picha

Python somo la 14: Jinsi ya kutumia For loop

Katika somo hili utakwend akujifunza matumizi ya for loop kwneye python

Jinsi ya kutumia for loop katika Python

Katika somo hili, tutajifunza jinsi ya kutumia for loop katika Python. Loop hutusaidia kurudia utekelezaji wa code mara nyingi kulingana na masharti husika. Python inatoa aina tofauti za loop, na leo tutaangazia for loop na for-in loop.

 

For Loop

For loop hutumika pale ambapo tunajua idadi ya mara ambayo code inapaswa kurudiwa. Kwa mfano, kama tunataka kutengeneza jedwali la kuzidisha la namba 7, ambapo tutazidisha 7 kwa namba kutoka 1 hadi 12, tunaweza kutumia for loop.

 

Kwenye kufanya loop kwneye  python tutatumia method ya range() kumaanisha kuanzia namba fulani hadi namba fulani. Mfano kwa maelezo niliotoa hapo juu, hii loop itakuwa kati ya 1 hadi 13 ni kwa sababu tebo ya saba itakuwa 1 hadi 12, hivyo hapo  ni kati ya moja na 13, ila hiyo 13 yenyewe haipo kwenye loop.

 

Mfano:

 

print("TEBO YA 7:")

for x in range(1, 13):  # range(1, 13) ina maana kuanzia 1 hadi 12

    print(7 * x)

 

Matokeo ya code hii ni jedwali la 7. Hii ni kwa sababu loop itazidisha 7 na kila namba kuanzia 1 hadi 12.

Kuboreshwa kwa kutumia Interpolation:

Unaweza kuboresha jinsi matokeo yanavyoonekana kwa kutumia f-string, ambayo inaruhusu kuongeza maelezo zaidi.

 

print("TEBO YA 7 ILIYOBORESHWA:")

for x in range(1, 13):

    print(f"{x} * 7 = {x * 7}")

 

Code hii itatoa matokeo yaliyoeleweka zaidi kama:

1 * 7 = 7

2 * 7 = 14

...

12 * 7 = 84

 

 


 

For-in Loop

For-in loop hutumika wakati tunafanya kazi na data kama vile list au map. Tofauti na for loop ya kawaida, hapa tunarudia moja kwa moja kila kipengele kilichopo kwenye data.

 

Mfano: Loop kwenye List

Tunaweza kutumia for-in loop kuonyesha jedwali la 7 moja kwa moja kutoka kwenye listi ya thamani zake.

print("TEBO YA 7 KWA KUTUMIA LIST:")

tebo = [7, 14, 21, 28, 35, 42, 49, 56, 63, 70, 77, 84]

for x in tebo:

    print(x)

 

Kufanya Mahesabu Ndani ya List:

Unaweza pia kutumia for-in loop kufanya mahesabu kwa kila kipengele cha list badala ya kuandika thamani zote.

print("TEBO YA 7 KWA MAHESABU NDANI YA LIST:")

tebo = [1, 2, 3, 4, 5, 6, 7, 8, 9, 10, 11, 12]

for x in tebo:

    print(f"{x} * 7 = {x * 7}")

 


 

Hitimisho

Kufikia hapa, umejifunza jinsi ya kutumia for loop na for-in loop katika Python. Unaweza kuendelea kufanya mazoezi zaidi kwa kutumia data tofauti na hali tofauti. Katika somo linalofuata, tutajifunza kuhusu while loop, ambayo hutumika pale ambapo idadi ya marudio haijulikani mapema.

 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-11-22 12:11:58 Topic: Python Main: Masomo File: Download PDF Views 634

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉5 Dua za Mitume na Manabii     👉6 web hosting    

Post zinazofanana:

Python somo la 19: Aina za Function

Katika somo hili utakwend akujifunza aina mbalimbali za function ambazo tunaweza kuzitumia kwenye python.

Soma Zaidi...
PYTHON - somo la 3: Jinsi ya kuandika variable kwenye python

Katika somo hili utajifunza maana ya variable, na sheria za kutengeneza variable kwenye python. Pia utajifunza maneno ambayo hayafai kutumiwa kama variable

Soma Zaidi...
Python somo la 44: Data Manipulation katika Django Templates

Katika somo hili utakwend akujifunza jinsi ya kucheza na data kuzibadili kwa namna mbali mbali kwenye template

Soma Zaidi...
Pthon somo la 41: Template Inheritance katika Django

Somo hili linazungumzia hatua ya kuunda navigation menu na kutumia template inheritance kwa njia ya kitaalamu katika Django.

Soma Zaidi...
Python somo la 22: Package kwenye Python

Hapa utakwenda kujifunz amaana ya package, aina zake na jinsi ya kuandika package.

Soma Zaidi...
Python somo la 53: Kutengeneza HTML Form na Django View kwa ajili ya kuingiza data

Katika somo hili tutaangalia jinsi ya kutengeneza fomu ya HTML kwa ajili ya kuingiza data kwenye jedwali la MenuItem, pamoja na kutengeneza view itakayopokea data hiyo na kuihifadhi kwenye database. Pia tutaunganisha form na URL route.

Soma Zaidi...