Python somo la 17: Jinsi ya kutumia user input

Katika somo hili uatkwenda kujifunz anamna ambavyo mtu anaweza kuingiza input kwneye system

Jinsi ya Kuchukua User Input: Python Version

User input ni taarifa ambazo mtumiaji wa programu huingiza kwenye programu. Python, kama Kotlin, hutoa njia rahisi za kushughulikia user input. Tofauti kubwa ni kwamba Python hutumia input() kwa kazi hii. Hapa kuna jinsi unavyoweza kutekeleza mambo hayo katika Python:

 


 

1. User Input ni Nini?

User input ni kila kitu ambacho mtumiaji wa programu anaingiza kama sehemu ya mwingiliano wake na programu. Hii inaweza kuwa jina, namba, au data nyingine yoyote.

 


 

2. Kupata User Input katika Python

Katika Python, tunatumia input() kwa ajili ya kuchukua user input. Maandishi yanayoonekana ndani ya input() hutumika kama ujumbe kwa mtumiaji.

Mfano:

# Kuomba jina kutoka kwa mtumiaji

print("Andika jina lako na kisha bonyeza Enter:")

name = input()

print(f"Jina lako ni {name}")

 

 


 

3. Kuhakikisha Aina ya Data

Python huchukulia input zote kama string. Ikiwa unahitaji aina tofauti ya data, kama vile namba, unapaswa kubadilisha aina ya data kwa kutumia int(), float(), au method nyingine zinazofaa.

Mfano wa Kuhesabu Umri:

# Kuomba mwaka wa kuzaliwa

print("Andika mwaka uliozaliwa:")

 

year_of_birth = int(input())

current_year = 2023

age = current_year - year_of_birth

print(f"Umri wako ni miaka {age}.")

 

Changamoto ambayo ipo kwneye code hizo hapo juu endapo mtu atainginza herufi badala ya namba, code zitaleta mrundikano wa error ambazo zitaprint mpaka location ya faili. Sasa hii sio namna nzuri ya kuonyesha error.

 

Sasa ili kuweza kudhibiti error vizuri. Kwa mfano mtu anaweza kuweka herufi badala ya namba. Ama akaweka namba katika mpangilio sio. Kudhibiti error tutatumia njia ya try na except value error. Katika try tutajaribu kufanya kile tunachokitaka. Na katuka except value error  tutaangalia kama tunachokitaka hakikufanikiwa tutaprint messeji ya error kiustaarabu.

# Kuomba mwaka wa kuzaliwa

print("Andika mwaka uliozaliwa:")

try:

    year_of_birth = int(input())

    current_year = 2023

    age = current_year - year_of_birth

    print(f"Umri wako ni miaka {age}.")

except ValueError:

    print("Tafadhali ingiza mwaka sahihi kwa nambari.")

 

Endapo kuna error itaonekana kama hivi hapo chini

 


 

4. Kubadilisha Thamani za Data

Katika Python, unaweza kubadilisha string kuwa namba kwa kutumia method kama int() au float(). Kama user input ni tupu au si namba, unaweza kutumia mbinu za kushughulikia makosa.

Mfano wa Kubadilisha Thamani ya Pesa:

# Kubadilisha TSH kuwa USD

print("Andika kiasi cha pesa za Kitanzania:")

try:

    tsh_amount = float(input())

    usd_amount = tsh_amount / 2500

    print(f"Tsh {tsh_amount} ni sawa na USD {usd_amount}.")

except ValueError:

    print("Tafadhali ingiza kiasi cha pesa kwa namba.")

 

 


 

5. Kuhakikisha Data ni Sahihi

Python inaruhusu ukaguzi wa data kwa kutumia if statement. Hii inasaidia kuhakikisha mtumiaji anaingiza data inayotarajiwa. Kwa mfano hapa tutatumia method ya isdigit() ili kuthibitisha kuwa je data zilizoingizwa zipo katika digit yaani namba. Kwa kutumia mfano huu unawez akutumia method nynginezo ambazo tumesha jifunza huko nyuma.

Mfano wa If Statement:

# Kuomba mwaka wa kuzaliwa na kuhakikisha input sahihi

print("Andika mwaka uliozaliwa:")

year_of_birth = input()

if year_of_birth.isdigit():

    age = 2023 - int(year_of_birth)

    print(f"Umri wako ni miaka {age}.")

else:

    print("Tafadhali ingiza mwaka kwa nambari.")

 

 


 

6. Opereta ya Default Value

Katika Python, unaweza kutumia or operator ni njia rahisi ya kutoa thamani ya msingi ikiwa user input ni tupu.

Mfano:

# Kutumia default value

print("Andika kiasi cha pesa za Kitanzania:")

tsh_amount = input() or "0"

try:

    tsh_amount = float(tsh_amount)

    usd_amount = tsh_amount / 2500

    print(f"Tsh {tsh_amount} ni sawa na USD {usd_amount:.2f}.")

except ValueError:

    print("Tafadhali ingiza kiasi cha pesa kwa namba.")

 

Utaona kwenye picha hapo chini, sikuweka thamani yeyote lakini sikupata error ni kwa saabu thamani ya default imetumika ambayo ni 0. 

 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Python Main: ICT File: Download PDF Views 540

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Python somo la 42: Template tag

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhsu Template Tag nini na kazi zake. Pia utajifunza sheria za uandishi wake.

Soma Zaidi...
PYTHON - somo la 7: Jinsi ya kubadili aina ya data

Katika soo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kubaduli aina moja ya data kwena aina nyingine. Kwa mfano unaweza kubadili namba kuwa string ama kubadili string kuwa nanda ama kubadili float kuwa int.

Soma Zaidi...
Python somo la 47: Jinsi ya kupokea na kuchakata fomu

Katika somo hili utakwend akujifunza jinsi ya kupokea na kuchakata fomu

Soma Zaidi...
Python somo la 44: Data Manipulation katika Django Templates

Katika somo hili utakwend akujifunza jinsi ya kucheza na data kuzibadili kwa namna mbali mbali kwenye template

Soma Zaidi...
Python somo la 18: Jinsi ya kuandika function

Katika somo hili utakwend akujifunza jinsi ya kuandika function, kuweka parameter na kuitumia function

Soma Zaidi...
Python somo la 51: Jinsi ya kutengeneza Model ya menu

Katika somo hili utakwend akujifunza ktengeneza model kwa ajili ya database table ya menu yetu.

Soma Zaidi...
PYTHON somo la 12: assignment operator, logical operator, identity oeprator na membership operator

Katika somo hili utakwenda kujfunza operator nyingine kama assignment operator logical, identity operator na membership operator.

Soma Zaidi...
Python somo la 26: Sheria za uandishi wa object

Katika somo hili utakwend akujifunza maana ya object, na sheria za kuandika object.

Soma Zaidi...
Python somo la 16: Jinsi ya kutumia break na continue kwenye loop

Katika somo hili tunakwenda kujifunza matumizi ya break na continue kwenye loop

Soma Zaidi...
PYTHON - somo la 2: Sheria za uandishi wa pyhton yaani syntax za python

Katika somo hili utakwenda kujifunza syntaxy za python yaani sheria na kanuni za kuandika code za python

Soma Zaidi...