Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
- Ni viumbe wa kiroho wenye mabawa.
- Ni viumbe wasio na matashi ya kimwili (kula, kunywa, kulala, n.k.)
- Hawana hiari katika kumuabudu Mwenyezi Mungu (s.w).
- Ni vimbe wasio na jinsia.
- Ni viumbe walioumbwa kutokana na Nuru.
Zifuatazo ni baadhi tu ya kazi za baadhi ya Malaika.
Malaika Jibril ndiye mhusika mkuu wa kupeleka wahyi kwa mitume na manabii.
Rejea Qur’an (81:19-20), (16:2) na (11:69-73).
Kila mtu anakundi la malaika nyuma na mbele yake kumlinda na mambo yaliyo nje na uwezo wake. Pia kuna malaika wa kulia anayeandika mema na wa kushoto anayeandika maovu ya mtu.
Rejea Qur’an (82:1-12), (50:17-18) na (13:11).
Hawa ni malaika ambao huzunguka katika makundi ya waumini anapotajwa ndani yake Mwenyezi Mungu (s.w) au kusomwa Qur’an Tukufu.
Rejea Qur’an (40:7), (42:5) na (17:78).
Pindi waumini wanapopigana katika kusimamisha haki, Mwenyezi Mungu (s.w) huteremsha malaika kuwasaidia.
Rejea Qur’an (3:123-126) na (8:12).
Watu waovu waliopindukia mipaka ya Mwenyezi Mungu (s.w) wakaonywa muda mrefu na wasionyeke huangamizwa na malaika maalum.
Rejea Qur’an (11:81-83).
Malakul-Maut ndiye mhusika mkuu na wengineo katika kutoa roho za viumbe.
Rejea Qur’an (32:11).
Malaika wanaohusika na kazi hii ni Munkar na Nakir.
Mipulizo ya Parapanda katika kufisha na kufufua viumbe siku ya Qiyama itafanywa na malaika Israfil.
Rejea Qur’an (39:68).
Hili kundi jingine la malaika watakaofanya kazi hiyo siku ya Qiyama.
Rejea Qur’an (41:30-32) na (39:73).
Kuna kundi la malaika watakaokuwa wanaadhibu watu waovu motoni. Mlinzi mkuu wa milango ya moto ni Malaika Maalik.
Rejea Qur’an (25:22), (74:26-30) na (43:77).
Kuna kundi la malaika maalum kwa kazi hii tu.
Rejea Qur’an (40:7).
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu mtazamo wa uislamu juu ya dini (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Kuamini Malaika ni imani ambayo pindi ikithibiti vema moyoni, huleta taathira kubwa sana katika maisha ya kila siku na hivyo kubadili kabisa tabia na mwenendo wa Muumini.
Soma Zaidi...Ilhamu ni moja katika njia ambazo Allah huwasiliana na wanadamu na kuwafundisha mambo mablimbali.
Soma Zaidi...Vipawa vya mwanaadamu ni sababu nyingine inayomfanya mwanaadamu asiweze kuishi bila ya kufuata dini moja au nyingine.
Soma Zaidi...Kwa kutumia akili yako unaweza kumtambua Allah bila ya shaka yeyote ile. Postbhii itakufundisha nafasi ya akilonkatika kutambuwa uwepo na Uwezo wa Allah.
Soma Zaidi...