picha

Python somo la 18: Jinsi ya kuandika function

Katika somo hili utakwend akujifunza jinsi ya kuandika function, kuweka parameter na kuitumia function

Jinsi ya Kuandika Function na Kuweka Parameter: Python Version

Katika somo hili, tutajifunza maana ya function, jinsi ya kuandika function, na jinsi ya kuweka parameters kwenye function katika Python.

 


 

Function ni Nini?

Function ni block ya code inayofanya kazi maalumu. Inasaidia kupunguza marudio ya code kwa kuruhusu matumizi yake mara nyingi bila kuiandika tena.

Mambo ya Kuzingatia kuhusu Functions:

  1. Function hutumika zaidi ya mara moja.

  2. Function haifanyi kazi mpaka iitwe (invoked).

  3. Function inaweza kupokea parameters ili kubadilisha tabia yake kulingana na mahitaji.

 


 

Jinsi ya Kuandika Function

Katika Python, function huandikwa kwa kutumia def ikifuatiwa na jina la function, mabano ya mviringo (), yakifuatiwa na alama ya ( : ) yaani nukta pacha bouble colon kisha ndipo  body ya function inafuata.

Mfano wa Msingi:

# Function rahisi inayochapisha ujumbe

def bongo():

    print("Bongoclass")

 

# Kuitwa kwa function

bongo()

 

 


 

Function Inayorudiwa Mara Nyingi

Function inaweza kuitwa mara nyingi kwa kutumia for loop.

Mfano:

# Function inayochapisha "Bongoclass"

def bongo():

    print("Bongoclass")

 

# Kuitumia mara 10

for i in range(10):

    bongo()

 

 


 

Jinsi ya Kuweka Parameter kwenye Function

Parameters ni viingilio vinavyotumwa kwa function wakati wa kuitwa, na vinaweza kubadilisha tabia ya function.

Mfano:

# Function inayochapisha ujumbe mara kadhaa

def bongo(idadi):

    for i in range(idadi):

        print("Bongoclass")

 

# Kuitumia function

idadi = int(input("Andika idadi ya mara za kuchapisha: "))

bongo(idadi)

 

 

Parameter na argument

Katika mfano hapo juu parameter ni idadi na argument ni hiyo namba utakayoweka. ina maana argument ni value ya hiyo parameter. mfano hapo nikiweka 6, ina maana parameter na idadi na argument ni 6. Nimeliweka wazi hili kwa sababu programmer wengi wanaoanza kujifunza wanapata tabu sana kutofautisha kati ya argument na parameter.


 

Function Zenye Parameters Nyingi

Unaweza kutumia parameters zaidi ya moja kwa kuzitenganisha kwa koma.

Mfano: Kujumlisha Namba Mbili:

# Function inayojumlisha namba mbili

def jumlisha(x, y):

    print(f"Jumla ya {x} na {y} ni: {x + y}")

 

# Kuitumia function

jumlisha(5, 7)

 

 


 

Programu ya Calculator Rahisi

Hii ni programu inayotumia parameters tatu: namba ya kwanza, operator ya hesabu, na namba ya pili.

Kwa kutumia if statement:

# Function ya calculator

def calculator(x, y, z):

    if y == "+":

        return x + z

    elif y == "-":

        return x - z

    elif y == "*":

        return x * z

    elif y == "/":

        return x / z

    else:

        return "Invalid operator"

 

# Kuitumia function

x = int(input("Namba ya kwanza: "))

y = input("Weka operator ya hesabu (+, -, *, /): ")

z = int(input("Namba ya pili: "))

print(f"Matokeo: {calculator(x, y, z)}")

 

Kwa kutumia match statement (Python 3.10+):

# Function ya calculator

def calculator(x, y, z):

    match y:

        case "+":

            return x + z

        case "-":

            return x - z

        case "*":

            return x * z

        case "/":

            return x / z

        case _:

            return "Invalid operator"

 

# Kuitumia function

x = int(input("Namba ya kwanza: "))

y = input("Weka operator ya hesabu (+, -, *, /): ")

z = int(input("Namba ya pili: "))

print(f"Matokeo: {calculator(x, y, z)}")

 

 


 

Function Zinazorudisha Thamani (Return Value)

Function inaweza kurudisha thamani badala ya kuchapisha moja kwa moja.

Mfano:

# Function inayojumlisha namba mbili

def jumlisha(x, y):

    return x + y

 

# Kuitumia function

result = jumlisha(5, 7)

print(f"Jumla: {result}")

 

 


 

Mfano wa Programu na Return

Hii ni calculator inayorudisha thamani badala ya kuichapisha.

def calculator(x, y, z):

    if y == "+":

        return x + z

    elif y == "-":

        return x - z

    elif y == "*":

        return x * z

    elif y == "/":

        return x / z

    else:

        return "Invalid operator"

 

x = int(input("Namba ya kwanza: "))

y = input("Weka operator ya hesabu (+, -, *, /): ")

z = int(input("Namba ya pili: "))

 

result = calculator(x, y, z)

print(f"Matokeo: {result}")

 

 


 

Mwisho

Katika somo hili, tumejifunza:

  1. Maana ya function.

  2. Jinsi ya kuandika function.

  3. Jinsi ya kutumia parameters na kurudisha thamani.

Somo linalofuata litaelezea aina za functions na mbinu za juu za kuzitumia kwa ufanisi zaidi.

 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-11-26 Topic: Python Main: ICT File: Download PDF Views 623

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 web hosting    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Python somo la 62 Kupakia picha (upload) na kuisoma kutoka kwenye database

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kushughulika na faili, kama ku upload faili kwenye django.

Soma Zaidi...
PYTHON somo la 12: assignment operator, logical operator, identity oeprator na membership operator

Katika somo hili utakwenda kujfunza operator nyingine kama assignment operator logical, identity operator na membership operator.

Soma Zaidi...
Python somo la 49: Jinsi ya ku host project ya Django

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya ku host website ya Django. Hapa tutakwenda kutuma plaform ya pythonanywhere.com.

Soma Zaidi...
Python somo la 26: Sheria za uandishi wa object

Katika somo hili utakwend akujifunza maana ya object, na sheria za kuandika object.

Soma Zaidi...
Python somo la 20: Aina za parameter kwenye function

Katika somo hili tutakwend akujifunza kwa urefu zaidi kuhusu parameter ambazo hutumika kwenye functions

Soma Zaidi...
Pthon somo la 41: Template Inheritance katika Django

Somo hili linazungumzia hatua ya kuunda navigation menu na kutumia template inheritance kwa njia ya kitaalamu katika Django.

Soma Zaidi...
Python somo la 23: Library kwenye python

Hapa utajifunza maana ya library, kazi zake aina zake na jinsi ya ku install lirary

Soma Zaidi...
Python somo la 16: Jinsi ya kutumia break na continue kwenye loop

Katika somo hili tunakwenda kujifunza matumizi ya break na continue kwenye loop

Soma Zaidi...
Python somo la 44: Data Manipulation katika Django Templates

Katika somo hili utakwend akujifunza jinsi ya kucheza na data kuzibadili kwa namna mbali mbali kwenye template

Soma Zaidi...
Python somo la 22: Package kwenye Python

Hapa utakwenda kujifunz amaana ya package, aina zake na jinsi ya kuandika package.

Soma Zaidi...