Menu



Python somo la 28: inheritance kwenye OOP

Katika somo hili utakwenda kujifunz amaana ya inheritance na sheria za kuiandika inheritance.

Inheritance in Python

Inheritance ni dhana inayoruhusu class moja (child class) kurithi sifa (properties) na tabia (methods) kutoka kwa class nyingine (parent class). Hii hurahisisha matumizi tena ya code na kuwezesha kuongeza vipengele bila kuharibu class asilia. Class inayorithiwa huitwa parent class yaani mzazi na class inayorithi huitwa child class yaani mtoto.

 


 

Vipengele Muhimu vya Inheritance:

  1. Parent Class: Class inayorithisha properties na methods zake.

  2. Child Class: Class inayorithi kutoka kwa parent class. Inaweza kuongeza au kurekebisha functionalities za parent class.

 


 

Aina za Inheritance:

  1. Single Inheritance: Child class inarithi kutoka kwa parent class moja.

  2. Multilevel Inheritance: Child class inarithi kutoka kwa parent class, ambayo nayo inarithi kutoka kwa parent mwingine.

  3. Hierarchical Inheritance: Parent class moja inarithiwa na child classes nyingi.

  4. Multiple Inheritance: Child class inarithi kutoka kwa parent classes zaidi ya moja.

 


 

 

Mfano wa Single Inheritance:

Ili kuweza kurithi kutoka kwenye parent class, tutaweka jins la class inayorithiwa  wwakati kunapotengeneza child class. Mfano kama parent class ni Animal na tukataka kuandika child class tutaandika hivi Dog(Animal)

Mfano:

class Animal:

    def speak(self):

        print("This animal speaks.")

 

class Dog(Animal):

    def bark(self):

        print("Woof! Woof!")

 

# Object creation

dog = Dog()

dog.speak()  # Method kutoka parent class

dog.bark()   # Method ya child class

 

Hapa, Dog ni child class inayorithi method speak() kutoka Animal.

 


 

Mfano wa Multilevel Inheritance:

class Animal:

    def speak(self):

        print("This animal speaks.")

 

class Mammal(Animal):

    def walk(self):

        print("This mammal walks.")

 

class Dog(Mammal):

    def bark(self):

        print("Woof! Woof!")

 

# Object creation

dog = Dog()

dog.speak()  # Method kutoka Animal

dog.walk()   # Method kutoka Mammal

dog.bark()   # Method ya Dog

 

 

 


 

Multiple Inheritance:

class Animal:

    def speak(self):

        print("This animal speaks.")

 

class Pet:

    def is_pet(self):

        print("This is a pet.")

 

class Dog(Animal, Pet):

    def bark(self):

        print("Woof! Woof!")

 

# Object creation

dog = Dog()

dog.speak()  # Method kutoka Animal

dog.is_pet() # Method kutoka Pet

dog.bark()   # Method ya Dog

 

 

 


 

Faida za Inheritance:

  1. Matumizi Tena ya Code: Hakuna haja ya kuandika code sawa mara kwa mara.

  2. Upanuzi wa Tabia: Unaweza kuongeza functionalities mpya kwenye child class bila kuharibu parent class.

  3. Kuonyesha Mahusiano Halisi: Inaonyesha urithi wa kihierarkia (Hierarchical Inheritance) wa tabia za vitu halisi.

 

Matumizi ya "super()" Keyword:

Inatumika kwenye child class kuita methods za parent class, hasa constructor __init__.

Mfano:

 

class Animal:

    def __init__(self, name):

        self.name = name

 

class Dog(Animal):

    def __init__(self, name, breed):

        super().__init__(name)  # Kuita constructor ya parent

        self.breed = breed

 

dog = Dog("Buddy", "Golden Retriever")

print(f"{dog.name} is a {dog.breed}.")

 

 


 

Inheritance hutoa nguvu kubwa ya kuunda code inayoweza kutumiwa tena na inayoweza kupanuliwa kwa urahisi.

 

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea

Ndio     Hapana     Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Python Main: Masomo File: Download PDF Views 134

Share On:

Facebook WhatsApp

Post zinazofanana:

PYTHON - somo la 8: method za namba zinazotumika kwenye python

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu number method yaani function zinazofanya kazi kwenye namba.

Soma Zaidi...
Python somo la 19: Aina za Function

Katika somo hili utakwend akujifunza aina mbalimbali za function ambazo tunaweza kuzitumia kwenye python.

Soma Zaidi...
PYTHON - somo la 1: Jinsi ya ku install python

Katika somo hili utajifunza kuhusu maana ya python na kazi zake. pia jinsi ya kuandaa kifaa chako kwa ajili ya somo.

Soma Zaidi...
Python somo la 24: Nini maana ya Object Oriented Programming

Hapa tunakwenda kujifunza kuhusu OOP ambapo ni miongoni mwa mitindo ya uandishi wa code

Soma Zaidi...
PYTHON - somo la 2: Sheria za uandishi wa pyhton yaani syntax za python

Katika somo hili utakwenda kujifunza syntaxy za python yaani sheria na kanuni za kuandika code za python

Soma Zaidi...
Python somo la 13: Kutumia condition statement - if, else, elif

Katika somo hili tutakwend akuziona aina za condition statement kwneye python na jinsi ya kuzitumia

Soma Zaidi...
Python somo la 26: Sheria za uandishi wa object

Katika somo hili utakwend akujifunza maana ya object, na sheria za kuandika object.

Soma Zaidi...
Python somo la 18: Jinsi ya kuandika function

Katika somo hili utakwend akujifunza jinsi ya kuandika function, kuweka parameter na kuitumia function

Soma Zaidi...
PYTHON - somo la 6: Jinsi ya kujuwa aina ya data iliyotumika

Katika somo hili utajifunza jisni ya kujuwa aina ya data iliyotumika kwenye python

Soma Zaidi...