image

PHP - somo la 13: Jinsi ya kuunganisha database na website

Katika somo hili utajifunza jinsi ya ku connect database, kwa kutumia php

Katika somo lililotangulia ulikuwa ni utangulizi wa course. hapa sasa ndipo tunakwenda kuanza somo letu rasmi. katika somo hili utakwenda kujifunza namna ya kuunganisha database kwenye faili la PHP. Hii ni hatuwa ya kwanza na muhimu unatakiwa uijuwe kama unataka kujifunza utengenezaji wa website na blog.

 

Ni kwa nini tunaunganisha PHP na databae?

Hili ni swali muhimu na ni la msingi sana. Jibu fupi ni kuwa ili uweze kuzisoma data zilizopo kwenye database kwenye blog yako ama website unahitaji uconnect na hiyo databse ili upate ruhusa ya kuziona hizo data,

 

Yaani ipo hivi, Fikiria kuwa una database inaitwa blog na  kwenye hiyo database kuna post kwa ajili ya blog yako. Sasa unataka hizo post zionekane kwenye blog yako. Kwanza utahitajika kuunganisha hiyo blog yako na hiyo database yako. kufanya hivi tutatumia php pamoja na ujuzi wa SQL kama tulivyojifunza katika course ya database. baada ya kuunganisha ndipo utaweza kuziweka hizo post kwenye ukurasa wa wavuti (web page)

Njia zinazotumika kuunganisha PHP na MySQL database

kwa maelezo ya w3school kuna njia kuu mbili za kuunganisha PHP na MySQL database. njia hizo ni:-

  1. MySQLi 
  2. PDO

Hiyi ya kwanza herufi i ina maana improved, na hiyo ya pili kirefu chake ni PHP Data Object) unaweza kutumia nji yeyote kati ya hizi. ila hii yenye MySQLi yenyewe inafanyakazi kwenye MySQL tu, lakini hiyo ya PDO inafanyakazi kwenye aina nyinginezo za database pamoja na hii ya MySQL.

 

Mambo muhimu kwenye wakati wa kkonect na database:

 

  1. kjuwa jina la database, passowd, na server
  2. kuanda variable kwa ajili ya kuunganisha na database.
  3. kufunguwa connection (open connection)
  4. kukonect kwenyewe (database connection)
  5. alert message hii ni kwa ajili ya kutoa taarifa kama kuna error ama kama umefanikiwa kukonnect
  6. kufunga connection

 

Kukonekt database kwa kutumia MySQLi:

kuna namna mbili ya kuunga database kwa kutumia MySQLi ambazo ni kama tutakavyoziona hapo chini. Unaweza kuchaguwa yeyote kati ya hizo. Utajifunza zaidi kuhusu njia hizi kwenye masomo yetu ya mbele.

  1. MySQLi object oriented
  2. MySQLi procedural

 

hatuwa kwa hatuwa kukonekt database:

 

 

tulisha jifunza namna ya kuandaa variable kwenye course ya PHP somo la 3. katika kukonekt na databse variable zako ni tatu, kwa ajili ya server, kwa ajili ya database (jina la database) na kwa ajili ya password. Variable zako zinaweza kuwa hizi:

$servername = "localhost";

$username = "username";

$password = "password"

 

localhost ni jina la server ambayo databse yetu ipo. kama unatumia wapserver, ama xamp au aWevServer kwa watumiaji wa simu basi jina la server yako ni localhost. uername ni jina la mtumiaji wa hiyo database. Hii ni akaunt inayomiliki hiyo databse. kama hujabadili jina ama username kwenye database yako basi jina lililopo ni root. na password kama unatumia local host mara nyingi password hakuna unaacha kama ilivyo, hivyo variable hapo zitasomeka  hivi

 

$servername = "localhost";

$username = "root";

$password = ""

 

 

 

Bada ya kuziweka variable zako sasa ni muda wa kuunganisha PHP na database kwa kutumia hizo variable. Kuna variable nyingine sasa tunatakiwa kuijuwa na hii ni muhimu kwa ajili ya kufanya hiki tunachokitaka. variable hii hutumiaka kuunganisha database. variable hii ni

$conn = new mysqli($servername, $username, $password);

variable $conn inakwenda kuwakilisha function new mysqli()ambapo ndani yake utawka variable zako za database name, server name na username. hivyo kusomeka

$conn = new mysqli($servername, $username, $password);

 

 

 

Hapa kuna jambo unatakiwa ulijuwe, ni kuwa unatakiwa uweke meseji ambayo itakueleza kama connection imefanikiwa ikuambie mfani you are connected. na kama connection imefele inatakiwa iseme mfano connection failed. kwa haraka haraka hapa utajuwa kuwa panatakiwa patumike condition sentenses kama tulivyojifunza kwenye php matumizi ya if, else, ifelse n.k.

