picha

Python somo la 18: Jinsi ya kuandika function

Katika somo hili utakwend akujifunza jinsi ya kuandika function, kuweka parameter na kuitumia function

Jinsi ya Kuandika Function na Kuweka Parameter: Python Version

Katika somo hili, tutajifunza maana ya function, jinsi ya kuandika function, na jinsi ya kuweka parameters kwenye function katika Python.

 


 

Function ni Nini?

Function ni block ya code inayofanya kazi maalumu. Inasaidia kupunguza marudio ya code kwa kuruhusu matumizi yake mara nyingi bila kuiandika tena.

Mambo ya Kuzingatia kuhusu Functions:

  1. Function hutumika zaidi ya mara moja.

  2. Function haifanyi kazi mpaka iitwe (invoked).

  3. Function inaweza kupokea parameters ili kubadilisha tabia yake kulingana na mahitaji.

 


 

Jinsi ya Kuandika Function

Katika Python, function huandikwa kwa kutumia def ikifuatiwa na jina la function, mabano ya mviringo (), yakifuatiwa na alama ya ( : ) yaani nukta pacha bouble colon kisha ndipo  body ya function inafuata.

Mfano wa Msingi:

# Function rahisi inayochapisha ujumbe

def bongo():

    print("Bongoclass")

 

# Kuitwa kwa function

bongo()

 

 


 

Function Inayorudiwa Mara Nyingi

Function inaweza kuitwa mara nyingi kwa kutumia for loop.

Mfano:

# Function inayochapisha "Bongoclass"

def bongo():

    print("Bongoclass")

 

# Kuitumia mara 10

for i in range(10):

    bongo()

 

 


 

Jinsi ya Kuweka Parameter kwenye Function

Parameters ni viingilio vinavyotumwa kwa function wakati wa kuitwa, na vinaweza kubadilisha tabia ya function.

Mfano:

# Function inayochapisha ujumbe mara kadhaa

def bongo(idadi):

    for i in range(idadi):

        print("Bongoclass")

 

# Kuitumia function

idadi = int(input("Andika idadi ya mara za kuchapisha: "))

bongo(idadi)

 

 

Parameter na argument

Katika mfano hapo juu parameter ni idadi na argument ni hiyo namba utakayoweka. ina maana argument ni value ya hiyo parameter. mfano hapo nikiweka 6, ina maana parameter na idadi na argument ni 6. Nimeliweka wazi hili kwa sababu programmer wengi wanaoanza kujifunza wanapata tabu sana kutofautisha kati ya argument na parameter.


 

Function Zenye Parameters Nyingi

Unaweza kutumia parameters zaidi ya moja kwa kuzitenganisha kwa koma.

Mfano: Kujumlisha Namba Mbili:

# Function inayojumlisha namba mbili

def jumlisha(x, y):

    print(f"Jumla ya {x} na {y} ni: {x + y}")

 

# Kuitumia function

jumlisha(5, 7)

 

 


 

Programu ya Calculator Rahisi

Hii ni programu inayotumia parameters tatu: namba ya kwanza, operator ya hesabu, na namba ya pili.

Kwa kutumia if statement:

# Function ya calculator

def calculator(x, y, z):

    if y == "+":

        return x + z

    elif y == "-":

        return x - z

    elif y == "*":

        return x * z

    elif y == "/":

        return x / z

    else:

        return "Invalid operator"

 

# Kuitumia function

x = int(input("Namba ya kwanza: "))

y = input("Weka operator ya hesabu (+, -, *, /): ")

z = int(input("Namba ya pili: "))

print(f"Matokeo: {calculator(x, y, z)}")

 

Kwa kutumia match statement (Python 3.10+):

# Function ya calculator

def calculator(x, y, z):

    match y:

        case "+":

            return x + z

        case "-":

            return x - z

        case "*":

            return x * z

        case "/":

            return x / z

        case _:

            return "Invalid operator"

 

# Kuitumia function

x = int(input("Namba ya kwanza: "))

y = input("Weka operator ya hesabu (+, -, *, /): ")

z = int(input("Namba ya pili: "))

print(f"Matokeo: {calculator(x, y, z)}")

 

 


 

Function Zinazorudisha Thamani (Return Value)

Function inaweza kurudisha thamani badala ya kuchapisha moja kwa moja.

