Katika somo hili utajifunza maana ya polymorphism na sheria za uandishi wake
Polymorphism ni mojawapo ya nguzo kuu za Object-Oriented Programming (OOP). Neno hili linatoka katika maneno ya Kigiriki "poly" (nyingi) na "morph" (umbo), likimaanisha kuwa kitu kimoja kinaweza kuwa na maumbo mengi. Katika Python, polymorphism inaruhusu methods, functions, au operators kufanya kazi tofauti kulingana na muktadha.
Method Polymorphism:
Hii inaruhusu methods zenye jina moja kutenda kazi tofauti kwenye class mbalimbali.
Operator Polymorphism:
Hii inaruhusu operator moja kama + kufanya kazi tofauti kulingana na aina za data.
Katika Python, class tofauti zinaweza kuwa na methods zenye jina moja lakini tabia tofauti.
class Bird:
def intro(self):
print("There are many types of birds.")
def flight(self):
print("Most birds can fly.")
class Sparrow(Bird):
def flight(self):
print("Sparrows can fly.")
class Ostrich(Bird):
def flight(self):
print("Ostriches cannot fly.")
# Objects
obj_bird = Bird()
obj_sparrow = Sparrow()
obj_ostrich = Ostrich()
obj_bird.intro()
obj_bird.flight()
obj_sparrow.intro()
obj_sparrow.flight()
obj_ostrich.intro()
obj_ostrich.flight()
Hapa, method flight() imebadilika kulingana na object inayoitwa, ingawa jina lake limebaki lilelile.
Operator moja kama + inaweza kutenda kazi tofauti kulingana na data inayoshughulikiwa.
# Integer addition
print(10 + 20) # Output: 30
# String concatenation
print("Hello" + " World") # Output: Hello World
Hii inaonyesha jinsi operator moja inaweza kubadilika kulingana na aina za data.
Unaweza kuwa na function moja inayofanya kazi kwa objects za class tofauti.
def make_sound(animal):
animal.sound()
class Dog:
def sound(self):
print("Woof! Woof!")
class Cat:
def sound(self):
print("Meow!")
# Objects
dog = Dog()
cat = Cat()
make_sound(dog)
make_sound(cat)
Hii inaonyesha jinsi function make_sound() inavyoweza kufanya kazi na objects tofauti (dog na cat) zinazoshiriki method ya jina moja sound().
Kubadilika: Inaruhusu code kuwa rahisi kubadilishwa na kutumiwa tena.
Urahisi: Inapunguza ugumu wa code kwa kuruhusu matumizi ya interface moja kwa objects tofauti.
Mwisho:
Katika somo linalofuata tutakwend akujifunz akuhusu inheritance
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu number method yaani function zinazofanya kazi kwenye namba.
Soma Zaidi...Katika somo hili tutakwend akuziona aina za condition statement kwneye python na jinsi ya kuzitumia
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujfnza kuhusu string method nyinginezo. Katika somo lililopita tulijifunza kuhusu string indexing.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwend akujifunza matumizi ya for loop kwneye python
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunz ajinsi ya kusoma mafaili na mitindo mbalimbali ya kusoma data
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwend akujifunza jinsi ya kuandika function, kuweka parameter na kuitumia function
Soma Zaidi...Katika somo hili tunakwenda kujifunza aina nyingine za data ambazo hutumika kwenye python.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza aina za data ambazo hutumika kwenye python. hapa utajifunza aina kuu 3 za data.
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunza kuhusu maana ya python na kazi zake. pia jinsi ya kuandaa kifaa chako kwa ajili ya somo.
Soma Zaidi...Katika soo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kubaduli aina moja ya data kwena aina nyingine. Kwa mfano unaweza kubadili namba kuwa string ama kubadili string kuwa nanda ama kubadili float kuwa int.
Soma Zaidi...