Katika somo hili utakwenda kujfnza kuhusu string method nyinginezo. Katika somo lililopita tulijifunza kuhusu string indexing.
1. Kubadili herufi ya kwanza ya string kuwa katika herufi kubwa
Kufanya hivi tutatumia function ya capitalize(). Mafano tuna neno bongoclass lote limeandikwa kwa herufi ndogo. Sasa tunataka kufanya herufi b kuwa B ili kisomeke Bongoclass.
string = 'bongoclass'
capitalized_string = string.capitalize()
print(capitalized_string)
2. Kubadili string yote kuwa katika herufi kubwa. Kufanya hivi tunatumia function ya upper(). Mfano neno letu la awali bongoclass tutalibadilisha kuwa BONGOCLASS.
string = 'bongoclass'
upper_string = string.upper()
print(upper_string)
3. Kujuwa idadi ya character kwenye string. Kufanya hivi tutatumia funvtion ya len(). Mfano neno letu bongoclass hapo tutakwenda kuhesabu ina character ngapi?
string = 'bongoclass'
print(len(string))
4. Kubadilisha sehemu ya string. Kufanya hivi tutatumia replace(). Kwa mfano hapo leno letu bongoclass tunataka liwe bongocare. Sasa function hii ina sehemu kuu 2 yaani parameter 2, ya kwanza ni kipande cha string ambacho unataka kukitoa. Na sehemu ya pili ni kipande cha string ambacho unakwenda kukiweka.
Kipande cha kwanza hapo tutawea class na kipande cha pili tutaweka care
string = 'bongoclass'
replace_string = string.replace('class', 'care')
print(replace_string)
...
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Umeionaje Makala hii.. ?
Katika somo hili tunakwenda kujifunza aina nyingine za data ambazo hutumika kwenye python.
Soma Zaidi...Hapa utajifunza maana ya library, kazi zake aina zake na jinsi ya ku install lirary
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza vipi django inaweza kuwasiliana na database, utajifunza kuusu orm na model
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwend akujifunz akuhusu nadharia ya data abstraction na kazi zake kwenye OOP
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunza maana ya variable, na sheria za kutengeneza variable kwenye python. Pia utajifunza maneno ambayo hayafai kutumiwa kama variable
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwend akujifunza jinsi ya kupokea na kuchakata fomu
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kushughulika na faili, kama ku upload faili kwenye django.
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunza jisni ya kujuwa aina ya data iliyotumika kwenye python
Soma Zaidi...Katika somo hili tutajifunza njia mbili muhimu za kuongeza data kwenye database katika project yetu ya pybongo (app: menu). Njia hizi ni: Kutumia Django Admin Kutumia Django Shell Utafahamu pia jinsi ya kusajili models kwenye admin, jinsi ya kuingia admin panel, na namna ya kutengeneza entries mpya za MenuItem.
Soma Zaidi...