Katika somo hili utakwend akujifunza aina mbalimbali za function ambazo tunaweza kuzitumia kwenye python.
Katika somo hili, tutachambua kwa kina aina za functions kwenye Python. Functions ni msingi muhimu wa programu, zikisaidia kuandaa msimbo ulioratibiwa vizuri na kurahisisha matumizi tena.
Functions zinaweza kugawanywa katika makundi mawili makuu:
Hizi ni functions unazotengeneza mwenyewe kulingana na mahitaji yako. Mfano:
def salamu():
print("Habari ya muda huu!")
salamu()
Hizi ni functions zilizojengwa ndani ya Python, kama vile print(), len(), na nyinginezo. Mfano:
print("Hii ni built-in function.")
Hizi ni functions rahisi zisizohitaji pembejeo wala kurudisha thamani yoyote.
def salamu_bila_kitu():
print("Habari! Hakuna parameter wala return.")
salamu_bila_kitu()
Hizi hupokea pembejeo kutoka kwa mtumiaji lakini hazirudishi thamani.
def jumlisha(x, y):
print(f"Jumla ya {x} na {y} ni: {x + y}")
jumlisha(4, 9)
Hizi hazihitaji pembejeo, lakini hurejesha thamani.
def jumla_bila_input():
x, y = 4, 6
return x + y
print(f"Jumla ni: {jumla_bila_input()}")
Hizi hupokea pembejeo na pia hurejesha thamani.
def eneo(urefu, upana):
return urefu * upana
print(f"Eneo ni: {eneo(6, 8)}")
Anonymous function, pia hujulikana kama lambda, haina jina rasmi na hutumika kwa misimbo rahisi.
Tunapotumia anonymous functions kwenye Python, tunatumia keyword lambda. Hii ni kwa sababu Python haitoi njia nyingine ya kutengeneza functions zisizo na jina moja kwa moja, tofauti na lugha zingine kama Kotlin.
Hapa kuna maelezo ya haraka kuhusu lambda functions kwenye Python:
Haina jina: Ndiyo maana inaitwa "anonymous function".
Rahisi na mfupi: Huandikwa kwa mstari mmoja.
Hutumia neno kuu (lambda): Neno hili linaonyesha tunatengeneza function isiyo na jina.
Hurejesha thamani moja kwa moja: Hakuna haja ya kutumia neno return — jibu la expression linarejeshwa moja kwa moja.
Mfano:
jumlisha = lambda x, y: x + y
print(f"Jumla ni: {jumlisha(4, 6)}")
Lambda pia inaweza kutumika bila parameter:
salamu = lambda: print("Salamu sana!")
salamu()
Tunatumia function kubadili mita kuwa kilomita kwa kugawanya thamani kwa 1000.
def badili_mita_kuwa_km(mita):
return mita / 1000
mita = float(input("Andika mita: "))
print(f"Kilomita: {badili_mita_kuwa_km(mita)}")
badili = lambda mita: mita / 1000
mita = float(input("Andika mita: "))
print(f"Kilomita: {badili(mita)}")
Scope ni wigo ambapo variable au function inaweza kufikiwa.
Variable ikitengenezwa ndani ya function itatumika ndani ya hiyo function tu. Hii inaitwa local variable. Kwa mfano hapo chini endapo uta print variable ujumbe nje ya function utapata error.
def salamu():
ujumbe = "Hujambo"
print(ujumbe)
salamu()
print(ujumbe)
# Hii itatoa error kwa sababu ujumbe haipo nje ya function.
Hii ni variable ambayo itatumika ndani ya function na nje. Variable hii inatengenezwa nje ya function kabla ya kuandika hiyo function. Kwa mfano hapo chini unawez aku print variable ujumbe popote pale.
ujumbe = "Hujambo"
def salamu():
print(ujumbe)
salamu()
print(ujumbe)
Recursive function hujiita yenyewe, mara nyingi hutumika kutatua matatizo kama factorial.
def factorial(n):
return 1 if n <= 1 else n * factorial(n - 1)
print(f"Factorial ya 5 ni: {factorial(5)}")
main() ni sehemu kuu ambapo programu huanza utekelezaji wake. Tutakuja kuzungumzia hapa kwa undani tutakapokuwa tunajifunz akuhusu module.
def main():
print("Karibu kwenye Python!")
if __name__ == "__main__":
main()
Katika somo hili, tumeelewa aina mbalimbali za functions kwenye Python, kutoka kwa zile za kawaida, zenye parameter, zenye return, hadi lambda na recursive. Katika somo linalofuata, tutajifunza matumizi ya kina ya parameters.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Umeionaje Makala hii.. ?
Katika somo hili utajifunz akutumia database kwenye python
Soma Zaidi...Katika somo hili tutakwend akuziona aina za condition statement kwneye python na jinsi ya kuzitumia
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwend akujifunza jinsi ya kuandika function, kuweka parameter na kuitumia function
Soma Zaidi...Katika somo hili tutaangalia jinsi ya kutengeneza fomu ya HTML kwa ajili ya kuingiza data kwenye jedwali la MenuItem, pamoja na kutengeneza view itakayopokea data hiyo na kuihifadhi kwenye database. Pia tutaunganisha form na URL route.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujfunza operator nyingine kama assignment operator logical, identity operator na membership operator.
Soma Zaidi...Hapa utajifunza maana ya library, kazi zake aina zake na jinsi ya ku install lirary
Soma Zaidi...Somo hili linazungumzia hatua ya kuunda navigation menu na kutumia template inheritance kwa njia ya kitaalamu katika Django.
Soma Zaidi...Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu string indexing. Kama tulivyojifunza kuhusu namba katika somo lililopita, basi hapa tutakwenda kucheza na string.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwend akujifunz ajinsi ya kutumia html kwneye python
Soma Zaidi...Hapa utakwenda kujifunz amaana ya package, aina zake na jinsi ya kuandika package.
Soma Zaidi...