Kwa namna gani Allah huwasiliana na wanadamu kwa kupitia ndoto.

Ndoto za kweli ni moja kati ya njia ambazo Allah huwasiliana na wanadamu.

(d) Ndoto za kweli

Njia nyingine ya kupata ujumbe kutoka kwa Allah ni njia ya ndoto za kweli. Historia inatuonyesha kuwa ndoto za Mitume daima zilikuwa zikitokea kweli; kwa hiyo ulikuwa ni ujumbe moja kwa moja kutoka kwa Allah (s.w). Ndio maana Nabii Ibrahim (a.s) alipoota kuwa anamchinja mwanawe, hakusita kutekeleza hilo kwa kuwa yeye na mtoto wake Ismail (a.s) walikuwa na uhakika kuwa ni amri kutoka kwa Allah kama inavyobaini katika Aya ifuatayo:

 

“… Ewe mwanangu! Hakika nimeona katika ndoto ya kwamba ninakuchinja. Basi fikiri, waonaje?” Akasema: “Ewe baba yangu! Fanya unayoamrishwa, utanikuta Insha-Allah miongoni mwa wanao subiri.” (37:102)


Kutokea kweli kwa ndoto ya Nabii Yusuf (a.s) kama inavyobainishwa katika Qur-an ni miongoni mwa ushahidi kuwa ndoto za Mitume ni ujumbe wa kweli na wa moja kwa moja (kama ndoto yen yewe ilivyo) kutoka kwa Allah (s.w). Hebu turejee kisa cha ndoto ya Nabii Yusuf (a.s) katika aya zifuatazo:

 

Kumbuka Yusuf alipomwambia baba yake: “Ewe baba yangu! Hakika nimeona katika ndoto nyota kumi na moja na jua na mwezi. Nimeviona vyote hivi vinanisujudia” (12:4)

 


Akasema (babaake): “Ewe mwanangu! Usiwasimulie ndoto yako (hii) nduguzo wasije wakakufanyia vitim bi (kwa ajili ya husda itakayow apanda). Hakika shetani kwa mw anaadam u ni adui aliye dhahiri (atawatia uchungu tu)”. (12:5)
Kutokea kweli kwa ndoto hii kunabainishwa katika aya ifuatayo:

 

(Na walipoingia kwa Yusuf), aliwainua wazazi wake na kuwaweka katika kiti (chake) cha ufalme. Na wote wakaporomoka kumsujudia. Na (Yusuf) akasema: “Ewe babaangu! Hii ndiyo (tafsiri) hakika ya ndoto yangu ya zamani. Bila shaka Mola wangu ameihakikisha. Na amen ifanyia ihsani akanitoa gerezani na akakuleteni nyinyi kutoka jangwani; baada ya shetani kuchochea baina yangu na ndugu zangu. Hakika Mola w angu ni mw enye kulifikia alitakalo. Bila shaka yeye ni mjuzi na mwenye hikima”. (12:100).


Kutokea kweli kwa ndoto ya Mtume (s.a.w) kuwa Waislamu watangia Makka kuhiji kwa salama bila ya kuzuiliwa na mtu yeyote. Ndoto hii ilitokea kweli kama tunavyofahamishwa katika aya ifuatayo:

 


Kw a yakini Mw enyezi Mungu amemhakikishia Mtume wake ndoto yake ya haki. Bila shaka nyinyi mtaingia katika Msikiti Mtukufu Insha-Allah kwa salama; mkinyoa vichwa vyenu na mkipunguza nywele (kama ilivyowajibu kufanya hivyo wakati wa Hija). Hamtakuwa na khofu. Na (Mwenyezi Mungu) anajua msiyoyajua. Basi kabla ya haya atakupeni kushinda kuliko karibu. (48:27)

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 1883

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

mitume

Labda itaulizwa: Kwanini Mtume Muhammad (s.

Soma Zaidi...
Kutowatii Wazazi katika kumuasi Allah (s.w)

"Na (wazazi wako) wakikushurutisha kunishirikisha na (yale) ambayo huna ilimu nayo, usiwatii; lakini kaa nao kwa wema hapa duniani (Maadamu ni wazee wako, ila usiwafuate tu mwenendo wao mbaya); Shika mwenendo wa wale wanaoelekea kwangu, kisha marejeo yenu

Soma Zaidi...
Mtazamo wa uislamh juu ya ibada

Katika kipengele hich tutajifunza dhana ya ibada katika uislamu,maana ua ibada

Soma Zaidi...
Sifa za Wanafiki zilizotajwa katika surat Hashir

Huwaoni wale wanafiki wanawaambia ndugu zao walio makafiri miongoni mwa watu waliopewa Kitabu (kabla yenu) Mayahudi (Wanawaambia): "Kama mkitolewa, (mkifukuzwa hapa) tutaondoka pamoja nanyi, wala hat utamtii yoyote kabisa juu yenu.

Soma Zaidi...
Kuamini vitabu vya mwenyezi Mungu (s.w)..

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Mtazamo wa uislamu juu ya Elimu, nini maana ya elimu na nani aliye elimika.

Ni nini maana ya Elimu na ni nani aliye elimika? Uislamu una mtazamo gani juu ya Elimu?

Soma Zaidi...
Elimu yenye manufaa

Elimu yenye manufaa Ni ipi? (EDK form 1:elimu yenye manufaa)

Soma Zaidi...
Ni lipi lengo la Elimu katika yislamu?

Ni lipi lengo kuu la Elimu katika uislamu (Edk form 1 Dhanaya Elimu)

Soma Zaidi...