Katika somo hili utajifunza jinsi ya kuandika while loop kwenye PHP
LOOP: FOR, WHILE, DO, FOREACH
Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu logical condition. Hapa tutajifunza kuweka masharti maalumu wakati wa kupata matokeo ya code.
Mfano unataka web yako iwe inasalimia kila mtu anapofunguwa. Sasa shakani zipo tatu ya asubuhi, ya mchana na ya usiku. Hivyo utaweka masharti endapo itakuwa ni asubuhi iwe inasalaminia kwa kusema habari ya asubuhi, na ikiwa ni mchana iseme habari ya mchana na ikiwa jioni iseme habari ya jioni.
Katika level 1 tulijifunza kuhusu if….. else na else if…… else. Katika level hii tutakwenda kujifunza condition zilizobakia ambazo ni: -
Ni nini maana ya loop?
Loop ni hali ya kuendelea kwa kujirudia rudia. Chukulia mfano una audio list sasa unataka ubplay moja iwe inajirudia rudia hapo utakuwa unafanya loop.
Sasa kwenye code loop ni pale code zinapojirudia rudia kufanya kazi (excute) kutokana na mashart yaliyowekwa (conditions).
Wacha tuone kwa mifano moja baada ya nyingine.
Hii ni loop ambayo code zitakuwa zinajirudia rudia kufanya kazi maadamu mashart yaliyowekwa yanaruhusu.
Mfano 1:
Tunataka kuandika kuorodhesha namba kutoka moja hadi 10. Hapo ni kuwa tutaanza kuandika kuanzia moja mpaka ifike kumi.
Inamaana kuwa namba zitaendelea kuandikwa maadamu kumi haijafikiwa. Itakapofikiwa tu basi hapo code zitawacha kufanya kazi.
Kanuni za kuandika while loop
while(shart) {
Code zinakaa hapa
}
Jinsi ya ku print tebo ya kwanza:
Kwanza tutaanza kuandaa variable. Tutaiita x kisha tuione thamani ya 0.
$x = 0;
Kisha sasa tutaweka while ndani yake shart letu ni kuwa $x iwe ni sawa ama ndogo kuliko 12. Hiyo 12 ndio mwisho wa tebo yetu. Hivyo itakuwa kama hivi while($x <=12).
Baada ya hapo tutaweka code ambazo zitakwenda kuandika tebo yetu kulingana na sharti hilo la kuwa ndogo ama sawasawa na 12. Hivyo itaonekana kama hivi {echo $x++}
Code nzima itakuwa hvi
<?php
$x = 0;
while($x <= 12){
echo $x++, "<br>";
}
?>
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua. Umeionaje Makala hii.. ? Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutumia database ya sqlite kwa kutumia PHP. Katika somo hili utajifunza jinsi ya kutuma email kwa kutumia email() function ya PHP. Hii ni njia rahisi zaidi ya kutuma email. Ila hufanya kazi kwenye hosting. Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutengeneza ukurasa wa kupost kwa kutumia html form Katika somo hili utajifunza jinsiya kufanya hashing taarifa muhimu kama password. Kufanya hashing kunaongeza usalama wa taarifa za waumiaji kwenye blog yako. katika somo hili utajifunza jinsi ya ku upload multiple file yaani mafaili mengi kwa wakati mmoja kwa kutumia PHP Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu Authentication header, najinsi ya kutuma taarifa hizo na kuzisoma Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu Cross - Orgn Resource Sharing ama inafupishwa kama CORSE header Katika somo hili utakwendakujifunza concept ya namespaces na jinsi inavyosaidi kwenye OOP Katika somo hili utakwenda kuhifunza kuhusu Custom header na aina zake Katika somo hii utakwenda kujifunza aina za http header na server variable. Hapa tutakwenda kuchambuwa mgawanyiko wa httpheader na kazi zake. ...
Download App Yetu
👉1
Madrasa kiganjani
👉2
Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
👉3
Simulizi za Hadithi Audio
👉4
kitabu cha Simulizi
👉5
Kitau cha Fiqh
👉6
Bongolite - Game zone - Play free game
Post zinazofanana:
PHP somo la 92: Jinsi ya kuunganisha php na database ya sqlite
PHP - somo la 43: Jinsi ya kutuma email kwa kutumia PHP
PHP BLOG - somo la 4: Jinsi ya kutengeneza ukurasa kwa ajili ya kupost
PHP - somo la 41: Jinsi ya kufanya hashing kwenye PHP
PHP - somo la 38: Jinsi ya ku upload mafaili zaidi ya moja kwa kutumia PHP
PHP somo la 80: Authentication header
PHP somo la 81: Cross - Orgn Resource Sharing - CORSE header
PHP somo la 60: namespace na matumizi yake kwenye PHP
PHP somo la 79: Custom header
PHP somo la 74: aina za http headerna server variable