Python somo la 60: Hashing na Encryption kwenye Django
Katika somo hili tutajifunza: Tofauti kati ya hashing na encryption Jinsi ya kufunga packages muhimu Jinsi ya kufanya hashing kwa maneno ya kawaida (mfano “bongoclass”) Jinsi ya kufanya encryption na decrypt kutumia Fernet Jinsi Django inahash password kupitia User model Mazoezi ya vitendo
Utangulizi
Katika mifumo ya kisasa ya web, usalama wa data ni jambo la lazima. Django imeshawekewa mifumo thabiti ya kusimamia usalama wa password, na tunao uwezo wa kuongeza hashing na encryption ya data yoyote tunayotaka kulinda. Tutatumia shell ili ku run mifano.
Kabla ya kuanza, ni muhimu kujua kwamba:
-
Hashing ni “one way”—haiwezi kurejeshwa.
-
Encryption ni “two way”—unaweza kusimba na kufumbua (encrypt na decrypt).
Sasa tuingie kwenye maelezo ya kina.
1. Tofauti kati ya hashing na encryption
| Kigezo | Hashing | Encryption |
|---|---|---|
| Maana | Kubadilisha data kuwa mfuatano wa herufi zisizorejesheka | Kusimba data ili isomeke, lakini inaweza kufumbuliwa |
| Mwelekeo | One-way | Two-way |
| Matumizi | Kusalimisha password, tokens | Kulinda data nyeti kama namba za kadi, emails n.k. |
| Mfano | SHA256, bcrypt | AES, Fernet |
2. Kufunga packages zinazohitajika
(a) Install package ya cryptography (kwa ajili ya encryption)
pip install cryptography
3. Hashing katika Django`
Hashing ni kubadilisha maneno tusiyopenda yasomeke kuwa “hash code” isiyoweza kurudishwa katika hali yake ya awali.
Django inakuja na hashing nyingi tayari:
-
SHA256
-
SHA1
-
PBKDF2 (default ya Django)
-
BCrypt
-
Argon2 (salama zaidi)
(a) Mfano rahisi wa hashing kwa kutumia Python ndani ya Django shell
import hashlib
data = "bongoclass"
hash1 = hashlib.sha256(data.encode()).hexdigest()
hash2 = hashlib.sha1(data.encode()).hexdigest()
hash3 = hashlib.md5(data.encode()).hexdigest()
print("SHA256:", hash1)
print("SHA1:", hash2)
print("MD5:", hash3)
? Hii inafanya hashing—HAIWEZI KUREJESHWA KINYUME.
4. Hashing password katika Django (User Model)
Django haibebi password kama ulivyoitoa.
Badala yake, hutumia hashing yenye salt. Hii tutakuja kujifunza zaidi tutakapokuwa tunafanya project.
Mfano wa kuweka password:
from django.contrib.auth.models import User
user = User.objects.create(username="sky")
user.set_password("bongoclass123")
user.save()
? set_password() inafanya:
-
Kuongeza salt
-
Kutumia PBKDF2 (default)
-
Kutengeneza hash yenye usalama mkubwa
Hakuna developer anayeweza kuona password halisi.
5. Encryption na Decryption kutumia Fernet (cryptography)
Tofauti na hashing, encryption inaweza kufumbuliwa kurudisha data ya mwanzo. Nikukumbushe tu kuwa tunapofanya encryption maana yake tunaficha data kwa kuziweka kwenye string maalumu ili mtu asiweze kuona data halisi. Hivyo ili kuirudisha data hiyo katika hali ya kawaida tunatakiwa tufanye decryption. hivyo decryption ni kinyume cha encryption. Jambo la kuzingatia ni kutumia key moja.
Hatua ya 1: Tengeneza key
Key ni kama password za hiyo data yako. Bila ya kuwa na key zilizo sahihi huwezi kuifunguwa data iliyofanyiwa hashing. Key zinatakiwa ziwe 32, na njia bora ya kutengeneza key hizo ni kwa ku run command hiyo hapo chini.
from cryptography.fernet import Fernet
print(Fernet.generate_key())
Itatoa kitu kama:
b'd4q6iHZaYe1pME1TYuRaeCCEe4bO4AUgOTaTSj9Bzg8='
Hatua ya 2: Weka kwenye settings.py
FERNET_KEY = b'd4q6iHZaYe1pME1TYuRaeCCEe4bO4AUgOTaTSj9Bzg8='
Hatua ya 3: Tumia encryption (mfano kwa email mafunzo@bongoclass.com)
from cryptography.fernet import Fernet
from django.conf import settings
cipher = Fernet(settings.FERNET_KEY)
email = "mafunzo@bongoclass.com"
encrypted = cipher.encrypt(email.encode())
print(encrypted)
Output inaweza kuwa kitu kama:
b'gAAAAABnggk0zJ7FT....'
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Simulizi za Hadithi Audio 👉2 Kitau cha Fiqh 👉3 Bongolite - Game zone - Play free game 👉4 Madrasa kiganjani 👉5 ai web app 👉6 Kitabu cha Afya
Post zinazofanana:
Python somo la 56: Kuongeza Data Katika Database kwa Kutumia Django Admin na Django Shell
Katika somo hili tutajifunza njia mbili muhimu za kuongeza data kwenye database katika project yetu ya pybongo (app: menu). Njia hizi ni: Kutumia Django Admin Kutumia Django Shell Utafahamu pia jinsi ya kusajili models kwenye admin, jinsi ya kuingia admin panel, na namna ya kutengeneza entries mpya za MenuItem.
Soma Zaidi...Python somo la 46: Kutengeneza Fomu na Kuituma kwa Django Template
Katika somo hili utakwenda kujifunza kutengeneza htmk form pamoja na kuituma.
Soma Zaidi...Python somo la 18: Jinsi ya kuandika function
Katika somo hili utakwend akujifunza jinsi ya kuandika function, kuweka parameter na kuitumia function
Soma Zaidi...Python somo la 16: Jinsi ya kutumia break na continue kwenye loop
Katika somo hili tunakwenda kujifunza matumizi ya break na continue kwenye loop
Soma Zaidi...PYTHON somo la 12: assignment operator, logical operator, identity oeprator na membership operator
Katika somo hili utakwenda kujfunza operator nyingine kama assignment operator logical, identity operator na membership operator.
Soma Zaidi...Python somo la 37: Jinsi ya ku install Django na kutengeneza project na app
Katika somo ili utajifunza hatuwa kwa hatuwa za ku install Django, kutengeneza project na kutengeneza app
Soma Zaidi...