picha

Python somo la 52: Kutengeneza table na kufanya Migrations Katika Django

Katika somo hili tutajifunza jinsi Django hutumia migrations kuunda na kubadilisha tables kwenye database kulingana na models tunazoandika. Tutapitia maana ya migration, hatua za kuitumia, umuhimu wake, misingi ya makemigrations na migrate, pamoja na mfano halisi kutoka kwenye project yetu ya pybongo (app: menu).

Utangulizi

Django haitengenezi table moja kwa moja mara tu unapounda model; badala yake hutumia mfumo wa migrations unaosimamia mabadiliko yote ya database. Hii inafanya kazi kuwa salama, rahisi, na isiyohitaji kuandika SQL mwenyewe. Somo hili litakufundisha jinsi migrations zinavyofanya kazi na namna ya kuzitumia kwa usahihi.

 

Nataka ukumbuke kuwa, kwneye somo lililopita nimekueleza kuwa model ni class ambayo ndio inaeleza structure ama muundo wa table zetu kwneye database. Sasa baada ya kutengeneza structure hiyo ama muundo wa hiyo table, hapa tutajifunza kufanya migration yaani kutengeneza table zenyewe kulingana na model. ni sawa na kusema kuwa tunazifanya model zituletee kitu tunachokitaka.

 

🟑 1. Migration ni nini?

Migration ni faili maalum linalotengenezwa na Django ili kurekodi na kutekeleza mabadiliko yote unayofanya kwenye model. Hili faili linaelezea Django jinsi ya:

Kwa kifupi:
Migration = Maelezo ya mabadiliko ya database yanayotokana na models.


🟑 2. Kwa nini Migration ni muhimu?


🟑 3. Namna Django Hutumia Migration

Django hutumia hatua mbili muhimu:


Hatua ya 1: Kutengeneza Migration

Baada ya kuunda au kubadilisha model, andika:

python manage.py makemigrations

Hii inasoma models zako na kutengeneza faili kama:

menu/migrations/0001_initial.py

Faili hili linaelezea Django kuwa unataka:

faili hili utalikuta kwneye folda linaloitwa migrations. na kila tutakapofanya migration basi faili ligine litatengenezwa.


Hatua ya 2: Kutekeleza Migration Kwenye Database

Baada ya kukamilisha hatua ya kwanza, sasa unaitekeleza kwa:

python manage.py migrate

Amri hii:


🟑 4. Mfano Kwenye Project Yetu: pybongo (app: menu)

Model tuliyotengeneza:

from django.db import models

class MenuItem(models.Model):
    jina = models.CharField(max_length=100)
    maelezo = models.TextField(blank=True)
    muda_upatikanaji = models.CharField(max_length=50)
    bei = models.DecimalField(max_digits=10, decimal_places=2)

    def __str__(self):
        return self.jina

Hatua:

python manage.py makemigrations
python manage.py migrate

Matokeo:

Hapo utaona mabadiliko kwnye faili la sqlite3 ambalo ndio faili la database. Huko mbeleni tutajifunza kuhusu aina nyingine za database.

...

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:45 Topic: Python Main: ICT File: Download PDF Views 197

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
πŸ‘‰1 Madrasa kiganjani    πŸ‘‰2 Dua za Mitume na Manabii    πŸ‘‰3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    πŸ‘‰4 web hosting    πŸ‘‰5 Kitabu cha Afya    πŸ‘‰6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

Python somo la 39: Jinsi ya Kuongeza Kurasa Nyingine Katika Django View

Katika somo hili utakwenda kujifunza zaidi kuhusu Jinsi ya Kuongeza Kurasa Nyingine Katika Django View

Soma Zaidi...
Python somo la 30: Data abstraction

Katika somo hili utakwend akujifunz akuhusu nadharia ya data abstraction na kazi zake kwenye OOP

Soma Zaidi...
Python somo la 19: Aina za Function

Katika somo hili utakwend akujifunza aina mbalimbali za function ambazo tunaweza kuzitumia kwenye python.

Soma Zaidi...
Python somo la 59: Kufanya Mahesabu (Aggregations) Katika Django

Katika somo hili tutajifunza jinsi ya kutumia Django ORM kufanya mahesabu mbalimbali kama Sum, Avg, Count, Max, Min, pamoja na kupunguza idadi ya items zinazoonekana kwenye dashboard (LIMIT). Pia tutajifunza namna ya kutengeneza β€œdifference” kati ya thamani kubwa na ndogo bila kubadilisha functions zozote ulizokwisha ziandika.

Soma Zaidi...
Python somo la 50: database kwneye django

Katika somo hili utakwenda kujifunza vipi django inaweza kuwasiliana na database, utajifunza kuusu orm na model

Soma Zaidi...
Python somo la 26: Sheria za uandishi wa object

Katika somo hili utakwend akujifunza maana ya object, na sheria za kuandika object.

Soma Zaidi...
Python somo la 17: Jinsi ya kutumia user input

Katika somo hili uatkwenda kujifunz anamna ambavyo mtu anaweza kuingiza input kwneye system

Soma Zaidi...
Python somo la 62 Kupakia picha (upload) na kuisoma kutoka kwenye database

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kushughulika na faili, kama ku upload faili kwenye django.

Soma Zaidi...
Python somo la 21: Module katika python

Katika somo hili utakwend akujifunz amaana ya module, kazi zake, aina zake na jinsi ya kuandika modile

Soma Zaidi...
Python somo la 29: Encaosulation kwneye python

Katika somo hili utajifunza maana ya encapsulation na sheria za uandishi wake

Soma Zaidi...