PHP -somo la 33: Matumizi ya while loop kwenye PHP

Katika somo hili utajifunza jinsi ya kuandika while loop kwenye PHP

LOOP: FOR,  WHILE,  DO, FOREACH

 

Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu logical condition. Hapa tutajifunza kuweka masharti maalumu wakati wa kupata matokeo ya code. 

 

Mfano unataka web yako iwe inasalimia kila mtu anapofunguwa.  Sasa shakani zipo tatu ya asubuhi, ya mchana na ya usiku. Hivyo utaweka masharti endapo itakuwa ni asubuhi iwe inasalaminia kwa kusema habari ya asubuhi,  na ikiwa ni mchana iseme habari ya mchana na ikiwa jioni iseme habari ya jioni. 

 

Katika level 1 tulijifunza kuhusu if….. else na else if…… else. Katika level hii tutakwenda kujifunza condition zilizobakia ambazo ni: -

  1. While
  2. For
  3. Do
  4. Foreach

 

Ni nini maana ya loop? 

Loop ni hali ya kuendelea kwa kujirudia rudia. Chukulia mfano una audio list sasa unataka ubplay moja iwe inajirudia rudia hapo utakuwa unafanya loop. 

 

Sasa kwenye code loop ni pale code zinapojirudia rudia kufanya kazi (excute) kutokana na mashart yaliyowekwa (conditions). 

 

Wacha tuone kwa mifano moja baada ya nyingine. 

 

  1. WHILE LOOP

Hii ni loop ambayo code zitakuwa zinajirudia rudia kufanya kazi maadamu mashart yaliyowekwa yanaruhusu. 

 

Mfano 1: 

Tunataka kuandika kuorodhesha namba kutoka moja hadi 10. Hapo ni kuwa tutaanza kuandika kuanzia moja mpaka ifike kumi. 

 

Inamaana kuwa namba zitaendelea kuandikwa maadamu kumi haijafikiwa. Itakapofikiwa tu basi hapo code zitawacha kufanya kazi. 

 

Kanuni za kuandika while loop

  1. Kwanza utaanza na neno while likifuatiwa na mabano. 
  2. Ndani ya mabano weka masharti yako yaani condition
  3. Kisha weka mabano mengine ambayo ndipo utaweka code zako ambazo zitafanya kazi kama masharti yatafikiwa. 
  4. Mabano ya kwanza ni haya () na ya pili ni haya {}
  5. Hivyo basi code zitaonekana katika mtindo huu

while(shart) {

Code zinakaa hapa

}

 

Jinsi ya ku print tebo ya kwanza: 

Kwanza tutaanza kuandaa variable.  Tutaiita x kisha tuione thamani ya 0.

$x = 0;

 

Kisha sasa tutaweka while ndani yake shart letu ni kuwa $x iwe ni sawa ama ndogo kuliko 12. Hiyo 12 ndio mwisho wa tebo yetu. Hivyo itakuwa kama hivi while($x <=12).

 

Baada ya hapo tutaweka code ambazo zitakwenda kuandika tebo yetu kulingana na sharti hilo la kuwa ndogo ama sawasawa na 12. Hivyo itaonekana kama hivi {echo $x++}

 

Code nzima itakuwa hvi

<?php

$x = 0;

while($x <= 12){

echo $x++, "<br>";

}

 

?>

...

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: PHP Main: ICT File: Download PDF Views 484

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Dua za Mitume na Manabii    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

PHP - somo la 62: Project ya CRUDE operation kwa kutumia PHP - OOP na MySQL database

Katika project hii utakwenda kujifunza jinsi ya kufanya CRUDE operation kwa kutumia PHP OOP na MySQL database.

Soma Zaidi...
PHP somo la 65: Jinsi ya kusoma data kwenye database kwa kutumia PDO

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kusoma data kwenye database kwa kutumia PDO.

Soma Zaidi...
PHP somo la 77: aina za http redirect

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu http redirect header

Soma Zaidi...
PHP - somo la 39: Jinsi ya kutengeneza mafaili na mafolda kwenye server kwa kutumia PHP

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kuzungumza na server ili kutengeneza mafaili, mafolda, kufuta na ku edit kwa kutumia PHP.

Soma Zaidi...
PHP - somo la 16: Jinsi ya kufuta tabale na database kwa kutumia php

Katika somo hili utajifunza jinsi ya kufuta table ya databse kwa kutumia PHP. Pia utajifunza jinsi ya kututa database yeto

Soma Zaidi...
PHP somo la 91: Mambo ya kuzingatia unapokuwa unashughulika na data za json

Haya ni mabo ya kuzingatia unapo encode ama ku decode data za json

Soma Zaidi...
PHP somo la 58: static method kwenye PHP

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu static method na inavtotumika kwenye OOP

Soma Zaidi...
PHP somo la 75: Content-Type Header

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu content-type header.

Soma Zaidi...
PHP somo la 83: Server Variables

Katika somo hili utakwend akujifunza kuhusu server variables

Soma Zaidi...
PHP somo la 87: Jinsi ya kuangalia error wakati wa ku decode na ku encode json data

Katika somo hili utakwenda kujifunza jisni ya kudhibiti error ambazo zinaweza kutokea wakati wa ku encode na ku decoe json data

Soma Zaidi...