picha

PYTHON - somo la 1: Jinsi ya ku install python

Katika somo hili utajifunza kuhusu maana ya python na kazi zake. pia jinsi ya kuandaa kifaa chako kwa ajili ya somo.

Python ni moja katika lugha za kikompyuta zilizo maarufu. Ilianzishwa mwaka 1991 na Guido van Rossum. Python ni moja katika high level programming language ambayo ni general programming language yaani inatumika kwenye field nyingi.

 

Python imekuwa ikifanyiwa marekebisho mengi toka ilipoanzishwa na sasa tupo katika toleo la 3 yaani python 3. Katika course hii tutakwenda kutumia toleo la 3 la python.

 

Matumizi ya python

  1. Hutumika kwenye kutengeneza website, web app na blog kama sever side langage. Yaani ku wasiliana na server .
  2. Hutumiaka kwenye kutengeneza software mbalimbali kama game
  3. Hutumika kufanya mahesabau kama kwenye takwimu.
  4. Pia huweza kutumika kuwa kama system scripting.

 

Python file extension:

Kama ilivyo kuwa language zote zina extension kama ilivyo hatml ni .html, php ni .php, basi na python ni .py. Mfano main.py

 

Maandalizi kwa ajili ya course hii:

 

Kwa watumiaji wa kompyuta:

Course zinazopatikana bongoclass zinalenga wanafunzi wa aina zote. Kwa wale wanaotumia kompyuta na wale waotumia simu janja. Sasa kwa wale wanaotumia kompyuta fuata maelekezo haya:-

  1. Kwanza install python. Njia rahisi ya kuistall python ni kuwa na python IDE. Ninapendelea utumie pytharm kutoka jetbrain. IDE hii ni rahisi kutumia na haihitaji configuration nyingine. Fuata link hii  https://www.jetbrains.com/pycharm/download/download-thanks.html?platform=windows&code=PCC
  2. Baada ya ku download install hiyo software. Hakikisha una internet ili kwamba kama itahitaji ongezeko la tools iweze ku download. Hata hivyo software hii ni ya offline
  3. Baada ya kumaliza ku install, bofya icon yake ili kuifunguwa. Hapo utakutana na ukurasa huu.

 

Hapo bofya palipoandika New Project.kisha utakuja ukurasa mwingine ambao ni huu

 

Kama ndio mara yako ya kwanza hapo usiset kitu chochote zaidi ya jina la project yako tu. hapo mwanzoni kabisha kuna palipoandikwa pythonProject 

Badili jina la project yako kutoka pythonProject kuwa jina unalotaka wewe. Kwa mfano mimi nitasema pythonMafunzo 

Baada ya hapo bofya create kwa chini upande wa kulia. Itaanza kuload ili kuandaa mazngira ya hiyo project yako. Baada ya kumaliza utakutana na ukurasa mkubwa ambao ndio uwanja wa kuanzika code zako.

 

Kwa upande wa kushoto kuna project root. Ambapo kuna faili linaonekana limefungka kwa upande wa kulia na kuna code utaziona. Faili hilo linaita main.py hilo ndio faili la kwanza la project yako.

 

Sasa fanuya hivi. Kwenye huo ukurasa uliofunguka upande wa kulia futa kila kitu kisha weka code hizi:

print("haloo bongoclass")

 

Baada ya hapo run hizo code kwa kubofya kialama cha ku play kilicho upande wa kulia kwa juu

 

Angalia kwa chini kuna ukurasa umefunguka. Ukurasa huo utaochesha vitu vitatu:-

  1. Location ya hilo faili
  2. Matokeo ya hizo code
  3. Uwepo wa error

 

Hiyo namba 1 inaonyesha hilo faili linapatikana wapi kwenye kompyuta yako. Hiyo namba 2 ndio matokeo ya code zetu. Kwa mfano hapo utaona haloo bongoclass hayo ni matokeo ya code ambayo tumeandika hapo juu. Ha hiyo namba tatu utaona kuwa code 0 kumaanisa kuwa hakuna tatizo. Kama umefiika hapo basi kompyuta yako ipo tayari kuendelea ku code python.

 

Location ya project yako:

Ili kujuwa mahali ilipo  project yako utakwenda kwenye local disc c, kisha user kisha jina la user wa kompyuta yako, kisha shuka mpaka chini utakuta folder limeandika pycharmProject. Hapo ndipo project yako utaikuta.

 

Kwa watumiaji wa kompyuta somo letu limeishia hapa. Tkutane somo la pili ambapo tutakwenda kuzungumzsia sheria za kuandika code ya python.

 

Kwa watumiaji wa simu:

  1. Ingia play store kisha tafuta app ina">...

    Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

    Zoezi la Maswali

    Endelea


    Umeionaje Makala hii.. ?

    Nzuri            Mbaya            Save
    Author: Rajabu image Tarehe: 2023-10-20 Topic: Python Main: ICT File: Download PDF Views 3159

    Share On:

    Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
    Sponsored links
    👉1 Kitabu cha Afya    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 Madrasa kiganjani    👉4 ai web app    👉5 Dua za Mitume na Manabii    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

    Post zinazofanana:

    PYHON - somo la 5: Aina za data list, turple, dictionary na boolean

    Katika somo hili tunakwenda kujifunza aina nyingine za data ambazo hutumika kwenye python.

    Soma Zaidi...
    Python somo la 23: Library kwenye python

    Hapa utajifunza maana ya library, kazi zake aina zake na jinsi ya ku install lirary

    Soma Zaidi...
    Python somo la 53: Kutengeneza HTML Form na Django View kwa ajili ya kuingiza data

    Katika somo hili tutaangalia jinsi ya kutengeneza fomu ya HTML kwa ajili ya kuingiza data kwenye jedwali la MenuItem, pamoja na kutengeneza view itakayopokea data hiyo na kuihifadhi kwenye database. Pia tutaunganisha form na URL route.

    Soma Zaidi...
    Python somo la 26: Sheria za uandishi wa object

    Katika somo hili utakwend akujifunza maana ya object, na sheria za kuandika object.

    Soma Zaidi...
    Python somo la 38: Kubadilisha landing page ya Django Framework

    Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kubadili ukurasa wa landing page wa Django na kuweka ukurasa tunaoutaka sisi.

    Soma Zaidi...
    Python somo la 56: Kuongeza Data Katika Database kwa Kutumia Django Admin na Django Shell

    Katika somo hili tutajifunza njia mbili muhimu za kuongeza data kwenye database katika project yetu ya pybongo (app: menu). Njia hizi ni: Kutumia Django Admin Kutumia Django Shell Utafahamu pia jinsi ya kusajili models kwenye admin, jinsi ya kuingia admin panel, na namna ya kutengeneza entries mpya za MenuItem.

    Soma Zaidi...
    Python somo la 22: Package kwenye Python

    Hapa utakwenda kujifunz amaana ya package, aina zake na jinsi ya kuandika package.

    Soma Zaidi...
    Python somo la 54: Jinsi ya Kusoma Data Kutoka Database kwenye Django

    Katika somo hili tutajifunza namna ya kusoma data kutoka kwenye database kupitia Django ORM, jinsi ya kuzipeleka kwenye view, na jinsi ya kuzionyesha kwenye HTML template.

    Soma Zaidi...
    Python somo la 34: Kutumia html kwneye python

    Katika somo hili utakwend akujifunz ajinsi ya kutumia html kwneye python

    Soma Zaidi...