picha

Python somo la 60: Hashing na Encryption kwenye Django

Katika somo hili tutajifunza: Tofauti kati ya hashing na encryption Jinsi ya kufunga packages muhimu Jinsi ya kufanya hashing kwa maneno ya kawaida (mfano “bongoclass”) Jinsi ya kufanya encryption na decrypt kutumia Fernet Jinsi Django inahash password kupitia User model Mazoezi ya vitendo

Utangulizi

Katika mifumo ya kisasa ya web, usalama wa data ni jambo la lazima. Django imeshawekewa mifumo thabiti ya kusimamia usalama wa password, na tunao uwezo wa kuongeza hashing na encryption ya data yoyote tunayotaka kulinda. Tutatumia shell ili ku run mifano.

Kabla ya kuanza, ni muhimu kujua kwamba:

Sasa tuingie kwenye maelezo ya kina.


1. Tofauti kati ya hashing na encryption

Kigezo Hashing Encryption
Maana Kubadilisha data kuwa mfuatano wa herufi zisizorejesheka Kusimba data ili isomeke, lakini inaweza kufumbuliwa
Mwelekeo One-way Two-way
Matumizi Kusalimisha password, tokens Kulinda data nyeti kama namba za kadi, emails n.k.
Mfano SHA256, bcrypt AES, Fernet

2. Kufunga packages zinazohitajika

(a) Install package ya cryptography (kwa ajili ya encryption)

pip install cryptography

3. Hashing katika Django`

Hashing ni kubadilisha maneno tusiyopenda yasomeke kuwa “hash code” isiyoweza kurudishwa katika hali yake ya awali.

Django inakuja na hashing nyingi tayari:

(a) Mfano rahisi wa hashing kwa kutumia Python ndani ya Django shell

import hashlib

data = "bongoclass"

hash1 = hashlib.sha256(data.encode()).hexdigest()
hash2 = hashlib.sha1(data.encode()).hexdigest()
hash3 = hashlib.md5(data.encode()).hexdigest()

print("SHA256:", hash1)
print("SHA1:", hash2)
print("MD5:", hash3)

? Hii inafanya hashing—HAIWEZI KUREJESHWA KINYUME.


4. Hashing password katika Django (User Model)

Django haibebi password kama ulivyoitoa.
Badala yake, hutumia hashing yenye salt. Hii tutakuja kujifunza zaidi tutakapokuwa tunafanya project.

Mfano wa kuweka password:

from django.contrib.auth.models import User

user = User.objects.create(username="sky")
user.set_password("bongoclass123")
user.save()

? set_password() inafanya:

Hakuna developer anayeweza kuona password halisi.

 


5. Encryption na Decryption kutumia Fernet (cryptography)

Tofauti na hashing, encryption inaweza kufumbuliwa kurudisha data ya mwanzo. Nikukumbushe tu kuwa tunapofanya encryption maana yake tunaficha data kwa kuziweka kwenye string maalumu ili mtu asiweze kuona data halisi. Hivyo ili kuirudisha data hiyo katika hali ya kawaida tunatakiwa tufanye decryption. hivyo decryption ni kinyume cha encryption. Jambo la kuzingatia ni kutumia key moja.

Hatua ya 1: Tengeneza key

Key ni kama password za hiyo data yako. Bila ya kuwa na key zilizo sahihi huwezi kuifunguwa data iliyofanyiwa hashing. Key zinatakiwa ziwe 32, na njia bora ya kutengeneza key hizo ni kwa ku run command hiyo hapo chini.

from cryptography.fernet import Fernet
print(Fernet.generate_key())

Itatoa kitu kama:

b'd4q6iHZaYe1pME1TYuRaeCCEe4bO4AUgOTaTSj9Bzg8='

Hatua ya 2: Weka kwenye settings.py

FERNET_KEY = b'd4q6iHZaYe1pME1TYuRaeCCEe4bO4AUgOTaTSj9Bzg8='

Hatua ya 3: Tumia encryption (mfano kwa email mafunzo@bongoclass.com)

from cryptography.fernet import Fernet
from django.conf import settings

cipher = Fernet(settings.FERNET_KEY)

email = "mafunzo@bongoclass.com"
encrypted = cipher.encrypt(email.encode())
print(encrypted)

Output inaweza kuwa kitu kama:

b'gAAAAABnggk0zJ7FT....'

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2025-11-30 22:40:58 Topic: Python Main: Masomo File: Download PDF Views 942

Share On:

Share follows: 68 | Unique share links followed: 2
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉3 Bongolite - Game zone - Play free game     👉4 Dua za Mitume na Manabii     👉5 Simulizi za Hadithi Audio     👉6 Kitau cha Fiqh    

Post zinazofanana:

Python somo la 50: database kwneye django

Katika somo hili utakwenda kujifunza vipi django inaweza kuwasiliana na database, utajifunza kuusu orm na model

Soma Zaidi...
Python somo la 48: Jinsi ya Kutumia JavaScript kwenye Fomu za Django

Katika somo hili tutakwend akujifunza kuhusi Jinsi ya Kutumia JavaScript kwenye Fomu za Django

Soma Zaidi...
PYTHON - somo la 10: string method na zinavyofanya kazi

Katika somo hili utakwenda kujfnza kuhusu string method nyinginezo. Katika somo lililopita tulijifunza kuhusu string indexing.

Soma Zaidi...
Python somo la 17: Jinsi ya kutumia user input

Katika somo hili uatkwenda kujifunz anamna ambavyo mtu anaweza kuingiza input kwneye system

Soma Zaidi...
PYTHON - somo la 8: method za namba zinazotumika kwenye python

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu number method yaani function zinazofanya kazi kwenye namba.

Soma Zaidi...
Python somo la 46: Kutengeneza Fomu na Kuituma kwa Django Template

Katika somo hili utakwenda kujifunza kutengeneza htmk form pamoja na kuituma.

Soma Zaidi...