picha

PHP - somo la 32: Jinsi ya kutumia filter_var() function kwenye PHP

Katika somo hili utajifunza jinsi ya kutumia filter_var() function kwa ajili ya kuchuja code zilizo hatari kwenye PHP file

FILTER YAANI UCHUJAJI WA TAARIFA:

Filter ni uchujaji wa taarifa. Katika ukurasa wa wavuti unahitaji kuchuja taarifa kwa ajili ya usalama. Tunatumia filter pia kuthibitisha uhalali na ukweli wa baadhi ya taarifa. Kwa mfano katika ukurasa wa kupokea madodoso, kuan kipengene cha kujaza email. Sasa tutahitaji filter ili kuweza kujuwa kama ni kweli hiyo taarifa iliyowekwa ni email ama sio.

 

Tunatumia filter pia kuondoa uchafu yaani taarifa ambazo hazihitajiki na kupata taarifa safi ambazo tunazihitaji. Baada ya ku filter hatuwa inayofuata ni ku validate yaani kuthibitisha uhalali wa hizo taarifa. Vitendo hivi kwa pamoja ni muhimu sana kwa ajili ya usalama wa taarifa, na kupunguza urahisi wa udukuzi wa taarifa kwenye database yako.

 

Ili kuchuja taarifa hizi kwanza utahitajika ku fanya sanitizing, baada yake unafanya validation. Sanitizing ndio ambayo itaondoa uchafu yaani visivyohitajika na validation ndo itathibitisha uhalali wa hizo taarifa. 

 

Ili kuweza kufanya filter tunatumia filter_var() na katikakufanya validation tutatumia parameter ya filter inayoitwa FILTER_VALIDATE na katika kufanya sanitizing tutatumia parameter inayoitwa FILTER_SANITIZE

 

Kuondoa tag za html

<?php

$html = "<h1 style='color: red'>Hello World!</h1>";

 

echo $html;

?>

Code hizo hapo juu zitaonyesha matokeo haya

 

Hapo utaona maandishi ni ya wekundu ni kwa sababu ya hizo html tag. Sasa ikiwa ninataka kupata matokeo hayo bila ya kutumia hizo html tag. Hapo tuta filter yaani tutachuja hizo tag za html tutaziondoa kabisa na kupata matokeo yasiyo athiriwa na html.

 

Hapa kwanza tutatengeneza variable mbili. Ya kwanza kwa ajili ya kuhifadhia hizo string zenye html variable hii tutaiita $html na itakuwa hivi $html = "<h1 style='color: red'>Hello World!</h1>" Baada ya hapo tutatengeneza variable ya pili ambayo itabeba thamani za variable ya kwanza baada ya kuchujwa. Hapa ndipo ambapo tutakwenda kuchuja hizo taarifa. Kwa kuwa data zetu ni string hivyo tutatumia FILTER_SANITIZE_STRING Kama paramater ya function yetu. Hivyo basi ndani ya function yetu kwenye argument au parameter kutakuwa na vitu viwili ambavyo ni string ya kwanza na sanitizng argument.

 

Pia function nzima itakuwa ni thamani ya variable yetu ya pili. Variable hii tutaiitwa $new. Hiindio itabeba function nzima ya kuchuja taarifa. Hivyo basi code zitaonekana kama hivi:-

<?php

$html = "<h1 style='color: red'>Hello World!</h1>";

$new = filter_var($html, FILTER_SANITIZE_STRING);

echo $new;

?>

 

...

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2023-10-18 Topic: PHP Main: ICT File: Download PDF Views 899

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 web hosting    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉5 Bongolite - Game zone - Play free game    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

PHP somo la 76: Aina za cache header

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu Aina za cache header

Soma Zaidi...
PHP somola 78: Cookie Headers

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu Cookie Headers

Soma Zaidi...
PHP BLOG - somo la 12: Jinsi ya kutumia prepared statement kwenye kusoma post za blog

Katika somo hili tutakwenda kutumia prepared ststement kwenye ku fetch data kutoka kwenye database.

Soma Zaidi...
PHP somo la 98: Library za PHP ambazo unaweza kutumia ORM

Somo hili litakwenda kukutajia baadhi ya library za php ambazo hutumika kwa matumizi ya ORM

Soma Zaidi...
PHP - somo la 40: Jinsi ya kutumia htaccess file kubadilisha muonekano wa link

Katika somo hili uatakwenda kujifunza jinsi ya kutumia htaccess ili kubadili muonekano wa link ya website ama blog ili kuifanya iwe rafiki zaidi.

Soma Zaidi...
PHP BLOG - somo la 6: Jinsi ya kutengeneza dashboard kwa ajili ya blog

katika post hii utajifunza jinsi ya kutengeneza ukurasa wa dashboard kwa ajili ya kutibti post

Soma Zaidi...
PHP BLOG - somo la 10: Jinsi ya kufanya sanitization

Katika somo hili utajifunza jinsi ya kufanya sanitization kwenye user input ili kuzuia sql injection kwenye database.

Soma Zaidi...
PHP - somo la 44: Nini cURL na ni yapi matumizi yake?

Katika somo hilibutajifunza maana ya cURL pamoja na matumini yake

Soma Zaidi...
PHP - somo la 47: Jifunze kuhusu sql injection na kuizuia

Katika somo hili utajwenda kujifunza jinsi ya kuzuia hacking kwenye website yako

Soma Zaidi...
PHP - somo la 2: sheria za uandishi wa code za PHP

Katika somo hili utajifunza kuhusu syntax za PHP

Soma Zaidi...