picha

Python somo la 18: Jinsi ya kuandika function

Katika somo hili utakwend akujifunza jinsi ya kuandika function, kuweka parameter na kuitumia function

Jinsi ya Kuandika Function na Kuweka Parameter: Python Version

Katika somo hili, tutajifunza maana ya function, jinsi ya kuandika function, na jinsi ya kuweka parameters kwenye function katika Python.

 


 

Function ni Nini?

Function ni block ya code inayofanya kazi maalumu. Inasaidia kupunguza marudio ya code kwa kuruhusu matumizi yake mara nyingi bila kuiandika tena.

Mambo ya Kuzingatia kuhusu Functions:

  1. Function hutumika zaidi ya mara moja.

  2. Function haifanyi kazi mpaka iitwe (invoked).

  3. Function inaweza kupokea parameters ili kubadilisha tabia yake kulingana na mahitaji.

 


 

Jinsi ya Kuandika Function

Katika Python, function huandikwa kwa kutumia def ikifuatiwa na jina la function, mabano ya mviringo (), yakifuatiwa na alama ya ( : ) yaani nukta pacha bouble colon kisha ndipo  body ya function inafuata.

Mfano wa Msingi:

# Function rahisi inayochapisha ujumbe

def bongo():

    print("Bongoclass")

 

# Kuitwa kwa function

bongo()

 

 


 

Function Inayorudiwa Mara Nyingi

Function inaweza kuitwa mara nyingi kwa kutumia for loop.

Mfano:

# Function inayochapisha "Bongoclass"

def bongo():

    print("Bongoclass")

 

# Kuitumia mara 10

for i in range(10):

    bongo()

 

 


 

Jinsi ya Kuweka Parameter kwenye Function

Parameters ni viingilio vinavyotumwa kwa function wakati wa kuitwa, na vinaweza kubadilisha tabia ya function.

Mfano:

# Function inayochapisha ujumbe mara kadhaa

def bongo(idadi):

    for i in range(idadi):

        print("Bongoclass")

 

# Kuitumia function

idadi = int(input("Andika idadi ya mara za kuchapisha: "))

bongo(idadi)

 

 

Parameter na argument

Katika mfano hapo juu parameter ni idadi na argument ni hiyo namba utakayoweka. ina maana argument ni value ya hiyo parameter. mfano hapo nikiweka 6, ina maana parameter na idadi na argument ni 6. Nimeliweka wazi hili kwa sababu programmer wengi wanaoanza kujifunza wanapata tabu sana kutofautisha kati ya argument na parameter.


 

Function Zenye Parameters Nyingi

Unaweza kutumia parameters zaidi ya moja kwa kuzitenganisha kwa koma.

Mfano: Kujumlisha Namba Mbili:

# Function inayojumlisha namba mbili

def jumlisha(x, y):

    print(f"Jumla ya {x} na {y} ni: {x + y}")

 

# Kuitumia function

jumlisha(5, 7)

 

 


 

Programu ya Calculator Rahisi

Hii ni programu inayotumia parameters tatu: namba ya kwanza, operator ya hesabu, na namba ya pili.

Kwa kutumia if statement:

# Function ya calculator

def calculator(x, y, z):

    if y == "+":

        return x + z

    elif y == "-":

        return x - z

    elif y == "*":

        return x * z

    elif y == "/":

        return x / z

    else:

        return "Invalid operator"

 

# Kuitumia function

x = int(input("Namba ya kwanza: "))

y = input("Weka operator ya hesabu (+, -, *, /): ")

z = int(input("Namba ya pili: "))

print(f"Matokeo: {calculator(x, y, z)}")

 

Kwa kutumia match statement (Python 3.10+):

# Function ya calculator

def calculator(x, y, z):

    match y:

        case "+":

            return x + z

        case "-":

            return x - z

        case "*":

            return x * z

        case "/":

            return x / z

        case _:

            return "Invalid operator"

 

# Kuitumia function

x = int(input("Namba ya kwanza: "))

y = input("Weka operator ya hesabu (+, -, *, /): ")

z = int(input("Namba ya pili: "))

print(f"Matokeo: {calculator(x, y, z)}")

 

 


 

Function Zinazorudisha Thamani (Return Value)

Function inaweza kurudisha thamani badala ya kuchapisha moja kwa moja.

