Katika somo hili utajifunza jinsi ya ku connect database, kwa kutumia php
Katika somo lililotangulia ulikuwa ni utangulizi wa course. hapa sasa ndipo tunakwenda kuanza somo letu rasmi. katika somo hili utakwenda kujifunza namna ya kuunganisha database kwenye faili la PHP. Hii ni hatuwa ya kwanza na muhimu unatakiwa uijuwe kama unataka kujifunza utengenezaji wa website na blog.
Ni kwa nini tunaunganisha PHP na databae?
Hili ni swali muhimu na ni la msingi sana. Jibu fupi ni kuwa ili uweze kuzisoma data zilizopo kwenye database kwenye blog yako ama website unahitaji uconnect na hiyo databse ili upate ruhusa ya kuziona hizo data,
Yaani ipo hivi, Fikiria kuwa una database inaitwa blog na kwenye hiyo database kuna post kwa ajili ya blog yako. Sasa unataka hizo post zionekane kwenye blog yako. Kwanza utahitajika kuunganisha hiyo blog yako na hiyo database yako. kufanya hivi tutatumia php pamoja na ujuzi wa SQL kama tulivyojifunza katika course ya database. baada ya kuunganisha ndipo utaweza kuziweka hizo post kwenye ukurasa wa wavuti (web page)
Njia zinazotumika kuunganisha PHP na MySQL database
kwa maelezo ya w3school kuna njia kuu mbili za kuunganisha PHP na MySQL database. njia hizo ni:-
Hiyi ya kwanza herufi i ina maana improved, na hiyo ya pili kirefu chake ni PHP Data Object) unaweza kutumia nji yeyote kati ya hizi. ila hii yenye MySQLi yenyewe inafanyakazi kwenye MySQL tu, lakini hiyo ya PDO inafanyakazi kwenye aina nyinginezo za database pamoja na hii ya MySQL.
Mambo muhimu kwenye wakati wa kkonect na database:
Kukonekt database kwa kutumia MySQLi:
kuna namna mbili ya kuunga database kwa kutumia MySQLi ambazo ni kama tutakavyoziona hapo chini. Unaweza kuchaguwa yeyote kati ya hizo. Utajifunza zaidi kuhusu njia hizi kwenye masomo yetu ya mbele.
hatuwa kwa hatuwa kukonekt database:
tulisha jifunza namna ya kuandaa variable kwenye course ya PHP somo la 3. katika kukonekt na databse variable zako ni tatu, kwa ajili ya server, kwa ajili ya database (jina la database) na kwa ajili ya password. Variable zako zinaweza kuwa hizi:
$servername = "localhost";
$username = "username";
$password = "password"
localhost ni jina la server ambayo databse yetu ipo. kama unatumia wapserver, ama xamp au aWevServer kwa watumiaji wa simu basi jina la server yako ni localhost. uername ni jina la mtumiaji wa hiyo database. Hii ni akaunt inayomiliki hiyo databse. kama hujabadili jina ama username kwenye database yako basi jina lililopo ni root. na password kama unatumia local host mara nyingi password hakuna unaacha kama ilivyo, hivyo variable hapo zitasomeka hivi
$servername = "localhost";
$username = "root";
$password = ""
Bada ya kuziweka variable zako sasa ni muda wa kuunganisha PHP na database kwa kutumia hizo variable. Kuna variable nyingine sasa tunatakiwa kuijuwa na hii ni muhimu kwa ajili ya kufanya hiki tunachokitaka. variable hii hutumiaka kuunganisha database. variable hii ni
$conn = new mysqli($servername, $username, $password);
variable $conn inakwenda kuwakilisha function new mysqli()ambapo ndani yake utawka variable zako za database name, server name na username. hivyo kusomeka
$conn = new mysqli($servername, $username, $password);
Hapa kuna jambo unatakiwa ulijuwe, ni kuwa unatakiwa uweke meseji ambayo itakueleza kama connection imefanikiwa ikuambie mfani you are connected. na kama connection imefele inatakiwa iseme mfano connection failed. kwa haraka haraka hapa utajuwa kuwa panatakiwa patumike condition sentenses kama tulivyojifunza kwenye php matumizi ya if, else, ifelse n.k.
kufanya hivi tutatumia
if (mysqli_connect_error()) {
die("connection failed " . mysqli_connect_error());
}
echo "you are connected";
Hapo panajionyesah wazi kuwa mysqli_connect_error() ni kwa ajili ya kuangalia kama connection imefanikiwa ama imefeli. kama imefele itareject (die) hivyo if itatupa matokeo connection failed. Na kama connection imefaniliwa if itatupa matokeo ya else itatupa matokeo ya you are connected.
Katika hali ya kawaida, connection hijifunga automatik. lakini pia unaweza kuifunga wewe mwenyewe punde tu baada ya kuconnect. kufanya hivyo utatumia $conn->close();kwa Myqli object oriented au mysqli_close($conn);kwa MySQLi procedural au $conn = null; kwa PDO
CONNECTION NZIMA IPO HIVI:
Tengeneza faili la php kisha lipejina mfano test.php. hakikisha unaweka faili hilo kwenye localhost server kama ulivyoelekezwa kwenye mafunzo ya php. Kisha pest code hizo hapo chini, load file, itakuletea meseji you are connected kama imesha connect.
$servername = "localhost";
$username = "root";
$password = "";
// Kufanya connection
$conn = new mysqli($servername, $username, $password);
// Kuangalia connection
if (mysqli_connect_error()) {
die("you are not connected: " . mysqli_connect_error());
}
echo "You are connected";
?>
hii itakupa matokeo
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowKatika somo hili utakwenda kujifunza jinsi jinsi ya ku edit ama ku update data na kuzifuta kwenye database kwa kutumia PDO
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunza jinsi ambavyo utaweza kutengeneza mfumo wa kuisajiki na ku login, kisha kuangalia usalama wa mfumo kwa kuzuia sql injection.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kukusanya taarifa za watumiaji kwa kutumia html form.
Soma Zaidi...Katika project hii utakwenda kujifunza jinsi ya kufanya CRUDE operation kwa kutumia PHP OOP na MySQL database.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza concept ya traits kwenye OOP. hii itakusaidia ku solve baadhi ya changamoto zinazotokana na inheritance
Soma Zaidi...katika somo hili utajfunza kukusanya taarifa za mafaili. kisha ku upload hayo mafaili. kisha kuandika hizo taarifa za mafaii kwenye database
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunza jinsiya kufanya hashing taarifa muhimu kama password. Kufanya hashing kunaongeza usalama wa taarifa za waumiaji kwenye blog yako.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kusoma muda kama saa na tarehe kwa kutumia PHP
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwend akujifunza jinsi ya kubadili json data na kuwaphp array ama php object. Kwa ufupi tunakwend aku decode json data kuwa phparray amaobject
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunza jinsi ya kukusanya taarifa ambazo watu wamezijaza kwa kutumia fomu ya html. Kisha utajifunza jinsi ya kuzisoma hizo taarifa.
Soma Zaidi...