Python somo la 19: Aina za Function

Katika somo hili utakwend akujifunza aina mbalimbali za function ambazo tunaweza kuzitumia kwenye python.

Aina za Functions kwenye Python

Katika somo hili, tutachambua kwa kina aina za functions kwenye Python. Functions ni msingi muhimu wa programu, zikisaidia kuandaa msimbo ulioratibiwa vizuri na kurahisisha matumizi tena.

 


 

Aina Kuu za Functions

Functions zinaweza kugawanywa katika makundi mawili makuu:

1. User-defined Functions

Hizi ni functions unazotengeneza mwenyewe kulingana na mahitaji yako. Mfano:

 

def salamu():

    print("Habari ya muda huu!")

    

salamu()

 

2. Built-in Functions

Hizi ni functions zilizojengwa ndani ya Python, kama vile print(), len(), na nyinginezo. Mfano:

print("Hii ni built-in function.")

 

 


 

Aina za Functions kulingana na Parameter na Return Type

1. Functions zisizo na Parameter wala Return

Hizi ni functions rahisi zisizohitaji pembejeo wala kurudisha thamani yoyote.

def salamu_bila_kitu():

    print("Habari! Hakuna parameter wala return.")

salamu_bila_kitu()

 

 


 

2. Functions zenye Parameter bila Return

Hizi hupokea pembejeo kutoka kwa mtumiaji lakini hazirudishi thamani.

def jumlisha(x, y):

    print(f"Jumla ya {x} na {y} ni: {x + y}")

 

jumlisha(4, 9)

 

 


 

3. Functions zisizo na Parameter lakini zenye Return

Hizi hazihitaji pembejeo, lakini hurejesha thamani.

 

def jumla_bila_input():

    x, y = 4, 6

    return x + y

 

print(f"Jumla ni: {jumla_bila_input()}")

 

 


 

4. Functions zenye Parameter na Return

Hizi hupokea pembejeo na pia hurejesha thamani.

 

def eneo(urefu, upana):

    return urefu * upana

 

print(f"Eneo ni: {eneo(6, 8)}")

 

 


 

Anonymous Functions (Lambda)

Anonymous function, pia hujulikana kama lambda, haina jina rasmi na hutumika kwa misimbo rahisi. 

Tunapotumia anonymous functions kwenye Python, tunatumia keyword lambda. Hii ni kwa sababu Python haitoi njia nyingine ya kutengeneza functions zisizo na jina moja kwa moja, tofauti na lugha zingine kama Kotlin.

Hapa kuna maelezo ya haraka kuhusu lambda functions kwenye Python:

 

Sifa za Lambda Functions

  1. Haina jina: Ndiyo maana inaitwa "anonymous function".

  2. Rahisi na mfupi: Huandikwa kwa mstari mmoja.

  3. Hutumia neno kuu (lambda): Neno hili linaonyesha tunatengeneza function isiyo na jina.

  4. Hurejesha thamani moja kwa moja: Hakuna haja ya kutumia neno return — jibu la expression linarejeshwa moja kwa moja.

 

Mfano:

jumlisha = lambda x, y: x + y

print(f"Jumla ni: {jumlisha(4, 6)}")

 

Lambda pia inaweza kutumika bila parameter:

salamu = lambda: print("Salamu sana!")

salamu()

 

 


 

Programu ya Kubadili Mita kuwa Kilomita

Tunatumia function kubadili mita kuwa kilomita kwa kugawanya thamani kwa 1000.

Programu ya kawaida:

 

def badili_mita_kuwa_km(mita):

    return mita / 1000

 

mita = float(input("Andika mita: "))

print(f"Kilomita: {badili_mita_kuwa_km(mita)}")

 

Lambda Function:

 

badili = lambda mita: mita / 1000

 

mita = float(input("Andika mita: "))

print(f"Kilomita: {badili(mita)}")

 

 


 

Scope katika Python

Scope ni wigo ambapo variable au function inaweza kufikiwa.