Mfano:

# Function inayojumlisha namba mbili

def jumlisha(x, y):

    return x + y

 

# Kuitumia function

result = jumlisha(5, 7)

print(f"Jumla: {result}")

 

 


 

Mfano wa Programu na Return

Hii ni calculator inayorudisha thamani badala ya kuichapisha.

def calculator(x, y, z):

    if y == "+":

        return x + z

    elif y == "-":

        return x - z

    elif y == "*":

        return x * z

    elif y == "/":

        return x / z

    else:

        return "Invalid operator"

 

x = int(input("Namba ya kwanza: "))

y = input("Weka operator ya hesabu (+, -, *, /): ")

z = int(input("Namba ya pili: "))

 

result = calculator(x, y, z)

print(f"Matokeo: {result}")

 

 


 

Mwisho

Katika somo hili, tumejifunza:

  1. Maana ya function.

  2. Jinsi ya kuandika function.

  3. Jinsi ya kutumia parameters na kurudisha thamani.

Somo linalofuata litaelezea aina za functions na mbinu za juu za kuzitumia kwa ufanisi zaidi.

 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Python Main: ICT File: Download PDF Views 479

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
πŸ‘‰1 Bongolite - Game zone - Play free game    πŸ‘‰2 Simulizi za Hadithi Audio    πŸ‘‰3 web hosting    πŸ‘‰4 kitabu cha Simulizi    πŸ‘‰5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    πŸ‘‰6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Python somo la 13: Kutumia condition statement - if, else, elif

Katika somo hili tutakwend akuziona aina za condition statement kwneye python na jinsi ya kuzitumia

Soma Zaidi...
Python somo la 49: Jinsi ya ku host project ya Django

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya ku host website ya Django. Hapa tutakwenda kutuma plaform ya pythonanywhere.com.

Soma Zaidi...
Python somo la 38: Kubadilisha landing page ya Django Framework

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kubadili ukurasa wa landing page wa Django na kuweka ukurasa tunaoutaka sisi.

Soma Zaidi...
PYTHON somo la 12: assignment operator, logical operator, identity oeprator na membership operator

Katika somo hili utakwenda kujfunza operator nyingine kama assignment operator logical, identity operator na membership operator.

Soma Zaidi...
Python somo la 25: Sheria za uandishi wa class

Katika somo hili utajifunza maana ya class, sheria za uandishi wake na mifano halisi

Soma Zaidi...
Python somo la 59: Kufanya Mahesabu (Aggregations) Katika Django

Katika somo hili tutajifunza jinsi ya kutumia Django ORM kufanya mahesabu mbalimbali kama Sum, Avg, Count, Max, Min, pamoja na kupunguza idadi ya items zinazoonekana kwenye dashboard (LIMIT). Pia tutajifunza namna ya kutengeneza β€œdifference” kati ya thamani kubwa na ndogo bila kubadilisha functions zozote ulizokwisha ziandika.

Soma Zaidi...
Python somo la 37: Jinsi ya ku install Django na kutengeneza project na app

Katika somo ili utajifunza hatuwa kwa hatuwa za ku install Django, kutengeneza project na kutengeneza app

Soma Zaidi...
PYHON - somo la 5: Aina za data list, turple, dictionary na boolean

Katika somo hili tunakwenda kujifunza aina nyingine za data ambazo hutumika kwenye python.

Soma Zaidi...
Python somo la 52: Kutengeneza table na kufanya Migrations Katika Django

Katika somo hili tutajifunza jinsi Django hutumia migrations kuunda na kubadilisha tables kwenye database kulingana na models tunazoandika. Tutapitia maana ya migration, hatua za kuitumia, umuhimu wake, misingi ya makemigrations na migrate, pamoja na mfano halisi kutoka kwenye project yetu ya pybongo (app: menu).

Soma Zaidi...
Python somo la 17: Jinsi ya kutumia user input

Katika somo hili uatkwenda kujifunz anamna ambavyo mtu anaweza kuingiza input kwneye system

Soma Zaidi...