picha

PHP - somo la 13: Jinsi ya kuunganisha database na website

Katika somo hili utajifunza jinsi ya ku connect database, kwa kutumia php

Katika somo lililotangulia ulikuwa ni utangulizi wa course. hapa sasa ndipo tunakwenda kuanza somo letu rasmi. katika somo hili utakwenda kujifunza namna ya kuunganisha database kwenye faili la PHP. Hii ni hatuwa ya kwanza na muhimu unatakiwa uijuwe kama unataka kujifunza utengenezaji wa website na blog.

 

Ni kwa nini tunaunganisha PHP na databae?

Hili ni swali muhimu na ni la msingi sana. Jibu fupi ni kuwa ili uweze kuzisoma data zilizopo kwenye database kwenye blog yako ama website unahitaji uconnect na hiyo databse ili upate ruhusa ya kuziona hizo data,

 

Yaani ipo hivi, Fikiria kuwa una database inaitwa blog na  kwenye hiyo database kuna post kwa ajili ya blog yako. Sasa unataka hizo post zionekane kwenye blog yako. Kwanza utahitajika kuunganisha hiyo blog yako na hiyo database yako. kufanya hivi tutatumia php pamoja na ujuzi wa SQL kama tulivyojifunza katika course ya database. baada ya kuunganisha ndipo utaweza kuziweka hizo post kwenye ukurasa wa wavuti (web page)

Njia zinazotumika kuunganisha PHP na MySQL database

kwa maelezo ya w3school kuna njia kuu mbili za kuunganisha PHP na MySQL database. njia hizo ni:-

  1. MySQLi 
  2. PDO

Hiyi ya kwanza herufi i ina maana improved, na hiyo ya pili kirefu chake ni PHP Data Object) unaweza kutumia nji yeyote kati ya hizi. ila hii yenye MySQLi yenyewe inafanyakazi kwenye MySQL tu, lakini hiyo ya PDO inafanyakazi kwenye aina nyinginezo za database pamoja na hii ya MySQL.

 

Mambo muhimu kwenye wakati wa kkonect na database:

 

  1. kjuwa jina la database, passowd, na server
  2. kuanda variable kwa ajili ya kuunganisha na database.
  3. kufunguwa connection (open connection)
  4. kukonect kwenyewe (database connection)
  5. alert message hii ni kwa ajili ya kutoa taarifa kama kuna error ama kama umefanikiwa kukonnect
  6. kufunga connection

 

Kukonekt database kwa kutumia MySQLi:

kuna namna mbili ya kuunga database kwa kutumia MySQLi ambazo ni kama tutakavyoziona hapo chini. Unaweza kuchaguwa yeyote kati ya hizo. Utajifunza zaidi kuhusu njia hizi kwenye masomo yetu ya mbele.

  1. MySQLi object oriented
  2. MySQLi procedural

 

hatuwa kwa hatuwa kukonekt database:

 

 

tulisha jifunza namna ya kuandaa variable kwenye course ya PHP somo la 3. katika kukonekt na databse variable zako ni tatu, kwa ajili ya server, kwa ajili ya database (jina la database) na kwa ajili ya password. Variable zako zinaweza kuwa hizi:

$servername = "localhost";

$username = "username";

$password = "password"

 

localhost ni jina la server ambayo databse yetu ipo. kama unatumia wapserver, ama xamp au aWevServer kwa watumiaji wa simu basi jina la server yako ni localhost. uername ni jina la mtumiaji wa hiyo database. Hii ni akaunt inayomiliki hiyo databse. kama hujabadili jina ama username kwenye database yako basi jina lililopo ni root. na password kama unatumia local host mara nyingi password hakuna unaacha kama ilivyo, hivyo variable hapo zitasomeka  hivi

 

$servername = "localhost";

$username = "root";

$password = ""

 

 

 

Bada ya kuziweka variable zako sasa ni muda wa kuunganisha PHP na database kwa kutumia hizo variable. Kuna variable nyingine sasa tunatakiwa kuijuwa na hii ni muhimu kwa ajili ya kufanya hiki tunachokitaka. variable hii hutumiaka kuunganisha database. variable hii ni

$conn = new mysqli($servername, $username, $password);

variable $conn inakwenda kuwakilisha function new mysqli()ambapo ndani yake utawka variable zako za database name, server name na username. hivyo kusomeka

$conn = new mysqli($servername, $username, $password);

 

 

 

Hapa kuna jambo unatakiwa ulijuwe, ni kuwa unatakiwa uweke meseji ambayo itakueleza kama connection imefanikiwa ikuambie mfani you are connected. na kama connection imefele inatakiwa iseme mfano connection failed. kwa haraka haraka hapa utajuwa kuwa panatakiwa patumike condition sentenses kama tulivyojifunza kwenye php matumizi ya if, else, ifelse n.k.

