Katika somo hili tutajifunza: Tofauti kati ya hashing na encryption Jinsi ya kufunga packages muhimu Jinsi ya kufanya hashing kwa maneno ya kawaida (mfano “bongoclass”) Jinsi ya kufanya encryption na decrypt kutumia Fernet Jinsi Django inahash password kupitia User model Mazoezi ya vitendo
Katika mifumo ya kisasa ya web, usalama wa data ni jambo la lazima. Django imeshawekewa mifumo thabiti ya kusimamia usalama wa password, na tunao uwezo wa kuongeza hashing na encryption ya data yoyote tunayotaka kulinda. Tutatumia shell ili ku run mifano.
Kabla ya kuanza, ni muhimu kujua kwamba:
Hashing ni “one way”—haiwezi kurejeshwa.
Encryption ni “two way”—unaweza kusimba na kufumbua (encrypt na decrypt).
Sasa tuingie kwenye maelezo ya kina.
| Kigezo | Hashing | Encryption |
|---|---|---|
| Maana | Kubadilisha data kuwa mfuatano wa herufi zisizorejesheka | Kusimba data ili isomeke, lakini inaweza kufumbuliwa |
| Mwelekeo | One-way | Two-way |
| Matumizi | Kusalimisha password, tokens | Kulinda data nyeti kama namba za kadi, emails n.k. |
| Mfano | SHA256, bcrypt | AES, Fernet |
pip install cryptography
Hashing ni kubadilisha maneno tusiyopenda yasomeke kuwa “hash code” isiyoweza kurudishwa katika hali yake ya awali.
Django inakuja na hashing nyingi tayari:
SHA256
SHA1
PBKDF2 (default ya Django)
BCrypt
Argon2 (salama zaidi)
import hashlib
data = "bongoclass"
hash1 = hashlib.sha256(data.encode()).hexdigest()
hash2 = hashlib.sha1(data.encode()).hexdigest()
hash3 = hashlib.md5(data.encode()).hexdigest()
print("SHA256:", hash1)
print("SHA1:", hash2)
print("MD5:", hash3)
👏 Hii inafanya hashing—HAIWEZI KUREJESHWA KINYUME.
Django haibebi password kama ulivyoitoa.
Badala yake, hutumia hashing yenye salt. Hii tutakuja kujifunza zaidi tutakapokuwa tunafanya project.
Mfano wa kuweka password:
from django.contrib.auth.models import User
user = User.objects.create(username="sky")
user.set_password("bongoclass123")
user.save()
💡 set_password() inafanya:
Kuongeza salt
Kutumia PBKDF2 (default)
Kutengeneza hash yenye usalama mkubwa
Hakuna developer anayeweza kuona password halisi.
Tofauti na hashing, encryption inaweza kufumbuliwa kurudisha data ya mwanzo. Nikukumbushe tu kuwa tunapofanya encryption maana yake tunaficha data kwa kuziweka kwenye string maalumu ili mtu asiweze kuona data halisi. Hivyo ili kuirudisha data hiyo katika hali ya kawaida tunatakiwa tufanye decryption. hivyo decryption ni kinyume cha encryption. Jambo la kuzingatia ni kutumia key moja.
Key ni kama password za hiyo data yako. Bila ya kuwa na key zilizo sahihi huwezi kuifunguwa data iliyofanyiwa hashing. Key zinatakiwa ziwe 32, na njia bora ya kutengeneza key hizo ni kwa ku run command hiyo hapo chini.
from cryptography.fernet import Fernet
print(Fernet.generate_key())
Itatoa kitu kama:
b'd4q6iHZaYe1pME1TYuRaeCCEe4bO4AUgOTaTSj9Bzg8='
settings.pyFERNET_KEY = b'd4q6iHZaYe1pME1TYuRaeCCEe4bO4AUgOTaTSj9Bzg8='
from cryptography.fernet import Fernet
from django.conf import settings
cipher = Fernet(settings.FERNET_KEY)
email = "mafunzo@bongoclass.com"
encrypted = cipher.encrypt(email.encode())
print(encrypted)
Output inaweza kuwa kitu kama:
b'gAAAAABnggk0zJ7FT....'
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
Katika somo hili, tutajifunza: Maana ya Python shell na umuhimu wake. Tofauti kati ya shell na terminal ya kawaida. Matumizi ya shell, hususan kwenye Django. Amri muhimu zaidi za Python shell, zilizotokana na models na views zako za pybongo.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujfunza operator nyingine kama assignment operator logical, identity operator na membership operator.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwend akujifunza jinsi ya kupokea na kuchakata fomu
Soma Zaidi...Katika somo hili tutakwend akujifunza kuhusi Jinsi ya Kutumia JavaScript kwenye Fomu za Django
Soma Zaidi...Katika somo hili uatajifunza jinsi gani unaweza kutumia view kma logic kuuma data kwenye template
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunza kuhusu maana ya python na kazi zake. pia jinsi ya kuandaa kifaa chako kwa ajili ya somo.
Soma Zaidi...Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu string indexing. Kama tulivyojifunza kuhusu namba katika somo lililopita, basi hapa tutakwenda kucheza na string.
Soma Zaidi...Katika somo hili tutajifunza jinsi Django hutumia migrations kuunda na kubadilisha tables kwenye database kulingana na models tunazoandika. Tutapitia maana ya migration, hatua za kuitumia, umuhimu wake, misingi ya makemigrations na migrate, pamoja na mfano halisi kutoka kwenye project yetu ya pybongo (app: menu).
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya ku host website ya Django. Hapa tutakwenda kutuma plaform ya pythonanywhere.com.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwend akujifunza ktengeneza model kwa ajili ya database table ya menu yetu.
Soma Zaidi...