PHP -somo la 33: Matumizi ya while loop kwenye PHP

Katika somo hili utajifunza jinsi ya kuandika while loop kwenye PHP

LOOP: FOR,  WHILE,  DO, FOREACH

 

Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu logical condition. Hapa tutajifunza kuweka masharti maalumu wakati wa kupata matokeo ya code. 

 

Mfano unataka web yako iwe inasalimia kila mtu anapofunguwa.  Sasa shakani zipo tatu ya asubuhi, ya mchana na ya usiku. Hivyo utaweka masharti endapo itakuwa ni asubuhi iwe inasalaminia kwa kusema habari ya asubuhi,  na ikiwa ni mchana iseme habari ya mchana na ikiwa jioni iseme habari ya jioni. 

 

Katika level 1 tulijifunza kuhusu if….. else na else if…… else. Katika level hii tutakwenda kujifunza condition zilizobakia ambazo ni: -

  1. While
  2. For
  3. Do
  4. Foreach

 

Ni nini maana ya loop? 

Loop ni hali ya kuendelea kwa kujirudia rudia. Chukulia mfano una audio list sasa unataka ubplay moja iwe inajirudia rudia hapo utakuwa unafanya loop. 

 

Sasa kwenye code loop ni pale code zinapojirudia rudia kufanya kazi (excute) kutokana na mashart yaliyowekwa (conditions). 

 

Wacha tuone kwa mifano moja baada ya nyingine. 

 

  1. WHILE LOOP

Hii ni loop ambayo code zitakuwa zinajirudia rudia kufanya kazi maadamu mashart yaliyowekwa yanaruhusu. 

 

Mfano 1: 

Tunataka kuandika kuorodhesha namba kutoka moja hadi 10. Hapo ni kuwa tutaanza kuandika kuanzia moja mpaka ifike kumi. 

 

Inamaana kuwa namba zitaendelea kuandikwa maadamu kumi haijafikiwa. Itakapofikiwa tu basi hapo code zitawacha kufanya kazi. 

 

Kanuni za kuandika while loop

  1. Kwanza utaanza na neno while likifuatiwa na mabano. 
  2. Ndani ya mabano weka masharti yako yaani condition
  3. Kisha weka mabano mengine ambayo ndipo utaweka code zako ambazo zitafanya kazi kama masharti yatafikiwa. 
  4. Mabano ya kwanza ni haya () na ya pili ni haya {}
  5. Hivyo basi code zitaonekana katika mtindo huu

while(shart) {

Code zinakaa hapa

}

 

Jinsi ya ku print tebo ya kwanza: 

Kwanza tutaanza kuandaa variable.  Tutaiita x kisha tuione thamani ya 0.

$x = 0;

 

Kisha sasa tutaweka while ndani yake shart letu ni kuwa $x iwe ni sawa ama ndogo kuliko 12. Hiyo 12 ndio mwisho wa tebo yetu. Hivyo itakuwa kama hivi while($x <=12).

 

Baada ya hapo tutaweka code ambazo zitakwenda kuandika tebo yetu kulingana na sharti hilo la kuwa ndogo ama sawasawa na 12. Hivyo itaonekana kama hivi {echo $x++}

 

Code nzima itakuwa hvi

<?php

$x = 0;

while($x <= 12){

echo $x++, "<br>";

}

 

?>

...

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: PHP Main: ICT File: Download PDF Views 376

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Madrasa kiganjani    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

PHP somo la 74: aina za http headerna server variable

Katika somo hii utakwenda kujifunza aina za http header na server variable. Hapa tutakwenda kuchambuwa mgawanyiko wa httpheader na kazi zake.

Soma Zaidi...
PHP - somo la 1: Maana ya PHP na jinsi inavyofanya kazi

Katika somo hili utakwenda kujifunza maana ya PHP na jinsi inavyofanya kazi

Soma Zaidi...
PHP somo la 84: Maana ya JSON na sheria za kuandika faili la json

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu Maana ya JSON na sheria za kuandika faili la json

Soma Zaidi...
PHP - somo la 21: Jinsi ya kutafuta kitu kwenye database kwa mutumia PHP

Katika somo hili utakwenda kujifundisha jinsi ya kutafuta taarifa maalumu kwenye database kwa kutumia PHP

Soma Zaidi...
PHP BLOG - somo la 3: Jinsi ya kutengeneza table kwenye databse kwa ajili ya blog

Hapa utajifunza jinsi ya kutengeneza table ambayo tutaitumia kwenye blog yetu

Soma Zaidi...
PHP - somo la 39: Jinsi ya kutengeneza mafaili na mafolda kwenye server kwa kutumia PHP

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kuzungumza na server ili kutengeneza mafaili, mafolda, kufuta na ku edit kwa kutumia PHP.

Soma Zaidi...
PHP -somo la 31: Matumizi ya include() na require() function kwenye php

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kuandika function za PHP kama require() na iclude()

Soma Zaidi...
PHP - somo la 32: Jinsi ya kutumia filter_var() function kwenye PHP

Katika somo hili utajifunza jinsi ya kutumia filter_var() function kwa ajili ya kuchuja code zilizo hatari kwenye PHP file

Soma Zaidi...
PHP - somo la 30: Baadhi function za PHP

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya ktumia baadhi ya function za php

Soma Zaidi...
PHP BLOG - somo la 1: Utangulizi na jinsi ya kuandaa kwa ajili ya somo

Katika course hii utakwenda kujifundisha jinsi ya lutengeneza blog kutoka mwanzo hadi mwisho.

Soma Zaidi...