishwa kushikamana nayo ni haya yafuatayo: (i)Kumuabudu Allah (s.
Soma Zaidi...Shahada mbili
Kwenye mada hii tutajifunza shahada mbili,tafsiri ya shahada kstika maisha ya kila siku.
Soma Zaidi...Mtazamo wa uislamh juu ya ibada
Katika kipengele hich tutajifunza dhana ya ibada katika uislamu,maana ua ibada
Soma Zaidi...