Mfano:

# Function inayojumlisha namba mbili

def jumlisha(x, y):

    return x + y

 

# Kuitumia function

result = jumlisha(5, 7)

print(f"Jumla: {result}")

 

 


 

Mfano wa Programu na Return

Hii ni calculator inayorudisha thamani badala ya kuichapisha.

def calculator(x, y, z):

    if y == "+":

        return x + z

    elif y == "-":

        return x - z

    elif y == "*":

        return x * z

    elif y == "/":

        return x / z

    else:

        return "Invalid operator"

 

x = int(input("Namba ya kwanza: "))

y = input("Weka operator ya hesabu (+, -, *, /): ")

z = int(input("Namba ya pili: "))

 

result = calculator(x, y, z)

print(f"Matokeo: {result}")

 

 


 

Mwisho

Katika somo hili, tumejifunza:

  1. Maana ya function.

  2. Jinsi ya kuandika function.

  3. Jinsi ya kutumia parameters na kurudisha thamani.

Somo linalofuata litaelezea aina za functions na mbinu za juu za kuzitumia kwa ufanisi zaidi.

 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-11-26 Topic: Python Main: ICT File: Download PDF Views 686

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
πŸ‘‰1 ai web app    πŸ‘‰2 Kitau cha Fiqh    πŸ‘‰3 web hosting    πŸ‘‰4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    πŸ‘‰5 Bongolite - Game zone - Play free game    πŸ‘‰6 Dua za Mitume na Manabii   

Post zinazofanana:

Python seomo la 55: Kutengeneza Simple Admin Dashboard ya CRUD

Katika somo hili tutajifunza jinsi ya kuunda dashboard rahisi ndani ya Django ambayo itaruhusu mtumiaji kuongeza, kusoma, kuhariri na kufuta taarifa za MenuItem bila kutumia Django built-in admin, bali kwa kutumia HTML templates na views tulizotengeneza sisi wenyewe.

Soma Zaidi...
Python somo la 29: Encaosulation kwneye python

Katika somo hili utajifunza maana ya encapsulation na sheria za uandishi wake

Soma Zaidi...
Python somo la 13: Kutumia condition statement - if, else, elif

Katika somo hili tutakwend akuziona aina za condition statement kwneye python na jinsi ya kuzitumia

Soma Zaidi...
Python somo la 19: Aina za Function

Katika somo hili utakwend akujifunza aina mbalimbali za function ambazo tunaweza kuzitumia kwenye python.

Soma Zaidi...
Python somo la 24: Nini maana ya Object Oriented Programming

Hapa tunakwenda kujifunza kuhusu OOP ambapo ni miongoni mwa mitindo ya uandishi wa code

Soma Zaidi...
Python somo la 38: Kubadilisha landing page ya Django Framework

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kubadili ukurasa wa landing page wa Django na kuweka ukurasa tunaoutaka sisi.

Soma Zaidi...
Python somo la 44: Data Manipulation katika Django Templates

Katika somo hili utakwend akujifunza jinsi ya kucheza na data kuzibadili kwa namna mbali mbali kwenye template

Soma Zaidi...
Python somo la 60: Hashing na Encryption kwenye Django

Katika somo hili tutajifunza: Tofauti kati ya hashing na encryption Jinsi ya kufunga packages muhimu Jinsi ya kufanya hashing kwa maneno ya kawaida (mfano β€œbongoclass”) Jinsi ya kufanya encryption na decrypt kutumia Fernet Jinsi Django inahash password kupitia User model Mazoezi ya vitendo

Soma Zaidi...
Python somo la 32: Jinsi ya kusoma mafaili

Katika somo hili utakwenda kujifunz ajinsi ya kusoma mafaili na mitindo mbalimbali ya kusoma data

Soma Zaidi...
Python somo la 28: inheritance kwenye OOP

Katika somo hili utakwenda kujifunz amaana ya inheritance na sheria za kuiandika inheritance.

Soma Zaidi...