 

kufanya hivi tutatumia

if (mysqli_connect_error()) {

die("connection failed " . mysqli_connect_error());

}

echo "you are connected";

 

Hapo panajionyesah wazi kuwa mysqli_connect_error() ni kwa ajili ya kuangalia kama connection imefanikiwa ama imefeli. kama imefele itareject (die) hivyo if itatupa matokeo connection failed. Na kama connection imefaniliwa if itatupa matokeo ya else itatupa matokeo ya you are connected.

 

 

 

Katika hali ya kawaida, connection hijifunga automatik. lakini pia unaweza kuifunga wewe mwenyewe punde tu baada ya kuconnect. kufanya hivyo utatumia $conn->close();kwa Myqli object oriented au mysqli_close($conn);kwa MySQLi procedural au $conn = null; kwa PDO

 

CONNECTION NZIMA IPO HIVI:

Tengeneza faili la php kisha lipejina mfano test.php. hakikisha unaweka faili hilo kwenye localhost server kama ulivyoelekezwa kwenye mafunzo ya php. Kisha pest code hizo hapo chini, load file, itakuletea meseji you are connected kama imesha connect.

 

 

$servername = "localhost";

$username = "root";

$password = "";

 

// Kufanya connection

$conn = new mysqli($servername, $username, $password);

 

// Kuangalia connection

if (mysqli_connect_error()) {

   die("you are not connected: " . mysqli_connect_error());

}

echo "You are connected";

?>

 

hii itakupa matokeo

kama ukij">...

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2023-10-18 Topic: PHP Main: ICT File: Download PDF Views 1642

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

PHP somo la 57: class traits kwenye PHP

Katika somo hili utakwenda kujifunza concept ya traits kwenye OOP. hii itakusaidia ku solve baadhi ya changamoto zinazotokana na inheritance

Soma Zaidi...
PHP somo la 61: jinsi ya kufanya loop kwenye class kw akutumia foreach loop

Katika somo hili utakwenda kujifunza concept ya iteration kwenye PHP OOP hapa tutakwenda kuiona jinsi inavyofanya kazi pamoja na foreach loop

Soma Zaidi...
PHP - somo la 42: Jinsi ya kufanya encryption na de cryption kwa kutumia PHP

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kufanya encryption na decryption kwa kutumia PHP. hii itakusaidia kuongeza usalama kwenye taarifa za watu

Soma Zaidi...
PHP - 9: Jinsi ya kuandika array kwenye PHP na kuzifanyia kazi

Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu array kwenye php, na jinsi zinavyoweza kufanya kazi

Soma Zaidi...
PHP -somo la 33: Matumizi ya while loop kwenye PHP

Katika somo hili utajifunza jinsi ya kuandika while loop kwenye PHP

Soma Zaidi...
PHP somo la 99: Jinsi ya kutumia ORM kwa kutumia library ya RedBeanPHP

Katika somo hili utakwenda kujifunza Jinsi ya kutumia ORM kwa kutumia library ya RedBeanPHP

Soma Zaidi...
PHP - somo la 23: Jinsi ya kutumia condition statement kwenye database kwa kutumia PHP

Katika somo hili utakwenda kuona namna ya kutuia if else kwenye data zilizopo kwenye database kwa kutumia PHP

Soma Zaidi...
PHP - somo la 29: Jinsi ya kaundika function kwenye php

Katika somo hili utakwenda kujifundisha kuhus matumizi ya function kwenye php. Pia utajifunza jinsi ya kuandika function

Soma Zaidi...
PHP somo la 75: Content-Type Header

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu content-type header.

Soma Zaidi...
PHP - somo la 32: Jinsi ya kutumia filter_var() function kwenye PHP

Katika somo hili utajifunza jinsi ya kutumia filter_var() function kwa ajili ya kuchuja code zilizo hatari kwenye PHP file

Soma Zaidi...