image

Mafunzo ya DATABASE MYSQL na SQL somo la 1

Karibu tena katika mafunzo yetu, na huu ni mwanzo wa mafunzoya DATABASE kwa kutumia MYSQL kwa lugha ya kiswahili. Na hili ni somo la kwanza, katka somo hili utajifunza jinsi ya kuandaa kifaa chako kwa ajili ya mafunzo.

MAFUNZO YA DATABASE SQL (MYSQL)

haya ni mafunzo ya DATABASE kwa kutumia software ya MYSQL. Katika mafunzo haya utajifunza namna ya kuthibiti taarifa kwnye database kwa kutumia software ya mysql.  Pamoja na mafunzo ya php na html utaweza pia kuzitumia taarifa hizi moja kwa oja kwenye blog ama website yako.

 

 

Mafunzo haya yatakujia kupitia mfundishaji wako Mr. Rajabu kutoka bongoclass. Mwisho wa mafunzo haya utaweza kumilii database yeko ya online ambapo utaweza kuweka na kupata taarifa popote ulipo kutoka kwenye kifaa chochote kile. Kumbukacourse hii inakuji free kabisa bila ya malipo. Unachotakiwa ni kushiriki vyema tu.

 

 

VIGEZO VYA KUSHIRIKI MAFUNZO:

  1. Uwe na simu janja yenye kiendeshi cha Android au uwe na kompyuta
  2. Uwe mjanja
  3. Una uzoefu wa kutumia software ama android App mbalimbali kama excel,
  4. Uweze kusoma na kuandika angalau maneno marahisi ya kiiingereza kama create, drop, user, select, where, into, update, order na mengine yanayofanana na haya.

 

 

MAANDALIZI YA SOMO:

Ili kuweza kuendelea na somo hili hakikisha kuwa umesakinisha App zifutazo kwenye kifaa chako.

  1. Kama unatumia simu AWEBSERVER tumia link hii https://play.google.com/store/apps/details?id=com.sylkat.apache

 

  1. Kama unatumia kompyuta download wampserver ama xamp vyema ukaanza na xamp maana wampserver wakati mwingine inasumbuwa kwenye kuinstall kama kompyta haipo update.

 

Baada ya kufukia hapo utakuwa umeshamaliza maandalizi ya somo.

 

 

JINSI YA KUANZA:

KAMA UNATUMIA SIMU:

  1. Funguwa App yako
  2. Bofya start kuanza huduma ya server iwe active
  3. Kwenye menu upande wa juu kuna kapicha kama suka sufuria kameandika Mysql bofya hapao.
  4. Bofya start ili kuanza huduma
  5. Utaona kulia mwa neno admin kuna link yenye sura hii 0.0.0.0:8080/mysqladmin
  6. Bofya kwenye link hiyo
  7. Utyaona kuna ukurasa ukekuja unakuhitaji kuweka user name na password
  8. Username weka root na password weka root
  9. Kisha bofya log in
  10. Utafunguka ukurasa mpya ambao utaona neno database kwa juu.

 

 

Kama umefika hatuwa hii HONGERA somo letu la kwanza litaanzia hapo

 

 

KAMA UNATUMIA KOMPYUTA:

Kama unatumia xamp

  1. Funguwa software ya xamp
  2. Kutafunguka kiukurasa kadogo kenye menu.
  3. Kwenye apache bofya start
  4. Kwenye Mysql bofya start
  5. Kisha kwenye Mysql bofya Admin
  6. Utaona kuna ukurasa mkubwa umefunguka kwenye browser yako.
  7. Neno databases utaliona kwa juu
  8. Hapa utakuwa upo tayari kwa somo lijalo.

 

 

KAMA UNATUMIA WAMPSERVER

  1. Ifunguwe hiyo software
  2. Nenda kwenye tray upande wa kulia utaikuta ipo active
  3. Right click
  4. Kwenye menu bofya phpmyadmin
  5. Ukurasa mpya utafunguka na neno database litaonekana kwa juu.
  6. Kama umefuka hatuwa hii upo tayari kwa somo linalofata.





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1772


Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

Mafunzo ya HTML level 1 somo la 8 (HTML basic level FOR BEGINNERS)
Katika somo hili la 8 mafunzo ya html level 8 utajifunza jinsi ya kuhost project ya html na kuwa live, watu wakaipitia na kusoma maudhui yake. Soma Zaidi...

Mafunzo ya php level 1 somo la tatu (3)
hili ni somo la tatu katika masomo ya php level 1. Hapa utajifunza zaidi kuhusu variable na namna ya kuitengeneza. Soma Zaidi...

Mafunzo ya HTML level 1 somo la 2 (HTML basic level FOR BEGINNERS)
Hili ni somo la pili katika mfululizo wa mafunzo ya html level ya 1 na hapa tutakwenda sasa kunanza somo letu rasmi, kwani katika somo la kwanza umejifunza jinsi ya kuandaa kifaa chako kwa ajili ya mafunzo. Soma Zaidi...

Mafunzo ya HTML kwa wenye kuanza (basic level)
Huu ni utangalizi wa mafunzo ya HTML kwa wenye kuanza level ya kwanza kwa lugha ya kiswahili. Haapa utapata msingi wa kuweza kutengeneza tovuti na blog. Soma Zaidi...

Mafunzo ya php level 1 somo la kwanza (1)
Karibu kwenye mafunzo ya PHP level 1 na hili ni somo la kwanza. Hapa utajifunza maana ya php, inavyofanya kazi pamoja na historia yake kwa ufupi Soma Zaidi...

Mafunzo ya DATABASE kwa kutumia MySQL DATABASE kwa kiswahili somo la 4
Huu ni mwendelezo wa mafunzo ya database kwa kutumia MySQL na hili ni somo la nne katika mlolongo wa masomo haya. Katika somo hili utajifuza jinsi ya kubadili jina la database na kufuta database. Pia tutajifunza kutumia SQL kufanya hayo. Soma Zaidi...

Mafunzo ya HTML Level 1 somo la 2 for beginner (html full course for beginners)
Somo la pili katika mafunzo ya HTML level 2. Katika somo hili utajifunza maana ya HTML pamoja na historia yake fupi. Soma Zaidi...

Mafunzo ya HTML level 1 somo la 5 (HTML basic level FOR BEGINNERS)
katika somo hili la tano kwenye mafunzo ya HTML level 1 utajifunza jinsi ya 1.Kuweka picha 2.Kuweka rangi 3.Kuweka linki 4.Kupangilia position na alignment ya maandishi 5.Kuongeza ukubwa wa herufi 6.Kukoment Soma Zaidi...

Mafunzo ya Database MySQL database somo la 10
Huu ni muendelezo wa mafunzo ya Database kwa kutumia MySQL na hili ni somo la 10. katika somo hili tutakwenda kuendelea namna ya kupangilia muonekano wa data zako kwenye database. Soma Zaidi...

Mafunzo ya DATABASE - MySQL somo la 7
Mafunzo ya database kwa utumia software ya MySQL kwa lugha ya kiswahili na hili ni somo la 7. Soma Zaidi...

Mafunzo ya database mySQl database somo la 11
huu ni muendelezo wa mafunzo ya Database klwa kutumia MySQL na hili ni somo la 11. katika somo hili tutaendelea kujifunza mpangilio wa muonekano wa data kwenye database. Soma Zaidi...

Mafunzo ya HTML Level 2 somo la 6 (HTML FULL COURSE FOR BEGINNERS LESSON 6)
Katika somo hili la 6 mafunzo ya HTML level 2, tutajfunza namna ya kugawa ukurasa wa wavuti wa html. Soma Zaidi...