picha

Python somo la 20: Aina za parameter kwenye function

Katika somo hili tutakwend akujifunza kwa urefu zaidi kuhusu parameter ambazo hutumika kwenye functions

Aina za Parameter Kwenye Function - Python

Katika somo hili, tutajadili aina za parameter zinazotumika kwenye Python function. Pia, tutaangazia jinsi ya kutumia parameter hizi kwa mpangilio sahihi na kufanya kazi na argument.

 


 

Utaratibu wa Parameter

Mfano:

 

def intro(umri: int, jinsia: str):

    print(f"Umri wako ni miaka {umri} na jinsia yako ni {jinsia}.")



def details():

    # Omba maelezo kutoka kwa mtumiaji

    umri = int(input("Andika umri wako: "))

    jinsia = input("Andika jinsia yako: ")

 

    # Piga intro() kwa kutumia maelezo yaliyotolewa

    intro(umri, jinsia)



# Simamia utekelezaji wa details()

details()



 

Ikiwa utachanganya mpangilio au aina ya data, Python itaripoti kosa.

 


 

Default Parameters

Mfano:

 

def salamu(umri: int, jinsia: str, makazi: str = "Tanzania"):

    print(f"Umri wako ni miaka {umri}, jinsia yako ni {jinsia}, unaishi {makazi}.")

 

# Programu inaanza moja kwa moja hapa

umri = int(input("Andika umri wako: "))

jinsia = input("Andika jinsia yako: ")

salamu(umri, jinsia)



 

Hapa, kama mtumiaji hatajaza sehemu ya makazi, itatumia thamani ya default Tanzania.

 


 

Optional Parameters

Mfano:

def salamu(umri: int, jinsia: str, mkoa: str = None):

    if mkoa:

        print(f"Umri wako ni miaka {umri}, jinsia yako ni {jinsia}, unaishi {mkoa}.")

    else:

        print(f"Umri wako ni miaka {umri}, jinsia yako ni {jinsia}.")

 

# Kuomba maingizo ya mtumiaji moja kwa moja

umri = int(input("Andika umri wako: "))

jinsia = input("Andika jinsia yako: ")

mkoa = input("Andika Mkoa unaoishi (acha wazi kama hakuna): ")

 

# Kuita function moja kwa moja

salamu(umri, jinsia, mkoa if mkoa else None)



 


 

Required Parameters

Mfano:

def salamu(umri: int, jinsia: str):

    print(f"Umri wako ni miaka {umri} na jinsia yako ni {jinsia}.")

salamu(7,)

 

Hapo lazima upate error kwa sababu hujaweka parameter ya pili.

 

Hii inahitaji argument zote mbili (umri na jinsia) ili kufanikisha utekelezaji.

 


 

Function Kama Parameter

Mfano:

def ongeza(a: int, b: int) -> int:

    return a + b

 

def toa(a: int, b: int) -> int:

    return a - b

 

def operesheni(func, x: int, y: int):

    return func(x, y)

 

# Kutumia function `ongeza` na `toa` kama parameter

result1 = operesheni(ongeza, 10, 5)

print(f"Matokeo ya ongeza: {result1}")  # Output: 15

 

result2 = operesheni(toa, 10, 5)

print(f"Matokeo ya toa: {result2}")  # Output: 5

 



Matumizi ya alama ( -> int: ).

Katika Python, sehemu -> int inajulikana kama type hint au type annotation. Inatumika kuonyesha aina ya thamani ambayo function inatarajiwa kurudisha (return type). Hii haibadilishi jinsi Python inavyotekeleza function, bali inatoa mwongozo kwa wasomaji wa msimbo au zana za uchambuzi wa msimbo kama linters au IDEs.

Mfano Rahisi:

 

def ongeza(a: int, b: int) -> int:

    return a + b

 


 

Function Kama Variable

Mfano:

def salamu():

    return "Habari! Karibu katika Python."

