Katika somo hili utakwend akujifunza matumizi ya for loop kwneye python
Jinsi ya kutumia for loop katika Python
Katika somo hili, tutajifunza jinsi ya kutumia for loop katika Python. Loop hutusaidia kurudia utekelezaji wa code mara nyingi kulingana na masharti husika. Python inatoa aina tofauti za loop, na leo tutaangazia for loop na for-in loop.
For loop hutumika pale ambapo tunajua idadi ya mara ambayo code inapaswa kurudiwa. Kwa mfano, kama tunataka kutengeneza jedwali la kuzidisha la namba 7, ambapo tutazidisha 7 kwa namba kutoka 1 hadi 12, tunaweza kutumia for loop.
print("TEBO YA 7:")
for x in range(1, 13): # range(1, 13) ina maana kuanzia 1 hadi 12
print(7 * x)
Matokeo ya code hii ni jedwali la 7. Hii ni kwa sababu loop itazidisha 7 na kila namba kuanzia 1 hadi 12.
Unaweza kuboresha jinsi matokeo yanavyoonekana kwa kutumia f-string, ambayo inaruhusu kuongeza maelezo zaidi.
print("TEBO YA 7 ILIYOBORESHWA:")
for x in range(1, 13):
print(f"{x} * 7 = {x * 7}")
Code hii itatoa matokeo yaliyoeleweka zaidi kama:
1 * 7 = 7
2 * 7 = 14
...
12 * 7 = 84
For-in loop hutumika wakati tunafanya kazi na data kama vile list au map. Tofauti na for loop ya kawaida, hapa tunarudia moja kwa moja kila kipengele kilichopo kwenye data.
Tunaweza kutumia for-in loop kuonyesha jedwali la 7 moja kwa moja kutoka kwenye listi ya thamani zake.
print("TEBO YA 7 KWA KUTUMIA LIST:")
tebo = [7, 14, 21, 28, 35, 42, 49, 56, 63, 70, 77, 84]
for x in tebo:
print(x)
Unaweza pia kutumia for-in loop kufanya mahesabu kwa kila kipengele cha list badala ya kuandika thamani zote.
print("TEBO YA 7 KWA MAHESABU NDANI YA LIST:")
tebo = [1, 2, 3, 4, 5, 6, 7, 8, 9, 10, 11, 12]
for x in tebo:
print(f"{x} * 7 = {x * 7}")
Kufikia hapa, umejifunza jinsi ya kutumia for loop na for-in loop katika Python. Unaweza kuendelea kufanya mazoezi zaidi kwa kutumia data tofauti na hali tofauti. Katika somo linalofuata, tutajifunza kuhusu while loop, ambayo hutumika pale ambapo idadi ya marudio haijulikani mapema.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Katika somo hili utakwend akujifunz anamna ya kuwez akupata taarifa zinazohusu faili
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunza maana ya class, sheria za uandishi wake na mifano halisi
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwend akujifunza aina mbalimbali za function ambazo tunaweza kuzitumia kwenye python.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunz ajinsi ya kusoma mafaili na mitindo mbalimbali ya kusoma data
Soma Zaidi...Katika somo hili uatkwenda kujifunz anamna ambavyo mtu anaweza kuingiza input kwneye system
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunz akutumia database kwenye python
Soma Zaidi...Hapa utakwenda kujifunz amaana ya package, aina zake na jinsi ya kuandika package.
Soma Zaidi...Katika somo hili tutakwend akujifunza kwa urefu zaidi kuhusu parameter ambazo hutumika kwenye functions
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwend akujifunza jinsi ya kuandika function, kuweka parameter na kuitumia function
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunza kuhusu maana ya python na kazi zake. pia jinsi ya kuandaa kifaa chako kwa ajili ya somo.
Soma Zaidi...