Katika somo hili tutakwend akujifunza jinsi ya kutumia while loop kwneye python
Katika somo hili, tutajifunza jinsi ya kutumia while loop na do while loop katika Python. Loop hizi hutumika kurudia utekelezaji wa code kulingana na masharti yaliyowekwa. Tofauti yao kuu ni jinsi wanavyoanza utekelezaji.
While loop hutumika pale ambapo hatujui idadi ya marudio, lakini tunataka code iendelee kurudiwa mradi sharti fulani limetimia.
Muundo wa while loop:
while condition:
# Code ya kurudiwa
# Increment/Decrement
print("ORODHA YA NAMBA")
x = 1
print(x)
while x < 12:
x += 1
print(x)
Hapa tutazidisha namba 7 kwa kila namba kuanzia 1 hadi 12.
print("TEBO YA 7")
x = 1
while x <= 12:
print(f"{x} * 7 = {x * 7}")
x += 1
Python haina do while loop kama ilivyo katika lugha kama Kotlin, lakini tunaweza kuunda dhana sawa kwa kutumia while loop pamoja na break. Katika do while loop, code huanza kutekelezwa mara moja hata kama sharti halijatimia, kisha sharti linakaguliwa. Tutajifunz akuhusu break na continue katika somo linalofuata.
While loop: Sharti hukaguliwa kwanza kabla ya code kutekelezwa.
Do while loop: Code hutekelezwa angalau mara moja kabla ya sharti kukaguliwa.
Katika somo hili, umejifunza jinsi ya kutumia while loop na jinsi ya kuunda do while loop katika Python. Unaweza kufanyia mazoezi kwa kubuni mifano yako, kama vile kuhesabu namba hata, kuunda jedwali la kuzidisha kwa namba nyingine, au kuonyesha orodha maalum.
Somo linalofuata: Tutaangazia jinsi ya kutumia break na continue kwenye loop ili kudhibiti mtiririko wa utekelezaji. Endelea kufanya mazoezi!
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Umeionaje Makala hii.. ?
Katika somo hili tutakwend akujifunza kwa urefu zaidi kuhusu parameter ambazo hutumika kwenye functions
Soma Zaidi...Katika somo hili tutajifunza namna ya kusoma data kutoka kwenye database kupitia Django ORM, jinsi ya kuzipeleka kwenye view, na jinsi ya kuzionyesha kwenye HTML template.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu number method yaani function zinazofanya kazi kwenye namba.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwend akujifunz akuhusu nadharia ya data abstraction na kazi zake kwenye OOP
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwend akujifunza jinsi ya kuandika function, kuweka parameter na kuitumia function
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunza maana ya variable, na sheria za kutengeneza variable kwenye python. Pia utajifunza maneno ambayo hayafai kutumiwa kama variable
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza vipi django inaweza kuwasiliana na database, utajifunza kuusu orm na model
Soma Zaidi...Katika somo ili utajifunza hatuwa kwa hatuwa za ku install Django, kutengeneza project na kutengeneza app
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya ku host website ya Django. Hapa tutakwenda kutuma plaform ya pythonanywhere.com.
Soma Zaidi...Ni nini maana ya django framework na inafanya kazi gani
Soma Zaidi...