picha

Python somo la 15: Jinsi ya kutumia while loop

Katika somo hili tutakwend akujifunza jinsi ya kutumia while loop kwneye python

Jinsi ya Kutumia while loop na do while loop katika Python

Katika somo hili, tutajifunza jinsi ya kutumia while loop na do while loop katika Python. Loop hizi hutumika kurudia utekelezaji wa code kulingana na masharti yaliyowekwa. Tofauti yao kuu ni jinsi wanavyoanza utekelezaji.

 


 

1. While Loop

While loop hutumika pale ambapo hatujui idadi ya marudio, lakini tunataka code iendelee kurudiwa mradi sharti fulani limetimia.

Muundo wa while loop:

while condition:

    # Code ya kurudiwa

    # Increment/Decrement

 

Mfano 1: Kuonyesha Orodha ya Namba

 

print("ORODHA YA NAMBA")

x = 1

print(x)

 

while x < 12:

    x += 1

    print(x)

 

Mfano 2: Kutengeneza Tebo ya 7

Hapa tutazidisha namba 7 kwa kila namba kuanzia 1 hadi 12.

print("TEBO YA 7")

x = 1

 

while x <= 12:

    print(f"{x} * 7 = {x * 7}")

    x += 1

 

 


 

2. Do-While Loop

Python haina do while loop kama ilivyo katika lugha kama Kotlin, lakini tunaweza kuunda dhana sawa kwa kutumia while loop pamoja na break. Katika do while loop, code huanza kutekelezwa mara moja hata kama sharti halijatimia, kisha sharti linakaguliwa. Tutajifunz akuhusu break na continue katika somo linalofuata.

 


 

Tofauti Kuu Kati ya while loop na do while loop:

 


 

Hitimisho

Katika somo hili, umejifunza jinsi ya kutumia while loop na jinsi ya kuunda do while loop katika Python. Unaweza kufanyia mazoezi kwa kubuni mifano yako, kama vile kuhesabu namba hata, kuunda jedwali la kuzidisha kwa namba nyingine, au kuonyesha orodha maalum.

Somo linalofuata: Tutaangazia jinsi ya kutumia break na continue kwenye loop ili kudhibiti mtiririko wa utekelezaji. Endelea kufanya mazoezi!

 

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-11-22 12:26:37 Topic: Python Main: Masomo File: Download PDF Views 1134

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Dua za Mitume na Manabii     👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Kitabu cha Afya     👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉6 Kitau cha Fiqh    

Post zinazofanana:

Python somo la 20: Aina za parameter kwenye function

Katika somo hili tutakwend akujifunza kwa urefu zaidi kuhusu parameter ambazo hutumika kwenye functions

Soma Zaidi...
Python somo la 35: Jinsi ya kutumia MYSQL kwenye python

Katika somo hili utajifunz akutumia database kwenye python

Soma Zaidi...
Python somo la 51: Jinsi ya kutengeneza Model ya menu

Katika somo hili utakwend akujifunza ktengeneza model kwa ajili ya database table ya menu yetu.

Soma Zaidi...
Python somo la 36: Django framework - Utangulizi

Ni nini maana ya django framework na inafanya kazi gani

Soma Zaidi...
Python somo la 34: Kutumia html kwneye python

Katika somo hili utakwend akujifunz ajinsi ya kutumia html kwneye python

Soma Zaidi...
Python somo la 27: polymorphism kwneye python

Katika somo hili utajifunza maana ya polymorphism na sheria za uandishi wake

Soma Zaidi...