Kumuamini malaika wa mwenyezi Mungu...

Kumuamini malaika wa mwenyezi Mungu...

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

  1. Kuamini Malaika wa Mwenyezi Mungu (s.w).

 

- Ni viumbe wa kiroho wenye mabawa.

- Ni viumbe wasio na matashi ya kimwili (kula, kunywa, kulala, n.k.)

- Hawana hiari katika kumuabudu Mwenyezi Mungu (s.w).

- Ni vimbe wasio na jinsia.

- Ni viumbe walioumbwa kutokana na Nuru.


 

            Zifuatazo ni baadhi tu ya kazi za baadhi ya Malaika.

  1. Kuleta Wahyi (ujumbe) kwa wanaadamu kutoka kwa Mwenyezi Mungu (s.w).

Malaika Jibril ndiye mhusika mkuu wa kupeleka wahyi kwa mitume na manabii.

Rejea Qur’an (81:19-20), (16:2) na (11:69-73).

 

  1. Kumchunga na Kumlinda kila mtu na kuandika amali zake nzuri na mbaya.

Kila mtu anakundi la malaika nyuma na mbele yake kumlinda na mambo yaliyo nje na uwezo wake. Pia kuna malaika wa kulia anayeandika mema na wa kushoto anayeandika maovu ya mtu.

Rejea Qur’an (82:1-12), (50:17-18) na (13:11).

 

  1. Kuwaombea Waumini maghufira kwa Mwenyezi Mungu (s.w).

Hawa ni malaika ambao huzunguka katika makundi ya waumini anapotajwa ndani yake Mwenyezi Mungu (s.w) au kusomwa Qur’an Tukufu.

Rejea Qur’an (40:7), (42:5) na (17:78).

 

  1. Kuwasaidia waumini katika vita vya kupambana na maadui wa Allah (s.w).

Pindi waumini wanapopigana katika kusimamisha haki, Mwenyezi Mungu (s.w) huteremsha malaika kuwasaidia.

Rejea Qur’an (3:123-126) na (8:12).

 

  1. Kuwaangamiza watu waovu waliopindukia mipaka.

Watu waovu waliopindukia mipaka ya Mwenyezi Mungu (s.w) wakaonywa muda mrefu na wasionyeke huangamizwa na malaika maalum.

Rejea Qur’an (11:81-83).

 

  1. Kutoa roho za viumbe.

Malakul-Maut ndiye mhusika mkuu na wengineo katika kutoa roho za viumbe.

Rejea Qur’an (32:11).

 

  1. Kuzihoji, kuzistarehesha au kuziadhibu roho za wafu kaburini.

Malaika wanaohusika na kazi hii ni Munkar na Nakir.

 

  1. Kupuliza Parapanda siku ya Qiyama.

Mipulizo ya Parapanda katika kufisha na kufufua viumbe siku ya Qiyama itafanywa na malaika Israfil.

Rejea Qur’an (39:68).

 

  1. Kuwaliwaza na kuwakaribisha watu wema peponi.

Hili kundi jingine la malaika watakaofanya kazi hiyo siku ya Qiyama.

Rejea Qur’an (41:30-32) na (39:73).

 

  1. Kuwasimanga na kuwaadhibu watu waovu motoni.

Kuna kundi la malaika watakaokuwa wanaadhibu watu waovu motoni. Mlinzi mkuu wa milango ya moto ni Malaika Maalik.

Rejea Qur’an (25:22), (74:26-30) na (43:77).

 

  1. Kumtukuza na kumsifu Mwenyezi Mungu (s.w).

Kuna kundi la malaika maalum kwa kazi hii tu.

Rejea Qur’an (40:7).

Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 1870

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Bongolite - Game zone - Play free game    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Kujiepusha na maringo na majivuno
Kujiepusha na maringo na majivuno

Maringo, majivuno, majigambo, dharau ni vipengele vya kibri.

Soma Zaidi...
Kumuamini malaika wa mwenyezi Mungu
Kumuamini malaika wa mwenyezi Mungu

Nguzo za Imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Mafundisho ya Mitume
Mafundisho ya Mitume

Mafundisho ya mitume ni eneo lingine linalo thibitisha kuwepo Allah (s.

Soma Zaidi...
Kutowatii Wazazi katika kumuasi Allah (s.w)
Kutowatii Wazazi katika kumuasi Allah (s.w)

"Na (wazazi wako) wakikushurutisha kunishirikisha na (yale) ambayo huna ilimu nayo, usiwatii; lakini kaa nao kwa wema hapa duniani (Maadamu ni wazee wako, ila usiwafuate tu mwenendo wao mbaya); Shika mwenendo wa wale wanaoelekea kwangu, kisha marejeo yenu

Soma Zaidi...
Lengo la kushushwa vitabu vya mwenyezi Mungu (s.w)
Lengo la kushushwa vitabu vya mwenyezi Mungu (s.w)

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
NGUZO ZA IMANI
NGUZO ZA IMANI

Tunajifunza katika Qur-an na hadithi sahihi kuwa Imani ya Kiislamu imejengwa juu ya nguzo sita zifuatazo:1 Kumuamini Allah (s.

Soma Zaidi...
Shahada mbili
Shahada mbili

Kwenye mada hii tutajifunza shahada mbili,tafsiri ya shahada kstika maisha ya kila siku.

Soma Zaidi...
Athari za kumuamini mwenyezi Mungu katika maisha ya kila siku
Athari za kumuamini mwenyezi Mungu katika maisha ya kila siku

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...