Katika somo hili utakwenda kujifunza zaidi kuhusu Jinsi ya Kuongeza Kurasa Nyingine Katika Django View
Baada ya kusanidi landing page katika Django kama tulivyojifunza kwenye somo lililopita, hatua inayofuata ni kuongeza kurasa nyingine kwenye mfumo wa tovuti, kama vile kurasa za nyumbani (home), wasiliana nasi (contact), blogu, na nyinginezo. Django hurahisisha sana zoezi hili kupitia mfumo wa views na URL patterns.
Katika somo hili, tutapanua app ya menu ndani ya mradi wa PyBongo kwa kuongeza views mpya kadhaa, kila moja ikiwa na maudhui yake, na tutaunganisha kila view na URL yake husika ili mtumiaji aweze kuifikia kwa urahisi kupitia kivinjari.
Hakikisha una yafuatayo tayari:
Django tayari imewekwa kwenye mazingira yako.
Mradi unaoitwa PyBongo uko tayari.
Ndani ya mradi, kuna app iitwayo menu.
Fungua faili menu/views.py kisha ongeza au hakikisha maudhui yafuatayo yapo:
from django.http import HttpResponse
def index(request):
return HttpResponse("<h1>Welcome Bongoclass.<h1>")
def home(request):
return HttpResponse("<p>This is the home page</p>")
def contact(request):
return HttpResponse("Phone number <b style='color:blue'>07653344</b>.")
def blog(request):
return HttpResponse("<u>bongoclass.com</u>")
Kila function hapo juu ni view ya Django inayoshughulikia aina fulani ya ukurasa. Zote zinatumia
HttpResponsekuwasilisha maudhui ya moja kwa moja kwa kivinjari.
Fungua au hariri faili menu/urls.py na hakikisha kila view imepewa URL yake kama ifuatavyo:
from django.urls import path
from . import views
urlpatterns = [
path('', views.index, name='index'),
path('home/', views.home, name='home'),
path('contact/', views.contact, name='contact'),
path('blog/', views.blog, name='blog'),
]
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Umeionaje Makala hii.. ?
Katika somo hili tutajifunza jinsi Django hutumia migrations kuunda na kubadilisha tables kwenye database kulingana na models tunazoandika. Tutapitia maana ya migration, hatua za kuitumia, umuhimu wake, misingi ya makemigrations na migrate, pamoja na mfano halisi kutoka kwenye project yetu ya pybongo (app: menu).
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwend akujifunza maana ya object, na sheria za kuandika object.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwend akujifunz akuhusu nadharia ya data abstraction na kazi zake kwenye OOP
Soma Zaidi...Katika somo hili tunakwenda kujifunza matumizi ya break na continue kwenye loop
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza kutengeneza htmk form pamoja na kuituma.
Soma Zaidi...Katika somo hili uatajifunza jinsi gani unaweza kutumia view kma logic kuuma data kwenye template
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunza maana ya encapsulation na sheria za uandishi wake
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwend akujifunza jinsi ya kuandika function, kuweka parameter na kuitumia function
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza syntaxy za python yaani sheria na kanuni za kuandika code za python
Soma Zaidi...Katika somo hili tutaangalia jinsi ya kutengeneza fomu ya HTML kwa ajili ya kuingiza data kwenye jedwali la MenuItem, pamoja na kutengeneza view itakayopokea data hiyo na kuihifadhi kwenye database. Pia tutaunganisha form na URL route.
Soma Zaidi...