picha

PHP - somo la 13: Jinsi ya kuunganisha database na website

Katika somo hili utajifunza jinsi ya ku connect database, kwa kutumia php

Katika somo lililotangulia ulikuwa ni utangulizi wa course. hapa sasa ndipo tunakwenda kuanza somo letu rasmi. katika somo hili utakwenda kujifunza namna ya kuunganisha database kwenye faili la PHP. Hii ni hatuwa ya kwanza na muhimu unatakiwa uijuwe kama unataka kujifunza utengenezaji wa website na blog.

 

Ni kwa nini tunaunganisha PHP na databae?

Hili ni swali muhimu na ni la msingi sana. Jibu fupi ni kuwa ili uweze kuzisoma data zilizopo kwenye database kwenye blog yako ama website unahitaji uconnect na hiyo databse ili upate ruhusa ya kuziona hizo data,

 

Yaani ipo hivi, Fikiria kuwa una database inaitwa blog na  kwenye hiyo database kuna post kwa ajili ya blog yako. Sasa unataka hizo post zionekane kwenye blog yako. Kwanza utahitajika kuunganisha hiyo blog yako na hiyo database yako. kufanya hivi tutatumia php pamoja na ujuzi wa SQL kama tulivyojifunza katika course ya database. baada ya kuunganisha ndipo utaweza kuziweka hizo post kwenye ukurasa wa wavuti (web page)

Njia zinazotumika kuunganisha PHP na MySQL database

kwa maelezo ya w3school kuna njia kuu mbili za kuunganisha PHP na MySQL database. njia hizo ni:-

  1. MySQLi 
  2. PDO

Hiyi ya kwanza herufi i ina maana improved, na hiyo ya pili kirefu chake ni PHP Data Object) unaweza kutumia nji yeyote kati ya hizi. ila hii yenye MySQLi yenyewe inafanyakazi kwenye MySQL tu, lakini hiyo ya PDO inafanyakazi kwenye aina nyinginezo za database pamoja na hii ya MySQL.

 

Mambo muhimu kwenye wakati wa kkonect na database:

 

  1. kjuwa jina la database, passowd, na server
  2. kuanda variable kwa ajili ya kuunganisha na database.
  3. kufunguwa connection (open connection)
  4. kukonect kwenyewe (database connection)
  5. alert message hii ni kwa ajili ya kutoa taarifa kama kuna error ama kama umefanikiwa kukonnect
  6. kufunga connection

 

Kukonekt database kwa kutumia MySQLi:

kuna namna mbili ya kuunga database kwa kutumia MySQLi ambazo ni kama tutakavyoziona hapo chini. Unaweza kuchaguwa yeyote kati ya hizo. Utajifunza zaidi kuhusu njia hizi kwenye masomo yetu ya mbele.

  1. MySQLi object oriented
  2. MySQLi procedural

 

hatuwa kwa hatuwa kukonekt database:

 

 

tulisha jifunza namna ya kuandaa variable kwenye course ya PHP somo la 3. katika kukonekt na databse variable zako ni tatu, kwa ajili ya server, kwa ajili ya database (jina la database) na kwa ajili ya password. Variable zako zinaweza kuwa hizi:

$servername = "localhost";

$username = "username";

$password = "password"

 

localhost ni jina la server ambayo databse yetu ipo. kama unatumia wapserver, ama xamp au aWevServer kwa watumiaji wa simu basi jina la server yako ni localhost. uername ni jina la mtumiaji wa hiyo database. Hii ni akaunt inayomiliki hiyo databse. kama hujabadili jina ama username kwenye database yako basi jina lililopo ni root. na password kama unatumia local host mara nyingi password hakuna unaacha kama ilivyo, hivyo variable hapo zitasomeka  hivi

 

$servername = "localhost";

$username = "root";

$password = ""

 

 

 

Bada ya kuziweka variable zako sasa ni muda wa kuunganisha PHP na database kwa kutumia hizo variable. Kuna variable nyingine sasa tunatakiwa kuijuwa na hii ni muhimu kwa ajili ya kufanya hiki tunachokitaka. variable hii hutumiaka kuunganisha database. variable hii ni

$conn = new mysqli($servername, $username, $password);

variable $conn inakwenda kuwakilisha function new mysqli()ambapo ndani yake utawka variable zako za database name, server name na username. hivyo kusomeka

$conn = new mysqli($servername, $username, $password);

 

 

 

Hapa kuna jambo unatakiwa ulijuwe, ni kuwa unatakiwa uweke meseji ambayo itakueleza kama connection imefanikiwa ikuambie mfani you are connected. na kama connection imefele inatakiwa iseme mfano connection failed. kwa haraka haraka hapa utajuwa kuwa panatakiwa patumike condition sentenses kama tulivyojifunza kwenye php matumizi ya if, else, ifelse n.k.

 

kufanya hivi tutatumia

if (mysqli_connect_error()) {

die("connection failed " . mysqli_connect_error());

}

echo "you are connected";

 

Hapo panajionyesah wazi kuwa mysqli_connect_error() ni kwa ajili ya kuangalia kama connection imefanikiwa ama imefeli. kama imefele itareject (die) hivyo if itatupa matokeo connection failed. Na kama connection imefaniliwa if itatupa matokeo ya else itatupa matokeo ya you are connected.

 

 

 

Katika hali ya kawaida, connection hijifunga automatik. lakini pia unaweza kuifunga wewe mwenyewe punde tu b...

Ingia sasa ili uweze kusoma makala hii yote.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: PHP Main: Masomo File: Download PDF Views 1779

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉2 ai web app     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Madrasa kiganjani     👉5 Kitabu cha Afya     👉6 Dua za Mitume na Manabii    

Post zinazofanana:

PHP somo la 68: Jinsi ya kutuma email kwa kutumia PHPMailer

Katika somo hili utakwenda kujifunza jisniya kutuma email kwa kutumia PHPMailer kwenye project ya PHP. Katika somo hili tutakwend akutuma email kwa kutumia localhost.

Soma Zaidi...
PHP BLOG - somo la 8: Jinsi ya kufuta post kwenye database

katika post hii utajifunza jinsi ya kufuta post kwenye database. pia utajifunza jinsi ya kufuta picha kwenye server

Soma Zaidi...
PHP somo la 58: static method kwenye PHP

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu static method na inavtotumika kwenye OOP

Soma Zaidi...
PHP somo la 99: Jinsi ya kutumia ORM kwa kutumia library ya RedBeanPHP

Katika somo hili utakwenda kujifunza Jinsi ya kutumia ORM kwa kutumia library ya RedBeanPHP

Soma Zaidi...
PHP somo la 51: Jinsi ya kutumia consctuct na destruct function

Katika somo hili utakwenda kujifunza kazi na matumizi ya construct function na desctruct function kwenye OOP

Soma Zaidi...
PHP somo la 100: Jinsi ya kutumia sql moja kwa moja kwenye ORM ya RedBeanPHP

Katika somo hili utakwend akujifunz ajinsi ya kuandika query ndani ya ORM. Hii inakupa uhuru wa kufanya kileunachotaka bila ya kuathiri usalama wa project

Soma Zaidi...