picha

PHP -somo la 31: Matumizi ya include() na require() function kwenye php

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kuandika function za PHP kama require() na iclude()

INCLUDE, REQUIRE,  INCLUDE_ONCE na REQUIRE_ONCE

Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu matumizi ya hizi function 3 ambazo kwa pamoja zinahusika na kuhusisha kuhusisha mafaili ya code kwenye mafaili mengi, bila ya kuziandika kila wakati.

 

include()

Incdude hutumika kama unataka kutumia code za faili falni kwenye faili lingine. Kwa mfano unataka kuunganisha database. Sasa kuna mafaili 10 ambayo yanahitaji kutumia database. Hivyo katika hali ya kawaida itakubidi uandike code za kuunganisha database kwenye mafaili yote hayo. Hivyo basi kwa kutumia include tutaandika code hizo kwenye faili moja. Kisha tutatumia function hii ili kuweza kuzitumia kwenye mafaili yote hayo.

Kwa mfano tunataka kuweka menu yetu kwenye kurasa zetu. Hivyo tofauti na kuziandika menu hizo kila ukurasa basi tutatumia include() ili kuweza kuzifikia. Wacha tuone mifano halizi.Hapo chini tutatengeneza mafaili mawili. Moja ni kwa ajili ya menu na lingine tutatumia include ili kuweza kuzitumia menu kwenye file lingine.

 

Faili ambalo tutali include tutaliita menu.php na faili ambalo ltakuwa linatumia hizo code tutaliita home.php. Sasa endapo tutafunguwa faili la home.php litaonesha menu ambazo zipo kwenye file lingine.

 

Menu.php

 

 

 

 

   Android

   Html

   Video

   Contact

 

 

 

 


 

Sasa tunakwenda kuzi include code hizi kwenye ukurasa wetu wa home.php. Na tupate matokeo sawa ya menu hii kwenye ikurasa huo.

 

home.php

 

include 'menu.php';

?>

 

Kwa kutumia mfano kama huu unaweza ku include block nyingi za code. Kufanya hivi kutakupubguzia sana kazi. Baada ya kuandika code hizohizo kila wakati sasa utatumia function hiyo na kuzi include.

 

INCLUDE_ONE()

Function hii hufanana na hiyo iliyotangulia. Utofauti ni kuwa include siku zote itakapotumika ina include code hizo bila hata ya kujali kama zilisha kuwepo ama tayari faili hilo umesha li include. Angalia mfano huu

include 'menu.php';

include 'menu.php';

?>

 

Hapo utaona faili tume li include mara mbili hivy linatupa matokeo mara mbili. Lakini sasa ukitumia include_once() kwanza itaangalia kama hilo faili tayari lipo, itainclude mara moja tu.Kwa fano hapo juu kama tutatumia include_once() tutapata matokeo mara moja tu.

 

Wacha nitumie lugha nyingine kukuelewesha. Yaani once ni neno la kiingereza linalomaanisha mara moja tu. Hivyo basi ukisema include_once yaani include hilo faili mara moja tu. Hivyo hata kama uta include mara mbtatu au zaidi zote hazitafanya kazi. Mara moja tu ndio itakayotumiwa. Angalia mfano hapo chini.

 

include_once 'menu.php';

include_once 'menu.php';

?>

 

Tumepata matokeo mara moja tu wakati tumeinclude mara mbili.

 

Hivyo basi katika mafaili muhimu kama database, ama class au yanayohusika kwenye login mara nyingi hapa tunatumia include_once na kwenye code za kawaida kama style na zile static file huwa tunatumia include.

 

REQUIRE() na REQUIRE_ONCE()

Katika php require() na require_once() hufanya kazi sawa na include() na include-once(). Utofauti wao ni kuwa endapo iclude faili ambalo limetakiwa kuwa katika include halipo code zinatoa warning lakini zinafanya kazi. Lakini endapo require imetumika na kama faili hakipo italeta error na hutoweza kuendelea na program.

 

Hapa chini nitakupa mifano 2 ambapo mafaili hayapo. Yaani nitatumia include kwa faili ambalo halipo uone inavyokuwa. Kisha nitatumia require kwa faili ambalo halipo na itakavyokuwa.

include 'head.php';

//ujumbe huu huwezi kuuona kama tungetumia reuire

echo "Haloo hapo juu faili halipo lakini php imeendelea kutoa matokeo ya code nyingine."

?>

...

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: PHP Main: ICT File: Download PDF Views 819

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉2 web hosting    👉3 Madrasa kiganjani    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

PHP somo la 80: Authentication header

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu Authentication header, najinsi ya kutuma taarifa hizo na kuzisoma

Soma Zaidi...
PHP - somo la 12: Jinsi ya kufanyia kazi taarifa zilizokusanywa kutoka kwa mtumiaji

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutumia taarifa ambazo zimekusanywa kutoka kwa mtumiaji ili kuweka kutatuwa hoja mbalimbali

Soma Zaidi...
PHP BLOG - somo la 3: Jinsi ya kutengeneza table kwenye databse kwa ajili ya blog

Hapa utajifunza jinsi ya kutengeneza table ambayo tutaitumia kwenye blog yetu

Soma Zaidi...
PHP BLOG - somo la 2: Jinsi ya kutengeneza database na kuiunganisha kwenye blog

Katika somo hili unakwenda kujifunza jinsi y kutengeneza database na kuungansha kwenye blog yetu.

Soma Zaidi...
PHP - somo la 2: sheria za uandishi wa code za PHP

Katika somo hili utajifunza kuhusu syntax za PHP

Soma Zaidi...
PHP somo la 86: JInsi ya ku decode json yaani kubadili json kuwa php data kama array ana object

Katika somo hili utakwend akujifunza jinsi ya kubadili json data na kuwaphp array ama php object. Kwa ufupi tunakwend aku decode json data kuwa phparray amaobject

Soma Zaidi...
PHP BLOG - somo la 4: Jinsi ya kutengeneza ukurasa kwa ajili ya kupost

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutengeneza ukurasa wa kupost kwa kutumia html form

Soma Zaidi...
PHP - somo la 8: jinsi ya kuandika constant kwenye PHP

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kuandika constant kwenye PHP. Pia utajifunza utofauti wake na variable

Soma Zaidi...
Jinsi ya kutuma Email kwa kutumia PHP

Katika post hii utakwenda kujifunza jinsi ya kutuma email kwa kutumia php function ya email()

Soma Zaidi...
PHP somo la 73: Maana ya http header

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu http header, maana yake na jinsi ya kusoma taarifa zilizopo kwenye http header.

Soma Zaidi...