PHP - somo la 32: Jinsi ya kutumia filter_var() function kwenye PHP

Katika somo hili utajifunza jinsi ya kutumia filter_var() function kwa ajili ya kuchuja code zilizo hatari kwenye PHP file

FILTER YAANI UCHUJAJI WA TAARIFA:

Filter ni uchujaji wa taarifa. Katika ukurasa wa wavuti unahitaji kuchuja taarifa kwa ajili ya usalama. Tunatumia filter pia kuthibitisha uhalali na ukweli wa baadhi ya taarifa. Kwa mfano katika ukurasa wa kupokea madodoso, kuan kipengene cha kujaza email. Sasa tutahitaji filter ili kuweza kujuwa kama ni kweli hiyo taarifa iliyowekwa ni email ama sio.

 

Tunatumia filter pia kuondoa uchafu yaani taarifa ambazo hazihitajiki na kupata taarifa safi ambazo tunazihitaji. Baada ya ku filter hatuwa inayofuata ni ku validate yaani kuthibitisha uhalali wa hizo taarifa. Vitendo hivi kwa pamoja ni muhimu sana kwa ajili ya usalama wa taarifa, na kupunguza urahisi wa udukuzi wa taarifa kwenye database yako.

 

Ili kuchuja taarifa hizi kwanza utahitajika ku fanya sanitizing, baada yake unafanya validation. Sanitizing ndio ambayo itaondoa uchafu yaani visivyohitajika na validation ndo itathibitisha uhalali wa hizo taarifa. 

 

Ili kuweza kufanya filter tunatumia filter_var() na katikakufanya validation tutatumia parameter ya filter inayoitwa FILTER_VALIDATE na katika kufanya sanitizing tutatumia parameter inayoitwa FILTER_SANITIZE

 

Kuondoa tag za html

<?php

$html = "<h1 style='color: red'>Hello World!</h1>";

 

echo $html;

?>

Code hizo hapo juu zitaonyesha matokeo haya

 

Hapo utaona maandishi ni ya wekundu ni kwa sababu ya hizo html tag. Sasa ikiwa ninataka kupata matokeo hayo bila ya kutumia hizo html tag. Hapo tuta filter yaani tutachuja hizo tag za html tutaziondoa kabisa na kupata matokeo yasiyo athiriwa na html.

 

Hapa kwanza tutatengeneza variable mbili. Ya kwanza kwa ajili ya kuhifadhia hizo string zenye html variable hii tutaiita $html na itakuwa hivi $html = "<h1 style='color: red'>Hello World!</h1>" Baada ya hapo tutatengeneza variable ya pili ambayo itabeba thamani za variable ya kwanza baada ya kuchujwa. Hapa ndipo ambapo tutakwenda kuchuja hizo taarifa. Kwa kuwa data zetu ni string hivyo tutatumia FILTER_SANITIZE_STRING Kama paramater ya function yetu. Hivyo basi ndani ya function yetu kwenye argument au parameter kutakuwa na vitu viwili ambavyo ni string ya kwanza na sanitizng argument.

 

Pia function nzima itakuwa ni thamani ya variable yetu ya pili. Variable hii tutaiitwa $new. Hiindio itabeba function nzima ya kuchuja taarifa. Hivyo basi code zitaonekana kama hivi:-

<?php

$html = "<h1 style='color: red'>Hello World!</h1>";

$new = filter_var($html, FILTER_SANITIZE_STRING);

echo $new;

?>

 

...

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: PHP Main: ICT File: Download PDF Views 630

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉2 Dua za Mitume na Manabii    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 web hosting    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

PHP somo la 94: Maana ya ORM na kazi zake

Katika somo hili utakwenda kujifunzo kuhusu teknolojia ya ORM na inavyotumika kulinda usalama wa database

Soma Zaidi...
PHP somo la 19: Jinsi ya kudhibiti mpangilio wa data baada ya kuzisoma

Katika somo hili utajifunza kupangilia data wakati wa kuzisoma kwenye database kw akutumia PHP

Soma Zaidi...
PHP somo la 92: Jinsi ya kuunganisha php na database ya sqlite

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutumia database ya sqlite kwa kutumia PHP.

Soma Zaidi...
PHP somo la 77: aina za http redirect

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu http redirect header

Soma Zaidi...
PHP - somo la 4: Aina za data zinazotumika kwenye PHP

Katika somo hili utakwenda kujifunza aina za data ambazo hutumika kwenye PHP

Soma Zaidi...
PHP - somo la 14: Jinsi ya kutengeneza database kwa kutumia PHP

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutumia PHP kutengeneza database kwenye mysql database.

Soma Zaidi...
PHP - somo la 27: aina za variable kwenye PHP

Katika somo hili utakwenda kujifunza aina kuu 3 za variable katika PHP mabzo ni local variable, global variable na static variable.

Soma Zaidi...
PHP somo la 90: Jinsi ya kutumia json data kama blog post

Katika somo hili utaweza kujifunza ni kwa nambna gani utaweza kutengeneza blog post na kuisoma kwa kutumia data za json

Soma Zaidi...
PHP - somo la 41: Jinsi ya kufanya hashing kwenye PHP

Katika somo hili utajifunza jinsiya kufanya hashing taarifa muhimu kama password. Kufanya hashing kunaongeza usalama wa taarifa za waumiaji kwenye blog yako.

Soma Zaidi...
PHP - somo la 24: Jinsi ya ku upload file kwenye database na kulisoma kw akutumia php

Katika somo hili utajifnza jinsi ya ku upload file kwenye database. Kisha utajifunza jinsi ya kulisoma faili hilo kwa kutumia php

Soma Zaidi...