Python somo la 18: Jinsi ya kuandika function
Katika somo hili utakwend akujifunza jinsi ya kuandika function, kuweka parameter na kuitumia function
Jinsi ya Kuandika Function na Kuweka Parameter: Python Version
Katika somo hili, tutajifunza maana ya function, jinsi ya kuandika function, na jinsi ya kuweka parameters kwenye function katika Python.
Function ni Nini?
Function ni block ya code inayofanya kazi maalumu. Inasaidia kupunguza marudio ya code kwa kuruhusu matumizi yake mara nyingi bila kuiandika tena.
Mambo ya Kuzingatia kuhusu Functions:
-
Function hutumika zaidi ya mara moja.
-
Function haifanyi kazi mpaka iitwe (invoked).
-
Function inaweza kupokea parameters ili kubadilisha tabia yake kulingana na mahitaji.
Jinsi ya Kuandika Function
Katika Python, function huandikwa kwa kutumia def ikifuatiwa na jina la function, mabano ya mviringo (), yakifuatiwa na alama ya ( : ) yaani nukta pacha bouble colon kisha ndipo body ya function inafuata.
Mfano wa Msingi:
# Function rahisi inayochapisha ujumbe
def bongo():
print("Bongoclass")
# Kuitwa kwa function
bongo()
Function Inayorudiwa Mara Nyingi
Function inaweza kuitwa mara nyingi kwa kutumia for loop.
Mfano:
# Function inayochapisha "Bongoclass"
def bongo():
print("Bongoclass")
# Kuitumia mara 10
for i in range(10):
bongo()
Jinsi ya Kuweka Parameter kwenye Function
Parameters ni viingilio vinavyotumwa kwa function wakati wa kuitwa, na vinaweza kubadilisha tabia ya function.
Mfano:
# Function inayochapisha ujumbe mara kadhaa
def bongo(idadi):
for i in range(idadi):
print("Bongoclass")
# Kuitumia function
idadi = int(input("Andika idadi ya mara za kuchapisha: "))
bongo(idadi)
Parameter na argument
Katika mfano hapo juu parameter ni idadi na argument ni hiyo namba utakayoweka. ina maana argument ni value ya hiyo parameter. mfano hapo nikiweka 6, ina maana parameter na idadi na argument ni 6. Nimeliweka wazi hili kwa sababu programmer wengi wanaoanza kujifunza wanapata tabu sana kutofautisha kati ya argument na parameter.
Function Zenye Parameters Nyingi
Unaweza kutumia parameters zaidi ya moja kwa kuzitenganisha kwa koma.
Mfano: Kujumlisha Namba Mbili:
# Function inayojumlisha namba mbili
def jumlisha(x, y):
print(f"Jumla ya {x} na {y} ni: {x + y}")
# Kuitumia function
jumlisha(5, 7)
Programu ya Calculator Rahisi
Hii ni programu inayotumia parameters tatu: namba ya kwanza, operator ya hesabu, na namba ya pili.
Kwa kutumia if statement:
# Function ya calculator
def calculator(x, y, z):
if y == "+":
return x + z
elif y == "-":
return x - z
elif y == "*":
return x * z
elif y == "/":
return x / z
else:
return "Invalid operator"
# Kuitumia function
x = int(input("Namba ya kwanza: "))
y = input("Weka operator ya hesabu (+, -, *, /): ")
z = int(input("Namba ya pili: "))
print(f"Matokeo: {calculator(x, y, z)}")
Kwa kutumia match statement (Python 3.10+):
# Function ya calculator
def calculator(x, y, z):
match y:
case "+":
return x + z
case "-":
return x - z
case "*":
return x * z
case "/":
return x / z
case _:
return "Invalid operator"
# Kuitumia function
x = int(input("Namba ya kwanza: "))
y = input("Weka operator ya hesabu (+, -, *, /): ")
z = int(input("Namba ya pili: "))
print(f"Matokeo: {calculator(x, y, z)}")
Function Zinazorudisha Thamani (Return Value)
Function inaweza kurudisha thamani badala ya kuchapisha moja kwa moja.
Mfano:
# Function inayojumlisha namba mbili
def jumlisha(x, y):
return x + y
# Kuitumia function
result = jumlisha(5, 7)
print(f"Jumla: {result}")
Mfano wa Programu na Return
Hii ni calculator inayorudisha thamani badala ya kuichapisha.
def calculator(x, y, z):
if y == "+":
return x + z
elif y == "-":
return x - z
elif y == "*":
return x * z
elif y == "/":
return x / z
else:
return "Invalid operator"
x = int(input("Namba ya kwanza: "))
y = input("Weka operator ya hesabu (+, -, *, /): ")
z = int(input("Namba ya pili: "))
result = calculator(x, y, z)
print(f"Matokeo: {result}")
Mwisho
Katika somo hili, tumejifunza:
-
Maana ya function.
-
Jinsi ya kuandika function.
-
Jinsi ya kutumia parameters na kurudisha thamani.
Somo linalofuata litaelezea aina za functions na mbinu za juu za kuzitumia kwa ufanisi zaidi.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Dua za Mitume na Manabii 👉2 Kitau cha Fiqh 👉3 Simulizi za Hadithi Audio 👉4 Kitabu cha Afya 👉5 web hosting 👉6 Bongolite - Game zone - Play free game
Post zinazofanana:
Python somo la 31: Jinsi ya kutengeneza faili na folder
Katika somo hili utajifunz ajinsi ya kutengeneza folda, faili na kuweka data kwneye faili
Soma Zaidi...PYTHON - somo la 4: Aina za data kwenye python
Katika somo hili utakwenda kujifunza aina za data ambazo hutumika kwenye python. hapa utajifunza aina kuu 3 za data.
Soma Zaidi...PYTHON - somo la 7: Jinsi ya kubadili aina ya data
Katika soo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kubaduli aina moja ya data kwena aina nyingine. Kwa mfano unaweza kubadili namba kuwa string ama kubadili string kuwa nanda ama kubadili float kuwa int.
Soma Zaidi...PYTHON - somo la 9: indexing katika strinfg
Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu string indexing. Kama tulivyojifunza kuhusu namba katika somo lililopita, basi hapa tutakwenda kucheza na string.
Soma Zaidi...Python somo la 58: Jinsi ya Kuboresha Django Admin
Katika somo hili tutajifunza mambo matatu muhimu ya kuboresha admin ya Django: Jinsi ya kubadili header za Django Admin Jinsi ya kuongeza columns zinazojitokeza kwenye admin list Jinsi ya kuweka limit ya rows zinazoonekana kwa kila ukurasa (pagination)
Soma Zaidi...PYTHON somo la 12: assignment operator, logical operator, identity oeprator na membership operator
Katika somo hili utakwenda kujfunza operator nyingine kama assignment operator logical, identity operator na membership operator.
Soma Zaidi...