image

PYTHON - somo la 1: Jinsi ya ku install python

Katika somo hili utajifunza kuhusu maana ya python na kazi zake. pia jinsi ya kuandaa kifaa chako kwa ajili ya somo.

Python ni moja katika lugha za kikompyuta zilizo maarufu. Ilianzishwa mwaka 1991 na Guido van Rossum. Python ni moja katika high level programming language ambayo ni general programming language yaani inatumika kwenye field nyingi.

 

Python imekuwa ikifanyiwa marekebisho mengi toka ilipoanzishwa na sasa tupo katika toleo la 3 yaani python 3. Katika course hii tutakwenda kutumia toleo la 3 la python.

 

Matumizi ya python

  1. Hutumika kwenye kutengeneza website, web app na blog kama sever side langage. Yaani ku wasiliana na server .
  2. Hutumiaka kwenye kutengeneza software mbalimbali kama game
  3. Hutumika kufanya mahesabau kama kwenye takwimu.
  4. Pia huweza kutumika kuwa kama system scripting.

 

Python file extension:

Kama ilivyo kuwa language zote zina extension kama ilivyo hatml ni .html, php ni .php, basi na python ni .py. Mfano main.py

 

Maandalizi kwa ajili ya course hii:

 

Kwa watumiaji wa kompyuta:

Course zinazopatikana bongoclass zinalenga wanafunzi wa aina zote. Kwa wale wanaotumia kompyuta na wale waotumia simu janja. Sasa kwa wale wanaotumia kompyuta fuata maelekezo haya:-

  1. Kwanza install python. Njia rahisi ya kuistall python ni kuwa na python IDE. Ninapendelea utumie pytharm kutoka jetbrain. IDE hii ni rahisi kutumia na haihitaji configuration nyingine. Fuata link hii  https://www.jetbrains.com/pycharm/download/download-thanks.html?platform=windows&code=PCC
  2. Baada ya ku download install hiyo software. Hakikisha una internet ili kwamba kama itahitaji ongezeko la tools iweze ku download. Hata hivyo software hii ni ya offline
  3. Baada ya kumaliza ku install, bofya icon yake ili kuifunguwa. Hapo utakutana na ukurasa huu.

 

Hapo bofya palipoandika New Project.kisha utakuja ukurasa mwingine ambao ni huu

 

Kama ndio mara yako ya kwanza hapo usiset kitu chochote zaidi ya jina la project yako tu. hapo mwanzoni kabisha kuna palipoandikwa pythonProject 

Badili jina la project yako kutoka pythonProject kuwa jina unalotaka wewe. Kwa mfano mimi nitasema pythonMafunzo 

Baada ya hapo bofya create kwa chini upande wa kulia. Itaanza kuload ili kuandaa mazngira ya hiyo project yako. Baada ya kumaliza utakutana na ukurasa mkubwa ambao ndio uwanja wa kuanzika code zako.

 

Kwa upande wa kushoto kuna project root. Ambapo kuna faili linaonekana limefungka kwa upande wa kulia na kuna code utaziona. Faili hilo linaita main.py hilo ndio faili la kwanza la project yako.

 

Sasa fanuya hivi. Kwenye huo ukurasa uliofunguka upande wa kulia futa kila kitu kisha weka code hizi:

print("haloo bongoclass")

 

Baada ya hapo run hizo code kwa kubofya kialama cha ku play kilicho upande wa kulia kwa juu

 

Angalia kwa chini kuna ukurasa umefunguka. Ukurasa huo utaochesha vitu vitatu:-

  1. Location ya hilo faili
  2. Matokeo ya hizo code
  3. Uwepo wa error

 

Hiyo namba 1 inaonyesha hilo faili linapatikana wapi kwenye kompyuta yako. Hiyo namba 2 ndio matokeo ya code zetu. Kwa mfano hapo utaona haloo bongoclass hayo ni matokeo ya code ambayo tumeandika hapo juu. Ha hiyo namba tatu utaona kuwa code 0 kumaanisa kuwa hakuna tatizo. Kama umefiika hapo basi kompyuta yako ipo tayari kuendelea ku code python.

 

Location ya project yako:

Ili kujuwa mahali ilipo  project yako utakwenda kwenye local disc c, kisha user kisha jina la user wa kompyuta yako, kisha shuka mpaka chini utakuta folder limeandika pycharmProject. Hapo ndipo project yako utaikuta.

 

Kwa watumiaji wa kompyuta somo letu limeishia hapa. Tkutane somo la pili ambapo tutakwenda kuzungumzsia sheria za kuandika code ya python.

 

Kwa watumiaji wa simu:

  1. Ingia play store kisha tafuta app inayoitwa Python 3 - IDE for Python 3 kam">...



    Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa





               

    Je! umeipenda hii post?
    Ndio            Hapana            Save post

    Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1574


    Sponsored links
    👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Madrasa kiganjani    

    Post zifazofanana:-

    PYTHON - somo la 9: indexing katika strinfg
    Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu string indexing. Kama tulivyojifunza kuhusu namba katika somo lililopita, basi hapa tutakwenda kucheza na string. Soma Zaidi...

    PYTHON somo la 12: assignment operator, logical operator, identity oeprator na membership operator
    Katika somo hili utakwenda kujfunza operator nyingine kama assignment operator logical, identity operator na membership operator. Soma Zaidi...

    PYTHON - somo la 3: Jinsi ya kuandika variable kwenye python
    Katika somo hili utajifunza maana ya variable, na sheria za kutengeneza variable kwenye python. Pia utajifunza maneno ambayo hayafai kutumiwa kama variable Soma Zaidi...

    PYTHON - somo la 8: method za namba zinazotumika kwenye python
    Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu number method yaani function zinazofanya kazi kwenye namba. Soma Zaidi...

    PYTHON - somo la 10: string method na zinavyofanya kazi
    Katika somo hili utakwenda kujfnza kuhusu string method nyinginezo. Katika somo lililopita tulijifunza kuhusu string indexing. Soma Zaidi...

    PYTHON - somo la 2: Sheria za uandishi wa pyhton yaani syntax za python
    Katika somo hili utakwenda kujifunza syntaxy za python yaani sheria na kanuni za kuandika code za python Soma Zaidi...

    PYTHON somo la 11: Matumizi ya comperison eperator katika python
    Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu operator. Hasa hapa tutakwend akujifunz akuhusu comparison operaor. Soma Zaidi...

    PYTHON - somo la 6: Jinsi ya kujuwa aina ya data iliyotumika
    Katika somo hili utajifunza jisni ya kujuwa aina ya data iliyotumika kwenye python Soma Zaidi...

    PYHON - somo la 5: Aina za data list, turple, dictionary na boolean
    Katika somo hili tunakwenda kujifunza aina nyingine za data ambazo hutumika kwenye python. Soma Zaidi...

    PYTHON - somo la 7: Jinsi ya kubadili aina ya data
    Katika soo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kubaduli aina moja ya data kwena aina nyingine. Kwa mfano unaweza kubadili namba kuwa string ama kubadili string kuwa nanda ama kubadili float kuwa int. Soma Zaidi...

    PYTHON - somo la 4: Aina za data kwenye python
    Katika somo hili utakwenda kujifunza aina za data ambazo hutumika kwenye python. hapa utajifunza aina kuu 3 za data. Soma Zaidi...

    PYTHON - somo la 1: Jinsi ya ku install python
    Katika somo hili utajifunza kuhusu maana ya python na kazi zake. pia jinsi ya kuandaa kifaa chako kwa ajili ya somo. Soma Zaidi...