Katika somo hilivutajifunza namna ya kutumia HTML form. Namna ya kuookea taarifa kutoka kwenye madodoso ya html form.
SOMO LA 11
HTML FORM
Ili uweze kujaza madodoso kwa kutumia fomu ya HTML utahitaji sehemu ya kwenda hayo madodoso baada ya kujazwa. Kwa kutumia HTML utaweza kutuma na kupokea taarifa zilizokazwa kutoka katika fomu ya html.
Angalia fomu hiyo hapo chini.
<html>
<form method="post" action="">
<label>first name</label>:<br>
<input type="text" name="firstname">
<br>
<label>last name</label><br>
<input type="text" name="lastname">
<input type="submit" name="">
</form>
</html>
Ukiingalia vyema fomu hii utagunduwa ipo katika namna hii:-
1.Kuna tag ya fomu <form kuonyesha kuwa hapa ndipo fomu inaanzia.
2.Katika tag ya form kuna attribute ambayo ni method <form method attribute hii kazi yake ni kueleza kuwa hizi taarifa za humu kwenye hii fomu baada ya kujazwa zitatumwa kwa njia ipi.
3.Katika attribute method value yake ni post. Hii ina maana njia itakayotumika kutuma taarifa hizi ni njia ya post.
4.Kisha kuna attribute nyingine ndani ta tag ya <form ambayo ni action, hii kazi yake ni kueleza je action zote katika fomu hii zitachakatwa katika faili lipi. Mfano kama utahitaji michakato ifanyikie kwingine kwa sababu za kiulinzi basi utaweka faili unalotaka kwenye value ya attribute action. Katika mfano wetu hapo juu ipengele hili kimeachwa wazi.inamaana action zote zitafanyika hapahapa.
5.Kuna lebo ya firstname na ya last name
6.Kisha kuna input type. Input type hapa ni taarifa ambazo unahitaji huyo mjazaji wa dodoso aweke. Kama unataka aweke email, hpo utaweka email. Katika mfano wetu huu input type ni text, yaani anachotakiwa ajaze mtu ni text ambazo ni herufi, namba na symbils.
7.Mwisho kuna batani ya kusabmit. Hii ndio batani ya kutumia dodoso. Yaani ukiibofya batani hii dodoso litakuwa limetumwa.batani hii yenyewe input type yake ni submit.
FORM METHODS
Kama nilivyogusia hapo juu ni kuwa method zipo mbili katika kutuma na kupokea madodoso kutoka kwenye html form moja ni POST na nyingine ni GET. Tunatumia post tunapotuma taarifa za siri, na tunatumia GET tunapotuma ama kupokea taarifa zisizo za usiri. Tutajifunza mengi zaidi kwenye mafunzo ya mbele. Na vinapotumika kwenye file huwa katika sura hii $_POST[''] au $_GET[''] ndani ya hayo mabano utaweka variable zako mfano $_POST['firstname'].
UKUSANYAJI WA DODOSO:
1.Kwanza lazima uandae fomu ya kuingiza hizo taarifa mfano tunahitaji kukusanya jina la kwanza na la pili. Hivyo fomu yetu itakuwa na input mbili.
Mfano:
<form method="post" action="#">
First name:<br>
<input type="text" name="firstname">
<br>
Last name:<br>
<input type="text" name="lastname">
<input type="submit" name="">
</form>
2.Kisha hatuwa inayofata ni kukusanya hizo taarifa yaani kuzipokea. Hapa tutahitaji kutengeneza variable ambazo zitapokea taarifa kutoka katika fomu. Variable hizi zinatakiwa zifanane na value ya name kwenye input type kwenye html form. Mfano kkwenye input type pale kwenye name ni firstname basi na variable yetu inatakiwa iwe hivyo hivyo firstname.
3.Kisha utaweka output kama itahitajika. Je unataka baada ya taarifa kukusanywa zifanye nini. Mfano tunataka zionyeshwe hivyo tutaunga jina la kwanz ana pili kupata jina zima.
