picha

PYTHON - somo la 9: indexing katika strinfg

Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu string indexing. Kama tulivyojifunza kuhusu namba katika somo lililopita, basi hapa tutakwenda kucheza na string.

Indexing:

Unapopewa string yeyote, katika python unaweza ku access yaani kufanyia kazi sehemu tu ya string hiyo na kuacha sehemu nyingine. Huko nyuma tulijifunza kuhusu habari hii ya indexing na nikakueleza kuwa string index inaanzia na 0. Sasa katika somo hili tutainga ndani zaidi katika kuijuwa indexing.

 

Katika somo letu hili tutakwenda kuifanyia kazi string hii Jifunze python na Bongoclass”

 

Mfano 1:

Katika mfano huu tutaona jinsi ya kufanya index kwa character ya mwanzo tu. yaani tunataka ku dislay haerufi ya mwanzo tu ambayo ni j. Kama nilivyokueleza kuwa indexing inaanzia na 0. Kwa hiyo character ya mwanzo itakuwa na index ya 0.

 

string = 'Jifunze python na Bongoclass'

print(string[0])

Hii itatupa jibu j

 

Mfano 2:

Kwa kupitia mfano huo unaweza ku display character yeyote unayotaka kwenye string yetu. Sasa kwa mfano tunataka ku display character ya 12 kwenye string.

string = 'Jifunze python na Bongoclass'

print(string[12])

 

Hii itakupa jibu o

 

Mfano 3:

Saa kwa mfano tunataka kudisplay character ya mwisho to, hapa unaweza kuhesabu ilikujuwa ipo index ya ngapi kisha utatumia mfano uliotangulia. Njia nyingine ni kutumia negative number yaani namba hasi.

 

Index inapokuwa na namba hasi maana yake imeanza kuhesabiwa kutoka mwisho. Sasa ukihesabu kutoka mwisho index haianzi na -0 ila inaanza na -1 kwa kuwa -0 itakuwa ni ile character ya kwanza kwenye index. Hivyo basi kupata character ya mwisho tutaandika hivi

string = 'Jifunze python na Bongoclass'

print(string[-1])

Hii itatupa jibu s

 

 

Mfano 4:

Kwa mfano kama huo ukitaka ku display character ya 4 kutoka mwisho tutatumai -4

string = 'Jifunze python na Bongoclass'

print(string[-4])

Hii itakupa jibu l

 

Mfano 5:

Pia unaweza ku display character zilizobaki kuanzia index ulioitaka. Mfano ninataka ku display kutoka character ya 8 hadi mwisho. Kufanya hivi utaandika index ya 8 ikifuatiwa na nukta pacha.

string = 'Jifunze python na Bongoclass'

print(string[8:])

Hii itatupa jibu python na Bongoclass

 

Mfano 6:

Kwa kutumia negative index unaweza pia kufanya hivyo. Ila utambuwe kuwa neg...

Ingia sasa ili uweze kusoma makala hii yote.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Python Main: Masomo File: Download PDF Views 1394

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game     👉2 ai web app     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitabu cha Afya     👉5 Simulizi za Hadithi Audio     👉6 Kitau cha Fiqh    

Post zinazofanana:

Python somo la 22: Package kwenye Python

Hapa utakwenda kujifunz amaana ya package, aina zake na jinsi ya kuandika package.

Soma Zaidi...
Python somo la 25: Sheria za uandishi wa class

Katika somo hili utajifunza maana ya class, sheria za uandishi wake na mifano halisi

Soma Zaidi...
Python somo la 23: Library kwenye python

Hapa utajifunza maana ya library, kazi zake aina zake na jinsi ya ku install lirary

Soma Zaidi...
Python somo la 36: Django framework - Utangulizi

Ni nini maana ya django framework na inafanya kazi gani

Soma Zaidi...
Python somo la 19: Aina za Function

Katika somo hili utakwend akujifunza aina mbalimbali za function ambazo tunaweza kuzitumia kwenye python.

Soma Zaidi...
Python somo la 50: database kwneye django

Katika somo hili utakwenda kujifunza vipi django inaweza kuwasiliana na database, utajifunza kuusu orm na model

Soma Zaidi...