picha

Python somo la 15: Jinsi ya kutumia while loop

Katika somo hili tutakwend akujifunza jinsi ya kutumia while loop kwneye python

Jinsi ya Kutumia while loop na do while loop katika Python

Katika somo hili, tutajifunza jinsi ya kutumia while loop na do while loop katika Python. Loop hizi hutumika kurudia utekelezaji wa code kulingana na masharti yaliyowekwa. Tofauti yao kuu ni jinsi wanavyoanza utekelezaji.

 


 

1. While Loop

While loop hutumika pale ambapo hatujui idadi ya marudio, lakini tunataka code iendelee kurudiwa mradi sharti fulani limetimia.

Muundo wa while loop:

while condition:

    # Code ya kurudiwa

    # Increment/Decrement

 

Mfano 1: Kuonyesha Orodha ya Namba

 

print("ORODHA YA NAMBA")

x = 1

print(x)

 

while x < 12:

    x += 1

    print(x)

 

Mfano 2: Kutengeneza Tebo ya 7

Hapa tutazidisha namba 7 kwa kila namba kuanzia 1 hadi 12.

print("TEBO YA 7")

x = 1

 

while x <= 12:

    print(f"{x} * 7 = {x * 7}")

    x += 1

 

 


 

2. Do-While Loop

Python haina do while loop kama ilivyo katika lugha kama Kotlin, lakini tunaweza kuunda dhana sawa kwa kutumia while loop pamoja na break. Katika do while loop, code huanza kutekelezwa mara moja hata kama sharti halijatimia, kisha sharti linakaguliwa. Tutajifunz akuhusu break na continue katika somo linalofuata.

 


 

Tofauti Kuu Kati ya while loop na do while loop:

 


 

Hitimisho

Katika somo hili, umejifunza jinsi ya kutumia while loop na jinsi ya kuunda do while loop katika Python. Unaweza kufanyia mazoezi kwa kubuni mifano yako, kama vile kuhesabu namba hata, kuunda jedwali la kuzidisha kwa namba nyingine, au kuonyesha orodha maalum.

Somo linalofuata: Tutaangazia jinsi ya kutumia break na continue kwenye loop ili kudhibiti mtiririko wa utekelezaji. Endelea kufanya mazoezi!

 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-11-22 12:26:37 Topic: Python Main: Masomo File: Download PDF Views 707

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉6 Dua za Mitume na Manabii    

Post zinazofanana:

Python somo 57: Matumizi ya Python shell

Katika somo hili, tutajifunza: Maana ya Python shell na umuhimu wake. Tofauti kati ya shell na terminal ya kawaida. Matumizi ya shell, hususan kwenye Django. Amri muhimu zaidi za Python shell, zilizotokana na models na views zako za pybongo.

Soma Zaidi...
Python somo la 30: Data abstraction

Katika somo hili utakwend akujifunz akuhusu nadharia ya data abstraction na kazi zake kwenye OOP

Soma Zaidi...
Python somo la 43: Kutuma Data kutoka View kwenda Template katika Django

Katika somo hili uatajifunza jinsi gani unaweza kutumia view kma logic kuuma data kwenye template

Soma Zaidi...
Python somo la 21: Module katika python

Katika somo hili utakwend akujifunz amaana ya module, kazi zake, aina zake na jinsi ya kuandika modile

Soma Zaidi...
Python somo la 27: polymorphism kwneye python

Katika somo hili utajifunza maana ya polymorphism na sheria za uandishi wake

Soma Zaidi...
Python somo la 62 Kupakia picha (upload) na kuisoma kutoka kwenye database

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kushughulika na faili, kama ku upload faili kwenye django.

Soma Zaidi...