 

# Kutumia function kama variable

ujumbe = salamu

 

# Kuitumia variable kuendesha function

print(ujumbe())  # Hii itachapisha: Habari! Karibu katika Python.



 

 


 

Callback Functions

 

Mfano:

# Function ya callback

def salamu():

    print("Habari kutoka salamu!")

 

# Function inayopokea callback

def tumia_callback(callback):

    print("Niko kwenye function kuu.")

    callback()  # Inatekeleza function ya callback

 

# Kuitumia

tumia_callback(salamu)

 

 

Maelezo ya Mfano:

  1. salamu() ni function ambayo tunatumia kama callback.

  2. tumia_callback(callback) ni function inayopokea function nyingine kama argument (callback).

  3. Ndani ya tumia_callback, function ya callback inaitwa kwa kutumia jina lake (callback()).

 

 


 

Mwisho

Katika somo hili, tumeona aina mbalimbali za parameter, jinsi ya kuzitumia, na umuhimu wake kwenye Python function. Katika somo lijalo, tutajadili methods zinazofanya kazi mbalimbali kwenye data.

 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-11-26 Topic: Python Main: ICT File: Download PDF Views 642

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉2 web hosting    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 Bongolite - Game zone - Play free game    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Dua za Mitume na Manabii   

Post zinazofanana:

Python somo 57: Matumizi ya Python shell

Katika somo hili, tutajifunza: Maana ya Python shell na umuhimu wake. Tofauti kati ya shell na terminal ya kawaida. Matumizi ya shell, hususan kwenye Django. Amri muhimu zaidi za Python shell, zilizotokana na models na views zako za pybongo.

Soma Zaidi...
Python somo la 26: Sheria za uandishi wa object

Katika somo hili utakwend akujifunza maana ya object, na sheria za kuandika object.

Soma Zaidi...
Python somo la 30: Data abstraction

Katika somo hili utakwend akujifunz akuhusu nadharia ya data abstraction na kazi zake kwenye OOP

Soma Zaidi...
PYTHON - somo la 1: Jinsi ya ku install python

Katika somo hili utajifunza kuhusu maana ya python na kazi zake. pia jinsi ya kuandaa kifaa chako kwa ajili ya somo.

Soma Zaidi...
Python somo la 50: database kwneye django

Katika somo hili utakwenda kujifunza vipi django inaweza kuwasiliana na database, utajifunza kuusu orm na model

Soma Zaidi...
Python somo la 17: Jinsi ya kutumia user input

Katika somo hili uatkwenda kujifunz anamna ambavyo mtu anaweza kuingiza input kwneye system

Soma Zaidi...
Python somo la 61: Jinsi ya kutuma email kwenye django

Katika maeneo ya development, tunahitaji kutuma email mara nyingi kwa madhumuni ya: Kujaribu mfumo wa OTP Password reset System notifications Activation codes Lakini mara nyingi hatutaki emails ziondoke kwenda kwa watu halisi wakati bado tupo kwenye majaribio.

Soma Zaidi...
Python somo la 53: Kutengeneza HTML Form na Django View kwa ajili ya kuingiza data

Katika somo hili tutaangalia jinsi ya kutengeneza fomu ya HTML kwa ajili ya kuingiza data kwenye jedwali la MenuItem, pamoja na kutengeneza view itakayopokea data hiyo na kuihifadhi kwenye database. Pia tutaunganisha form na URL route.

Soma Zaidi...
Python somo la 44: Data Manipulation katika Django Templates

Katika somo hili utakwend akujifunza jinsi ya kucheza na data kuzibadili kwa namna mbali mbali kwenye template

Soma Zaidi...
Python somo la 45: Kutumia Loops na Conditions katika Django Templates

Katika somo hili utakwend akujifunza kuchakata data kwa Kutumia Loops na Conditions katika Django Templates

Soma Zaidi...