Katika somo hili utajifunza jinsi ya kuandika while loop kwenye PHP
LOOP: FOR, WHILE, DO, FOREACH
Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu logical condition. Hapa tutajifunza kuweka masharti maalumu wakati wa kupata matokeo ya code.
Mfano unataka web yako iwe inasalimia kila mtu anapofunguwa. Sasa shakani zipo tatu ya asubuhi, ya mchana na ya usiku. Hivyo utaweka masharti endapo itakuwa ni asubuhi iwe inasalaminia kwa kusema habari ya asubuhi, na ikiwa ni mchana iseme habari ya mchana na ikiwa jioni iseme habari ya jioni.
Katika level 1 tulijifunza kuhusu if….. else na else if…… else. Katika level hii tutakwenda kujifunza condition zilizobakia ambazo ni: -
Ni nini maana ya loop?
Loop ni hali ya kuendelea kwa kujirudia rudia. Chukulia mfano una audio list sasa unataka ubplay moja iwe inajirudia rudia hapo utakuwa unafanya loop.
Sasa kwenye code loop ni pale code zinapojirudia rudia kufanya kazi (excute) kutokana na mashart yaliyowekwa (conditions).
Wacha tuone kwa mifano moja baada ya nyingine.
Hii ni loop ambayo code zitakuwa zinajirudia rudia kufanya kazi maadamu mashart yaliyowekwa yanaruhusu.
Mfano 1:
Tunataka kuandika kuorodhesha namba kutoka moja hadi 10. Hapo ni kuwa tutaanza kuandika kuanzia moja mpaka ifike kumi.
Inamaana kuwa namba zitaendelea kuandikwa maadamu kumi haijafikiwa. Itakapofikiwa tu basi hapo code zitawacha kufanya kazi.
Kanuni za kuandika while loop
while(shart) {
Code zinakaa hapa
}
Jinsi ya ku print tebo ya kwanza:
Kwanza tutaanza kuandaa variable. Tutaiita x kisha tuione thamani ya 0.
$x = 0;
Kisha sasa tutaweka while ndani yake shart letu ni kuwa $x iwe ni sawa ama ndogo kuliko 12. Hiyo 12 ndio mwisho wa tebo yetu. Hivyo itakuwa kama hivi while($x <=12).
Baada ya hapo tutaweka code ambazo zitakwenda kuandika tebo yetu kulingana na sharti hilo la kuwa ndogo ama sawasawa na 12. Hivyo itaonekana kama hivi {echo $x++}
Code nzima itakuwa hvi
<?php
$x = 0;
while($x <= 12){
echo $x++, "<br>";
}
?>
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu Umeionaje Makala hii.. ? Katika somo hii utakwenda kujifunza aina za http header na server variable. Hapa tutakwenda kuchambuwa mgawanyiko wa httpheader na kazi zake. Katika somo hili utakwenda kujifunza maana ya PHP na jinsi inavyofanya kazi Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu Maana ya JSON na sheria za kuandika faili la json Katika somo hili utakwenda kujifundisha jinsi ya kutafuta taarifa maalumu kwenye database kwa kutumia PHP Hapa utajifunza jinsi ya kutengeneza table ambayo tutaitumia kwenye blog yetu Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kuzungumza na server ili kutengeneza mafaili, mafolda, kufuta na ku edit kwa kutumia PHP. Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kuandika function za PHP kama require() na iclude() Katika somo hili utajifunza jinsi ya kutumia filter_var() function kwa ajili ya kuchuja code zilizo hatari kwenye PHP file Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya ktumia baadhi ya function za php Katika course hii utakwenda kujifundisha jinsi ya lutengeneza blog kutoka mwanzo hadi mwisho. ...
👉1
Simulizi za Hadithi Audio
👉2
Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
👉3
Kitau cha Fiqh
👉4
Madrasa kiganjani
👉5
kitabu cha Simulizi
👉6
Kitabu cha Afya
Post zinazofanana:
PHP somo la 74: aina za http headerna server variable
PHP - somo la 1: Maana ya PHP na jinsi inavyofanya kazi
PHP somo la 84: Maana ya JSON na sheria za kuandika faili la json
PHP - somo la 21: Jinsi ya kutafuta kitu kwenye database kwa mutumia PHP
PHP BLOG - somo la 3: Jinsi ya kutengeneza table kwenye databse kwa ajili ya blog
PHP - somo la 39: Jinsi ya kutengeneza mafaili na mafolda kwenye server kwa kutumia PHP
PHP -somo la 31: Matumizi ya include() na require() function kwenye php
PHP - somo la 32: Jinsi ya kutumia filter_var() function kwenye PHP
PHP - somo la 30: Baadhi function za PHP
PHP BLOG - somo la 1: Utangulizi na jinsi ya kuandaa kwa ajili ya somo