Katika somo hili utajifunza maana ya class, sheria za uandishi wake na mifano halisi
Class ni mojawapo ya nguzo muhimu za Object-Oriented Programming (OOP). Inarejelea blueprint au prototype inayotumika kuunda objects. Class ni aina ya mantiki ambayo inabeba attributes (tabia au mali) na methods (mbinu au kazi) ambazo zinaweza kufanywa na objects zinazotokana na hiyo class.
Fikiria mfano wa kufuatilia mbwa mbalimbali ambao wanaweza kuwa na attributes kama breed (aina) na age (umri). Ikiwa tutatumia orodha (list), inaweza kuwa vigumu kuunganisha sifa hizi kwa mpangilio mzuri, hasa tunapokuwa na mbwa wengi. Class hutatua tatizo hili kwa kupangilia data kwa njia inayoweza kudhibitiwa.
Classes zinaundwa kwa kutumia neno kuu la Python: class.
Attributes ni aina ya variables zinazohusiana na class.
Attributes zinaweza kufikiwa kupitia dot operator (.), kwa mfano: MyClass.MyAttribute.
Muundo wa class huandikwa kama ifuatavyo:
class ClassName:
# Statements au methods hapa
pass
class Dog:
pass
Attributes ni zile sifa ama properties ambazo class itakuwa nazo. Kwa mfano tukisema mbwa ndio class hivyo mbwa atakuwa na sifa kama umri, aina yake.
Tunatumia __init__() hii ni constructor ambayo inatumika kuweka attributes kwenye class. Hivyo tunaweza kuweka attribute hivi __init__(self, breed, age) baada ya hapo tutakwenda kuweka hizo attribute mfano tutaandika hivi self.breed = breed hapa tumetumia keyword self kuashiria class dog.
class Dog:
def __init__(self, breed, age):
self.breed = breed # Attribute ya aina ya mbwa
self.age = age # Attribute ya umri wa mbwa
Kwa nini tumetumia keyword self
Keyword self hutumika kuelezea class iliyopo yaani current class. Hapo ina maanisha self.age kuwa self inawakilisha class ya dog. Hata hivyo ijapokuwa keyword self ndio hutumika zaidi unaweza kuweka keyword yeyote unayoitwaka kama mbadala wa self.
Jinsi ya kuandika method kwneye class
Method huandikwa sawa na function kwani method ni function ambayo inahusishwa na class. Ndani ya class function haziitwi function bali huitwa method.
Mfano
Tuna class inayoitwa student hii itausu taarifa za mwanafunzi. Taarifa hizo ni attributes ambazo ni jina na umri.
class Student:
def __init__(self, name, age):
self.name = name
self.age = age
Sasa tunataka kuweka method inayoitwa introduce ambayo itahusika na mwanafunzi kujitambulisha jina lake na umri. Katika kutengeneza hiyo method kitu kicha kuzingatia ni kuihusisha na hiyo class. Hapa tutatumia keyword self kama ambavyo imeelezewa huko awali.
Mfano:
class Student:
def __init__(self, name, age):
self.name = name
self.age = age
def introduce(self):
return f"My name is {self.name}, and I am {self.age} years old."
Katika mfano huo class ni student, attributes ni name na age, method ni introduce. Kitu kilichobaki hapo ni kutengeneza object.
Mwisho:
Katika somo linalofuata tutakwenda kujifunza jinsi ya kutengeneza object.
Je! umeipenda hii post?
Ndio Hapana Save post
Rajabu Tarehe 2024-12-02 18:08:22 Topic: Python Main: Masomo File: Download PDF Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 97
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya
👉2 Madrasa kiganjani
👉3 Simulizi za Hadithi Audio
👉4 Kitau cha Fiqh
👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
👉6 kitabu cha Simulizi
Python somo la 30: Data abstraction
Katika somo hili utakwend akujifunz akuhusu nadharia ya data abstraction na kazi zake kwenye OOP Soma Zaidi...
PYTHON - somo la 1: Jinsi ya ku install python
Katika somo hili utajifunza kuhusu maana ya python na kazi zake. pia jinsi ya kuandaa kifaa chako kwa ajili ya somo. Soma Zaidi...
Python somo la 32: Jinsi ya kusoma mafaili
Katika somo hili utakwenda kujifunz ajinsi ya kusoma mafaili na mitindo mbalimbali ya kusoma data Soma Zaidi...
Python somo la 20: Aina za parameter kwenye function
Katika somo hili tutakwend akujifunza kwa urefu zaidi kuhusu parameter ambazo hutumika kwenye functions Soma Zaidi...
PYTHON - somo la 10: string method na zinavyofanya kazi
Katika somo hili utakwenda kujfnza kuhusu string method nyinginezo. Katika somo lililopita tulijifunza kuhusu string indexing. Soma Zaidi...
Python somo la 21: Module katika python
Katika somo hili utakwend akujifunz amaana ya module, kazi zake, aina zake na jinsi ya kuandika modile Soma Zaidi...
PYTHON - somo la 3: Jinsi ya kuandika variable kwenye python
Katika somo hili utajifunza maana ya variable, na sheria za kutengeneza variable kwenye python. Pia utajifunza maneno ambayo hayafai kutumiwa kama variable Soma Zaidi...
Python somo la 13: Kutumia condition statement - if, else, elif
Katika somo hili tutakwend akuziona aina za condition statement kwneye python na jinsi ya kuzitumia Soma Zaidi...
Python somo la 34: Kutumia html kwneye python
Katika somo hili utakwend akujifunz ajinsi ya kutumia html kwneye python Soma Zaidi...
Python somo la 18: Jinsi ya kuandika function
Katika somo hili utakwend akujifunza jinsi ya kuandika function, kuweka parameter na kuitumia function Soma Zaidi...
Python somo la 14: Jinsi ya kutumia For loop
Katika somo hili utakwend akujifunza matumizi ya for loop kwneye python Soma Zaidi...
PYTHON - somo la 2: Sheria za uandishi wa pyhton yaani syntax za python
Katika somo hili utakwenda kujifunza syntaxy za python yaani sheria na kanuni za kuandika code za python Soma Zaidi...