Menu



Python somo la 21: Module katika python

Katika somo hili utakwend akujifunz amaana ya module, kazi zake, aina zake na jinsi ya kuandika modile

Module kwenye Python

 


 

Maana ya Module

Module kwenye Python ni faili la Python linaloweza kuwa na msimbo wa programu (code), vigezo, kazi (functions), au madarasa (classes) ambayo yanaweza kutumika tena katika miradi tofauti ya programu.

Kwa maneno rahisi, module ni njia ya kugawa msimbo (code) wako katika vipande vidogo vilivyoandaliwa vizuri ili kurahisisha utunzaji na utumiaji wa msimbo huo.

 

Kwa maelezo rahisi:, tuseme tuna program ya mahesau, ambayo ina mafaili 3 na kila faili likawa na kazi yake. Mfano tukawa na faili la addition.py, division.py na multiplication.py ikawa tuapotaka kujumlisha tunatumia function zilizopo kwneye addition.py, kugawanya tunatumia divisionn.py na  hivyo hayo mafaili yote yanajulikana kama module.

 


 

Aina za Module

Kuna aina kuu mbili za modules kwenye Python:

  1. Built-in Modules (Zilizo tayari kwenye Python): Hizi ni modules zinazokuja na Python. Mfano:

  2. User-defined Modules (Zilizoandikwa na mtumiaji): Hizi ni modules unazotengeneza mwenyewe kulingana na mahitaji ya mradi wako.

 


 

Kazi za Modules

Modules zina faida nyingi, ikiwa ni pamoja na:

  1. Urejelevu wa msimbo (Code Reusability): Module inakuruhusu kutumia tena msimbo uleule kwenye miradi tofauti.

  2. Kupunguza ukubwa wa programu: Kwa kugawa msimbo katika modules ndogo, programu yako inakuwa rahisi kudhibiti.

  3. Kukuza urahisi wa kushirikiana: Developers wanaweza kushirikiana kwa kutumia modules tofauti kwa kazi tofauti.

  4. Kupunguza makosa: Kwa kuweka msimbo katika modules, ni rahisi kufuatilia na kurekebisha makosa.

 


 

Jinsi Modules Zinavyofanya Kazi

 


 

Mifano ya Kutumia Modules

1. Kutumia Built-in Modules

(a) Math Module:

 

import math

print(math.sqrt(16))  # Mzizi wa pili wa 16

print(math.pi)        # Thamani ya pi

 



(b) Random Module:

 

import random

print(random.randint(1, 10))  # Chagua namba ya bahati nasibu kati ya 1 na 10

 

 

(c) Datetime Module:

import datetime

sasa = datetime.datetime.now()

print(f"Tarehe na muda wa sasa: {sasa}")

 

 

2. Kutumia User-defined Modules

Wacha tuone Jinsi ya kutengeneza module yako mwneyewe na kuitumia kwenye project. Kwa mfano tunataka kutengeneza module ambayo tutaitumia katika kutoa salamu. 

(a) Kwanza, unda faili salamu.py:

# salamu.py

def asubuhi(jina):

    return f"Habari za asubuhi, {jina}!"

 

def jioni(jina):

    return f"Habari za jioni, {jina}!"

 

 

(b) Kisha, tumia module hiyo kwenye faili lingine main.py:

Utaanza kwanza ku import modile ya salamu kwa kuandika jina la module. Mfano import salamu

 

# main.py

import salamu

print(salamu.asubuhi("Amina"))

print(salamu.jioni("John"))



 

 


 

Hatua kwa Hatua: Jinsi ya Kuandika Module

Hatua ya 1: Tengeneza Faili la Python

Module ni faili la .py. Kwa mfano, unda faili linaloitwa hesabu.py na uandike kazi kadhaa ndani yake:

 

# hesabu.py

def jumla(a, b):

    return a + b

 

def tofauti(a, b):

    return a - b

 

def eneo_mraba(urefu, upana):

    return urefu * upana

 

