Katika somo hili utajifunza maana ya encapsulation na sheria za uandishi wake
Encapsulation ni dhana ya kuficha data ya ndani ya object ili isiweze kufikiwa moja kwa moja kutoka nje ya class.
Hii inamaanisha kuwa property au method iliyo ndani ya class haiwezi kufikiwa au kubadilishwa moja kwa moja kutoka nje.
Kwa kutumia encapsulation, tunaweza kudhibiti jinsi data inavyopatikana au kubadilishwa kupitia mbinu (methods) maalum.
Lengo kuu ni:
Kulinda data dhidi ya mabadiliko yasiyotarajiwa.
Kuweka mipaka ya ufikiaji ili kuboresha usalama wa programu.
Ulinzi wa Data: Inawezesha kudhibiti jinsi property na method za object zinavyofikiwa au kubadilishwa.
Kupunguza Makosa: Inazuia mabadiliko yasiyoidhinishwa kwenye data.
Rahisi Kudhibiti: Programu inakuwa rahisi kuelewa, kudumisha, na kufanya marekebisho bila kuvunja sehemu nyingine.
Usalama: Huzuia ufikiaji wa moja kwa moja wa data muhimu kutoka nje ya class.
Ili kufanikisha encapsulation, tunatumia viwango vya ufikiaji vya property na method kwenye class. Python hutoa viwango vitatu vya msingi:
Property na method zinazoonekana na kufikiwa moja kwa moja kutoka nje ya class.
Kwa kawaida attribute zinakuwa ni public by default.
Mfano:
class Example:
def __init__(self):
self.data = "Public Data" # Public
obj = Example()
print(obj.data) # Inaweza kufikiwa moja kwa moja
Property na method zinazofikiwa ndani ya class husika na class zilizorithi (subclasses). Kuhusu class zinazorithi tutajifunza mbeleni.
Hutangulizwa na alama ya underscore moja _.
class Example:
def __init__(self):
self.data = "Protected Data" # Private attribute
# Kufikia private attribute moja kwa moja nje ya class
obj = Example()
print(obj.data)
Katika mfano huo tumeweza kuprint attribute data bila ya tatizo nje ya class. Huu ni mfano wa public. Lakini sasa hebu tufanye attribute data kuwa protected.
Mfano
class Example:
def __init__(self):
self._data = "Protected Data" # Private attribute
# Kufikia private attribute moja kwa moja nje ya class
obj = Example()
print(obj._data)
Pia kuna namna ambavyo protected inaweza kutumika lakini sio njia inayoshauriwa kutumia yaani haipendezi.
Mfano:class Example:
def __init__(self):
self._data = "Protected Data" # Protected
obj = Example()
print(obj._data) # Inaweza kufikiwa lakini haipendekezwi
Mfano wa kurithi protected
class Parent:
def __init__(self):
self._data = "Protected Data" # Protected attribute
def display_data(self):
print(f"Data from Parent: {self._data}")
class Child(Parent):
def modify_data(self, new_data):
self._data = new_data # Accessing and modifying protected attribute
print(f"Data modified in Child: {self._data}")
# Kutengeneza object ya Child class
child_obj = Child()
# Kufikia na kuonyesha protected attribute kupitia parent method
child_obj.display_data() # Output: Data from Parent: Protected Data
# Kufikia na kubadilisha protected attribute kupitia child method
child_obj.modify_data("New Protected Data") # Output: Data modified in Child: New Protected Data
# Kuhakikisha mabadiliko yanadumu
child_obj.display_data() # Output: Data from Parent: New Protected Data">
...
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Katika somo hili utakwenda kujfnza kuhusu string method nyinginezo. Katika somo lililopita tulijifunza kuhusu string indexing.
Soma Zaidi...Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu string indexing. Kama tulivyojifunza kuhusu namba katika somo lililopita, basi hapa tutakwenda kucheza na string.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu number method yaani function zinazofanya kazi kwenye namba.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunz ajinsi ya kusoma mafaili na mitindo mbalimbali ya kusoma data
Soma Zaidi...Ni nini maana ya django framework na inafanya kazi gani
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwend akujifunza aina mbalimbali za function ambazo tunaweza kuzitumia kwenye python.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwend akujifunza matumizi ya for loop kwneye python
Soma Zaidi...Katika somo hili tutakwend akujifunza kwa urefu zaidi kuhusu parameter ambazo hutumika kwenye functions
Soma Zaidi...Katika somo hili uatajifunza jinsi gani unaweza kutumia view kma logic kuuma data kwenye template
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunz akutumia database kwenye python
Soma Zaidi...