picha

Python somo la 15: Jinsi ya kutumia while loop

Katika somo hili tutakwend akujifunza jinsi ya kutumia while loop kwneye python

Jinsi ya Kutumia while loop na do while loop katika Python

Katika somo hili, tutajifunza jinsi ya kutumia while loop na do while loop katika Python. Loop hizi hutumika kurudia utekelezaji wa code kulingana na masharti yaliyowekwa. Tofauti yao kuu ni jinsi wanavyoanza utekelezaji.

 


 

1. While Loop

While loop hutumika pale ambapo hatujui idadi ya marudio, lakini tunataka code iendelee kurudiwa mradi sharti fulani limetimia.

Muundo wa while loop:

while condition:

    # Code ya kurudiwa

    # Increment/Decrement

 

Mfano 1: Kuonyesha Orodha ya Namba

 

print("ORODHA YA NAMBA")

x = 1

print(x)

 

while x < 12:

    x += 1

    print(x)

 

Mfano 2: Kutengeneza Tebo ya 7

Hapa tutazidisha namba 7 kwa kila namba kuanzia 1 hadi 12.

print("TEBO YA 7")

x = 1

 

while x <= 12:

    print(f"{x} * 7 = {x * 7}")

    x += 1

 

 


 

2. Do-While Loop

Python haina do while loop kama ilivyo katika lugha kama Kotlin, lakini tunaweza kuunda dhana sawa kwa kutumia while loop pamoja na break. Katika do while loop, code huanza kutekelezwa mara moja hata kama sharti halijatimia, kisha sharti linakaguliwa. Tutajifunz akuhusu break na continue katika somo linalofuata.

 


 

Tofauti Kuu Kati ya while loop na do while loop:

 


 

Hitimisho

Katika somo hili, umejifunza jinsi ya kutumia while loop na jinsi ya kuunda do while loop katika Python. Unaweza kufanyia mazoezi kwa kubuni mifano yako, kama vile kuhesabu namba hata, kuunda jedwali la kuzidisha kwa namba nyingine, au kuonyesha orodha maalum.

Somo linalofuata: Tutaangazia jinsi ya kutumia break na continue kwenye loop ili kudhibiti mtiririko wa utekelezaji. Endelea kufanya mazoezi!

 

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-11-22 12:26:37 Topic: Python Main: Masomo File: Download PDF Views 942

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
πŸ‘‰1 Madrasa kiganjani     πŸ‘‰2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     πŸ‘‰3 ai web app     πŸ‘‰4 web hosting     πŸ‘‰5 kitabu cha Simulizi     πŸ‘‰6 Kitau cha Fiqh    

Post zinazofanana:

Python somo la 62 Kupakia picha (upload) na kuisoma kutoka kwenye database

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kushughulika na faili, kama ku upload faili kwenye django.

Soma Zaidi...
Python somo la 60: Hashing na Encryption kwenye Django

Katika somo hili tutajifunza: Tofauti kati ya hashing na encryption Jinsi ya kufunga packages muhimu Jinsi ya kufanya hashing kwa maneno ya kawaida (mfano β€œbongoclass”) Jinsi ya kufanya encryption na decrypt kutumia Fernet Jinsi Django inahash password kupitia User model Mazoezi ya vitendo

Soma Zaidi...
Python somo la 39: Jinsi ya Kuongeza Kurasa Nyingine Katika Django View

Katika somo hili utakwenda kujifunza zaidi kuhusu Jinsi ya Kuongeza Kurasa Nyingine Katika Django View

Soma Zaidi...
Python somo la 33: Jinsi ya kupata taarifa za faili

Katika somo hili utakwend akujifunz anamna ya kuwez akupata taarifa zinazohusu faili

Soma Zaidi...
Python somo la 19: Aina za Function

Katika somo hili utakwend akujifunza aina mbalimbali za function ambazo tunaweza kuzitumia kwenye python.

Soma Zaidi...