picha

Mafunzo ya DATABASE MYSQL na SQL somo la 1

Karibu tena katika mafunzo yetu, na huu ni mwanzo wa mafunzoya DATABASE kwa kutumia MYSQL kwa lugha ya kiswahili. Na hili ni somo la kwanza, katka somo hili utajifunza jinsi ya kuandaa kifaa chako kwa ajili ya mafunzo.

MAFUNZO YA DATABASE SQL (MYSQL)

haya ni mafunzo ya DATABASE kwa kutumia software ya MYSQL. Katika mafunzo haya utajifunza namna ya kuthibiti taarifa kwnye database kwa kutumia software ya mysql.  Pamoja na mafunzo ya php na html utaweza pia kuzitumia taarifa hizi moja kwa oja kwenye blog ama website yako.

 

 

Mafunzo haya yatakujia kupitia mfundishaji wako Mr. Rajabu kutoka bongoclass. Mwisho wa mafunzo haya utaweza kumilii database yeko ya online ambapo utaweza kuweka na kupata taarifa popote ulipo kutoka kwenye kifaa chochote kile. Kumbukacourse hii inakuji free kabisa bila ya malipo. Unachotakiwa ni kushiriki vyema tu.

 

 

VIGEZO VYA KUSHIRIKI MAFUNZO:

  1. Uwe na simu janja yenye kiendeshi cha Android au uwe na kompyuta
  2. Uwe mjanja
  3. Una uzoefu wa kutumia software ama android App mbalimbali kama excel,
  4. Uweze kusoma na kuandika angalau maneno marahisi ya kiiingereza kama create, drop, user, select, where, into, update, order na mengine yanayofanana na haya.

 

 

MAANDALIZI YA SOMO:

Ili kuweza kuendelea na somo hili hakikisha kuwa umesakinisha App zifutazo kwenye kifaa chako.

  1. Kama unatumia simu AWEBSERVER tumia link hii https://play.google.com/store/apps/details?id=com.sylkat.apache

 

  1. Kama unatumia kompyuta download wampserver ama xamp vyema ukaanza na xamp maana wampserver wakati mwingine inasumbuwa kwenye kuinstall kama kompyta haipo update.

 

Baada ya kufukia hapo utakuwa umeshamaliza maandalizi ya somo.

 

 

JINSI YA KUANZA:

KAMA UNATUMIA SIMU:

  1. Funguwa App yako
  2. Bofya start kuanza huduma ya server iwe active
  3. Kwenye menu upande wa juu kuna kapicha kama suka sufuria kameandika Mysql bofya hapao.
  4. Bofya start ili kuanza huduma
  5. Utaona kulia mwa neno admin kuna link yenye sura hii 0.0.0.0:8080/mysqladmin
  6. Bofya kwenye link hiyo
  7. Utyaona kuna ukurasa ukekuja unakuhitaji kuweka user name na password
  8. Username weka root na password weka root
  9. Kisha bofya log in
  10. Utafunguka ukurasa mpya ambao utaona neno database kwa juu.

 

 

Kama umefika hatuwa hii HONGERA somo letu la kwanza litaanzia hapo

 

 

KAMA UNATUMIA KOMPYUTA:

Kama unatumia xamp

  1. Funguwa software ya xamp
  2. Kutafunguka kiukurasa kadogo kenye menu.
  3. Kwenye apache bofya start
  4. Kwenye Mysql bofya start
  5. Kisha kwenye Mysql bofya Admin
  6. Utaona kuna ukurasa mkubwa umefunguka kwenye browser yako.
  7. Neno databases utaliona kwa juu
  8. Hapa utakuwa upo tayari kwa somo lijalo.

 

 

KAMA UNATUMIA WAMPSERVER

  1. Ifunguwe hiyo software
  2. Nenda kwenye tray upande wa kulia utaikuta ipo active
  3. Right click
  4. Kwenye menu bofya phpmyadmin
  5. Ukurasa mpya utafunguka na neno database litaonekana kwa juu.
  6. Kama umefuka hatuwa hii upo tayari kwa somo linalofata.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2021/11/14/Sunday - 09:51:12 am Topic: Tehama Main: Jifunze File: Download PDF Views 2628

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉2 web hosting    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 Simulizi za Hadithi Audio    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 ai web app   

Post zinazofanana:

Mafunzo ya php level 1 somo la nne (4)

somo hili la 4 katika mafunzo ya PHP level 1 utajifunza aina za data mabazo php inakwenda kuzitumia.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya HTML Level 2 somo la 4 (HTML FULL COURSE FOR BEGINNERS LESSON 4)

Karibu tena katika somo la nne la mafunzo ya HTML level2 html full course for beginners. Katika somo hili utajifunza kuhusu attributes na namna zinavyofanya kazi

Soma Zaidi...
Php level 1 somo la saba (7)

Hili ni somo la saba, mafunzo ya php level 1. Katika somo hili utajifunza jinsi ya kuandika function yako mwenyewe.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya HTML Level 2 somo la 8 (HTML FULL COURSE FOR BEGINNERS LESSON 8)

Hili ni somo la mwisho mafunzo ya HTML level 2 (html full course for beginners)

Soma Zaidi...
Mafunzo ya HTML level 1 somo la 6 (HTML basic level FOR BEGINNERS)

hili ni somo la sita katika mfululizo wa mafunzo ya HTML level 1. Katika somo hili tutajifunza mambo makuu matatu ambayo ni kuweka menyu, kuweka background color na kufanya faili lako liwe responsive.

Soma Zaidi...
PHP level 1 somo la kumi (10)

Somo la 10 mafunzo ya php level 1. Katika somo hili utajifunza kuhusu condition statement.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya database MySQL database somo la 9

haya ni mafunzo ya database kwa kutumia MySQl na hili ni somo la 9. katika soo hili utajifunza namna ya kusoma ama kutumia taarifa zilizomo kwenye DATABASE.

Soma Zaidi...
PHP level 1 somo la tano (5)

Haya ni mafunzo ya php na hili ni somo la tano. Katika somovhili utajifunza namna ya kutengeneza functions.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya html level 2 (html full course for beginners)

haya ni mafunzo ya HTML level 2 kwa wenye kuanza. Mafunzo haya ni muendelezo wa level 1 html. Katika course hii utajifunza mengi zaidi lu;iko level1 pia tutazidi kuboresha project yetu.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya HTML Level 2 somo la 6 (HTML FULL COURSE FOR BEGINNERS LESSON 6)

Katika somo hili la 6 mafunzo ya HTML level 2, tutajfunza namna ya kugawa ukurasa wa wavuti wa html.

Soma Zaidi...