Hapa tunakwenda kujifunza kuhusu OOP ambapo ni miongoni mwa mitindo ya uandishi wa code
Katika somo hili, utajifunza:
Maana ya Object-Oriented Programming (OOP).
Faida za kutumia OOP.
Features za msingi za OOP.
OOP ni kifupisho cha maneno Object-Oriented Programming. Hii ni moja ya mitindo ya programming paradigm inayotumika kuunda programu kwa kuzingatia dhana ya vitu (objects). Mbali na OOP, kuna mitindo mingine ya programming kama:
Imperative Programming: Njia ya kuandika programu kwa maagizo ya hatua kwa hatua.
Declarative Programming: Kuelezea kile kinachotakiwa kufanyika badala ya jinsi ya kukifanya.
Procedural Programming: Kuandika programu kwa kutumia taratibu (procedures).
Functional Programming: Kutoa msisitizo kwa functions zisizo na hali (stateless functions).
Python ni lugha ya programu inayounga mkono OOP, ambapo kila kitu kinaweza kuchukuliwa kama object. Katika OOP, object inaweza kuwa kitu chochote, kwa mfano gari, simu, au mbuzi. Kila object huwa na:
Sifa zake (attributes), kama vile rangi, ukubwa, au uzito.
Tabia zake (behaviors), kama vile kutembea, kuimba, au kufungua.
Rahisi kuelewa na kuzitumia: Code inakuwa rahisi kusoma kwa sababu ya upangaji mzuri.
Kufanya kazi katika timu: Rahisi kushirikiana kwani kila sehemu ya programu inaweza kutengenezwa kama module.
Kupunguza kurudia code: Hutumia reusability kupitia inheritance na methods.
Inarahisisha programu kubwa: Inatoa mfumo wa kugawanya kazi ngumu kuwa ndogo kwa kutumia classes.
Utunzaji wa code (maintenance): Ni rahisi kusahihisha makosa au kuongeza vipengele vipya.
Dhana kuu za OOP ambazo ni msingi wa Python ni:
Class: Kiolezo cha kuunda objects. Hii ni kama ramani.
Object: Ni mfano wa class. Inawakilisha kitu halisi.
Encapsulation: Kuwasilisha data na tabia kama kitu kimoja huku ukilinda data kwa kutumia private attributes.
Inheritance: Uwezo wa class kurithi sifa na tabia za class nyingine.
Polymorphism: Uwezo wa kutumia jina moja la method kwa behavior tofauti.
Abstraction: Kuficha maelezo yasiyo ya lazima na kuonyesha mambo muhimu tu.
Properties: Hizi ni kama variables ndani ya class ambazo huhifadhi sifa za object.
Methods: Hizi ni kama functions ndani ya class zinazowakilisha tabia au vitendo vya object.
Somo linalofuata litahusu jinsi ya kuunda class na object kwa kutumia Python
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Umeionaje Makala hii.. ?
Katika somo hili utakwend akujifunza aina mbalimbali za function ambazo tunaweza kuzitumia kwenye python.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwend akujifunz anamna ya kuwez akupata taarifa zinazohusu faili
Soma Zaidi...Katika soo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kubaduli aina moja ya data kwena aina nyingine. Kwa mfano unaweza kubadili namba kuwa string ama kubadili string kuwa nanda ama kubadili float kuwa int.
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunza kuhusu maana ya python na kazi zake. pia jinsi ya kuandaa kifaa chako kwa ajili ya somo.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza aina za data ambazo hutumika kwenye python. hapa utajifunza aina kuu 3 za data.
Soma Zaidi...Katika somo hili tunakwenda kujifunza aina nyingine za data ambazo hutumika kwenye python.
Soma Zaidi...Katika maeneo ya development, tunahitaji kutuma email mara nyingi kwa madhumuni ya: Kujaribu mfumo wa OTP Password reset System notifications Activation codes Lakini mara nyingi hatutaki emails ziondoke kwenda kwa watu halisi wakati bado tupo kwenye majaribio.
Soma Zaidi...Katika somo hili tutajifunza jinsi ya kutumia Django ORM kufanya mahesabu mbalimbali kama Sum, Avg, Count, Max, Min, pamoja na kupunguza idadi ya items zinazoonekana kwenye dashboard (LIMIT). Pia tutajifunza namna ya kutengeneza βdifferenceβ kati ya thamani kubwa na ndogo bila kubadilisha functions zozote ulizokwisha ziandika.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwend akujifunz amaana ya module, kazi zake, aina zake na jinsi ya kuandika modile
Soma Zaidi...