Python somo la 15: Jinsi ya kutumia while loop
Katika somo hili tutakwend akujifunza jinsi ya kutumia while loop kwneye python
Jinsi ya Kutumia while loop na do while loop katika Python
Katika somo hili, tutajifunza jinsi ya kutumia while loop na do while loop katika Python. Loop hizi hutumika kurudia utekelezaji wa code kulingana na masharti yaliyowekwa. Tofauti yao kuu ni jinsi wanavyoanza utekelezaji.
1. While Loop
While loop hutumika pale ambapo hatujui idadi ya marudio, lakini tunataka code iendelee kurudiwa mradi sharti fulani limetimia.
Muundo wa while loop:
while condition:
# Code ya kurudiwa
# Increment/Decrement
Mfano 1: Kuonyesha Orodha ya Namba
print("ORODHA YA NAMBA")
x = 1
print(x)
while x < 12:
x += 1
print(x)
Mfano 2: Kutengeneza Tebo ya 7
Hapa tutazidisha namba 7 kwa kila namba kuanzia 1 hadi 12.
print("TEBO YA 7")
x = 1
while x <= 12:
print(f"{x} * 7 = {x * 7}")
x += 1
2. Do-While Loop
Python haina do while loop kama ilivyo katika lugha kama Kotlin, lakini tunaweza kuunda dhana sawa kwa kutumia while loop pamoja na break. Katika do while loop, code huanza kutekelezwa mara moja hata kama sharti halijatimia, kisha sharti linakaguliwa. Tutajifunz akuhusu break na continue katika somo linalofuata.
Tofauti Kuu Kati ya while loop na do while loop:
-
While loop: Sharti hukaguliwa kwanza kabla ya code kutekelezwa. -
Do while loop: Code hutekelezwa angalau mara moja kabla ya sharti kukaguliwa.
Hitimisho
Katika somo hili, umejifunza jinsi ya kutumia while loop na jinsi ya kuunda do while loop katika Python. Unaweza kufanyia mazoezi kwa kubuni mifano yako, kama vile kuhesabu namba hata, kuunda jedwali la kuzidisha kwa namba nyingine, au kuonyesha orodha maalum.
Somo linalofuata: Tutaangazia jinsi ya kutumia break na continue kwenye loop ili kudhibiti mtiririko wa utekelezaji. Endelea kufanya mazoezi!
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Dua za Mitume na Manabii 👉2 kitabu cha Simulizi 👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉4 Kitabu cha Afya 👉5 Madrasa kiganjani 👉6 Simulizi za Hadithi Audio
Post zinazofanana:
Python somo la 35: Jinsi ya kutumia MYSQL kwenye python
Katika somo hili utajifunz akutumia database kwenye python
Soma Zaidi...Python somo la 62 Kupakia picha (upload) na kuisoma kutoka kwenye database
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kushughulika na faili, kama ku upload faili kwenye django.
Soma Zaidi...Python somo la 42: Template tag
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhsu Template Tag nini na kazi zake. Pia utajifunza sheria za uandishi wake.
Soma Zaidi...Python somo 57: Matumizi ya Python shell
Katika somo hili, tutajifunza: Maana ya Python shell na umuhimu wake. Tofauti kati ya shell na terminal ya kawaida. Matumizi ya shell, hususan kwenye Django. Amri muhimu zaidi za Python shell, zilizotokana na models na views zako za pybongo.
Soma Zaidi...Python somo la 32: Jinsi ya kusoma mafaili
Katika somo hili utakwenda kujifunz ajinsi ya kusoma mafaili na mitindo mbalimbali ya kusoma data
Soma Zaidi...Python somo la 16: Jinsi ya kutumia break na continue kwenye loop
Katika somo hili tunakwenda kujifunza matumizi ya break na continue kwenye loop
Soma Zaidi...