Katika somo hili utakwend akujifunza aina mbalimbali za function ambazo tunaweza kuzitumia kwenye python.
Katika somo hili, tutachambua kwa kina aina za functions kwenye Python. Functions ni msingi muhimu wa programu, zikisaidia kuandaa msimbo ulioratibiwa vizuri na kurahisisha matumizi tena.
Functions zinaweza kugawanywa katika makundi mawili makuu:
Hizi ni functions unazotengeneza mwenyewe kulingana na mahitaji yako. Mfano:
def salamu():
print("Habari ya muda huu!")
salamu()
Hizi ni functions zilizojengwa ndani ya Python, kama vile print(), len(), na nyinginezo. Mfano:
print("Hii ni built-in function.")
Hizi ni functions rahisi zisizohitaji pembejeo wala kurudisha thamani yoyote.
def salamu_bila_kitu():
print("Habari! Hakuna parameter wala return.")
salamu_bila_kitu()
Hizi hupokea pembejeo kutoka kwa mtumiaji lakini hazirudishi thamani.
def jumlisha(x, y):
print(f"Jumla ya {x} na {y} ni: {x + y}")
jumlisha(4, 9)
Hizi hazihitaji pembejeo, lakini hurejesha thamani.
def jumla_bila_input():
x, y = 4, 6
return x + y
print(f"Jumla ni: {jumla_bila_input()}")
Hizi hupokea pembejeo na pia hurejesha thamani.
def eneo(urefu, upana):
return urefu * upana
print(f"Eneo ni: {eneo(6, 8)}")
Anonymous function, pia hujulikana kama lambda, haina jina rasmi na hutumika kwa misimbo rahisi.
Tunapotumia anonymous functions kwenye Python, tunatumia keyword lambda. Hii ni kwa sababu Python haitoi njia nyingine ya kutengeneza functions zisizo na jina moja kwa moja, tofauti na lugha zingine kama Kotlin.
Hapa kuna maelezo ya haraka kuhusu lambda functions kwenye Python:
Haina jina: Ndiyo maana inaitwa "anonymous function".
Rahisi na mfupi: Huandikwa kwa mstari mmoja.
Hutumia neno kuu (lambda): Neno hili linaonyesha tunatengeneza function isiyo na jina.
Hurejesha thamani moja kwa moja: Hakuna haja ya kutumia neno return — jibu la expression linarejeshwa moja kwa moja.
Mfano:
jumlisha = lambda x, y: x + y
print(f"Jumla ni: {jumlisha(4, 6)}")
Lambda pia inaweza kutumika bila parameter:
salamu = lambda: print("Salamu sana!")
salamu()
Tunatumia function kubadili mita kuwa kilomita kwa kugawanya thamani kwa 1000.
def badili_mita_kuwa_km(mita):
return mita / 1000
mita = float(input("Andika mita: "))
print(f"Kilomita: {badili_mita_kuwa_km(mita)}")
badili = lambda mita: mita / 1000
mita = float(input("Andika mita: "))
print(f"Kilomita: {badili(mita)}")
Scope ni wigo ambapo variable au function inaweza kufikiwa.
Variable ikitengenezwa ndani ya function itatumika ndani ya hiyo function tu. Hii inaitwa local variable. Kwa mfano hapo chini endapo uta print variable ujumbe nje ya function utapata error.
def salamu():
ujumbe = "Hujambo"
print(ujumbe)
salamu()
print(ujumbe)
# Hii itatoa error kwa sababu ujumbe haipo nje ya function.
Hii ni variable ambayo itatumika ndani ya function na nje. Variable hii inatengenezwa nje ya function kabla ya kuandika hiyo function. Kwa mfano hapo chini unawez aku print variable ujumbe popote pale.
ujumbe = "Hujambo"
def salamu():
print(ujumbe)
salamu()
print(ujumbe)
Recursive function hujiita yenyewe, mara nyingi hutumika kutatua matatizo kama factorial.
def factorial(n):
return 1 if n <= 1 else n * factorial(n - 1)
print(f"Factorial ya 5 ni: {factorial(5)}")
main() ni sehemu kuu ambapo programu huanza utekelezaji wake. Tutakuja kuzungumzia hapa kwa undani tutakapokuwa tunajifunz akuhusu module.
def main():
print("Karibu kwenye Python!")
if __name__ == "__main__":
main()
Katika somo hili, tumeelewa aina mbalimbali za functions kwenye Python, kutoka kwa zile za kawaida, zenye parameter, zenye return, hadi lambda na recursive. Katika somo linalofuata, tutajifunza matumizi ya kina ya parameters.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Katika somo hili utajifunza maana ya variable, na sheria za kutengeneza variable kwenye python. Pia utajifunza maneno ambayo hayafai kutumiwa kama variable
Soma Zaidi...Katika somo hili tunakwenda kujifunza matumizi ya break na continue kwenye loop
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhsu Template Tag nini na kazi zake. Pia utajifunza sheria za uandishi wake.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunz amaana ya inheritance na sheria za kuiandika inheritance.
Soma Zaidi...Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu string indexing. Kama tulivyojifunza kuhusu namba katika somo lililopita, basi hapa tutakwenda kucheza na string.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwend akujifunz amaana ya module, kazi zake, aina zake na jinsi ya kuandika modile
Soma Zaidi...Katika somo hili tutakwend akujifunza kwa urefu zaidi kuhusu parameter ambazo hutumika kwenye functions
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunz ajinsi ya kusoma mafaili na mitindo mbalimbali ya kusoma data
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza zaidi kuhusu Jinsi ya Kuongeza Kurasa Nyingine Katika Django View
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza kutengeneza htmk form pamoja na kuituma.
Soma Zaidi...