Python somo la 20: Aina za parameter kwenye function

Katika somo hili tutakwend akujifunza kwa urefu zaidi kuhusu parameter ambazo hutumika kwenye functions

Aina za Parameter Kwenye Function - Python

Katika somo hili, tutajadili aina za parameter zinazotumika kwenye Python function. Pia, tutaangazia jinsi ya kutumia parameter hizi kwa mpangilio sahihi na kufanya kazi na argument.

 


 

Utaratibu wa Parameter

Mfano:

 

def intro(umri: int, jinsia: str):

    print(f"Umri wako ni miaka {umri} na jinsia yako ni {jinsia}.")



def details():

    # Omba maelezo kutoka kwa mtumiaji

    umri = int(input("Andika umri wako: "))

    jinsia = input("Andika jinsia yako: ")

 

    # Piga intro() kwa kutumia maelezo yaliyotolewa

    intro(umri, jinsia)



# Simamia utekelezaji wa details()

details()



 

Ikiwa utachanganya mpangilio au aina ya data, Python itaripoti kosa.

 


 

Default Parameters

Mfano:

 

def salamu(umri: int, jinsia: str, makazi: str = "Tanzania"):

    print(f"Umri wako ni miaka {umri}, jinsia yako ni {jinsia}, unaishi {makazi}.")

 

# Programu inaanza moja kwa moja hapa

umri = int(input("Andika umri wako: "))

jinsia = input("Andika jinsia yako: ")

salamu(umri, jinsia)



 

Hapa, kama mtumiaji hatajaza sehemu ya makazi, itatumia thamani ya default Tanzania.

 


 

Optional Parameters

Mfano:

def salamu(umri: int, jinsia: str, mkoa: str = None):

    if mkoa:

        print(f"Umri wako ni miaka {umri}, jinsia yako ni {jinsia}, unaishi {mkoa}.")

    else:

        print(f"Umri wako ni miaka {umri}, jinsia yako ni {jinsia}.")

 

# Kuomba maingizo ya mtumiaji moja kwa moja

umri = int(input("Andika umri wako: "))

jinsia = input("Andika jinsia yako: ")

mkoa = input("Andika Mkoa unaoishi (acha wazi kama hakuna): ")

 

# Kuita function moja kwa moja

salamu(umri, jinsia, mkoa if mkoa else None)



 


 

Required Parameters

Mfano:

def salamu(umri: int, jinsia: str):

    print(f"Umri wako ni miaka {umri} na jinsia yako ni {jinsia}.")

salamu(7,)

 

Hapo lazima upate error kwa sababu hujaweka parameter ya pili.

 

Hii inahitaji argument zote mbili (umri na jinsia) ili kufanikisha utekelezaji.

 


 

Function Kama Parameter

Mfano:

def ongeza(a: int, b: int) -> int:

    return a + b

 

def toa(a: int, b: int) -> int:

    return a - b

 

def operesheni(func, x: int, y: int):

    return func(x, y)

 

# Kutumia function `ongeza` na `toa` kama parameter

result1 = operesheni(ongeza, 10, 5)

print(f"Matokeo ya ongeza: {result1}")  # Output: 15

 

result2 = operesheni(toa, 10, 5)

print(f"Matokeo ya toa: {result2}")  # Output: 5

 



Matumizi ya alama ( -> int: ).

Katika Python, sehemu -> int inajulikana kama type hint au type annotation. Inatumika kuonyesha aina ya thamani ambayo function inatarajiwa kurudisha (return type). Hii haibadilishi jinsi Python inavyotekeleza function, bali inatoa mwongozo kwa wasomaji wa msimbo au zana za uchambuzi wa msimbo kama linters au IDEs.

Mfano Rahisi:

 

def ongeza(a: int, b: int) -> int:

    return a + b

 


 

Function Kama Variable

Mfano:

def salamu():

    return "Habari! Karibu katika Python."

 

# Kutumia function kama variable

ujumbe = salamu

 

# Kuitumia variable kuendesha function

print(ujumbe())  # Hii itachapisha: Habari! Karibu katika Python.



 

 


 

Callback Functions

 

Mfano:

# Function ya callback

def salamu():

    print("Habari kutoka salamu!")

 

# Function inayopokea callback

def tumia_callback(callback):

    print("Niko kwenye function kuu.")

    callback()  # Inatekeleza function ya callback

 

# Kuitumia

tumia_callback(salamu)

 

 

Maelezo ya Mfano:

  1. salamu() ni function ambayo tunatumia kama callback.

  2. tumia_callback(callback) ni function inayopokea function nyingine kama argument (callback).

  3. Ndani ya tumia_callback, function ya callback inaitwa kwa kutumia jina lake (callback()).

 

 


 

Mwisho

Katika somo hili, tumeona aina mbalimbali za parameter, jinsi ya kuzitumia, na umuhimu wake kwenye Python function. Katika somo lijalo, tutajadili methods zinazofanya kazi mbalimbali kwenye data.

 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Python Main: ICT File: Download PDF Views 395

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉3 Dua za Mitume na Manabii    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

Python somo la 32: Jinsi ya kusoma mafaili

Katika somo hili utakwenda kujifunz ajinsi ya kusoma mafaili na mitindo mbalimbali ya kusoma data

Soma Zaidi...
PYHON - somo la 5: Aina za data list, turple, dictionary na boolean

Katika somo hili tunakwenda kujifunza aina nyingine za data ambazo hutumika kwenye python.

Soma Zaidi...
Python somo la 40: Jinsi ya Kuunda Simple Navigation Menu Katika Django

Katika somo hili utajifunza Jinsi ya Kuunda Simple Navigation Menu Katika Django kwa kutumia template

Soma Zaidi...
Python somo la 48: Jinsi ya Kutumia JavaScript kwenye Fomu za Django

Katika somo hili tutakwend akujifunza kuhusi Jinsi ya Kutumia JavaScript kwenye Fomu za Django

Soma Zaidi...
Python somo la 49: Jinsi ya ku host project ya Django

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya ku host website ya Django. Hapa tutakwenda kutuma plaform ya pythonanywhere.com.

Soma Zaidi...
Python somo la 27: polymorphism kwneye python

Katika somo hili utajifunza maana ya polymorphism na sheria za uandishi wake

Soma Zaidi...
PYTHON - somo la 8: method za namba zinazotumika kwenye python

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu number method yaani function zinazofanya kazi kwenye namba.

Soma Zaidi...
PYTHON somo la 12: assignment operator, logical operator, identity oeprator na membership operator

Katika somo hili utakwenda kujfunza operator nyingine kama assignment operator logical, identity operator na membership operator.

Soma Zaidi...
Python somo la 17: Jinsi ya kutumia user input

Katika somo hili uatkwenda kujifunz anamna ambavyo mtu anaweza kuingiza input kwneye system

Soma Zaidi...
Python somo la 36: Django framework - Utangulizi

Ni nini maana ya django framework na inafanya kazi gani

Soma Zaidi...