 

kufanya hivi tutatumia

if (mysqli_connect_error()) {

die("connection failed " . mysqli_connect_error());

}

echo "you are connected";

 

Hapo panajionyesah wazi kuwa mysqli_connect_error() ni kwa ajili ya kuangalia kama connection imefanikiwa ama imefeli. kama imefele itareject (die) hivyo if itatupa matokeo connection failed. Na kama connection imefaniliwa if itatupa matokeo ya else itatupa matokeo ya you are connected.

 

 

 

Katika hali ya kawaida, connection hijifunga automatik. lakini pia unaweza kuifunga wewe mwenyewe punde tu baada ya kuconnect. kufanya hivyo utatumia $conn->close();kwa Myqli object oriented au mysqli_close($conn);kwa MySQLi procedural au $conn = null; kwa PDO

 

CONNECTION NZIMA IPO HIVI:

Tengeneza faili la php kisha lipejina mfano test.php. hakikisha unaweka faili hilo kwenye localhost server kama ulivyoelekezwa kwenye mafunzo ya php. Kisha pest code hizo hapo chini, load file, itakuletea meseji you are connected kama imesha connect.

 

 

$servername = "localhost";

$username = "root";

$password = "";

 

// Kufanya connection

$conn = new mysqli($servername, $username, $password);

 

// Kuangalia connection

if (mysqli_connect_error()) {

   die("you are not connected: " . mysqli_connect_error());

}

echo "You are connected";

?>

 

hii itakupa matokeo

kama ukijaribu kubadilisha hapo mfano wela user">...



Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 351


Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

PHP - somo la 43: Jinsi ya kutuma email kwa kutumia PHP
Katika somo hili utajifunza jinsi ya kutuma email kwa kutumia email() function ya PHP. Hii ni njia rahisi zaidi ya kutuma email. Ila hufanya kazi kwenye hosting. Soma Zaidi...

PHP somo la 67: Project ya CUDE operaton wa utuma OOP na PDO
Katika somo hii utakwenda kujifunza jinsi ya kufanya CRUDE operation kwa kutumia PDO. crude operation inahusu create, read, update. Delete. Soma Zaidi...

PHP somola 63: Jinsi ya ku connect database kwa kutumia PDO na faida zake
Katika soo hili utakwenda kujifunza umuhmu wa kutumia PDO kwenye PHP kwa ajili ya kutumia database. Soma Zaidi...

PHP somo la 74: aina za http headerna server variable
Katika somo hii utakwenda kujifunza aina za http header na server variable. Hapa tutakwenda kuchambuwa mgawanyiko wa httpheader na kazi zake. Soma Zaidi...

PHP - somo la 23: Jinsi ya kutumia condition statement kwenye database kwa kutumia PHP
Katika somo hili utakwenda kuona namna ya kutuia if else kwenye data zilizopo kwenye database kwa kutumia PHP Soma Zaidi...

PHP somo la 51: Jinsi ya kutumia consctuct na destruct function
Katika somo hili utakwenda kujifunza kazi na matumizi ya construct function na desctruct function kwenye OOP Soma Zaidi...

PHP somola 69: jinsi ya kutuma email kwa watu zaidi ya mmoja kwa kutumia PHPMailer
Katika somo il utajifunza kutuma email kwa watu wengi kwa kutumia PHPMailer. Pia utajifunza jinsi ya kuweka Carbon Copy na Blind Carbon Copy Soma Zaidi...

PHP somo la 50: Jinsi ya kutengeneza CLASS na OBJECT kwenye PHP OOP
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutengeneza class na object. Tunakwenda kutumia mfano wetu wa hapo juu kwa ajili ya kukamilisha somo hili. Soma Zaidi...

PHP - somo la 34: Jinsi ya kutumia do loop, while loop na foreach kwenye PHP
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu aina za loop DO, FOR, FOREACH LOOPS kwenye PHP Soma Zaidi...

PHP somo la 57: class traits kwenye PHP
Katika somo hili utakwenda kujifunza concept ya traits kwenye OOP. hii itakusaidia ku solve baadhi ya changamoto zinazotokana na inheritance Soma Zaidi...

PHP somo la 86: JInsi ya ku decode json yaani kubadili json kuwa php data kama array ana object
Katika somo hili utakwend akujifunza jinsi ya kubadili json data na kuwaphp array ama php object. Kwa ufupi tunakwend aku decode json data kuwa phparray amaobject Soma Zaidi...

PHP somo la 84: Maana ya JSON na sheria za kuandika faili la json
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu Maana ya JSON na sheria za kuandika faili la json Soma Zaidi...