Python somo la 60: Hashing na Encryption kwenye Django
Katika somo hili tutajifunza: Tofauti kati ya hashing na encryption Jinsi ya kufunga packages muhimu Jinsi ya kufanya hashing kwa maneno ya kawaida (mfano “bongoclass”) Jinsi ya kufanya encryption na decrypt kutumia Fernet Jinsi Django inahash password kupitia User model Mazoezi ya vitendo
Utangulizi
Katika mifumo ya kisasa ya web, usalama wa data ni jambo la lazima. Django imeshawekewa mifumo thabiti ya kusimamia usalama wa password, na tunao uwezo wa kuongeza hashing na encryption ya data yoyote tunayotaka kulinda. Tutatumia shell ili ku run mifano.
Kabla ya kuanza, ni muhimu kujua kwamba:
-
Hashing ni “one way”—haiwezi kurejeshwa.
-
Encryption ni “two way”—unaweza kusimba na kufumbua (encrypt na decrypt).
Sasa tuingie kwenye maelezo ya kina.
1. Tofauti kati ya hashing na encryption
| Kigezo | Hashing | Encryption |
|---|---|---|
| Maana | Kubadilisha data kuwa mfuatano wa herufi zisizorejesheka | Kusimba data ili isomeke, lakini inaweza kufumbuliwa |
| Mwelekeo | One-way | Two-way |
| Matumizi | Kusalimisha password, tokens | Kulinda data nyeti kama namba za kadi, emails n.k. |
| Mfano | SHA256, bcrypt | AES, Fernet |
2. Kufunga packages zinazohitajika
(a) Install package ya cryptography (kwa ajili ya encryption)
pip install cryptography
3. Hashing katika Django`
Hashing ni kubadilisha maneno tusiyopenda yasomeke kuwa “hash code” isiyoweza kurudishwa katika hali yake ya awali.
Django inakuja na hashing nyingi tayari:
-
SHA256
-
SHA1
-
PBKDF2 (default ya Django)
-
BCrypt
-
Argon2 (salama zaidi)
(a) Mfano rahisi wa hashing kwa kutumia Python ndani ya Django shell
import hashlib
data = "bongoclass"
hash1 = hashlib.sha256(data.encode()).hexdigest()
hash2 = hashlib.sha1(data.encode()).hexdigest()
hash3 = hashlib.md5(data.encode()).hexdigest()
print("SHA256:", hash1)
print("SHA1:", hash2)
print("MD5:", hash3)
? Hii inafanya hashing—HAIWEZI KUREJESHWA KINYUME.
4. Hashing password katika Django (User Model)
Django haibebi password kama ulivyoitoa.
Badala yake, hutumia hashing yenye salt. Hii tutakuja kujifunza zaidi tutakapokuwa tunafanya project.
Mfano wa kuweka password:
from django.contrib.auth.models import User
user = User.objects.create(username="sky")
user.set_password("bongoclass123")
user.save()
? set_password() inafanya:
-
Kuongeza salt
-
Kutumia PBKDF2 (default)
-
Kutengeneza hash yenye usalama mkubwa
Hakuna developer anayeweza kuona password halisi.
5. Encryption na Decryption kutumia Fernet (cryptography)
Tofauti na hashing, encryption inaweza kufumbuliwa kurudisha data ya mwanzo. Nikukumbushe tu kuwa tunapofanya encryption maana yake tunaficha data kwa kuziweka kwenye string maalumu ili mtu asiweze kuona data halisi. Hivyo ili kuirudisha data hiyo katika hali ya kawaida tunatakiwa tufanye decryption. hivyo decryption ni kinyume cha encryption. Jambo la kuzingatia ni kutumia key moja.
Hatua ya 1: Tengeneza key
Key ni kama password za hiyo data yako. Bila ya kuwa na key zilizo sahihi huwezi kuifunguwa data iliyofanyiwa hashing. Key zinatakiwa ziwe 32, na njia bora ya kutengeneza key hizo ni kwa ku run command hiyo hapo chini.
from cryptography.fernet import Fernet
print(Fernet.generate_key())
Itatoa kitu kama:
b'd4q6iHZaYe1pME1TYuRaeCCEe4bO4AUgOTaTSj9Bzg8='
Hatua ya 2: Weka kwenye settings.py
FERNET_KEY = b'd4q6iHZaYe1pME1TYuRaeCCEe4bO4AUgOTaTSj9Bzg8='
Hatua ya 3: Tumia encryption (mfano kwa email mafunzo@bongoclass.com)
from cryptography.fernet import Fernet
from django.conf import settings
cipher = Fernet(settings.FERNET_KEY)
email = "mafunzo@bongoclass.com"
encrypted = cipher.encrypt(email.encode())
print(encrypted)
Output inaweza kuwa kitu kama:
b'gAAAAABnggk0zJ7FT....'
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitau cha Fiqh 👉2 Bongolite - Game zone - Play free game 👉3 Dua za Mitume na Manabii 👉4 Madrasa kiganjani 👉5 kitabu cha Simulizi 👉6 Simulizi za Hadithi Audio
Post zinazofanana:
Python somo la 44: Data Manipulation katika Django Templates
Katika somo hili utakwend akujifunza jinsi ya kucheza na data kuzibadili kwa namna mbali mbali kwenye template
Soma Zaidi...Python somo la 59: Kufanya Mahesabu (Aggregations) Katika Django
Katika somo hili tutajifunza jinsi ya kutumia Django ORM kufanya mahesabu mbalimbali kama Sum, Avg, Count, Max, Min, pamoja na kupunguza idadi ya items zinazoonekana kwenye dashboard (LIMIT). Pia tutajifunza namna ya kutengeneza “difference” kati ya thamani kubwa na ndogo bila kubadilisha functions zozote ulizokwisha ziandika.
Soma Zaidi...Python somo la 50: database kwneye django
Katika somo hili utakwenda kujifunza vipi django inaweza kuwasiliana na database, utajifunza kuusu orm na model
Soma Zaidi...PYHON - somo la 5: Aina za data list, turple, dictionary na boolean
Katika somo hili tunakwenda kujifunza aina nyingine za data ambazo hutumika kwenye python.
Soma Zaidi...Python somo la 15: Jinsi ya kutumia while loop
Katika somo hili tutakwend akujifunza jinsi ya kutumia while loop kwneye python
Soma Zaidi...Python somo la 29: Encaosulation kwneye python
Katika somo hili utajifunza maana ya encapsulation na sheria za uandishi wake
Soma Zaidi...