Hapa tunakwenda kujifunza kuhusu OOP ambapo ni miongoni mwa mitindo ya uandishi wa code
Katika somo hili, utajifunza:
Maana ya Object-Oriented Programming (OOP).
Faida za kutumia OOP.
Features za msingi za OOP.
OOP ni kifupisho cha maneno Object-Oriented Programming. Hii ni moja ya mitindo ya programming paradigm inayotumika kuunda programu kwa kuzingatia dhana ya vitu (objects). Mbali na OOP, kuna mitindo mingine ya programming kama:
Imperative Programming: Njia ya kuandika programu kwa maagizo ya hatua kwa hatua.
Declarative Programming: Kuelezea kile kinachotakiwa kufanyika badala ya jinsi ya kukifanya.
Procedural Programming: Kuandika programu kwa kutumia taratibu (procedures).
Functional Programming: Kutoa msisitizo kwa functions zisizo na hali (stateless functions).
Python ni lugha ya programu inayounga mkono OOP, ambapo kila kitu kinaweza kuchukuliwa kama object. Katika OOP, object inaweza kuwa kitu chochote, kwa mfano gari, simu, au mbuzi. Kila object huwa na:
Sifa zake (attributes), kama vile rangi, ukubwa, au uzito.
Tabia zake (behaviors), kama vile kutembea, kuimba, au kufungua.
Rahisi kuelewa na kuzitumia: Code inakuwa rahisi kusoma kwa sababu ya upangaji mzuri.
Kufanya kazi katika timu: Rahisi kushirikiana kwani kila sehemu ya programu inaweza kutengenezwa kama module.
Kupunguza kurudia code: Hutumia reusability kupitia inheritance na methods.
Inarahisisha programu kubwa: Inatoa mfumo wa kugawanya kazi ngumu kuwa ndogo kwa kutumia classes.
Utunzaji wa code (maintenance): Ni rahisi kusahihisha makosa au kuongeza vipengele vipya.
Dhana kuu za OOP ambazo ni msingi wa Python ni:
Class: Kiolezo cha kuunda objects. Hii ni kama ramani.
Object: Ni mfano wa class. Inawakilisha kitu halisi.
Encapsulation: Kuwasilisha data na tabia kama kitu kimoja huku ukilinda data kwa kutumia private attributes.
Inheritance: Uwezo wa class kurithi sifa na tabia za class nyingine.
Polymorphism: Uwezo wa kutumia jina moja la method kwa behavior tofauti.
Abstraction: Kuficha maelezo yasiyo ya lazima na kuonyesha mambo muhimu tu.
Properties: Hizi ni kama variables ndani ya class ambazo huhifadhi sifa za object.
Methods: Hizi ni kama functions ndani ya class zinazowakilisha tabia au vitendo vya object.
Somo linalofuata litahusu jinsi ya kuunda class na object kwa kutumia Python
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Umeionaje Makala hii.. ?
Katika somo ili utajifunza hatuwa kwa hatuwa za ku install Django, kutengeneza project na kutengeneza app
Soma Zaidi...Katika somo hili tutakwend akujifunza jinsi ya kutumia while loop kwneye python
Soma Zaidi...Katika somo hili uatkwenda kujifunz anamna ambavyo mtu anaweza kuingiza input kwneye system
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunza maana ya class, sheria za uandishi wake na mifano halisi
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwend akujifunza maana ya object, na sheria za kuandika object.
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunz akutumia database kwenye python
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunza kuhusu maana ya python na kazi zake. pia jinsi ya kuandaa kifaa chako kwa ajili ya somo.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunz ajinsi ya kusoma mafaili na mitindo mbalimbali ya kusoma data
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya ku host website ya Django. Hapa tutakwenda kutuma plaform ya pythonanywhere.com.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu operator. Hasa hapa tutakwend akujifunz akuhusu comparison operaor.
Soma Zaidi...