Katika somo hili uatkwenda kujifunz anamna ambavyo mtu anaweza kuingiza input kwneye system
User input ni taarifa ambazo mtumiaji wa programu huingiza kwenye programu. Python, kama Kotlin, hutoa njia rahisi za kushughulikia user input. Tofauti kubwa ni kwamba Python hutumia input() kwa kazi hii. Hapa kuna jinsi unavyoweza kutekeleza mambo hayo katika Python:
User input ni kila kitu ambacho mtumiaji wa programu anaingiza kama sehemu ya mwingiliano wake na programu. Hii inaweza kuwa jina, namba, au data nyingine yoyote.
Katika Python, tunatumia input() kwa ajili ya kuchukua user input. Maandishi yanayoonekana ndani ya input() hutumika kama ujumbe kwa mtumiaji.
Mfano:
# Kuomba jina kutoka kwa mtumiaji
print("Andika jina lako na kisha bonyeza Enter:")
name = input()
print(f"Jina lako ni {name}")
Python huchukulia input zote kama string. Ikiwa unahitaji aina tofauti ya data, kama vile namba, unapaswa kubadilisha aina ya data kwa kutumia int(), float(), au method nyingine zinazofaa.
Mfano wa Kuhesabu Umri:
# Kuomba mwaka wa kuzaliwa
print("Andika mwaka uliozaliwa:")
year_of_birth = int(input())
current_year = 2023
age = current_year - year_of_birth
print(f"Umri wako ni miaka {age}.")
Changamoto ambayo ipo kwneye code hizo hapo juu endapo mtu atainginza herufi badala ya namba, code zitaleta mrundikano wa error ambazo zitaprint mpaka location ya faili. Sasa hii sio namna nzuri ya kuonyesha error.
Sasa ili kuweza kudhibiti error vizuri. Kwa mfano mtu anaweza kuweka herufi badala ya namba. Ama akaweka namba katika mpangilio sio. Kudhibiti error tutatumia njia ya try na except value error. Katika try tutajaribu kufanya kile tunachokitaka. Na katuka except value error tutaangalia kama tunachokitaka hakikufanikiwa tutaprint messeji ya error kiustaarabu.
# Kuomba mwaka wa kuzaliwa
print("Andika mwaka uliozaliwa:")
try:
year_of_birth = int(input())
current_year = 2023
age = current_year - year_of_birth
print(f"Umri wako ni miaka {age}.")
except ValueError:
print("Tafadhali ingiza mwaka sahihi kwa nambari.")
Endapo kuna error itaonekana kama hivi hapo chini
Katika Python, unaweza kubadilisha string kuwa namba kwa kutumia method kama int() au float(). Kama user input ni tupu au si namba, unaweza kutumia mbinu za kushughulikia makosa.
Mfano wa Kubadilisha Thamani ya Pesa:
# Kubadilisha TSH kuwa USD
print("Andika kiasi cha pesa za Kitanzania:")
try:
tsh_amount = float(input())
usd_amount = tsh_amount / 2500
print(f"Tsh {tsh_amount} ni sawa na USD {usd_amount}.")
except ValueError:
print("Tafadhali ingiza kiasi cha pesa kwa namba.")
Python inaruhusu ukaguzi wa data kwa kutumia if statement. Hii inasaidia kuhakikisha mtumiaji anaingiza data inayotarajiwa. Kwa mfano hapa tutatumia method ya isdigit() ili kuthibitisha kuwa je data zilizoingizwa zipo katika digit yaani namba. Kwa kutumia mfano huu unawez akutumia method nynginezo ambazo tumesha jifunza huko nyuma.
Mfano wa If Statement:
# Kuomba mwaka wa kuzaliwa na kuhakikisha input sahihi
print("Andika mwaka uliozaliwa:")
year_of_birth = input()
if year_of_birth.isdigit():
age = 2023 - int(year_of_birth)
print(f"Umri wako ni miaka {age}.")
else:
print("Tafadhali ingiza mwaka kwa nambari.")
Katika Python, unaweza kutumia or operator ni njia rahisi ya kutoa thamani ya msingi ikiwa user input ni tupu.
Mfano:
# Kutumia default value
print("Andika kiasi cha pesa za Kitanzania:")
tsh_amount = input() or "0"
try:
tsh_amount = float(tsh_amount)
usd_amount = tsh_amount / 2500
print(f"Tsh {tsh_amount} ni sawa na USD {usd_amount:.2f}.")
except ValueError:
print("Tafadhali ingiza kiasi cha pesa kwa namba.")
Utaona kwenye picha hapo chini, sikuweka thamani yeyote lakini sikupata error ni kwa saabu thamani ya default imetumika ambayo ni 0.
Download Post hii hapa
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Katika somo hili tutakwend akujifunza kwa urefu zaidi kuhusu parameter ambazo hutumika kwenye functions
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunza maana ya encapsulation na sheria za uandishi wake
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza vipi django inaweza kuwasiliana na database, utajifunza kuusu orm na model
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunza jisni ya kujuwa aina ya data iliyotumika kwenye python
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwend akujifunza matumizi ya for loop kwneye python
Soma Zaidi...Somo hili linazungumzia hatua ya kuunda navigation menu na kutumia template inheritance kwa njia ya kitaalamu katika Django.
Soma Zaidi...Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu string indexing. Kama tulivyojifunza kuhusu namba katika somo lililopita, basi hapa tutakwenda kucheza na string.
Soma Zaidi...Katika somo hili tutakwend akuziona aina za condition statement kwneye python na jinsi ya kuzitumia
Soma Zaidi...Katika somo hili tutakwend akujifunza jinsi ya kutumia while loop kwneye python
Soma Zaidi...