Variable ndani ya function (Local Scope):

Variable ikitengenezwa ndani ya function itatumika ndani ya hiyo function tu. Hii inaitwa local variable. Kwa mfano hapo chini endapo uta print variable ujumbe nje ya function utapata error.

def salamu():

    ujumbe = "Hujambo"

    print(ujumbe)

 

salamu()

print(ujumbe)  

# Hii itatoa error kwa sababu ujumbe haipo nje ya function.



Variable ya kimataifa (Global Scope):

Hii ni variable ambayo itatumika ndani ya function na nje. Variable hii inatengenezwa nje ya function kabla ya kuandika hiyo function. Kwa mfano hapo chini unawez aku print variable ujumbe popote pale.

 

ujumbe = "Hujambo"

 

def salamu():

    print(ujumbe)

 

salamu()

print(ujumbe)

 

 


 

Recursive Functions

Recursive function hujiita yenyewe, mara nyingi hutumika kutatua matatizo kama factorial.

 

def factorial(n):

    return 1 if n <= 1 else n * factorial(n - 1)

 

print(f"Factorial ya 5 ni: {factorial(5)}")

 

 


 

Main Function

main() ni sehemu kuu ambapo programu huanza utekelezaji wake. Tutakuja kuzungumzia hapa kwa undani tutakapokuwa tunajifunz akuhusu module.

 

def main():

    print("Karibu kwenye Python!")

 

if __name__ == "__main__":

    main()

 

 


 

Hitimisho

Katika somo hili, tumeelewa aina mbalimbali za functions kwenye Python, kutoka kwa zile za kawaida, zenye parameter, zenye return, hadi lambda na recursive. Katika somo linalofuata, tutajifunza matumizi ya kina ya parameters.

 

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Python Main: ICT File: Download PDF Views 141

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Madrasa kiganjani    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

Python somo la 18: Jinsi ya kuandika function

Katika somo hili utakwend akujifunza jinsi ya kuandika function, kuweka parameter na kuitumia function

Soma Zaidi...
PYTHON - somo la 1: Jinsi ya ku install python

Katika somo hili utajifunza kuhusu maana ya python na kazi zake. pia jinsi ya kuandaa kifaa chako kwa ajili ya somo.

Soma Zaidi...
Python somo la 24: Nini maana ya Object Oriented Programming

Hapa tunakwenda kujifunza kuhusu OOP ambapo ni miongoni mwa mitindo ya uandishi wa code

Soma Zaidi...
Python somo la 13: Kutumia condition statement - if, else, elif

Katika somo hili tutakwend akuziona aina za condition statement kwneye python na jinsi ya kuzitumia

Soma Zaidi...
Python somo la 29: Encaosulation kwneye python

Katika somo hili utajifunza maana ya encapsulation na sheria za uandishi wake

Soma Zaidi...
Python somo la 25: Sheria za uandishi wa class

Katika somo hili utajifunza maana ya class, sheria za uandishi wake na mifano halisi

Soma Zaidi...
Python somo la 22: Package kwenye Python

Hapa utakwenda kujifunz amaana ya package, aina zake na jinsi ya kuandika package.

Soma Zaidi...
Python somo la 16: Jinsi ya kutumia break na continue kwenye loop

Katika somo hili tunakwenda kujifunza matumizi ya break na continue kwenye loop

Soma Zaidi...
PYTHON - somo la 9: indexing katika strinfg

Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu string indexing. Kama tulivyojifunza kuhusu namba katika somo lililopita, basi hapa tutakwenda kucheza na string.

Soma Zaidi...
PYTHON - somo la 10: string method na zinavyofanya kazi

Katika somo hili utakwenda kujfnza kuhusu string method nyinginezo. Katika somo lililopita tulijifunza kuhusu string indexing.

Soma Zaidi...