Python somo la 60: Hashing na Encryption kwenye Django
Katika somo hili tutajifunza: Tofauti kati ya hashing na encryption Jinsi ya kufunga packages muhimu Jinsi ya kufanya hashing kwa maneno ya kawaida (mfano “bongoclass”) Jinsi ya kufanya encryption na decrypt kutumia Fernet Jinsi Django inahash password kupitia User model Mazoezi ya vitendo
Utangulizi
Katika mifumo ya kisasa ya web, usalama wa data ni jambo la lazima. Django imeshawekewa mifumo thabiti ya kusimamia usalama wa password, na tunao uwezo wa kuongeza hashing na encryption ya data yoyote tunayotaka kulinda. Tutatumia shell ili ku run mifano.
Kabla ya kuanza, ni muhimu kujua kwamba:
-
Hashing ni “one way”—haiwezi kurejeshwa.
-
Encryption ni “two way”—unaweza kusimba na kufumbua (encrypt na decrypt).
Sasa tuingie kwenye maelezo ya kina.
1. Tofauti kati ya hashing na encryption
| Kigezo | Hashing | Encryption |
|---|---|---|
| Maana | Kubadilisha data kuwa mfuatano wa herufi zisizorejesheka | Kusimba data ili isomeke, lakini inaweza kufumbuliwa |
| Mwelekeo | One-way | Two-way |
| Matumizi | Kusalimisha password, tokens | Kulinda data nyeti kama namba za kadi, emails n.k. |
| Mfano | SHA256, bcrypt | AES, Fernet |
2. Kufunga packages zinazohitajika
(a) Install package ya cryptography (kwa ajili ya encryption)
pip install cryptography
3. Hashing katika Django`
Hashing ni kubadilisha maneno tusiyopenda yasomeke kuwa “hash code” isiyoweza kurudishwa katika hali yake ya awali.
Django inakuja na hashing nyingi tayari:
-
SHA256
-
SHA1
-
PBKDF2 (default ya Django)
-
BCrypt
-
Argon2 (salama zaidi)
(a) Mfano rahisi wa hashing kwa kutumia Python ndani ya Django shell
import hashlib
data = "bongoclass"
hash1 = hashlib.sha256(data.encode()).hexdigest()
hash2 = hashlib.sha1(data.encode()).hexdigest()
hash3 = hashlib.md5(data.encode()).hexdigest()
print("SHA256:", hash1)
print("SHA1:", hash2)
print("MD5:", hash3)
? Hii inafanya hashing—HAIWEZI KUREJESHWA KINYUME.
4. Hashing password katika Django (User Model)
Django haibebi password kama ulivyoitoa.
Badala yake, hutumia hashing yenye salt. Hii tutakuja kujifunza zaidi tutakapokuwa tunafanya project.
Mfano wa kuweka password:
from django.contrib.auth.models import User
user = User.objects.create(username="sky")
user.set_password("bongoclass123")
user.save()
? set_password() inafanya:
-
Kuongeza salt
-
Kutumia PBKDF2 (default)
-
Kutengeneza hash yenye usalama mkubwa
Hakuna developer anayeweza kuona password halisi.
5. Encryption na Decryption kutumia Fernet (cryptography)
Tofauti na hashing, encryption inaweza kufumbuliwa kurudisha data ya mwanzo. Nikukumbushe tu kuwa tunapofanya encryption maana yake tunaficha data kwa kuziweka kwenye string maalumu ili mtu asiweze kuona data halisi. Hivyo ili kuirudisha data hiyo katika hali ya kawaida tunatakiwa tufanye decryption. hivyo decryption ni kinyume cha encryption. Jambo la kuzingatia ni kutumia key moja.
Hatua ya 1: Tengeneza key
Key ni kama password za hiyo data yako. Bila ya kuwa na key zilizo sahihi huwezi kuifunguwa data iliyofanyiwa hashing. Key zinatakiwa ziwe 32, na njia bora ya kutengeneza key hizo ni kwa ku run command hiyo hapo chini.
from cryptography.fernet import Fernet
print(Fernet.generate_key())
Itatoa kitu kama:
b'd4q6iHZaYe1pME1TYuRaeCCEe4bO4AUgOTaTSj9Bzg8='
Hatua ya 2: Weka kwenye settings.py
FERNET_KEY = b'd4q6iHZaYe1pME1TYuRaeCCEe4bO4AUgOTaTSj9Bzg8='
Hatua ya 3: Tumia encryption (mfano kwa email mafunzo@bongoclass.com)
from cryptography.fernet import Fernet
from django.conf import settings
cipher = Fernet(settings.FERNET_KEY)
email = "mafunzo@bongoclass.com"
encrypted = cipher.encrypt(email.encode())
print(encrypted)
Output inaweza kuwa kitu kama:
b'gAAAAABnggk0zJ7FT....'
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Dua za Mitume na Manabii 👉2 ai web app 👉3 kitabu cha Simulizi 👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉5 Bongolite - Game zone - Play free game 👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Post zinazofanana:
PYTHON - somo la 9: indexing katika strinfg
Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu string indexing. Kama tulivyojifunza kuhusu namba katika somo lililopita, basi hapa tutakwenda kucheza na string.
Soma Zaidi...Python somo la 24: Nini maana ya Object Oriented Programming
Hapa tunakwenda kujifunza kuhusu OOP ambapo ni miongoni mwa mitindo ya uandishi wa code
Soma Zaidi...Python somo la 62 Kupakia picha (upload) na kuisoma kutoka kwenye database
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kushughulika na faili, kama ku upload faili kwenye django.
Soma Zaidi...Python somo la 31: Jinsi ya kutengeneza faili na folder
Katika somo hili utajifunz ajinsi ya kutengeneza folda, faili na kuweka data kwneye faili
Soma Zaidi...Python somo la 45: Kutumia Loops na Conditions katika Django Templates
Katika somo hili utakwend akujifunza kuchakata data kwa Kutumia Loops na Conditions katika Django Templates
Soma Zaidi...Python somo la 42: Template tag
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhsu Template Tag nini na kazi zake. Pia utajifunza sheria za uandishi wake.
Soma Zaidi...