Katika somo hili utajifunza jinsi ya kuandika while loop kwenye PHP
LOOP: FOR, WHILE, DO, FOREACH
Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu logical condition. Hapa tutajifunza kuweka masharti maalumu wakati wa kupata matokeo ya code.
Mfano unataka web yako iwe inasalimia kila mtu anapofunguwa. Sasa shakani zipo tatu ya asubuhi, ya mchana na ya usiku. Hivyo utaweka masharti endapo itakuwa ni asubuhi iwe inasalaminia kwa kusema habari ya asubuhi, na ikiwa ni mchana iseme habari ya mchana na ikiwa jioni iseme habari ya jioni.
Katika level 1 tulijifunza kuhusu if….. else na else if…… else. Katika level hii tutakwenda kujifunza condition zilizobakia ambazo ni: -
Ni nini maana ya loop?
Loop ni hali ya kuendelea kwa kujirudia rudia. Chukulia mfano una audio list sasa unataka ubplay moja iwe inajirudia rudia hapo utakuwa unafanya loop.
Sasa kwenye code loop ni pale code zinapojirudia rudia kufanya kazi (excute) kutokana na mashart yaliyowekwa (conditions).
Wacha tuone kwa mifano moja baada ya nyingine.
Hii ni loop ambayo code zitakuwa zinajirudia rudia kufanya kazi maadamu mashart yaliyowekwa yanaruhusu.
Mfano 1:
Tunataka kuandika kuorodhesha namba kutoka moja hadi 10. Hapo ni kuwa tutaanza kuandika kuanzia moja mpaka ifike kumi.
Inamaana kuwa namba zitaendelea kuandikwa maadamu kumi haijafikiwa. Itakapofikiwa tu basi hapo code zitawacha kufanya kazi.
Kanuni za kuandika while loop
while(shart) {
Code zinakaa hapa
}
Jinsi ya ku print tebo ya kwanza:
Kwanza tutaanza kuandaa variable. Tutaiita x kisha tuione thamani ya 0.
$x = 0;
Kisha sasa tutaweka while ndani yake shart letu ni kuwa $x iwe ni sawa ama ndogo kuliko 12. Hiyo 12 ndio mwisho wa tebo yetu. Hivyo itakuwa kama hivi while($x <=12).
Baada ya hapo tutaweka code ambazo zitakwenda kuandika tebo yetu kulingana na sharti hilo la kuwa ndogo ama sawasawa na 12. Hivyo itaonekana kama hivi {echo $x++}
Code nzima itakuwa hvi
<?php
$x = 0;
while($x <= 12){
echo $x++, "<br>";
}
?>
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu Umeionaje Makala hii.. ? Katika post hii utakwenda kujifunza jinsi ya kutuma email kwa kutumia php function ya email() Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu http header, maana yake na jinsi ya kusoma taarifa zilizopo kwenye http header. Katika somo hili uttakwend akujifunz ajinsi ambavyo utaweza kutengeneza simple ORM yakwako mwenyewe Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu Cookie Headers Katika somo hili utakwend kujifunza kuhusu static property na jnsi inavyotumika Katika somo hili utakwenda kujifunza aina kuu 3 za variable katika PHP mabzo ni local variable, global variable na static variable. Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu Maana ya JSON na sheria za kuandika faili la json Katika somo hili utakwenda kujifunza jisniya kutuma email kwa kutumia PHPMailer kwenye project ya PHP. Katika somo hili tutakwend akutuma email kwa kutumia localhost. Katika somo hili utakwend akujifunza ni kwa namna gani utaweza kuzitumiadata za jsonkwenye program yako Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu function kwenye PHP na jinsi ya kuweza kuzitumia ...
👉1
Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
👉2
Kitabu cha Afya
👉3
kitabu cha Simulizi
👉4
Kitau cha Fiqh
👉5
Bongolite - Game zone - Play free game
👉6
Madrasa kiganjani
Post zinazofanana:
Jinsi ya kutuma Email kwa kutumia PHP
PHP somo la 73: Maana ya http header
PHP somo la 95: Jinsi ya kutengeneza customer ORM
PHP somola 78: Cookie Headers
PHP somo la 59: static property kwenye PHP
PHP - somo la 27: aina za variable kwenye PHP
PHP somo la 84: Maana ya JSON na sheria za kuandika faili la json
PHP somo la 68: Jinsi ya kutuma email kwa kutumia PHPMailer
PHP somo la 89: Jinsi ya kutumia data za json kwenye program ya php na html
PHP - somo la 5: Maana ya function na jinsi inavyotengenezwa kwa ktumia PHP