Katika somo hili utakwenda kujifunz amaana ya inheritance na sheria za kuiandika inheritance.
Inheritance ni dhana inayoruhusu class moja (child class) kurithi sifa (properties) na tabia (methods) kutoka kwa class nyingine (parent class). Hii hurahisisha matumizi tena ya code na kuwezesha kuongeza vipengele bila kuharibu class asilia. Class inayorithiwa huitwa parent class yaani mzazi na class inayorithi huitwa child class yaani mtoto.
Parent Class: Class inayorithisha properties na methods zake.
Child Class: Class inayorithi kutoka kwa parent class. Inaweza kuongeza au kurekebisha functionalities za parent class.
Single Inheritance: Child class inarithi kutoka kwa parent class moja.
Multilevel Inheritance: Child class inarithi kutoka kwa parent class, ambayo nayo inarithi kutoka kwa parent mwingine.
Hierarchical Inheritance: Parent class moja inarithiwa na child classes nyingi.
Multiple Inheritance: Child class inarithi kutoka kwa parent classes zaidi ya moja.
Ili kuweza kurithi kutoka kwenye parent class, tutaweka jins la class inayorithiwa wwakati kunapotengeneza child class. Mfano kama parent class ni Animal na tukataka kuandika child class tutaandika hivi Dog(Animal)
Mfano:
class Animal:
def speak(self):
print("This animal speaks.")
class Dog(Animal):
def bark(self):
print("Woof! Woof!")
# Object creation
dog = Dog()
dog.speak() # Method kutoka parent class
dog.bark() # Method ya child class
Hapa, Dog ni child class inayorithi method speak() kutoka Animal.
class Animal:
def speak(self):
print("This animal speaks.")
class Mammal(Animal):
def walk(self):
print("This mammal walks.")
class Dog(Mammal):
def bark(self):
print("Woof! Woof!")
# Object creation
dog = Dog()
dog.speak() # Method kutoka Animal
dog.walk() # Method kutoka Mammal
dog.bark() # Method ya Dog
class Animal:
def speak(self):
print("This animal speaks.")
class Pet:
def is_pet(self):
print("This is a pet.")
class Dog(Animal, Pet):
def bark(self):
print("Woof! Woof!")
# Object creation
dog = Dog()
dog.speak() # Method kutoka Animal
dog.is_pet() # Method kutoka Pet
dog.bark() # Method ya Dog
Matumizi Tena ya Code: Hakuna haja ya kuandika code sawa mara kwa mara.
Upanuzi wa Tabia: Unaweza kuongeza functionalities mpya kwenye child class bila kuharibu parent class.
Kuonyesha Mahusiano Halisi: Inaonyesha urithi wa kihierarkia (Hierarchical Inheritance) wa tabia za vitu halisi.
Inatumika kwenye child class kuita methods za parent class, hasa constructor __init__.
class Animal:
def __init__(self, name):
self.name = name
class Dog(Animal):
def __init__(self, name, breed):
super().__init__(name) # Kuita constructor ya parent
self.breed = breed
dog = Dog("Buddy", "Golden Retriever")
print(f"{dog.name} is a {dog.breed}.")
Inheritance hutoa nguvu kubwa ya kuunda code inayoweza kutumiwa tena na inayoweza kupanuliwa kwa urahisi.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Umeionaje Makala hii.. ?
Katika somo hili tutajifunza jinsi Django hutumia migrations kuunda na kubadilisha tables kwenye database kulingana na models tunazoandika. Tutapitia maana ya migration, hatua za kuitumia, umuhimu wake, misingi ya makemigrations na migrate, pamoja na mfano halisi kutoka kwenye project yetu ya pybongo (app: menu).
Soma Zaidi...Katika somo hili tutakwend akujifunza jinsi ya kutumia while loop kwneye python
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunza maana ya variable, na sheria za kutengeneza variable kwenye python. Pia utajifunza maneno ambayo hayafai kutumiwa kama variable
Soma Zaidi...Katika somo hili tunakwenda kujifunza aina nyingine za data ambazo hutumika kwenye python.
Soma Zaidi...Katika somo hili tutajifunza jinsi ya kutumia Django ORM kufanya mahesabu mbalimbali kama Sum, Avg, Count, Max, Min, pamoja na kupunguza idadi ya items zinazoonekana kwenye dashboard (LIMIT). Pia tutajifunza namna ya kutengeneza βdifferenceβ kati ya thamani kubwa na ndogo bila kubadilisha functions zozote ulizokwisha ziandika.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza kutengeneza htmk form pamoja na kuituma.
Soma Zaidi...Hapa utakwenda kujifunz amaana ya package, aina zake na jinsi ya kuandika package.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kushughulika na faili, kama ku upload faili kwenye django.
Soma Zaidi...Katika somo hili tutajifunza namna ya kusoma data kutoka kwenye database kupitia Django ORM, jinsi ya kuzipeleka kwenye view, na jinsi ya kuzionyesha kwenye HTML template.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwend akujifunza matumizi ya for loop kwneye python
Soma Zaidi...