Python somo la 25: Sheria za uandishi wa class

Katika somo hili utajifunza maana ya class, sheria za uandishi wake na mifano halisi

 

Classes in Python

Class ni mojawapo ya nguzo muhimu za Object-Oriented Programming (OOP). Inarejelea blueprint au prototype inayotumika kuunda objects. Class ni aina ya mantiki ambayo inabeba attributes (tabia au mali) na methods (mbinu au kazi) ambazo zinaweza kufanywa na objects zinazotokana na hiyo class.

 

Kwa Nini Tunahitaji Class?

Fikiria mfano wa kufuatilia mbwa mbalimbali ambao wanaweza kuwa na attributes kama breed (aina) na age (umri). Ikiwa tutatumia orodha (list), inaweza kuwa vigumu kuunganisha sifa hizi kwa mpangilio mzuri, hasa tunapokuwa na mbwa wengi. Class hutatua tatizo hili kwa kupangilia data kwa njia inayoweza kudhibitiwa.

 

Pointi Muhimu Kuhusu Class:

 

Muundo wa Class:

Muundo wa class huandikwa kama ifuatavyo:

class ClassName:

    # Statements au methods hapa

    pass

 

Mfano wa Class Tupu:

class Dog:

    pass

Katika Python, pass ni kauli inayotumika kama kishikizo (placeholder) pale ambapo hakuna msimbo (code) unaohitajika kutekelezwa (excuted) kwa wakati huo. Hutumika zaidi katika hali ambapo sintaksia inahitaji kauli fulani, lakini kwa sasa hakuna hatua yoyote inayohitajika katika sehemu hiyo.

 

Kuunda Class Yenye Attribute:

Attributes ni zile sifa ama properties ambazo class itakuwa nazo. Kwa mfano tukisema mbwa ndio class hivyo mbwa atakuwa na sifa kama umri, aina yake.

Tunatumia __init__() hii ni constructor ambayo inatumika kuweka attributes kwenye class. Hivyo tunaweza kuweka attribute hivi __init__(self, breed, age) baada ya hapo tutakwenda kuweka hizo attribute mfano tutaandika hivi self.breed = breed hapa tumetumia keyword self kuashiria class dog.

class Dog:

    def __init__(self, breed, age):

        self.breed = breed  # Attribute ya aina ya mbwa

        self.age = age      # Attribute ya umri wa mbwa

 

Kwa nini tumetumia keyword self

Keyword self hutumika kuelezea class iliyopo yaani current class. Hapo ina maanisha self.age kuwa self inawakilisha class ya dog. Hata hivyo ijapokuwa keyword self ndio hutumika zaidi unaweza kuweka keyword yeyote unayoitwaka kama mbadala wa self.

 

Jinsi ya kuandika method kwneye class

Method huandikwa sawa na function kwani method ni function ambayo inahusishwa na class. Ndani ya class function haziitwi function bali huitwa method. 

Mfano

Tuna class inayoitwa student hii itausu taarifa za mwanafunzi. Taarifa hizo ni attributes ambazo ni jina na umri. 

class Student:

    def __init__(self, name, age):

        self.name = name

        self.age = age

Sasa tunataka kuweka method inayoitwa introduce ambayo itahusika na mwanafunzi kujitambulisha jina lake na umri. Katika kutengeneza hiyo method kitu kicha kuzingatia ni kuihusisha na hiyo class. Hapa tutatumia keyword self kama ambavyo imeelezewa huko awali.

Mfano:

class Student:

    def __init__(self, name, age):

        self.name = name

        self.age = age

 

    def introduce(self):

        return f"My name is {self.name}, and I am {self.age} years old."

Katika mfano huo class ni student, attributes ni name na age, method ni introduce. Kitu kilichobaki hapo ni kutengeneza object. 

 

Mwisho:

Katika somo linalofuata tutakwenda kujifunza jinsi ya kutengeneza object.

 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Python Main: ICT File: Download PDF Views 225

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 Bongolite - Game zone - Play free game    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

Python somo la 16: Jinsi ya kutumia break na continue kwenye loop

Katika somo hili tunakwenda kujifunza matumizi ya break na continue kwenye loop

Soma Zaidi...
Python somo la 21: Module katika python

Katika somo hili utakwend akujifunz amaana ya module, kazi zake, aina zake na jinsi ya kuandika modile

Soma Zaidi...
Python somo la 14: Jinsi ya kutumia For loop

Katika somo hili utakwend akujifunza matumizi ya for loop kwneye python

Soma Zaidi...
PYTHON - somo la 2: Sheria za uandishi wa pyhton yaani syntax za python

Katika somo hili utakwenda kujifunza syntaxy za python yaani sheria na kanuni za kuandika code za python

Soma Zaidi...
Python somo la 19: Aina za Function

Katika somo hili utakwend akujifunza aina mbalimbali za function ambazo tunaweza kuzitumia kwenye python.

Soma Zaidi...
Python somo la 39: Jinsi ya Kuongeza Kurasa Nyingine Katika Django View

Katika somo hili utakwenda kujifunza zaidi kuhusu Jinsi ya Kuongeza Kurasa Nyingine Katika Django View

Soma Zaidi...
Python somo la 47: Jinsi ya kupokea na kuchakata fomu

Katika somo hili utakwend akujifunza jinsi ya kupokea na kuchakata fomu

Soma Zaidi...
Python somo la 35: Jinsi ya kutumia MYSQL kwenye python

Katika somo hili utajifunz akutumia database kwenye python

Soma Zaidi...
Python somo la 15: Jinsi ya kutumia while loop

Katika somo hili tutakwend akujifunza jinsi ya kutumia while loop kwneye python

Soma Zaidi...