Katika somo hili utajifunza maana ya encapsulation na sheria za uandishi wake
Encapsulation ni dhana ya kuficha data ya ndani ya object ili isiweze kufikiwa moja kwa moja kutoka nje ya class.
Hii inamaanisha kuwa property au method iliyo ndani ya class haiwezi kufikiwa au kubadilishwa moja kwa moja kutoka nje.
Kwa kutumia encapsulation, tunaweza kudhibiti jinsi data inavyopatikana au kubadilishwa kupitia mbinu (methods) maalum.
Lengo kuu ni:
Kulinda data dhidi ya mabadiliko yasiyotarajiwa.
Kuweka mipaka ya ufikiaji ili kuboresha usalama wa programu.
Ulinzi wa Data: Inawezesha kudhibiti jinsi property na method za object zinavyofikiwa au kubadilishwa.
Kupunguza Makosa: Inazuia mabadiliko yasiyoidhinishwa kwenye data.
Rahisi Kudhibiti: Programu inakuwa rahisi kuelewa, kudumisha, na kufanya marekebisho bila kuvunja sehemu nyingine.
Usalama: Huzuia ufikiaji wa moja kwa moja wa data muhimu kutoka nje ya class.
Ili kufanikisha encapsulation, tunatumia viwango vya ufikiaji vya property na method kwenye class. Python hutoa viwango vitatu vya msingi:
Property na method zinazoonekana na kufikiwa moja kwa moja kutoka nje ya class.
Kwa kawaida attribute zinakuwa ni public by default.
Mfano:
class Example:
def __init__(self):
self.data = "Public Data" # Public
obj = Example()
print(obj.data) # Inaweza kufikiwa moja kwa moja
Property na method zinazofikiwa ndani ya class husika na class zilizorithi (subclasses). Kuhusu class zinazorithi tutajifunza mbeleni.
Hutangulizwa na alama ya underscore moja _.
class Example:
def __init__(self):
self.data = "Protected Data" # Private attribute
# Kufikia private attribute moja kwa moja nje ya class
obj = Example()
print(obj.data)
Katika mfano huo tumeweza kuprint attribute data bila ya tatizo nje ya class. Huu ni mfano wa public. Lakini sasa hebu tufanye attribute data kuwa protected.
Mfano
class Example:
def __init__(self):
self._data = "Protected Data" # Private attribute
# Kufikia private attribute moja kwa moja nje ya class
obj = Example()
print(obj._data)
Pia kuna namna ambavyo protected inaweza kutumika lakini sio njia inayoshauriwa kutumia yaani haipendezi.
Mfano:class Example:
def __init__(self):
self._data = "Protected Data" # Protected
obj = Example()
print(obj._data) # Inaweza kufikiwa lakini haipendekezwi
Mfano wa kurithi protected
class Parent:
def __init__(self):
self._data = "Protected Data" # Protected attribute
def display_data(self):
print(f"Data from Parent: {self._data}")
class Child(Parent):
def modify_data(self, new_data):
self._data = new_data # Accessing and modifying protected attribute
print(f"Data modified in Child: {self._data}")
# Kutengeneza object ya Child class
child_obj = Child()
# Kufikia na kuonyesha protected attribute kupitia parent method
child_obj.display_data() # Output: Data from Parent: Protected Data
# Kufikia na kubadilisha protected attribute kupitia child method
child_obj.modify_data("New Protected Data") # Output: Data modified in Child: New Protected Data
# Kuhakikisha mabadiliko yanadumu
child_obj.display_data() # Output: Data from Parent: New Protected Data
...
Je! umeipenda hii post?
Rajabu
Tarehe 2024-12-03 17:15:53 Topic: Python
Main: Masomo
File: Download PDF
Share On
Facebook
or
Whatsapp
Imesomwa mara 87
Sponsored links
PYTHON - somo la 4: Aina za data kwenye python
Python somo la 28: inheritance kwenye OOP
PYTHON - somo la 1: Jinsi ya ku install python
Python somo la 15: Jinsi ya kutumia while loop
Python somo la 18: Jinsi ya kuandika function
Python somo la 14: Jinsi ya kutumia For loop
Python somo la 19: Aina za Function
Python somo la 16: Jinsi ya kutumia break na continue kwenye loop
Python somo la 23: Library kwenye python
Python somo la 24: Nini maana ya Object Oriented Programming
Python somo la 13: Kutumia condition statement - if, else, elif
Python somo la 22: Package kwenye Python
Nicheki WhatsApp kwa maswali
Ndio Hapana Save post
👉1 Kitau cha Fiqh
👉2 Simulizi za Hadithi Audio
👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
👉4 Kitabu cha Afya
👉5 kitabu cha Simulizi
👉6 Madrasa kiganjani
Post zifazofanana:-
Katika somo hili utakwenda kujifunza aina za data ambazo hutumika kwenye python. hapa utajifunza aina kuu 3 za data. Soma Zaidi...
Katika somo hili utakwenda kujifunz amaana ya inheritance na sheria za kuiandika inheritance. Soma Zaidi...
Katika somo hili utajifunza kuhusu maana ya python na kazi zake. pia jinsi ya kuandaa kifaa chako kwa ajili ya somo. Soma Zaidi...
Katika somo hili tutakwend akujifunza jinsi ya kutumia while loop kwneye python Soma Zaidi...
Katika somo hili utakwend akujifunza jinsi ya kuandika function, kuweka parameter na kuitumia function Soma Zaidi...
Katika somo hili utakwend akujifunza matumizi ya for loop kwneye python Soma Zaidi...
Katika somo hili utakwend akujifunza aina mbalimbali za function ambazo tunaweza kuzitumia kwenye python. Soma Zaidi...
Katika somo hili tunakwenda kujifunza matumizi ya break na continue kwenye loop Soma Zaidi...
Hapa utajifunza maana ya library, kazi zake aina zake na jinsi ya ku install lirary Soma Zaidi...
Hapa tunakwenda kujifunza kuhusu OOP ambapo ni miongoni mwa mitindo ya uandishi wa code Soma Zaidi...
Katika somo hili tutakwend akuziona aina za condition statement kwneye python na jinsi ya kuzitumia Soma Zaidi...
Hapa utakwenda kujifunz amaana ya package, aina zake na jinsi ya kuandika package. Soma Zaidi...