picha

Mafunzo ya DATABASE MYSQL na SQL somo la 1

Karibu tena katika mafunzo yetu, na huu ni mwanzo wa mafunzoya DATABASE kwa kutumia MYSQL kwa lugha ya kiswahili. Na hili ni somo la kwanza, katka somo hili utajifunza jinsi ya kuandaa kifaa chako kwa ajili ya mafunzo.

MAFUNZO YA DATABASE SQL (MYSQL)

haya ni mafunzo ya DATABASE kwa kutumia software ya MYSQL. Katika mafunzo haya utajifunza namna ya kuthibiti taarifa kwnye database kwa kutumia software ya mysql.  Pamoja na mafunzo ya php na html utaweza pia kuzitumia taarifa hizi moja kwa oja kwenye blog ama website yako.

 

 

Mafunzo haya yatakujia kupitia mfundishaji wako Mr. Rajabu kutoka bongoclass. Mwisho wa mafunzo haya utaweza kumilii database yeko ya online ambapo utaweza kuweka na kupata taarifa popote ulipo kutoka kwenye kifaa chochote kile. Kumbukacourse hii inakuji free kabisa bila ya malipo. Unachotakiwa ni kushiriki vyema tu.

 

 

VIGEZO VYA KUSHIRIKI MAFUNZO:

  1. Uwe na simu janja yenye kiendeshi cha Android au uwe na kompyuta
  2. Uwe mjanja
  3. Una uzoefu wa kutumia software ama android App mbalimbali kama excel,
  4. Uweze kusoma na kuandika angalau maneno marahisi ya kiiingereza kama create, drop, user, select, where, into, update, order na mengine yanayofanana na haya.

 

 

MAANDALIZI YA SOMO:

Ili kuweza kuendelea na somo hili hakikisha kuwa umesakinisha App zifutazo kwenye kifaa chako.

  1. Kama unatumia simu AWEBSERVER tumia link hii https://play.google.com/store/apps/details?id=com.sylkat.apache

 

  1. Kama unatumia kompyuta download wampserver ama xamp vyema ukaanza na xamp maana wampserver wakati mwingine inasumbuwa kwenye kuinstall kama kompyta haipo update.

 

Baada ya kufukia hapo utakuwa umeshamaliza maandalizi ya somo.

 

 

JINSI YA KUANZA:

KAMA UNATUMIA SIMU:

  1. Funguwa App yako
  2. Bofya start kuanza huduma ya server iwe active
  3. Kwenye menu upande wa juu kuna kapicha kama suka sufuria kameandika Mysql bofya hapao.
  4. Bofya start ili kuanza huduma
  5. Utaona kulia mwa neno admin kuna link yenye sura hii 0.0.0.0:8080/mysqladmin
  6. Bofya kwenye link hiyo
  7. Utyaona kuna ukurasa ukekuja unakuhitaji kuweka user name na password
  8. Username weka root na password weka root
  9. Kisha bofya log in
  10. Utafunguka ukurasa mpya ambao utaona neno database kwa juu.

 

 

Kama umefika hatuwa hii HONGERA somo letu la kwanza litaanzia hapo

 

 

KAMA UNATUMIA KOMPYUTA:

Kama unatumia xamp

  1. Funguwa software ya xamp
  2. Kutafunguka kiukurasa kadogo kenye menu.
  3. Kwenye apache bofya start
  4. Kwenye Mysql bofya start
  5. Kisha kwenye Mysql bofya Admin
  6. Utaona kuna ukurasa mkubwa umefunguka kwenye browser yako.
  7. Neno databases utaliona kwa juu
  8. Hapa utakuwa upo tayari kwa somo lijalo.

 

 

KAMA UNATUMIA WAMPSERVER

  1. Ifunguwe hiyo software
  2. Nenda kwenye tray upande wa kulia utaikuta ipo active
  3. Right click
  4. Kwenye menu bofya phpmyadmin
  5. Ukurasa mpya utafunguka na neno database litaonekana kwa juu.
  6. Kama umefuka hatuwa hii upo tayari kwa somo linalofata.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Tehama Main: Post File: Download PDF Views 2665

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 ai web app     👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitau cha Fiqh     👉5 Simulizi za Hadithi Audio     👉6 Kitabu cha Afya    

Post zinazofanana:

Mafunzo ya database mySQl database somo la 11

huu ni muendelezo wa mafunzo ya Database klwa kutumia MySQL na hili ni somo la 11. katika somo hili tutaendelea kujifunza mpangilio wa muonekano wa data kwenye database.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya HTML kwa wenye kuanza (basic level)

Huu ni utangalizi wa mafunzo ya HTML kwa wenye kuanza level ya kwanza kwa lugha ya kiswahili. Haapa utapata msingi wa kuweza kutengeneza tovuti na blog.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya DATABASE - MySQL database somo la 5

Huu ni muendelezo wa mafunzo ya DATABASE kwa kutumia software ya MySQL na hili ni somo la tano. katika somo hili utajifunza type of data yaani aina ya taarifa ambazo unaweza kuzihifadhi kwenye database yako.

Soma Zaidi...
Php level 1 somo la saba (7)

Hili ni somo la saba, mafunzo ya php level 1. Katika somo hili utajifunza jinsi ya kuandika function yako mwenyewe.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya database MySQL somo la 3

Huu ni mwendelezo wa mafunzo ya database na jinsi ya kutengeneza bloga na website na hili ni somo la tatu. hapa utajifunza jinsiya kutengeneza database yako kwa mara ya kwanza.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya DATABASE - MySQL database somo la 8

Huuu ni muendeleo wa mafunzo ya database kwa lugha ya kiswahili, na hili ni somo la nane. Katika somo hli utajifunza namna ya kuweka taarifa kwenye database, kuzfuta na kuziediti yaani kuzifanyia marekebisho.

Soma Zaidi...