Python somo la 15: Jinsi ya kutumia while loop
Katika somo hili tutakwend akujifunza jinsi ya kutumia while loop kwneye python
Jinsi ya Kutumia while loop na do while loop katika Python
Katika somo hili, tutajifunza jinsi ya kutumia while loop na do while loop katika Python. Loop hizi hutumika kurudia utekelezaji wa code kulingana na masharti yaliyowekwa. Tofauti yao kuu ni jinsi wanavyoanza utekelezaji.
1. While Loop
While loop hutumika pale ambapo hatujui idadi ya marudio, lakini tunataka code iendelee kurudiwa mradi sharti fulani limetimia.
Muundo wa while loop:
while condition:
# Code ya kurudiwa
# Increment/Decrement
Mfano 1: Kuonyesha Orodha ya Namba
print("ORODHA YA NAMBA")
x = 1
print(x)
while x < 12:
x += 1
print(x)
Mfano 2: Kutengeneza Tebo ya 7
Hapa tutazidisha namba 7 kwa kila namba kuanzia 1 hadi 12.
print("TEBO YA 7")
x = 1
while x <= 12:
print(f"{x} * 7 = {x * 7}")
x += 1
2. Do-While Loop
Python haina do while loop kama ilivyo katika lugha kama Kotlin, lakini tunaweza kuunda dhana sawa kwa kutumia while loop pamoja na break. Katika do while loop, code huanza kutekelezwa mara moja hata kama sharti halijatimia, kisha sharti linakaguliwa. Tutajifunz akuhusu break na continue katika somo linalofuata.
Tofauti Kuu Kati ya while loop na do while loop:
-
While loop: Sharti hukaguliwa kwanza kabla ya code kutekelezwa. -
Do while loop: Code hutekelezwa angalau mara moja kabla ya sharti kukaguliwa.
Hitimisho
Katika somo hili, umejifunza jinsi ya kutumia while loop na jinsi ya kuunda do while loop katika Python. Unaweza kufanyia mazoezi kwa kubuni mifano yako, kama vile kuhesabu namba hata, kuunda jedwali la kuzidisha kwa namba nyingine, au kuonyesha orodha maalum.
Somo linalofuata: Tutaangazia jinsi ya kutumia break na continue kwenye loop ili kudhibiti mtiririko wa utekelezaji. Endelea kufanya mazoezi!
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game 👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉4 web hosting 👉5 kitabu cha Simulizi 👉6 Madrasa kiganjani
Post zinazofanana:
Python somo la 52: Kutengeneza table na kufanya Migrations Katika Django
Katika somo hili tutajifunza jinsi Django hutumia migrations kuunda na kubadilisha tables kwenye database kulingana na models tunazoandika. Tutapitia maana ya migration, hatua za kuitumia, umuhimu wake, misingi ya makemigrations na migrate, pamoja na mfano halisi kutoka kwenye project yetu ya pybongo (app: menu).
Soma Zaidi...PYHON - somo la 5: Aina za data list, turple, dictionary na boolean
Katika somo hili tunakwenda kujifunza aina nyingine za data ambazo hutumika kwenye python.
Soma Zaidi...Python somo la 20: Aina za parameter kwenye function
Katika somo hili tutakwend akujifunza kwa urefu zaidi kuhusu parameter ambazo hutumika kwenye functions
Soma Zaidi...Python somo la 35: Jinsi ya kutumia MYSQL kwenye python
Katika somo hili utajifunz akutumia database kwenye python
Soma Zaidi...PYTHON - somo la 10: string method na zinavyofanya kazi
Katika somo hili utakwenda kujfnza kuhusu string method nyinginezo. Katika somo lililopita tulijifunza kuhusu string indexing.
Soma Zaidi...Python somo la 49: Jinsi ya ku host project ya Django
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya ku host website ya Django. Hapa tutakwenda kutuma plaform ya pythonanywhere.com.
Soma Zaidi...