Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kuandika function za PHP kama require() na iclude()
INCLUDE, REQUIRE, INCLUDE_ONCE na REQUIRE_ONCE
Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu matumizi ya hizi function 3 ambazo kwa pamoja zinahusika na kuhusisha kuhusisha mafaili ya code kwenye mafaili mengi, bila ya kuziandika kila wakati.
include()
Incdude hutumika kama unataka kutumia code za faili falni kwenye faili lingine. Kwa mfano unataka kuunganisha database. Sasa kuna mafaili 10 ambayo yanahitaji kutumia database. Hivyo katika hali ya kawaida itakubidi uandike code za kuunganisha database kwenye mafaili yote hayo. Hivyo basi kwa kutumia include tutaandika code hizo kwenye faili moja. Kisha tutatumia function hii ili kuweza kuzitumia kwenye mafaili yote hayo.
Kwa mfano tunataka kuweka menu yetu kwenye kurasa zetu. Hivyo tofauti na kuziandika menu hizo kila ukurasa basi tutatumia include() ili kuweza kuzifikia. Wacha tuone mifano halizi.Hapo chini tutatengeneza mafaili mawili. Moja ni kwa ajili ya menu na lingine tutatumia include ili kuweza kuzitumia menu kwenye file lingine.
Faili ambalo tutali include tutaliita menu.php na faili ambalo ltakuwa linatumia hizo code tutaliita home.php. Sasa endapo tutafunguwa faili la home.php litaonesha menu ambazo zipo kwenye file lingine.
Menu.php
Android
Html
Video
Contact
Sasa tunakwenda kuzi include code hizi kwenye ukurasa wetu wa home.php. Na tupate matokeo sawa ya menu hii kwenye ikurasa huo.
home.php
include 'menu.php';
?>
Kwa kutumia mfano kama huu unaweza ku include block nyingi za code. Kufanya hivi kutakupubguzia sana kazi. Baada ya kuandika code hizohizo kila wakati sasa utatumia function hiyo na kuzi include.
INCLUDE_ONE()
Function hii hufanana na hiyo iliyotangulia. Utofauti ni kuwa include siku zote itakapotumika ina include code hizo bila hata ya kujali kama zilisha kuwepo ama tayari faili hilo umesha li include. Angalia mfano huu
include 'menu.php';
include 'menu.php';
?>
Hapo utaona faili tume li include mara mbili hivy linatupa matokeo mara mbili. Lakini sasa ukitumia include_once() kwanza itaangalia kama hilo faili tayari lipo, itainclude mara moja tu.Kwa fano hapo juu kama tutatumia include_once() tutapata matokeo mara moja tu.
Wacha nitumie lugha nyingine kukuelewesha. Yaani once ni neno la kiingereza linalomaanisha mara moja tu. Hivyo basi ukisema include_once yaani include hilo faili mara moja tu. Hivyo hata kama uta include mara mbtatu au zaidi zote hazitafanya kazi. Mara moja tu ndio itakayotumiwa. Angalia mfano hapo chini.
include_once 'menu.php';
include_once 'menu.php';
?>
Tumepata matokeo mara moja tu wakati tumeinclude mara mbili.
Hivyo basi katika mafaili muhimu kama database, ama class au yanayohusika kwenye login mara nyingi hapa tunatumia include_once na kwenye code za kawaida kama style na zile static file huwa tunatumia include.
REQUIRE() na REQUIRE_ONCE()
Katika php require() na require_once() hufanya kazi sawa na include() na include-once(). Utofauti wao ni kuwa endapo iclude faili ambalo limetakiwa kuwa katika include halipo code zinatoa warning lakini zinafanya kazi. Lakini endapo require imetumika na kama faili hakipo italeta error na hutoweza kuendelea na program.
Hapa chini nitakupa mifano 2 ambapo mafaili hayapo. Yaani nitatumia include kwa faili ambalo halipo uone inavyokuwa. Kisha nitatumia require kwa faili ambalo halipo na itakavyokuwa.
include 'head.php';
//ujumbe huu huwezi kuuona kama tungetumia reuire
echo "Haloo hapo juu faili halipo lakini php imeendelea kutoa matokeo ya code nyingine."
?>
...
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
Katika somo hili utakwenda kujifunza concept ya iteration kwenye PHP OOP hapa tutakwenda kuiona jinsi inavyofanya kazi pamoja na foreach loop
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza jisniya kutuma email kwa kutumia PHPMailer kwenye project ya PHP. Katika somo hili tutakwend akutuma email kwa kutumia localhost.
Soma Zaidi...Somo hili litakwenda kukutajia baadhi ya library za php ambazo hutumika kwa matumizi ya ORM
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutumia PDO kutengeneza database, kuteneneza table na kuingiza data moja na zaidi ya moja.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu Cookie Headers
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza kazi na matumizi ya construct function na desctruct function kwenye OOP
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutumia constatnt kwenye class.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwend akujifunza ni kwa namna gani utaweza kuzitumiadata za jsonkwenye program yako
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutumia taarifa ambazo zimekusanywa kutoka kwa mtumiaji ili kuweka kutatuwa hoja mbalimbali
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza aina za data ambazo hutumika kwenye PHP
Soma Zaidi...