Katika somo hili utakwend akujifunza matumizi ya for loop kwneye python
Jinsi ya kutumia for loop katika Python
Katika somo hili, tutajifunza jinsi ya kutumia for loop katika Python. Loop hutusaidia kurudia utekelezaji wa code mara nyingi kulingana na masharti husika. Python inatoa aina tofauti za loop, na leo tutaangazia for loop na for-in loop.
For loop hutumika pale ambapo tunajua idadi ya mara ambayo code inapaswa kurudiwa. Kwa mfano, kama tunataka kutengeneza jedwali la kuzidisha la namba 7, ambapo tutazidisha 7 kwa namba kutoka 1 hadi 12, tunaweza kutumia for loop.
print("TEBO YA 7:")
for x in range(1, 13): # range(1, 13) ina maana kuanzia 1 hadi 12
print(7 * x)
Matokeo ya code hii ni jedwali la 7. Hii ni kwa sababu loop itazidisha 7 na kila namba kuanzia 1 hadi 12.
Unaweza kuboresha jinsi matokeo yanavyoonekana kwa kutumia f-string, ambayo inaruhusu kuongeza maelezo zaidi.
print("TEBO YA 7 ILIYOBORESHWA:")
for x in range(1, 13):
print(f"{x} * 7 = {x * 7}")
Code hii itatoa matokeo yaliyoeleweka zaidi kama:
1 * 7 = 7
2 * 7 = 14
...
12 * 7 = 84
For-in loop hutumika wakati tunafanya kazi na data kama vile list au map. Tofauti na for loop ya kawaida, hapa tunarudia moja kwa moja kila kipengele kilichopo kwenye data.
Tunaweza kutumia for-in loop kuonyesha jedwali la 7 moja kwa moja kutoka kwenye listi ya thamani zake.
print("TEBO YA 7 KWA KUTUMIA LIST:")
tebo = [7, 14, 21, 28, 35, 42, 49, 56, 63, 70, 77, 84]
for x in tebo:
print(x)
Unaweza pia kutumia for-in loop kufanya mahesabu kwa kila kipengele cha list badala ya kuandika thamani zote.
print("TEBO YA 7 KWA MAHESABU NDANI YA LIST:")
tebo = [1, 2, 3, 4, 5, 6, 7, 8, 9, 10, 11, 12]
for x in tebo:
print(f"{x} * 7 = {x * 7}")
Kufikia hapa, umejifunza jinsi ya kutumia for loop na for-in loop katika Python. Unaweza kuendelea kufanya mazoezi zaidi kwa kutumia data tofauti na hali tofauti. Katika somo linalofuata, tutajifunza kuhusu while loop, ambayo hutumika pale ambapo idadi ya marudio haijulikani mapema.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Umeionaje Makala hii.. ?
Katika somo hili uatkwenda kujifunz anamna ambavyo mtu anaweza kuingiza input kwneye system
Soma Zaidi...Somo hili linazungumzia hatua ya kuunda navigation menu na kutumia template inheritance kwa njia ya kitaalamu katika Django.
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunz ajinsi ya kutengeneza folda, faili na kuweka data kwneye faili
Soma Zaidi...Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu string indexing. Kama tulivyojifunza kuhusu namba katika somo lililopita, basi hapa tutakwenda kucheza na string.
Soma Zaidi...Hapa tunakwenda kujifunza kuhusu OOP ambapo ni miongoni mwa mitindo ya uandishi wa code
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunz ajinsi ya kusoma mafaili na mitindo mbalimbali ya kusoma data
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu operator. Hasa hapa tutakwend akujifunz akuhusu comparison operaor.
Soma Zaidi...Katika somo hili tutajifunza namna ya kusoma data kutoka kwenye database kupitia Django ORM, jinsi ya kuzipeleka kwenye view, na jinsi ya kuzionyesha kwenye HTML template.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza kutengeneza htmk form pamoja na kuituma.
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunz akutumia database kwenye python
Soma Zaidi...