Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kuandika function za PHP kama require() na iclude()
INCLUDE, REQUIRE, INCLUDE_ONCE na REQUIRE_ONCE
Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu matumizi ya hizi function 3 ambazo kwa pamoja zinahusika na kuhusisha kuhusisha mafaili ya code kwenye mafaili mengi, bila ya kuziandika kila wakati.
include()
Incdude hutumika kama unataka kutumia code za faili falni kwenye faili lingine. Kwa mfano unataka kuunganisha database. Sasa kuna mafaili 10 ambayo yanahitaji kutumia database. Hivyo katika hali ya kawaida itakubidi uandike code za kuunganisha database kwenye mafaili yote hayo. Hivyo basi kwa kutumia include tutaandika code hizo kwenye faili moja. Kisha tutatumia function hii ili kuweza kuzitumia kwenye mafaili yote hayo.
Kwa mfano tunataka kuweka menu yetu kwenye kurasa zetu. Hivyo tofauti na kuziandika menu hizo kila ukurasa basi tutatumia include() ili kuweza kuzifikia. Wacha tuone mifano halizi.Hapo chini tutatengeneza mafaili mawili. Moja ni kwa ajili ya menu na lingine tutatumia include ili kuweza kuzitumia menu kwenye file lingine.
Faili ambalo tutali include tutaliita menu.php na faili ambalo ltakuwa linatumia hizo code tutaliita home.php. Sasa endapo tutafunguwa faili la home.php litaonesha menu ambazo zipo kwenye file lingine.
Menu.php
Android
Html
Video
Contact
Sasa tunakwenda kuzi include code hizi kwenye ukurasa wetu wa home.php. Na tupate matokeo sawa ya menu hii kwenye ikurasa huo.
home.php
include 'menu.php';
?>
Kwa kutumia mfano kama huu unaweza ku include block nyingi za code. Kufanya hivi kutakupubguzia sana kazi. Baada ya kuandika code hizohizo kila wakati sasa utatumia function hiyo na kuzi include.
INCLUDE_ONE()
Function hii hufanana na hiyo iliyotangulia. Utofauti ni kuwa include siku zote itakapotumika ina include code hizo bila hata ya kujali kama zilisha kuwepo ama tayari faili hilo umesha li include. Angalia mfano huu
include 'menu.php';
include 'menu.php';
?>
Hapo utaona faili tume li include mara mbili hivy linatupa matokeo mara mbili. Lakini sasa ukitumia include_once() kwanza itaangalia kama hilo faili tayari lipo, itainclude mara moja tu.Kwa fano hapo juu kama tutatumia include_once() tutapata matokeo mara moja tu.
Wacha nitumie lugha nyingine kukuelewesha. Yaani once ni neno la kiingereza linalomaanisha mara moja tu. Hivyo basi ukisema include_once yaani include hilo faili mara moja tu. Hivyo hata kama uta include mara mbtatu au zaidi zote hazitafanya kazi. Mara moja tu ndio itakayotumiwa. Angalia mfano hapo chini.
include_once 'menu.php';
include_once 'menu.php';
?>
Tumepata matokeo mara moja tu wakati tumeinclude mara mbili.
Hivyo basi katika mafaili muhimu kama database, ama class au yanayohusika kwenye login mara nyingi hapa tunatumia include_once na kwenye code za kawaida kama style na zile static file huwa tunatumia include.
REQUIRE() na REQUIRE_ONCE()
Katika php require() na require_once() hufanya kazi sawa na include() na include-once(). Utofauti wao ni kuwa endapo iclude faili ambalo limetakiwa kuwa katika include halipo code zinatoa warning lakini zinafanya kazi. Lakini endapo require imetumika na kama faili hakipo italeta error na hutoweza kuendelea na program.
Hapa chini nitakupa mifano 2 ambapo mafaili hayapo. Yaani nitatumia include kwa faili ambalo halipo uone inavyokuwa. Kisha nitatumia require kwa faili ambalo halipo na itakavyokuwa.
include 'head.php';
//ujumbe huu huwezi kuuona kama tungetumia reuire
echo "Haloo hapo juu faili halipo lakini php imeendelea kutoa matokeo ya code nyingine."
?>
...
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutengeneza class na object. Tunakwenda kutumia mfano wetu wa hapo juu kwa ajili ya kukamilisha somo hili.
Soma Zaidi...Hapa utajifunza jinsi ya kutengeneza table ambayo tutaitumia kwenye blog yetu
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kuona namna ya kutuia if else kwenye data zilizopo kwenye database kwa kutumia PHP
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutumia constatnt kwenye class.
Soma Zaidi...Katika somo hil utawenda kujifunza jinsi ya ku edit post kwenye databse
Soma Zaidi...katika post hii utajifunza jinsi ya kufuta post kwenye database. pia utajifunza jinsi ya kufuta picha kwenye server
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunza jinsi ya kufanya sanitization kwenye user input ili kuzuia sql injection kwenye database.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya ku generate PDF automatik kutoka kwenye php code , html, javascript na css.
Soma Zaidi...katika somo hili utajfunza kukusanya taarifa za mafaili. kisha ku upload hayo mafaili. kisha kuandika hizo taarifa za mafaii kwenye database
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu access modifier ili kuweza kuthibiti nama ya kuzitumia properties kwenye class.
Soma Zaidi...