Katika somo hili utakwend akujifunza aina mbalimbali za function ambazo tunaweza kuzitumia kwenye python.
Katika somo hili, tutachambua kwa kina aina za functions kwenye Python. Functions ni msingi muhimu wa programu, zikisaidia kuandaa msimbo ulioratibiwa vizuri na kurahisisha matumizi tena.
Functions zinaweza kugawanywa katika makundi mawili makuu:
Hizi ni functions unazotengeneza mwenyewe kulingana na mahitaji yako. Mfano:
def salamu():
print("Habari ya muda huu!")
salamu()
Hizi ni functions zilizojengwa ndani ya Python, kama vile print(), len(), na nyinginezo. Mfano:
print("Hii ni built-in function.")
Hizi ni functions rahisi zisizohitaji pembejeo wala kurudisha thamani yoyote.
def salamu_bila_kitu():
print("Habari! Hakuna parameter wala return.")
salamu_bila_kitu()
Hizi hupokea pembejeo kutoka kwa mtumiaji lakini hazirudishi thamani.
def jumlisha(x, y):
print(f"Jumla ya {x} na {y} ni: {x + y}")
jumlisha(4, 9)
Hizi hazihitaji pembejeo, lakini hurejesha thamani.
def jumla_bila_input():
x, y = 4, 6
return x + y
print(f"Jumla ni: {jumla_bila_input()}")
Hizi hupokea pembejeo na pia hurejesha thamani.
def eneo(urefu, upana):
return urefu * upana
print(f"Eneo ni: {eneo(6, 8)}")
Anonymous function, pia hujulikana kama lambda, haina jina rasmi na hutumika kwa misimbo rahisi.
Tunapotumia anonymous functions kwenye Python, tunatumia keyword lambda. Hii ni kwa sababu Python haitoi njia nyingine ya kutengeneza functions zisizo na jina moja kwa moja, tofauti na lugha zingine kama Kotlin.
Hapa kuna maelezo ya haraka kuhusu lambda functions kwenye Python:
Haina jina: Ndiyo maana inaitwa "anonymous function".
Rahisi na mfupi: Huandikwa kwa mstari mmoja.
Hutumia neno kuu (lambda): Neno hili linaonyesha tunatengeneza function isiyo na jina.
Hurejesha thamani moja kwa moja: Hakuna haja ya kutumia neno return — jibu la expression linarejeshwa moja kwa moja.
Mfano:
jumlisha = lambda x, y: x + y
print(f"Jumla ni: {jumlisha(4, 6)}")
Lambda pia inaweza kutumika bila parameter:
salamu = lambda: print("Salamu sana!")
salamu()
Tunatumia function kubadili mita kuwa kilomita kwa kugawanya thamani kwa 1000.
def badili_mita_kuwa_km(mita):
return mita / 1000
mita = float(input("Andika mita: "))
print(f"Kilomita: {badili_mita_kuwa_km(mita)}")
badili = lambda mita: mita / 1000
mita = float(input("Andika mita: "))
print(f"Kilomita: {badili(mita)}")
Scope ni wigo ambapo variable au function inaweza kufikiwa.
Variable ikitengenezwa ndani ya function itatumika ndani ya hiyo function tu. Hii inaitwa local variable. Kwa mfano hapo chini endapo uta print variable ujumbe nje ya function utapata error.
def salamu():
ujumbe = "Hujambo"
print(ujumbe)
salamu()
print(ujumbe)
# Hii itatoa error kwa sababu ujumbe haipo nje ya function.
Hii ni variable ambayo itatumika ndani ya function na nje. Variable hii inatengenezwa nje ya function kabla ya kuandika hiyo function. Kwa mfano hapo chini unawez aku print variable ujumbe popote pale.
ujumbe = "Hujambo"
def salamu():
print(ujumbe)
salamu()
print(ujumbe)
Recursive function hujiita yenyewe, mara nyingi hutumika kutatua matatizo kama factorial.
def factorial(n):
return 1 if n <= 1 else n * factorial(n - 1)
print(f"Factorial ya 5 ni: {factorial(5)}")
main() ni sehemu kuu ambapo programu huanza utekelezaji wake. Tutakuja kuzungumzia hapa kwa undani tutakapokuwa tunajifunz akuhusu module.
def main():
print("Karibu kwenye Python!")
if __name__ == "__main__":
main()
Katika somo hili, tumeelewa aina mbalimbali za functions kwenye Python, kutoka kwa zile za kawaida, zenye parameter, zenye return, hadi lambda na recursive. Katika somo linalofuata, tutajifunza matumizi ya kina ya parameters.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowKatika somo hili utajifunza maana ya encapsulation na sheria za uandishi wake
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunza maana ya class, sheria za uandishi wake na mifano halisi
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunz ajinsi ya kutengeneza folda, faili na kuweka data kwneye faili
Soma Zaidi...Katika somo hili tunakwenda kujifunza aina nyingine za data ambazo hutumika kwenye python.
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunza jisni ya kujuwa aina ya data iliyotumika kwenye python
Soma Zaidi...Katika somo hili uatkwenda kujifunz anamna ambavyo mtu anaweza kuingiza input kwneye system
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwend akujifunz akuhusu nadharia ya data abstraction na kazi zake kwenye OOP
Soma Zaidi...Hapa tunakwenda kujifunza kuhusu OOP ambapo ni miongoni mwa mitindo ya uandishi wa code
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujfnza kuhusu string method nyinginezo. Katika somo lililopita tulijifunza kuhusu string indexing.
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunza kuhusu maana ya python na kazi zake. pia jinsi ya kuandaa kifaa chako kwa ajili ya somo.
Soma Zaidi...