Katika somo hili utakwend akujifunza jinsi ya kuandika function, kuweka parameter na kuitumia function
Katika somo hili, tutajifunza maana ya function, jinsi ya kuandika function, na jinsi ya kuweka parameters kwenye function katika Python.
Function ni block ya code inayofanya kazi maalumu. Inasaidia kupunguza marudio ya code kwa kuruhusu matumizi yake mara nyingi bila kuiandika tena.
Mambo ya Kuzingatia kuhusu Functions:
Function hutumika zaidi ya mara moja.
Function haifanyi kazi mpaka iitwe (invoked).
Function inaweza kupokea parameters ili kubadilisha tabia yake kulingana na mahitaji.
Katika Python, function huandikwa kwa kutumia def ikifuatiwa na jina la function, mabano ya mviringo (), yakifuatiwa na alama ya ( : ) yaani nukta pacha bouble colon kisha ndipo body ya function inafuata.
Mfano wa Msingi:
# Function rahisi inayochapisha ujumbe
def bongo():
print("Bongoclass")
# Kuitwa kwa function
bongo()
Function inaweza kuitwa mara nyingi kwa kutumia for loop.
Mfano:
# Function inayochapisha "Bongoclass"
def bongo():
print("Bongoclass")
# Kuitumia mara 10
for i in range(10):
bongo()
Parameters ni viingilio vinavyotumwa kwa function wakati wa kuitwa, na vinaweza kubadilisha tabia ya function.
Mfano:
# Function inayochapisha ujumbe mara kadhaa
def bongo(idadi):
for i in range(idadi):
print("Bongoclass")
# Kuitumia function
idadi = int(input("Andika idadi ya mara za kuchapisha: "))
bongo(idadi)
Parameter na argument
Katika mfano hapo juu parameter ni idadi na argument ni hiyo namba utakayoweka. ina maana argument ni value ya hiyo parameter. mfano hapo nikiweka 6, ina maana parameter na idadi na argument ni 6. Nimeliweka wazi hili kwa sababu programmer wengi wanaoanza kujifunza wanapata tabu sana kutofautisha kati ya argument na parameter.
Unaweza kutumia parameters zaidi ya moja kwa kuzitenganisha kwa koma.
Mfano: Kujumlisha Namba Mbili:
# Function inayojumlisha namba mbili
def jumlisha(x, y):
print(f"Jumla ya {x} na {y} ni: {x + y}")
# Kuitumia function
jumlisha(5, 7)
Hii ni programu inayotumia parameters tatu: namba ya kwanza, operator ya hesabu, na namba ya pili.
Kwa kutumia if statement:
# Function ya calculator
def calculator(x, y, z):
if y == "+":
return x + z
elif y == "-":
return x - z
elif y == "*":
return x * z
elif y == "/":
return x / z
else:
return "Invalid operator"
# Kuitumia function
x = int(input("Namba ya kwanza: "))
y = input("Weka operator ya hesabu (+, -, *, /): ")
z = int(input("Namba ya pili: "))
print(f"Matokeo: {calculator(x, y, z)}")
Kwa kutumia match statement (Python 3.10+):
# Function ya calculator
def calculator(x, y, z):
match y:
case "+":
return x + z
case "-":
return x - z
case "*":
return x * z
case "/":
return x / z
case _:
return "Invalid operator"
# Kuitumia function
x = int(input("Namba ya kwanza: "))
y = input("Weka operator ya hesabu (+, -, *, /): ")
z = int(input("Namba ya pili: "))
print(f"Matokeo: {calculator(x, y, z)}")
Function inaweza kurudisha thamani badala ya kuchapisha moja kwa moja.
Mfano:
# Function inayojumlisha namba mbili
def jumlisha(x, y):
return x + y
# Kuitumia function
result = jumlisha(5, 7)
print(f"Jumla: {result}")
Hii ni calculator inayorudisha thamani badala ya kuichapisha.
def calculator(x, y, z):
if y == "+":
return x + z
elif y == "-":
return x - z
elif y == "*":
return x * z
elif y == "/":
return x / z
else:
return "Invalid operator"
x = int(input("Namba ya kwanza: "))
y = input("Weka operator ya hesabu (+, -, *, /): ")
z = int(input("Namba ya pili: "))
result = calculator(x, y, z)
print(f"Matokeo: {result}")
Katika somo hili, tumejifunza:
Maana ya function.
Jinsi ya kuandika function.
Jinsi ya kutumia parameters na kurudisha thamani.
Somo linalofuata litaelezea aina za functions na mbinu za juu za kuzitumia kwa ufanisi zaidi.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
Katika somo hili tutakwend akujifunza jinsi ya kutumia while loop kwneye python
Soma Zaidi...Katika somo hili tutakwend akujifunza kwa urefu zaidi kuhusu parameter ambazo hutumika kwenye functions
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kushughulika na faili, kama ku upload faili kwenye django.
Soma Zaidi...Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu string indexing. Kama tulivyojifunza kuhusu namba katika somo lililopita, basi hapa tutakwenda kucheza na string.
Soma Zaidi...Katika somo hili tutakwend akuziona aina za condition statement kwneye python na jinsi ya kuzitumia
Soma Zaidi...Katika somo hili uatajifunza jinsi gani unaweza kutumia view kma logic kuuma data kwenye template
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunza jisni ya kujuwa aina ya data iliyotumika kwenye python
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunza maana ya encapsulation na sheria za uandishi wake
Soma Zaidi...Katika somo hili, tutajifunza: Maana ya Python shell na umuhimu wake. Tofauti kati ya shell na terminal ya kawaida. Matumizi ya shell, hususan kwenye Django. Amri muhimu zaidi za Python shell, zilizotokana na models na views zako za pybongo.
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunza maana ya variable, na sheria za kutengeneza variable kwenye python. Pia utajifunza maneno ambayo hayafai kutumiwa kama variable
Soma Zaidi...