4.Haya yote hufanyakika kwenye lile faili ulilolitaja kwenye action. Kama hukutaja faili basi code zeote za kufanya haya zifanyike kwenye faili moja na hiyo html form.
Cheki mfano wa code nzima hapo chini
<html>
<form method="post" action="#">
First name:<br>
<input type="text" name="firstname">
<br>
Last name:<br>
<input type="text" name="lastname">
<input type="submit" name="">
</form></html>
<?php
$firstname=$_POST['firstname'];
$lastname=$_POST['lastname'];
$fullname = "$firstname, $lastname"
echo $fullname;
?>
Kwa mfano huu mty ataingiza jina la kwanza kisha la pili, kisha variable ya full name itachanganya firstname na lastname ili kupata fullname. Baada ya hapo echo itadisplay full name.
Vyema kufanyia mazoezi tofautitofauti mifano hii. Katika muendelezo wa masomo haya tutakuja jifunza kwa mfano kama huu kuhifadhi taarifa hizi kwenye database.
Huu ndio mwisho wa masomo haya ya PHP level hii ya kwanza. Tutamalizia project kwenye kipindi cha 12 kisha tutafunga course. Course itakayofata itaingia ndani zaidi katika mafunzo haya. Hivyo nakusihi endelea kuwa nami hadi mwisho.
Mafunzo haya yanakujia kwa ihsani ya bongoclass
Web: www.bongoclass.com
Email:mafunzo@bongoclass.com
Phone: 0774069753 unaweza kunicheki wasap kwa link hii https://wa.me/message/7CTQP5BSWBR5I1
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Umeionaje Makala hii.. ?
Hapa utajifunza utofauti kati ya php constant na variable. Na hili ni somo la nane katika mfululizo wa masomo haya ya php level 1.
Soma Zaidi...Huu ni muendelezo wa mafunzo ya database kwa kutumia MySQL na hili ni somo la 6. Katika somo hili tutakwenda kuona jinsi ya kutengeneza table kwa kutumia MySQL na kwa kutuma SQL.
Soma Zaidi...Ktika somo hili la 7 utajifunza namna ya kuandaa na kujiandaa kutengeneza website ama blog. Pia utajifunza maandalizi ya kuhost
Soma Zaidi...Katika somo hili la php level 1 somo la 6 utajifunza namna ya kutumia tarehe yaani function date() kwenye PHP
Soma Zaidi...Haya ni mafunzo ya php na hili ni somo la tano. Katika somovhili utajifunza namna ya kutengeneza functions.
Soma Zaidi...Huu ni mwendelezo wa mafunzo ya database kwa kutumia MySQL na hili ni somo la nne katika mlolongo wa masomo haya. Katika somo hili utajifuza jinsi ya kubadili jina la database na kufuta database. Pia tutajifunza kutumia SQL kufanya hayo.
Soma Zaidi...Karibu tena katika somo la nne la mafunzo ya HTML level2 html full course for beginners. Katika somo hili utajifunza kuhusu attributes na namna zinavyofanya kazi
Soma Zaidi...Haya ni mafunzo ya HTML kwa wanaoanza level ya kwanza, na hili ni somo la kwanza katika masomo 8 yatakayokujia katika mtiririko wa course hii.
Soma Zaidi...Karibu tena katika mafunzo yetu, na huu ni mwanzo wa mafunzoya DATABASE kwa kutumia MYSQL kwa lugha ya kiswahili. Na hili ni somo la kwanza, katka somo hili utajifunza jinsi ya kuandaa kifaa chako kwa ajili ya mafunzo.
Soma Zaidi...Huu ni mwendelezo wa mafunzo ya DATABASE kwa kutumia MySQL na hili ni somo la pili. Hapa tutakwenda kuona kwa ufupi ni nini DATABASE
Soma Zaidi...