Python somo la 18: Jinsi ya kuandika function

Python somo la 18: Jinsi ya kuandika function

Katika somo hili utakwend akujifunza jinsi ya kuandika function, kuweka parameter na kuitumia function

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Jinsi ya Kuandika Function na Kuweka Parameter: Python Version

Katika somo hili, tutajifunza maana ya function, jinsi ya kuandika function, na jinsi ya kuweka parameters kwenye function katika Python.

 


 

Function ni Nini?

Function ni block ya code inayofanya kazi maalumu. Inasaidia kupunguza marudio ya code kwa kuruhusu matumizi yake mara nyingi bila kuiandika tena.

Mambo ya Kuzingatia kuhusu Functions:

  1. Function hutumika zaidi ya mara moja.

  2. Function haifanyi kazi mpaka iitwe (invoked).

  3. Function inaweza kupokea parameters ili kubadilisha tabia yake kulingana na mahitaji.

 


 

Jinsi ya Kuandika Function

Katika Python, function huandikwa kwa kutumia def ikifuatiwa na jina la function, mabano ya mviringo (), yakifuatiwa na alama ya ( : ) yaani nukta pacha bouble colon kisha ndipo  body ya function inafuata.

Mfano wa Msingi:

# Function rahisi inayochapisha ujumbe

def bongo():

    print("Bongoclass")

 

# Kuitwa kwa function

bongo()

 

 


 

Function Inayorudiwa Mara Nyingi

Function inaweza kuitwa mara nyingi kwa kutumia for loop.

Mfano:

# Function inayochapisha "Bongoclass"

def bongo():

    print("Bongoclass")

 

# Kuitumia mara 10

for i in range(10):

    bongo()

 

 


 

Jinsi ya Kuweka Parameter kwenye Function

Parameters ni viingilio vinavyotumwa kwa function wakati wa kuitwa, na vinaweza kubadilisha tabia ya function.

Mfano:

# Function inayochapisha ujumbe mara kadhaa

def bongo(idadi):

    for i in range(idadi):

        print("Bongoclass")

 

# Kuitumia function

idadi = int(input("Andika idadi ya mara za kuchapisha: "))

bongo(idadi)

 

 

Parameter na argument

Katika mfano hapo juu parameter ni idadi na argument ni hiyo namba utakayoweka. ina maana argument ni value ya hiyo parameter. mfano hapo nikiweka 6, ina maana parameter na idadi na argument ni 6. Nimeliweka wazi hili kwa sababu programmer wengi wanaoanza kujifunza wanapata tabu sana kutofautisha kati ya argument na parameter.


 

Function Zenye Parameters Nyingi

Unaweza kutumia parameters zaidi ya moja kwa kuzitenganisha kwa koma.

Mfano: Kujumlisha Namba Mbili:

# Function inayojumlisha namba mbili

def jumlisha(x, y):

    print(f"Jumla ya {x} na {y} ni: {x + y}")

 

# Kuitumia function

jumlisha(5, 7)

 

 


 

Programu ya Calculator Rahisi

Hii ni programu inayotumia parameters tatu: namba ya kwanza, operator ya hesabu, na namba ya pili.

Kwa kutumia if statement:

# Function ya calculator

def calculator(x, y, z):

    if y == "+":

        return x + z

    elif y == "-":

        return x - z

    elif y == "*":

        return x * z

    elif y == "/":

        return x / z

    else:

        return "Invalid operator"

 

# Kuitumia function

x = int(input("Namba ya kwanza: "))

y = input("Weka operator ya hesabu (+, -, *, /): ")

z = int(input("Namba ya pili: "))

print(f"Matokeo: {calculator(x, y, z)}")

 

Kwa kutumia match statement (Python 3.10+):

# Function ya calculator

def calculator(x, y, z):

    match y:

        case "+":

            return x + z

        case "-":

            return x - z

        case "*":

            return x * z

        case "/":

            return x / z

        case _:

            return "Invalid operator"

 

# Kuitumia function

x = int(input("Namba ya kwanza: "))

y = input("Weka operator ya hesabu (+, -, *, /): ")

z = int(input("Namba ya pili: "))

print(f"Matokeo: {calculator(x, y, z)}")

 

 


 

Function Zinazorudisha Thamani (Return Value)

Function inaweza kurudisha thamani badala ya kuchapisha moja kwa moja.

