PHP level 1 somo la sita (6)

Katika somo hili la php level 1 somo la 6 utajifunza namna ya kutumia tarehe yaani function date() kwenye PHP

SOMO LA SITA

PHP FUNCTIONS KUONYESHA TAREHE NA SAA:
Kwa kutumia php unaweza kuonyesha saa muda wowote kwa kutumia mistari michache ya code.
Katika php function inayotumika kwa ajili yakuonyesha tarehe na saa ni date(). kwa kutumia function hii una hiyari uonyesha tarehetu, ama siku tu, ama saa tu …. Katika php function inakupasa utambuwe haya:-
1.Y humaanisha mwaka yaani Year
2.m humaanisha mwezi yaani Month
3.d humaanisha siku yaani date
4.l humaanisha siku katka wiki
5.h humaanisha saa yaani hour
6.m humaanisha dakika yaani minute
7.S humaanisha sekunde yaani second
8.a humaanisha Ante meridiem (Am) na Post meridiem (Pm)
wacha tuone mifano hapo chini:-


 

1.Mfano wa kwanza
<?php
echo "today is", "<br><br>",
date("Y/m/d/l");
?>
Hii itakupa mwaka, mwezi, tarehe na siku katika wiki.

Kama unataka kuonyesha mwaka pekee, utaweka Y tu kwenye function


 

2.Mfano 2
<?php
echo "today is", "<br><br>",
date("Y");
?>
Hii itakupa mwaka tu

3.Mfano
<?php
echo "today is", "<br><br>",
date("m");
?>
Hii itakupa mwez tu


4.Mfano
<?php
echo "today is", "<br><br>",
date("d");
?>
Hii itakupa tarehe ya leo


 

5.Mfano
<?php
echo "today is", "<br><br>",
date("l");
?>
Hii itakupa jila la siku ya wiki ya leo kama ni juma tatu, ama jumanne ama vinginevyo


 

6.Mfano
<?php
echo "the time is " .
date("h:i:sa");
?>

Hii itakupa saa, dakika, sekunde na kama Am ama Pm.
Ukitaka kuonyesha saa tupu utaweza kufanya kama ilivyofanywa juu kwenye tarehe.


 

7.Mfano
<?php
echo "the time is " .
date("h");
?>
Hii itaonyesha saa tu.


 

SAA KWA ZONE
Changamoto utakayoipata kwenye php function iliyotumika hapo juu utaona kuwa masaa hayaposawa na ilvyo saa yako. Hii ni kutokana na kuwa time zone iliyotumika ni tofauti. Hivyo basi itakupasa kujuwa time zote yako ili uweze kupata saa sahihi. Kufanya hivi tutatumia function hii date_default_timezone_set()

Ili kuweka timezone, kwanza uweke region au bara kwa mfano tanzania ipo Africa kisha weka alama / kisha weka time zone. Kwa mfano Tanzania ipo kwenye timezone ya Nairobi hivyo utaandika Africa/Nairobi


 

8.Mfano
<?php
date_default_timezone_set("Africa/Nairobi");
echo "the time is " . date("h:i:sa");
?>
Hii itaonyesha saa kulingana na timezone ya East Africa, ambayo inachukuliwa nairobi.


 

COPYRIGHT KWENYE TOVUTI
Hivi umesha tembelea tovuti na blog, halafu chini utaona mwaka ilipoanzishwa mpaka mwaka wa sasa. Nikijuze kuwa ule mwaka wa sasa hubadilika automatiki, na hakuna haja ya kubadili, haya utayafanya kwa kutumia php. Mfano


 

9.Mfano
&copy: 2018 - <?php echo date("Y");
?>

Hii itakupa matokeo ©: 2018 - 2021

Tutajifunza zaidi kuhusu kalenda katika masomo yatakayofata.


 

Mafunzo haya yanakujia kwa ihsani ya bongoclass
Web: www.bongoclass.com
Email:mafunzo@bongoclass.com
Phone: 0774069753 unaweza kunicheki wasap kwa link hii https://wa.me/message/7CTQP5BSWBR5I1

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Je umeipenda post hii ?

Ndio            Hapana            Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tehama Main: Jifunze File: Download PDF Views 1184

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 Simulizi za Hadithi Audio    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Mafunzo ya HTML level 1 somo la 1 (HTML basic level FOR BEGINNERS)

Haya ni mafunzo ya HTML kwa wanaoanza level ya kwanza, na hili ni somo la kwanza katika masomo 8 yatakayokujia katika mtiririko wa course hii.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya DATABASE kwa kutumia MySQL DATABASE kwa kiswahili somo la 4

Huu ni mwendelezo wa mafunzo ya database kwa kutumia MySQL na hili ni somo la nne katika mlolongo wa masomo haya. Katika somo hili utajifuza jinsi ya kubadili jina la database na kufuta database. Pia tutajifunza kutumia SQL kufanya hayo.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya DATABASE - MySQL database somo la 8

Huuu ni muendeleo wa mafunzo ya database kwa lugha ya kiswahili, na hili ni somo la nane. Katika somo hli utajifunza namna ya kuweka taarifa kwenye database, kuzfuta na kuziediti yaani kuzifanyia marekebisho.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya HTML level 1 somo la 8 (HTML basic level FOR BEGINNERS)

Katika somo hili la 8 mafunzo ya html level 8 utajifunza jinsi ya kuhost project ya html na kuwa live, watu wakaipitia na kusoma maudhui yake.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya Database MySQL DATABASE somo la 2

Huu ni mwendelezo wa mafunzo ya DATABASE kwa kutumia MySQL na hili ni somo la pili. Hapa tutakwenda kuona kwa ufupi ni nini DATABASE

Soma Zaidi...
Mafunzo ya php level 1 somo la pili (2)

hili ni somo la pili katika mfululizo wa mafunzo haya ya php level 1 na hapa utajifunza namna ya kuandika faili klako la kwanza la php.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya database MySQL database somo la 9

haya ni mafunzo ya database kwa kutumia MySQl na hili ni somo la 9. katika soo hili utajifunza namna ya kusoma ama kutumia taarifa zilizomo kwenye DATABASE.

Soma Zaidi...
PHP level 1 somo la kumi na mbili (12) final

Mafunzo ya php level 1 somo ka 12 mwisho wa mafunzo. Hapa utaona project ambazo unaweza kufanya kutokana na mafunzo haya.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya HTML level 1 somo la 4 (HTML basic level FOR BEGINNERS)

Hili ni somo la nne katika mafunzo ya html basic level. Hapa tutakwenda kuona jinsi ya kuzifanyia kazi tag ambazo umejifunza katika somo lililotangulia.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya database MySQL - DATABASE somo la 6

Huu ni muendelezo wa mafunzo ya database kwa kutumia MySQL na hili ni somo la 6. Katika somo hili tutakwenda kuona jinsi ya kutengeneza table kwa kutumia MySQL na kwa kutuma SQL.

Soma Zaidi...