picha

PHP -somo la 33: Matumizi ya while loop kwenye PHP

Katika somo hili utajifunza jinsi ya kuandika while loop kwenye PHP

LOOP: FOR,  WHILE,  DO, FOREACH

 

Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu logical condition. Hapa tutajifunza kuweka masharti maalumu wakati wa kupata matokeo ya code. 

 

Mfano unataka web yako iwe inasalimia kila mtu anapofunguwa.  Sasa shakani zipo tatu ya asubuhi, ya mchana na ya usiku. Hivyo utaweka masharti endapo itakuwa ni asubuhi iwe inasalaminia kwa kusema habari ya asubuhi,  na ikiwa ni mchana iseme habari ya mchana na ikiwa jioni iseme habari ya jioni. 

 

Katika level 1 tulijifunza kuhusu if….. else na else if…… else. Katika level hii tutakwenda kujifunza condition zilizobakia ambazo ni: -

  1. While
  2. For
  3. Do
  4. Foreach

 

Ni nini maana ya loop? 

Loop ni hali ya kuendelea kwa kujirudia rudia. Chukulia mfano una audio list sasa unataka ubplay moja iwe inajirudia rudia hapo utakuwa unafanya loop. 

 

Sasa kwenye code loop ni pale code zinapojirudia rudia kufanya kazi (excute) kutokana na mashart yaliyowekwa (conditions). 

 

Wacha tuone kwa mifano moja baada ya nyingine. 

 

  1. WHILE LOOP

Hii ni loop ambayo code zitakuwa zinajirudia rudia kufanya kazi maadamu mashart yaliyowekwa yanaruhusu. 

 

Mfano 1: 

Tunataka kuandika kuorodhesha namba kutoka moja hadi 10. Hapo ni kuwa tutaanza kuandika kuanzia moja mpaka ifike kumi. 

 

Inamaana kuwa namba zitaendelea kuandikwa maadamu kumi haijafikiwa. Itakapofikiwa tu basi hapo code zitawacha kufanya kazi. 

 

Kanuni za kuandika while loop

  1. Kwanza utaanza na neno while likifuatiwa na mabano. 
  2. Ndani ya mabano weka masharti yako yaani condition
  3. Kisha weka mabano mengine ambayo ndipo utaweka code zako ambazo zitafanya kazi kama masharti yatafikiwa. 
  4. Mabano ya kwanza ni haya () na ya pili ni haya {}
  5. Hivyo basi code zitaonekana katika mtindo huu

while(shart) {

Code zinakaa hapa

}

 

Jinsi ya ku print tebo ya kwanza: 

Kwanza tutaanza kuandaa variable.  Tutaiita x kisha tuione thamani ya 0.

$x = 0;

 

Kisha sasa tutaweka while ndani yake shart letu ni kuwa $x iwe ni sawa ama ndogo kuliko 12. Hiyo 12 ndio mwisho wa tebo yetu. Hivyo itakuwa kama hivi while($x <=12).

 

Baada ya hapo tutaweka code ambazo zitakwenda kuandika tebo yetu kulingana na sharti hilo la kuwa ndogo ama sawasawa na 12. Hivyo itaonekana kama hivi {echo $x++}

 

Code nzima itakuwa hvi

<?php

$x = 0;

while($x <= 12){

echo $x++, "<br>";

}

 

?>

...

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2023-10-18 Topic: PHP Main: ICT File: Download PDF Views 756

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 ai web app    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 web hosting   

Post zinazofanana:

PHP - somo la 10: Jinsi ya kundika condition statement if, ifelse na switch case

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu condition statements if, ifelse na switch case. Hata utajifunza jnsi ya kuziandika na zinavyofanya kazi

Soma Zaidi...
PHP - somo la 37: Jinsi ya kutengeneza blog post kwa kutumia PHP

Katika somo hili utajifunza jinsi ambavyo unaweza kutengeneza blog ambayo utaweza ku upload faili na kuandika makala kwa kutumia PHP

Soma Zaidi...
PHP BLOG - somo la 3: Jinsi ya kutengeneza table kwenye databse kwa ajili ya blog

Hapa utajifunza jinsi ya kutengeneza table ambayo tutaitumia kwenye blog yetu

Soma Zaidi...
PHP somo la 66: Jinsi ya ku edit data na kufuta kwenye database kwa kutumia PDO

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi jinsi ya ku edit ama ku update data na kuzifuta kwenye database kwa kutumia PDO

Soma Zaidi...
PHP - somo la 2: sheria za uandishi wa code za PHP

Katika somo hili utajifunza kuhusu syntax za PHP

Soma Zaidi...
PHP BLOG - somo la 7: Jinsi ya kutengeneza ukurasa wa kusoma post kwenye blog

HApa utakwenda kujifunza sasa namna ya kuzisoma post kutoka kwenye blog

Soma Zaidi...
PHP - somo la 32: Jinsi ya kutumia filter_var() function kwenye PHP

Katika somo hili utajifunza jinsi ya kutumia filter_var() function kwa ajili ya kuchuja code zilizo hatari kwenye PHP file

Soma Zaidi...
PHP - somo la 45: Jinsi ya kutuma sms kwa kutumia PHP

Katika soko hili takwenda kujufunza jinsi ya kutuma sms kwa kutumia PHP. Hii itasaidia kama unataka kutuma OTP yaqni Onetime password

Soma Zaidi...
PHP somo la 52: Aina za access modifire na zinavyotofautiana.

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu access modifier ili kuweza kuthibiti nama ya kuzitumia properties kwenye class.

Soma Zaidi...
Jinsi ya kupata location ya mtu lwa kutumia IP address

Katika post hii utajifunza jinsi ya kupata taarifa muhimu za mtumiaji kw akutumia Ip address yake.

Soma Zaidi...