Katika somo hili uatkwenda kujifunz anamna ambavyo mtu anaweza kuingiza input kwneye system
User input ni taarifa ambazo mtumiaji wa programu huingiza kwenye programu. Python, kama Kotlin, hutoa njia rahisi za kushughulikia user input. Tofauti kubwa ni kwamba Python hutumia input() kwa kazi hii. Hapa kuna jinsi unavyoweza kutekeleza mambo hayo katika Python:
User input ni kila kitu ambacho mtumiaji wa programu anaingiza kama sehemu ya mwingiliano wake na programu. Hii inaweza kuwa jina, namba, au data nyingine yoyote.
Katika Python, tunatumia input() kwa ajili ya kuchukua user input. Maandishi yanayoonekana ndani ya input() hutumika kama ujumbe kwa mtumiaji.
Mfano:
# Kuomba jina kutoka kwa mtumiaji
print("Andika jina lako na kisha bonyeza Enter:")
name = input()
print(f"Jina lako ni {name}")
Python huchukulia input zote kama string. Ikiwa unahitaji aina tofauti ya data, kama vile namba, unapaswa kubadilisha aina ya data kwa kutumia int(), float(), au method nyingine zinazofaa.
Mfano wa Kuhesabu Umri:
# Kuomba mwaka wa kuzaliwa
print("Andika mwaka uliozaliwa:")
year_of_birth = int(input())
current_year = 2023
age = current_year - year_of_birth
print(f"Umri wako ni miaka {age}.")
Changamoto ambayo ipo kwneye code hizo hapo juu endapo mtu atainginza herufi badala ya namba, code zitaleta mrundikano wa error ambazo zitaprint mpaka location ya faili. Sasa hii sio namna nzuri ya kuonyesha error.
Sasa ili kuweza kudhibiti error vizuri. Kwa mfano mtu anaweza kuweka herufi badala ya namba. Ama akaweka namba katika mpangilio sio. Kudhibiti error tutatumia njia ya try na except value error. Katika try tutajaribu kufanya kile tunachokitaka. Na katuka except value error tutaangalia kama tunachokitaka hakikufanikiwa tutaprint messeji ya error kiustaarabu.
# Kuomba mwaka wa kuzaliwa
print("Andika mwaka uliozaliwa:")
try:
year_of_birth = int(input())
current_year = 2023
age = current_year - year_of_birth
print(f"Umri wako ni miaka {age}.")
except ValueError:
print("Tafadhali ingiza mwaka sahihi kwa nambari.")
Endapo kuna error itaonekana kama hivi hapo chini
Katika Python, unaweza kubadilisha string kuwa namba kwa kutumia method kama int() au float(). Kama user input ni tupu au si namba, unaweza kutumia mbinu za kushughulikia makosa.
Mfano wa Kubadilisha Thamani ya Pesa:
# Kubadilisha TSH kuwa USD
print("Andika kiasi cha pesa za Kitanzania:")
try:
tsh_amount = float(input())
usd_amount = tsh_amount / 2500
print(f"Tsh {tsh_amount} ni sawa na USD {usd_amount}.")
except ValueError:
print("Tafadhali ingiza kiasi cha pesa kwa namba.")
Python inaruhusu ukaguzi wa data kwa kutumia if statement. Hii inasaidia kuhakikisha mtumiaji anaingiza data inayotarajiwa. Kwa mfano hapa tutatumia method ya isdigit() ili kuthibitisha kuwa je data zilizoingizwa zipo katika digit yaani namba. Kwa kutumia mfano huu unawez akutumia method nynginezo ambazo tumesha jifunza huko nyuma.
Mfano wa If Statement:
# Kuomba mwaka wa kuzaliwa na kuhakikisha input sahihi
print("Andika mwaka uliozaliwa:")
year_of_birth = input()
if year_of_birth.isdigit():
age = 2023 - int(year_of_birth)
print(f"Umri wako ni miaka {age}.")
else:
print("Tafadhali ingiza mwaka kwa nambari.")
Katika Python, unaweza kutumia or operator ni njia rahisi ya kutoa thamani ya msingi ikiwa user input ni tupu.
Mfano:
# Kutumia default value
print("Andika kiasi cha pesa za Kitanzania:")
tsh_amount = input() or "0"
try:
tsh_amount = float(tsh_amount)
usd_amount = tsh_amount / 2500
print(f"Tsh {tsh_amount} ni sawa na USD {usd_amount:.2f}.")
except ValueError:
print("Tafadhali ingiza kiasi cha pesa kwa namba.")
Utaona kwenye picha hapo chini, sikuweka thamani yeyote lakini sikupata error ni kwa saabu thamani ya default imetumika ambayo ni 0.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Umeionaje Makala hii.. ?
Katika soo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kubaduli aina moja ya data kwena aina nyingine. Kwa mfano unaweza kubadili namba kuwa string ama kubadili string kuwa nanda ama kubadili float kuwa int.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwend akujifunz ajinsi ya kutumia html kwneye python
Soma Zaidi...Katika somo hili tutajifunza njia mbili muhimu za kuongeza data kwenye database katika project yetu ya pybongo (app: menu). Njia hizi ni: Kutumia Django Admin Kutumia Django Shell Utafahamu pia jinsi ya kusajili models kwenye admin, jinsi ya kuingia admin panel, na namna ya kutengeneza entries mpya za MenuItem.
Soma Zaidi...Katika somo hili tutaangalia jinsi ya kutengeneza fomu ya HTML kwa ajili ya kuingiza data kwenye jedwali la MenuItem, pamoja na kutengeneza view itakayopokea data hiyo na kuihifadhi kwenye database. Pia tutaunganisha form na URL route.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwend akujifunza matumizi ya for loop kwneye python
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunz amaana ya inheritance na sheria za kuiandika inheritance.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujfunza operator nyingine kama assignment operator logical, identity operator na membership operator.
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunza Jinsi ya Kuunda Simple Navigation Menu Katika Django kwa kutumia template
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwend akujifunza aina mbalimbali za function ambazo tunaweza kuzitumia kwenye python.
Soma Zaidi...Katika maeneo ya development, tunahitaji kutuma email mara nyingi kwa madhumuni ya: Kujaribu mfumo wa OTP Password reset System notifications Activation codes Lakini mara nyingi hatutaki emails ziondoke kwenda kwa watu halisi wakati bado tupo kwenye majaribio.
Soma Zaidi...