image

Kumuamini malaika wa mwenyezi Mungu...

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

  1. Kuamini Malaika wa Mwenyezi Mungu (s.w).

 

- Ni viumbe wa kiroho wenye mabawa.

- Ni viumbe wasio na matashi ya kimwili (kula, kunywa, kulala, n.k.)

- Hawana hiari katika kumuabudu Mwenyezi Mungu (s.w).

- Ni vimbe wasio na jinsia.

- Ni viumbe walioumbwa kutokana na Nuru.


 

            Zifuatazo ni baadhi tu ya kazi za baadhi ya Malaika.

  1. Kuleta Wahyi (ujumbe) kwa wanaadamu kutoka kwa Mwenyezi Mungu (s.w).

Malaika Jibril ndiye mhusika mkuu wa kupeleka wahyi kwa mitume na manabii.

Rejea Qur’an (81:19-20), (16:2) na (11:69-73).

 

  1. Kumchunga na Kumlinda kila mtu na kuandika amali zake nzuri na mbaya.

Kila mtu anakundi la malaika nyuma na mbele yake kumlinda na mambo yaliyo nje na uwezo wake. Pia kuna malaika wa kulia anayeandika mema na wa kushoto anayeandika maovu ya mtu.

Rejea Qur’an (82:1-12), (50:17-18) na (13:11).

 

  1. Kuwaombea Waumini maghufira kwa Mwenyezi Mungu (s.w).

Hawa ni malaika ambao huzunguka katika makundi ya waumini anapotajwa ndani yake Mwenyezi Mungu (s.w) au kusomwa Qur’an Tukufu.

Rejea Qur’an (40:7), (42:5) na (17:78).

 

  1. Kuwasaidia waumini katika vita vya kupambana na maadui wa Allah (s.w).

Pindi waumini wanapopigana katika kusimamisha haki, Mwenyezi Mungu (s.w) huteremsha malaika kuwasaidia.

Rejea Qur’an (3:123-126) na (8:12).

 

  1. Kuwaangamiza watu waovu waliopindukia mipaka.

Watu waovu waliopindukia mipaka ya Mwenyezi Mungu (s.w) wakaonywa muda mrefu na wasionyeke huangamizwa na malaika maalum.

Rejea Qur’an (11:81-83).

 

  1. Kutoa roho za viumbe.

Malakul-Maut ndiye mhusika mkuu na wengineo katika kutoa roho za viumbe.

Rejea Qur’an (32:11).

 

  1. Kuzihoji, kuzistarehesha au kuziadhibu roho za wafu kaburini.

Malaika wanaohusika na kazi hii ni Munkar na Nakir.

 

  1. Kupuliza Parapanda siku ya Qiyama.

Mipulizo ya Parapanda katika kufisha na kufufua viumbe siku ya Qiyama itafanywa na malaika Israfil.

Rejea Qur’an (39:68).

 

  1. Kuwaliwaza na kuwakaribisha watu wema peponi.

Hili kundi jingine la malaika watakaofanya kazi hiyo siku ya Qiyama.

Rejea Qur’an (41:30-32) na (39:73).

 

  1. Kuwasimanga na kuwaadhibu watu waovu motoni.

Kuna kundi la malaika watakaokuwa wanaadhibu watu waovu motoni. Mlinzi mkuu wa milango ya moto ni Malaika Maalik.

Rejea Qur’an (25:22), (74:26-30) na (43:77).

 

  1. Kumtukuza na kumsifu Mwenyezi Mungu (s.w).

Kuna kundi la malaika maalum kwa kazi hii tu.

Rejea Qur’an (40:7).





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1426


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

MAANA NA HUKUMU YA TAJWIDI
Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa Soma Zaidi...

ALAMA YA MUUMINI WA UKWELI KATIKA UISLAMU
عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه و سلم قَالَ: "مَنْ كَانَ يُؤْمِنُ بِاَللَّهِ وَالْيَوْمِ... Soma Zaidi...

Kubisha hodi katika nyakati za faragha katika familia
“Enyi mlioamini! Soma Zaidi...

Nguzo za imani
Zifuatazo Ni nguzo za imani (EDK form 2: elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Imani ya Kiislamu na ni nani muumini?
Soma Zaidi...

Neema Alizotunukiwa Nabii Daudi(a.s)
Soma Zaidi...

Kwa nini hakuna haja ya Mtume mwingine baada ya Muhammad
Na tukiutafiti Uislamu kwa makini kama mfumo kamili wa maisha tunaona unadhihiri ukweli wa aya hii ya Qur-an. Soma Zaidi...

Mazingatio kabla ya kuosha maiti
Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2:dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Tawhiid
Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Kujiepusha na kukaribia zinaa
Si zinaa tu iliyoharamishwa bali hata yale yote yanayotengeneza mazingira na kuchochea kufanyika kwa zinaa nayo pia yameharamishwa. Soma Zaidi...

Athari za vita vya Uhud
Vita vya uhudi viliweza kuleta athari nyingi. Post hii itakuletea athari baadhi za vita hivyo. Soma Zaidi...

Himizo la kuwasamehe waliotukosea
“Na wasiape wale wakarimu na wenye wasaa miongoni mwenu, kujizuia kuwasaidia jamaa zao, maskini na wale waliohama kwa ajili ya Dini ya Allah; na wasamehe na waachilie mbali (wapuuze yaliyopita). Soma Zaidi...