Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
- Ni viumbe wa kiroho wenye mabawa.
- Ni viumbe wasio na matashi ya kimwili (kula, kunywa, kulala, n.k.)
- Hawana hiari katika kumuabudu Mwenyezi Mungu (s.w).
- Ni vimbe wasio na jinsia.
- Ni viumbe walioumbwa kutokana na Nuru.
Zifuatazo ni baadhi tu ya kazi za baadhi ya Malaika.
Malaika Jibril ndiye mhusika mkuu wa kupeleka wahyi kwa mitume na manabii.
Rejea Qur’an (81:19-20), (16:2) na (11:69-73).
Kila mtu anakundi la malaika nyuma na mbele yake kumlinda na mambo yaliyo nje na uwezo wake. Pia kuna malaika wa kulia anayeandika mema na wa kushoto anayeandika maovu ya mtu.
Rejea Qur’an (82:1-12), (50:17-18) na (13:11).
Hawa ni malaika ambao huzunguka katika makundi ya waumini anapotajwa ndani yake Mwenyezi Mungu (s.w) au kusomwa Qur’an Tukufu.
Rejea Qur’an (40:7), (42:5) na (17:78).
Pindi waumini wanapopigana katika kusimamisha haki, Mwenyezi Mungu (s.w) huteremsha malaika kuwasaidia.
Rejea Qur’an (3:123-126) na (8:12).
Watu waovu waliopindukia mipaka ya Mwenyezi Mungu (s.w) wakaonywa muda mrefu na wasionyeke huangamizwa na malaika maalum.
Rejea Qur’an (11:81-83).
Malakul-Maut ndiye mhusika mkuu na wengineo katika kutoa roho za viumbe.
Rejea Qur’an (32:11).
Malaika wanaohusika na kazi hii ni Munkar na Nakir.
Mipulizo ya Parapanda katika kufisha na kufufua viumbe siku ya Qiyama itafanywa na malaika Israfil.
Rejea Qur’an (39:68).
Hili kundi jingine la malaika watakaofanya kazi hiyo siku ya Qiyama.
Rejea Qur’an (41:30-32) na (39:73).
Kuna kundi la malaika watakaokuwa wanaadhibu watu waovu motoni. Mlinzi mkuu wa milango ya moto ni Malaika Maalik.
Rejea Qur’an (25:22), (74:26-30) na (43:77).
Kuna kundi la malaika maalum kwa kazi hii tu.
Rejea Qur’an (40:7).
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Haki ya ElimuKatika Uislamu kujielimisha ni faradhi inayowahusu Waislamu wote, wanaume na wanawake: "Soma kwa jina ?
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwend akujifunz akuhusu nuzo 6 za imani ya uislamu na pia utajifunz akuhusu mafunzo yanayoweza kupatikana kwenye Nguzo hizi.
Soma Zaidi...Mgawanyo wa elimu usiokubalika katika uislamu unasababishwa na nini? (EDK form 1: mgawanyo wa elimu usiokubalika katika uislamu unasababishwa na sababu zifuatazo)
Soma Zaidi...Kipengele hichi kinahusu mgawanyiko wa elimu usiokubalika katika uislamu.sababu za mgawanyiko wa elimu udio sahihi katika uislamu.
Soma Zaidi...Kwa nini katika uislamu elimu imepewa nafasi ya kwanza ( EDK form 1 Dahana ya elimu)
Soma Zaidi...Kwenye kipengele hichi titajifunza maana ya uislamu,na maana nyingine tofauti.
Soma Zaidi...Mgawanyo wa elimu usiokubalika katika uislamu Ni upi? (EDK form 1: mgawanyo wa elimu usiokubalika katika uislamu)
Soma Zaidi...