picha

Python somo la 15: Jinsi ya kutumia while loop

Katika somo hili tutakwend akujifunza jinsi ya kutumia while loop kwneye python

Jinsi ya Kutumia while loop na do while loop katika Python

Katika somo hili, tutajifunza jinsi ya kutumia while loop na do while loop katika Python. Loop hizi hutumika kurudia utekelezaji wa code kulingana na masharti yaliyowekwa. Tofauti yao kuu ni jinsi wanavyoanza utekelezaji.

 


 

1. While Loop

While loop hutumika pale ambapo hatujui idadi ya marudio, lakini tunataka code iendelee kurudiwa mradi sharti fulani limetimia.

Muundo wa while loop:

while condition:

    # Code ya kurudiwa

    # Increment/Decrement

 

Mfano 1: Kuonyesha Orodha ya Namba

 

print("ORODHA YA NAMBA")

x = 1

print(x)

 

while x < 12:

    x += 1

    print(x)

 

Mfano 2: Kutengeneza Tebo ya 7

Hapa tutazidisha namba 7 kwa kila namba kuanzia 1 hadi 12.

print("TEBO YA 7")

x = 1

 

while x <= 12:

    print(f"{x} * 7 = {x * 7}")

    x += 1

 

 


 

2. Do-While Loop

Python haina do while loop kama ilivyo katika lugha kama Kotlin, lakini tunaweza kuunda dhana sawa kwa kutumia while loop pamoja na break. Katika do while loop, code huanza kutekelezwa mara moja hata kama sharti halijatimia, kisha sharti linakaguliwa. Tutajifunz akuhusu break na continue katika somo linalofuata.

 


 

Tofauti Kuu Kati ya while loop na do while loop:

 


 

Hitimisho

Katika somo hili, umejifunza jinsi ya kutumia while loop na jinsi ya kuunda do while loop katika Python. Unaweza kufanyia mazoezi kwa kubuni mifano yako, kama vile kuhesabu namba hata, kuunda jedwali la kuzidisha kwa namba nyingine, au kuonyesha orodha maalum.

Somo linalofuata: Tutaangazia jinsi ya kutumia break na continue kwenye loop ili kudhibiti mtiririko wa utekelezaji. Endelea kufanya mazoezi!

 

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-11-22 12:26:37 Topic: Python Main: Masomo File: Download PDF Views 1077

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉3 Simulizi za Hadithi Audio     👉4 Madrasa kiganjani     👉5 Kitabu cha Afya     👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    

Post zinazofanana:

Python somo la 45: Kutumia Loops na Conditions katika Django Templates

Katika somo hili utakwend akujifunza kuchakata data kwa Kutumia Loops na Conditions katika Django Templates

Soma Zaidi...
Python somo la 33: Jinsi ya kupata taarifa za faili

Katika somo hili utakwend akujifunz anamna ya kuwez akupata taarifa zinazohusu faili

Soma Zaidi...
Python somo la 37: Jinsi ya ku install Django na kutengeneza project na app

Katika somo ili utajifunza hatuwa kwa hatuwa za ku install Django, kutengeneza project na kutengeneza app

Soma Zaidi...
Python somo la 23: Library kwenye python

Hapa utajifunza maana ya library, kazi zake aina zake na jinsi ya ku install lirary

Soma Zaidi...
Python somo la 54: Jinsi ya Kusoma Data Kutoka Database kwenye Django

Katika somo hili tutajifunza namna ya kusoma data kutoka kwenye database kupitia Django ORM, jinsi ya kuzipeleka kwenye view, na jinsi ya kuzionyesha kwenye HTML template.

Soma Zaidi...
PYTHON - somo la 10: string method na zinavyofanya kazi

Katika somo hili utakwenda kujfnza kuhusu string method nyinginezo. Katika somo lililopita tulijifunza kuhusu string indexing.

Soma Zaidi...