Mfano:

# Function inayojumlisha namba mbili

def jumlisha(x, y):

    return x + y

 

# Kuitumia function

result = jumlisha(5, 7)

print(f"Jumla: {result}")

 

 


 

Mfano wa Programu na Return

Hii ni calculator inayorudisha thamani badala ya kuichapisha.

def calculator(x, y, z):

    if y == "+":

        return x + z

    elif y == "-":

        return x - z

    elif y == "*":

        return x * z

    elif y == "/":

        return x / z

    else:

        return "Invalid operator"

 

x = int(input("Namba ya kwanza: "))

y = input("Weka operator ya hesabu (+, -, *, /): ")

z = int(input("Namba ya pili: "))

 

result = calculator(x, y, z)

print(f"Matokeo: {result}")

 

 


 

Mwisho

Katika somo hili, tumejifunza:

  1. Maana ya function.

  2. Jinsi ya kuandika function.

  3. Jinsi ya kutumia parameters na kurudisha thamani.

Somo linalofuata litaelezea aina za functions na mbinu za juu za kuzitumia kwa ufanisi zaidi.

 

Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Python Main: ICT File: Download PDF Views 235

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 Madrasa kiganjani    👉5 Bongolite - Game zone - Play free game    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

PYTHON somo la 11: Matumizi ya comperison eperator katika python
PYTHON somo la 11: Matumizi ya comperison eperator katika python

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu operator. Hasa hapa tutakwend akujifunz akuhusu comparison operaor.

Soma Zaidi...
PYTHON - somo la 9: indexing katika strinfg
PYTHON - somo la 9: indexing katika strinfg

Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu string indexing. Kama tulivyojifunza kuhusu namba katika somo lililopita, basi hapa tutakwenda kucheza na string.

Soma Zaidi...
Python somo la 35: Jinsi ya kutumia MYSQL kwenye python
Python somo la 35: Jinsi ya kutumia MYSQL kwenye python

Katika somo hili utajifunz akutumia database kwenye python

Soma Zaidi...
Python somo la 24: Nini maana ya Object Oriented Programming
Python somo la 24: Nini maana ya Object Oriented Programming

Hapa tunakwenda kujifunza kuhusu OOP ambapo ni miongoni mwa mitindo ya uandishi wa code

Soma Zaidi...
Python somo la 44: Data Manipulation katika Django Templates
Python somo la 44: Data Manipulation katika Django Templates

Katika somo hili utakwend akujifunza jinsi ya kucheza na data kuzibadili kwa namna mbali mbali kwenye template

Soma Zaidi...
Python somo la 13: Kutumia condition statement - if, else, elif
Python somo la 13: Kutumia condition statement - if, else, elif

Katika somo hili tutakwend akuziona aina za condition statement kwneye python na jinsi ya kuzitumia

Soma Zaidi...
Python somo la 32: Jinsi ya kusoma mafaili
Python somo la 32: Jinsi ya kusoma mafaili

Katika somo hili utakwenda kujifunz ajinsi ya kusoma mafaili na mitindo mbalimbali ya kusoma data

Soma Zaidi...
Pthon somo la 41: Template Inheritance katika Django
Pthon somo la 41: Template Inheritance katika Django

Somo hili linazungumzia hatua ya kuunda navigation menu na kutumia template inheritance kwa njia ya kitaalamu katika Django.

Soma Zaidi...
Python somo la 21: Module katika python
Python somo la 21: Module katika python

Katika somo hili utakwend akujifunz amaana ya module, kazi zake, aina zake na jinsi ya kuandika modile

Soma Zaidi...
Python somo la 25: Sheria za uandishi wa class
Python somo la 25: Sheria za uandishi wa class

Katika somo hili utajifunza maana ya class, sheria za uandishi wake na mifano halisi

Soma Zaidi...