PYTHON - somo la 9: indexing katika strinfg
Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu string indexing. Kama tulivyojifunza kuhusu namba katika somo lililopita, basi hapa tutakwenda kucheza na string.
Indexing:
Unapopewa string yeyote, katika python unaweza ku access yaani kufanyia kazi sehemu tu ya string hiyo na kuacha sehemu nyingine. Huko nyuma tulijifunza kuhusu habari hii ya indexing na nikakueleza kuwa string index inaanzia na 0. Sasa katika somo hili tutainga ndani zaidi katika kuijuwa indexing.
Katika somo letu hili tutakwenda kuifanyia kazi string hii ‘Jifunze python na Bongoclass”
Mfano 1:
Katika mfano huu tutaona jinsi ya kufanya index kwa character ya mwanzo tu. yaani tunataka ku dislay haerufi ya mwanzo tu ambayo ni j. Kama nilivyokueleza kuwa indexing inaanzia na 0. Kwa hiyo character ya mwanzo itakuwa na index ya 0.
string = 'Jifunze python na Bongoclass'
print(string[0])
Hii itatupa jibu j
Mfano 2:
Kwa kupitia mfano huo unaweza ku display character yeyote unayotaka kwenye string yetu. Sasa kwa mfano tunataka ku display character ya 12 kwenye string.
string = 'Jifunze python na Bongoclass'
print(string[12])
Hii itakupa jibu o
Mfano 3:
Saa kwa mfano tunataka kudisplay character ya mwisho to, hapa unaweza kuhesabu ilikujuwa ipo index ya ngapi kisha utatumia mfano uliotangulia. Njia nyingine ni kutumia negative number yaani namba hasi.
Index inapokuwa na namba hasi maana yake imeanza kuhesabiwa kutoka mwisho. Sasa ukihesabu kutoka mwisho index haianzi na -0 ila inaanza na -1 kwa kuwa -0 itakuwa ni ile character ya kwanza kwenye index. Hivyo basi kupata character ya mwisho tutaandika hivi
string = 'Jifunze python na Bongoclass'
print(string[-1])
Hii itatupa jibu s
Mfano 4:
Kwa mfano kama huo ukitaka ku display character ya 4 kutoka mwisho tutatumai -4
string = 'Jifunze python na Bongoclass'
print(string[-4])
Hii itakupa jibu l
Mfano 5:
Pia unaweza ku display character zilizobaki kuanzia index ulioitaka. Mfano ninataka ku display kutoka character ya 8 hadi mwisho. Kufanya hivi utaandika index ya 8 ikifuatiwa na nukta pacha.
string = 'Jifunze python na Bongoclass'
print(string[8:])
Hii itatupa jibu python na Bongoclass
Mfano 6:
Kwa kutumia negative index unaweza pia kufanya hivyo. Ila utambuwe kuwa neg...
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 web hosting 👉2 Simulizi za Hadithi Audio 👉3 Bongolite - Game zone - Play free game 👉4 Dua za Mitume na Manabii 👉5 kitabu cha Simulizi 👉6 Kitau cha Fiqh
Post zinazofanana:
Python somo la 48: Jinsi ya Kutumia JavaScript kwenye Fomu za Django
Katika somo hili tutakwend akujifunza kuhusi Jinsi ya Kutumia JavaScript kwenye Fomu za Django
Soma Zaidi...Python somo la 33: Jinsi ya kupata taarifa za faili
Katika somo hili utakwend akujifunz anamna ya kuwez akupata taarifa zinazohusu faili
Soma Zaidi...Python somo la 30: Data abstraction
Katika somo hili utakwend akujifunz akuhusu nadharia ya data abstraction na kazi zake kwenye OOP
Soma Zaidi...Python somo la 16: Jinsi ya kutumia break na continue kwenye loop
Katika somo hili tunakwenda kujifunza matumizi ya break na continue kwenye loop
Soma Zaidi...Python somo la 14: Jinsi ya kutumia For loop
Katika somo hili utakwend akujifunza matumizi ya for loop kwneye python
Soma Zaidi...Python somo la 18: Jinsi ya kuandika function
Katika somo hili utakwend akujifunza jinsi ya kuandika function, kuweka parameter na kuitumia function
Soma Zaidi...