PHP -somo la 33: Matumizi ya while loop kwenye PHP

Katika somo hili utajifunza jinsi ya kuandika while loop kwenye PHP

LOOP: FOR,  WHILE,  DO, FOREACH

 

Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu logical condition. Hapa tutajifunza kuweka masharti maalumu wakati wa kupata matokeo ya code. 

 

Mfano unataka web yako iwe inasalimia kila mtu anapofunguwa.  Sasa shakani zipo tatu ya asubuhi, ya mchana na ya usiku. Hivyo utaweka masharti endapo itakuwa ni asubuhi iwe inasalaminia kwa kusema habari ya asubuhi,  na ikiwa ni mchana iseme habari ya mchana na ikiwa jioni iseme habari ya jioni. 

 

Katika level 1 tulijifunza kuhusu if….. else na else if…… else. Katika level hii tutakwenda kujifunza condition zilizobakia ambazo ni: -

  1. While
  2. For
  3. Do
  4. Foreach

 

Ni nini maana ya loop? 

Loop ni hali ya kuendelea kwa kujirudia rudia. Chukulia mfano una audio list sasa unataka ubplay moja iwe inajirudia rudia hapo utakuwa unafanya loop. 

 

Sasa kwenye code loop ni pale code zinapojirudia rudia kufanya kazi (excute) kutokana na mashart yaliyowekwa (conditions). 

 

Wacha tuone kwa mifano moja baada ya nyingine. 

 

  1. WHILE LOOP

Hii ni loop ambayo code zitakuwa zinajirudia rudia kufanya kazi maadamu mashart yaliyowekwa yanaruhusu. 

 

Mfano 1: 

Tunataka kuandika kuorodhesha namba kutoka moja hadi 10. Hapo ni kuwa tutaanza kuandika kuanzia moja mpaka ifike kumi. 

 

Inamaana kuwa namba zitaendelea kuandikwa maadamu kumi haijafikiwa. Itakapofikiwa tu basi hapo code zitawacha kufanya kazi. 

 

Kanuni za kuandika while loop

  1. Kwanza utaanza na neno while likifuatiwa na mabano. 
  2. Ndani ya mabano weka masharti yako yaani condition
  3. Kisha weka mabano mengine ambayo ndipo utaweka code zako ambazo zitafanya kazi kama masharti yatafikiwa. 
  4. Mabano ya kwanza ni haya () na ya pili ni haya {}
  5. Hivyo basi code zitaonekana katika mtindo huu

while(shart) {

Code zinakaa hapa

}

 

Jinsi ya ku print tebo ya kwanza: 

Kwanza tutaanza kuandaa variable.  Tutaiita x kisha tuione thamani ya 0.

$x = 0;

 

Kisha sasa tutaweka while ndani yake shart letu ni kuwa $x iwe ni sawa ama ndogo kuliko 12. Hiyo 12 ndio mwisho wa tebo yetu. Hivyo itakuwa kama hivi while($x <=12).

 

Baada ya hapo tutaweka code ambazo zitakwenda kuandika tebo yetu kulingana na sharti hilo la kuwa ndogo ama sawasawa na 12. Hivyo itaonekana kama hivi {echo $x++}

 

Code nzima itakuwa hvi

<?php

$x = 0;

while($x <= 12){

echo $x++, "<br>";

}

 

?>

...

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: PHP Main: ICT File: Download PDF Views 624

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Dua za Mitume na Manabii    👉4 Bongolite - Game zone - Play free game    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina   

Post zinazofanana:

PHP - somo la 3: Maana ya variable na inavyoandika kwenye PHP

Katika somo hili utakwenda kujifunza kujusu PHP variable, maana yake na sheria za uandishi wa variable

Soma Zaidi...
PHP - somo la 15: Jinsi ya kutengeneza table kwenye database kwa kutumia PHP

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutumia PHP kutengeneza tabale kwenye database ya mysql .

Soma Zaidi...
PHP BLOG - somo la 2: Jinsi ya kutengeneza database na kuiunganisha kwenye blog

Katika somo hili unakwenda kujifunza jinsi y kutengeneza database na kuungansha kwenye blog yetu.

Soma Zaidi...
PHP - somo la 5: Maana ya function na jinsi inavyotengenezwa kwa ktumia PHP

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu function kwenye PHP na jinsi ya kuweza kuzitumia

Soma Zaidi...
PHP somo la 57: class traits kwenye PHP

Katika somo hili utakwenda kujifunza concept ya traits kwenye OOP. hii itakusaidia ku solve baadhi ya changamoto zinazotokana na inheritance

Soma Zaidi...
PHP somo la 90: Jinsi ya kutumia json data kama blog post

Katika somo hili utaweza kujifunza ni kwa nambna gani utaweza kutengeneza blog post na kuisoma kwa kutumia data za json

Soma Zaidi...
PHP somo la 91: Mambo ya kuzingatia unapokuwa unashughulika na data za json

Haya ni mabo ya kuzingatia unapo encode ama ku decode data za json

Soma Zaidi...
PHP - somo la 1: Maana ya PHP na jinsi inavyofanya kazi

Katika somo hili utakwenda kujifunza maana ya PHP na jinsi inavyofanya kazi

Soma Zaidi...
PHP somola 78: Cookie Headers

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu Cookie Headers

Soma Zaidi...
PHP - somo la 12: Jinsi ya kufanyia kazi taarifa zilizokusanywa kutoka kwa mtumiaji

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutumia taarifa ambazo zimekusanywa kutoka kwa mtumiaji ili kuweka kutatuwa hoja mbalimbali

Soma Zaidi...