Navigation Menu



Mafunzo ya DATABASE MYSQL na SQL somo la 1

Karibu tena katika mafunzo yetu, na huu ni mwanzo wa mafunzoya DATABASE kwa kutumia MYSQL kwa lugha ya kiswahili. Na hili ni somo la kwanza, katka somo hili utajifunza jinsi ya kuandaa kifaa chako kwa ajili ya mafunzo.

MAFUNZO YA DATABASE SQL (MYSQL)

haya ni mafunzo ya DATABASE kwa kutumia software ya MYSQL. Katika mafunzo haya utajifunza namna ya kuthibiti taarifa kwnye database kwa kutumia software ya mysql.  Pamoja na mafunzo ya php na html utaweza pia kuzitumia taarifa hizi moja kwa oja kwenye blog ama website yako.

 

 

Mafunzo haya yatakujia kupitia mfundishaji wako Mr. Rajabu kutoka bongoclass. Mwisho wa mafunzo haya utaweza kumilii database yeko ya online ambapo utaweza kuweka na kupata taarifa popote ulipo kutoka kwenye kifaa chochote kile. Kumbukacourse hii inakuji free kabisa bila ya malipo. Unachotakiwa ni kushiriki vyema tu.

 

 

VIGEZO VYA KUSHIRIKI MAFUNZO:

  1. Uwe na simu janja yenye kiendeshi cha Android au uwe na kompyuta
  2. Uwe mjanja
  3. Una uzoefu wa kutumia software ama android App mbalimbali kama excel,
  4. Uweze kusoma na kuandika angalau maneno marahisi ya kiiingereza kama create, drop, user, select, where, into, update, order na mengine yanayofanana na haya.

 

 

MAANDALIZI YA SOMO:

Ili kuweza kuendelea na somo hili hakikisha kuwa umesakinisha App zifutazo kwenye kifaa chako.

  1. Kama unatumia simu AWEBSERVER tumia link hii https://play.google.com/store/apps/details?id=com.sylkat.apache

 

  1. Kama unatumia kompyuta download wampserver ama xamp vyema ukaanza na xamp maana wampserver wakati mwingine inasumbuwa kwenye kuinstall kama kompyta haipo update.

 

Baada ya kufukia hapo utakuwa umeshamaliza maandalizi ya somo.

 

 

JINSI YA KUANZA:

KAMA UNATUMIA SIMU:

  1. Funguwa App yako
  2. Bofya start kuanza huduma ya server iwe active
  3. Kwenye menu upande wa juu kuna kapicha kama suka sufuria kameandika Mysql bofya hapao.
  4. Bofya start ili kuanza huduma
  5. Utaona kulia mwa neno admin kuna link yenye sura hii 0.0.0.0:8080/mysqladmin
  6. Bofya kwenye link hiyo
  7. Utyaona kuna ukurasa ukekuja unakuhitaji kuweka user name na password
  8. Username weka root na password weka root
  9. Kisha bofya log in
  10. Utafunguka ukurasa mpya ambao utaona neno database kwa juu.

 

 

Kama umefika hatuwa hii HONGERA somo letu la kwanza litaanzia hapo

 

 

KAMA UNATUMIA KOMPYUTA:

Kama unatumia xamp

  1. Funguwa software ya xamp
  2. Kutafunguka kiukurasa kadogo kenye menu.
  3. Kwenye apache bofya start
  4. Kwenye Mysql bofya start
  5. Kisha kwenye Mysql bofya Admin
  6. Utaona kuna ukurasa mkubwa umefunguka kwenye browser yako.
  7. Neno databases utaliona kwa juu
  8. Hapa utakuwa upo tayari kwa somo lijalo.

 

 

KAMA UNATUMIA WAMPSERVER

  1. Ifunguwe hiyo software
  2. Nenda kwenye tray upande wa kulia utaikuta ipo active
  3. Right click
  4. Kwenye menu bofya phpmyadmin
  5. Ukurasa mpya utafunguka na neno database litaonekana kwa juu.
  6. Kama umefuka hatuwa hii upo tayari kwa somo linalofata.

Download app yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download

Download Now Bongoclass

           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu image Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Tehama Main: Post File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Views 1966


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Simulizi za Hadithi Audio     👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉4 Kitau cha Fiqh     👉5 Kitabu cha Afya     👉6 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Mafunzo ya HTML level 1 somo la 3 (HTML basic level FOR BEGINNERS)
Hili ni somo la Tatu katika mfululizo wetu wa mafunzo ya HTML kwa basic level kwa wanaoanza kujifunza. Hapa tutakwenda kujifunza tag za html ambazo huwa zinatumika katika uandishi. Soma Zaidi...

Mafunzo ya HTML Level 2 somo la 8 (HTML FULL COURSE FOR BEGINNERS LESSON 8)
Hili ni somo la mwisho mafunzo ya HTML level 2 (html full course for beginners) Soma Zaidi...

PHP level 1 somo la nane (8)
Hapa utajifunza utofauti kati ya php constant na variable. Na hili ni somo la nane katika mfululizo wa masomo haya ya php level 1. Soma Zaidi...

Mafunzo ya HTML level 1 somo la 6 (HTML basic level FOR BEGINNERS)
hili ni somo la sita katika mfululizo wa mafunzo ya HTML level 1. Katika somo hili tutajifunza mambo makuu matatu ambayo ni kuweka menyu, kuweka background color na kufanya faili lako liwe responsive. Soma Zaidi...

PHP level 1 somo la tisa (9).
Somo la nane mafunzo ya php, katika somo hili utajifunza kuhusu array na jinsi ya kutengeneza array. Soma Zaidi...

Mafunzo ya database MySQL somo la 3
Huu ni mwendelezo wa mafunzo ya database na jinsi ya kutengeneza bloga na website na hili ni somo la tatu. hapa utajifunza jinsiya kutengeneza database yako kwa mara ya kwanza. Soma Zaidi...

Mafunzo ya DATABASE - MySQL database somo la 5
Huu ni muendelezo wa mafunzo ya DATABASE kwa kutumia software ya MySQL na hili ni somo la tano. katika somo hili utajifunza type of data yaani aina ya taarifa ambazo unaweza kuzihifadhi kwenye database yako. Soma Zaidi...

Mafunzo ya HTML level 1 somo la 5 (HTML basic level FOR BEGINNERS)
katika somo hili la tano kwenye mafunzo ya HTML level 1 utajifunza jinsi ya 1.Kuweka picha 2.Kuweka rangi 3.Kuweka linki 4.Kupangilia position na alignment ya maandishi 5.Kuongeza ukubwa wa herufi 6.Kukoment Soma Zaidi...

Mafunzo ya Database MySQL database somo la 10
Huu ni muendelezo wa mafunzo ya Database kwa kutumia MySQL na hili ni somo la 10. katika somo hili tutakwenda kuendelea namna ya kupangilia muonekano wa data zako kwenye database. Soma Zaidi...

Mafunzo ya HTML Level 2 somo la 7 (HTML FULL COURSE FOR BEGINNERS LESSON 7)
Ktika somo hili la 7 utajifunza namna ya kuandaa na kujiandaa kutengeneza website ama blog. Pia utajifunza maandalizi ya kuhost Soma Zaidi...