Python somo la 15: Jinsi ya kutumia while loop
Katika somo hili tutakwend akujifunza jinsi ya kutumia while loop kwneye python
Jinsi ya Kutumia while loop na do while loop katika Python
Katika somo hili, tutajifunza jinsi ya kutumia while loop na do while loop katika Python. Loop hizi hutumika kurudia utekelezaji wa code kulingana na masharti yaliyowekwa. Tofauti yao kuu ni jinsi wanavyoanza utekelezaji.
1. While Loop
While loop hutumika pale ambapo hatujui idadi ya marudio, lakini tunataka code iendelee kurudiwa mradi sharti fulani limetimia.
Muundo wa while loop:
while condition:
# Code ya kurudiwa
# Increment/Decrement
Mfano 1: Kuonyesha Orodha ya Namba
print("ORODHA YA NAMBA")
x = 1
print(x)
while x < 12:
x += 1
print(x)
Mfano 2: Kutengeneza Tebo ya 7
Hapa tutazidisha namba 7 kwa kila namba kuanzia 1 hadi 12.
print("TEBO YA 7")
x = 1
while x <= 12:
print(f"{x} * 7 = {x * 7}")
x += 1
2. Do-While Loop
Python haina do while loop kama ilivyo katika lugha kama Kotlin, lakini tunaweza kuunda dhana sawa kwa kutumia while loop pamoja na break. Katika do while loop, code huanza kutekelezwa mara moja hata kama sharti halijatimia, kisha sharti linakaguliwa. Tutajifunz akuhusu break na continue katika somo linalofuata.
Tofauti Kuu Kati ya while loop na do while loop:
-
While loop: Sharti hukaguliwa kwanza kabla ya code kutekelezwa. -
Do while loop: Code hutekelezwa angalau mara moja kabla ya sharti kukaguliwa.
Hitimisho
Katika somo hili, umejifunza jinsi ya kutumia while loop na jinsi ya kuunda do while loop katika Python. Unaweza kufanyia mazoezi kwa kubuni mifano yako, kama vile kuhesabu namba hata, kuunda jedwali la kuzidisha kwa namba nyingine, au kuonyesha orodha maalum.
Somo linalofuata: Tutaangazia jinsi ya kutumia break na continue kwenye loop ili kudhibiti mtiririko wa utekelezaji. Endelea kufanya mazoezi!
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 Madrasa kiganjani π2 Bongolite - Game zone - Play free game π3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) π4 Dua za Mitume na Manabii π5 kitabu cha Simulizi π6 Simulizi za Hadithi Audio
Post zinazofanana:
Python somo la 62 Kupakia picha (upload) na kuisoma kutoka kwenye database
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kushughulika na faili, kama ku upload faili kwenye django.
Soma Zaidi...Python somo la 19: Aina za Function
Katika somo hili utakwend akujifunza aina mbalimbali za function ambazo tunaweza kuzitumia kwenye python.
Soma Zaidi...Python somo la 37: Jinsi ya ku install Django na kutengeneza project na app
Katika somo ili utajifunza hatuwa kwa hatuwa za ku install Django, kutengeneza project na kutengeneza app
Soma Zaidi...Python somo la 59: Kufanya Mahesabu (Aggregations) Katika Django
Katika somo hili tutajifunza jinsi ya kutumia Django ORM kufanya mahesabu mbalimbali kama Sum, Avg, Count, Max, Min, pamoja na kupunguza idadi ya items zinazoonekana kwenye dashboard (LIMIT). Pia tutajifunza namna ya kutengeneza βdifferenceβ kati ya thamani kubwa na ndogo bila kubadilisha functions zozote ulizokwisha ziandika.
Soma Zaidi...PYTHON somo la 11: Matumizi ya comperison eperator katika python
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu operator. Hasa hapa tutakwend akujifunz akuhusu comparison operaor.
Soma Zaidi...Python somo la 40: Jinsi ya Kuunda Simple Navigation Menu Katika Django
Katika somo hili utajifunza Jinsi ya Kuunda Simple Navigation Menu Katika Django kwa kutumia template
Soma Zaidi...