Hatua ya 2: Tumia Module kwenye Programu Nyingine

Unda faili lingine main.py na ulete kazi kutoka kwenye hesabu.py:

 

# main.py

import hesabu

 

print(hesabu.jumla(5, 3))         # 8

print(hesabu.tofauti(10, 4))      # 6

print(hesabu.eneo_mraba(4, 5))    # 20



Module zaidi ya moja:

Pia unaweza ku import module zaidi ya moja na kufaya kazi kwenye ukurasa mmoja. Kwa mfano tutatumia module zote mbili hapo juu kwneye main.py

# main.py

import salamu

import hesabu



print(salamu.asubuhi("Amina"))

print(salamu.jioni("John"))

 

print(hesabu.jumla(5, 3))         # 8

print(hesabu.tofauti(10, 4))      # 6

print(hesabu.eneo_mraba(4, 5))    # 20

 

 

Hatua ya 3: Leta Kazi Maalum Kutoka Kwenye Module

Unaweza kuchagua kazi maalum kutoka kwenye module badala ya kuleta kila kitu: Yaani mfano hapo kwenye module yetu ya hesabu kuna function 3, sasa badala ya ku import faili zima, tunaweza ku imprt sehemu tu ya hiyo module. Mfano tunataka kutumia function mbili tu ambazo ni jumla na eneo_mraba.  Kufanya hivi tutatumia keyword from ikifuatiwa na  import ikifuatiwa na hiyo function tunayoitaka. Na sio tu function inaweza kuwa class n.k

 

from hesabu import jumla, eneo_mraba

 

print(jumla(7, 2))               # 9

print(eneo_mraba(6, 3))          # 18

 

Hatua ya 4: Badilisha Jina la Module au Kazi

Unaweza kutumia as kubadilisha jina la module au kazi:

 

import hesabu as h

print(h.jumla(10, 5))            # 15

 

 


 

Hitimisho

Modules kwenye Python ni zana muhimu kwa urahisi wa kupanga na kutumia tena msimbo. Zinakuja katika aina mbili:

  1. Built-in modules kama math na random.

  2. User-defined modules unazoweza kutengeneza mwenyewe.

 

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea

Ndio     Hapana     Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Python Main: Masomo File: Download PDF Views 204

Share On:

Facebook WhatsApp

Post zinazofanana:

Python somo la 15: Jinsi ya kutumia while loop

Katika somo hili tutakwend akujifunza jinsi ya kutumia while loop kwneye python

Soma Zaidi...
Python somo la 31: Jinsi ya kutengeneza faili na folder

Katika somo hili utajifunz ajinsi ya kutengeneza folda, faili na kuweka data kwneye faili

Soma Zaidi...
PYTHON - somo la 9: indexing katika strinfg

Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu string indexing. Kama tulivyojifunza kuhusu namba katika somo lililopita, basi hapa tutakwenda kucheza na string.

Soma Zaidi...
PYTHON somo la 12: assignment operator, logical operator, identity oeprator na membership operator

Katika somo hili utakwenda kujfunza operator nyingine kama assignment operator logical, identity operator na membership operator.

Soma Zaidi...
PYTHON - somo la 4: Aina za data kwenye python

Katika somo hili utakwenda kujifunza aina za data ambazo hutumika kwenye python. hapa utajifunza aina kuu 3 za data.

Soma Zaidi...
Python somo la 20: Aina za parameter kwenye function

Katika somo hili tutakwend akujifunza kwa urefu zaidi kuhusu parameter ambazo hutumika kwenye functions

Soma Zaidi...
PYTHON - somo la 6: Jinsi ya kujuwa aina ya data iliyotumika

Katika somo hili utajifunza jisni ya kujuwa aina ya data iliyotumika kwenye python

Soma Zaidi...
Python somo la 29: Encaosulation kwneye python

Katika somo hili utajifunza maana ya encapsulation na sheria za uandishi wake

Soma Zaidi...
Python somo la 14: Jinsi ya kutumia For loop

Katika somo hili utakwend akujifunza matumizi ya for loop kwneye python

Soma Zaidi...