picha

PYTHON - somo la 9: indexing katika strinfg

Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu string indexing. Kama tulivyojifunza kuhusu namba katika somo lililopita, basi hapa tutakwenda kucheza na string.

Indexing:

Unapopewa string yeyote, katika python unaweza ku access yaani kufanyia kazi sehemu tu ya string hiyo na kuacha sehemu nyingine. Huko nyuma tulijifunza kuhusu habari hii ya indexing na nikakueleza kuwa string index inaanzia na 0. Sasa katika somo hili tutainga ndani zaidi katika kuijuwa indexing.

 

Katika somo letu hili tutakwenda kuifanyia kazi string hii Jifunze python na Bongoclass”

 

Mfano 1:

Katika mfano huu tutaona jinsi ya kufanya index kwa character ya mwanzo tu. yaani tunataka ku dislay haerufi ya mwanzo tu ambayo ni j. Kama nilivyokueleza kuwa indexing inaanzia na 0. Kwa hiyo character ya mwanzo itakuwa na index ya 0.

 

string = 'Jifunze python na Bongoclass'

print(string[0])

Hii itatupa jibu j

 

Mfano 2:

Kwa kupitia mfano huo unaweza ku display character yeyote unayotaka kwenye string yetu. Sasa kwa mfano tunataka ku display character ya 12 kwenye string.

string = 'Jifunze python na Bongoclass'

print(string[12])

 

Hii itakupa jibu o

 

Mfano 3:

Saa kwa mfano tunataka kudisplay character ya mwisho to, hapa unaweza kuhesabu ilikujuwa ipo index ya ngapi kisha utatumia mfano uliotangulia. Njia nyingine ni kutumia negative number yaani namba hasi.

 

Index inapokuwa na namba hasi maana yake imeanza kuhesabiwa kutoka mwisho. Sasa ukihesabu kutoka mwisho index haianzi na -0 ila inaanza na -1 kwa kuwa -0 itakuwa ni ile character ya kwanza kwenye index. Hivyo basi kupata character ya mwisho tutaandika hivi

string = 'Jifunze python na Bongoclass'

print(string[-1])

Hii itatupa jibu s

 

 

Mfano 4:

Kwa mfano kama huo ukitaka ku display character ya 4 kutoka mwisho tutatumai -4

string = 'Jifunze python na Bongoclass'

print(string[-4])

Hii itakupa jibu l

 

Mfano 5:

Pia unaweza ku display character zilizobaki kuanzia index ulioitaka. Mfano ninataka ku display kutoka character ya 8 hadi mwisho. Kufanya hivi utaandika index ya 8 ikifuatiwa na nukta pacha.

string = 'Jifunze python na Bongoclass'

print(string[8:])

Hii itatupa jibu python na Bongoclass

 

Mfano 6:

Kwa kutumia negative index unaweza pia kufanya hivyo. Ila utambuwe kuwa neg...

Ingia sasa ili uweze kusoma makala hii yote.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Python Main: Masomo File: Download PDF Views 1418

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio     👉2 Dua za Mitume na Manabii     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 web hosting     👉5 Bongolite - Game zone - Play free game     👉6 Madrasa kiganjani    

Post zinazofanana:

Python seomo la 55: Kutengeneza Simple Admin Dashboard ya CRUD

Katika somo hili tutajifunza jinsi ya kuunda dashboard rahisi ndani ya Django ambayo itaruhusu mtumiaji kuongeza, kusoma, kuhariri na kufuta taarifa za MenuItem bila kutumia Django built-in admin, bali kwa kutumia HTML templates na views tulizotengeneza sisi wenyewe.

Soma Zaidi...
Python somo la 36: Django framework - Utangulizi

Ni nini maana ya django framework na inafanya kazi gani

Soma Zaidi...
Python somo la 44: Data Manipulation katika Django Templates

Katika somo hili utakwend akujifunza jinsi ya kucheza na data kuzibadili kwa namna mbali mbali kwenye template

Soma Zaidi...
Python somo la 24: Nini maana ya Object Oriented Programming

Hapa tunakwenda kujifunza kuhusu OOP ambapo ni miongoni mwa mitindo ya uandishi wa code

Soma Zaidi...
Python somo la 39: Jinsi ya Kuongeza Kurasa Nyingine Katika Django View

Katika somo hili utakwenda kujifunza zaidi kuhusu Jinsi ya Kuongeza Kurasa Nyingine Katika Django View

Soma Zaidi...
Python somo la 30: Data abstraction

Katika somo hili utakwend akujifunz akuhusu nadharia ya data abstraction na kazi zake kwenye OOP

Soma Zaidi...