picha

Python somo la 15: Jinsi ya kutumia while loop

Katika somo hili tutakwend akujifunza jinsi ya kutumia while loop kwneye python

Jinsi ya Kutumia while loop na do while loop katika Python

Katika somo hili, tutajifunza jinsi ya kutumia while loop na do while loop katika Python. Loop hizi hutumika kurudia utekelezaji wa code kulingana na masharti yaliyowekwa. Tofauti yao kuu ni jinsi wanavyoanza utekelezaji.

 


 

1. While Loop

While loop hutumika pale ambapo hatujui idadi ya marudio, lakini tunataka code iendelee kurudiwa mradi sharti fulani limetimia.

Muundo wa while loop:

while condition:

    # Code ya kurudiwa

    # Increment/Decrement

 

Mfano 1: Kuonyesha Orodha ya Namba

 

print("ORODHA YA NAMBA")

x = 1

print(x)

 

while x < 12:

    x += 1

    print(x)

 

Mfano 2: Kutengeneza Tebo ya 7

Hapa tutazidisha namba 7 kwa kila namba kuanzia 1 hadi 12.

print("TEBO YA 7")

x = 1

 

while x <= 12:

    print(f"{x} * 7 = {x * 7}")

    x += 1

 

 


 

2. Do-While Loop

Python haina do while loop kama ilivyo katika lugha kama Kotlin, lakini tunaweza kuunda dhana sawa kwa kutumia while loop pamoja na break. Katika do while loop, code huanza kutekelezwa mara moja hata kama sharti halijatimia, kisha sharti linakaguliwa. Tutajifunz akuhusu break na continue katika somo linalofuata.

 


 

Tofauti Kuu Kati ya while loop na do while loop:

 


 

Hitimisho

Katika somo hili, umejifunza jinsi ya kutumia while loop na jinsi ya kuunda do while loop katika Python. Unaweza kufanyia mazoezi kwa kubuni mifano yako, kama vile kuhesabu namba hata, kuunda jedwali la kuzidisha kwa namba nyingine, au kuonyesha orodha maalum.

Somo linalofuata: Tutaangazia jinsi ya kutumia break na continue kwenye loop ili kudhibiti mtiririko wa utekelezaji. Endelea kufanya mazoezi!

 

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-11-22 12:26:37 Topic: Python Main: Masomo File: Download PDF Views 976

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 web hosting     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Dua za Mitume na Manabii     👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉6 Kitau cha Fiqh    

Post zinazofanana:

Python somo la 18: Jinsi ya kuandika function

Katika somo hili utakwend akujifunza jinsi ya kuandika function, kuweka parameter na kuitumia function

Soma Zaidi...
PYTHON - somo la 10: string method na zinavyofanya kazi

Katika somo hili utakwenda kujfnza kuhusu string method nyinginezo. Katika somo lililopita tulijifunza kuhusu string indexing.

Soma Zaidi...
Python somo 57: Matumizi ya Python shell

Katika somo hili, tutajifunza: Maana ya Python shell na umuhimu wake. Tofauti kati ya shell na terminal ya kawaida. Matumizi ya shell, hususan kwenye Django. Amri muhimu zaidi za Python shell, zilizotokana na models na views zako za pybongo.

Soma Zaidi...
Python somo la 24: Nini maana ya Object Oriented Programming

Hapa tunakwenda kujifunza kuhusu OOP ambapo ni miongoni mwa mitindo ya uandishi wa code

Soma Zaidi...
Python somo la 20: Aina za parameter kwenye function

Katika somo hili tutakwend akujifunza kwa urefu zaidi kuhusu parameter ambazo hutumika kwenye functions

Soma Zaidi...
Python somo la 40: Jinsi ya Kuunda Simple Navigation Menu Katika Django

Katika somo hili utajifunza Jinsi ya Kuunda Simple Navigation Menu Katika Django kwa kutumia template

Soma Zaidi...