Katika somo hili la php level 1 somo la 6 utajifunza namna ya kutumia tarehe yaani function date() kwenye PHP
SOMO LA SITA
PHP FUNCTIONS KUONYESHA TAREHE NA SAA:
Kwa kutumia php unaweza kuonyesha saa muda wowote kwa kutumia mistari michache ya code.
Katika php function inayotumika kwa ajili yakuonyesha tarehe na saa ni date(). kwa kutumia function hii una hiyari uonyesha tarehetu, ama siku tu, ama saa tu …. Katika php function inakupasa utambuwe haya:-
1.Y humaanisha mwaka yaani Year
2.m humaanisha mwezi yaani Month
3.d humaanisha siku yaani date
4.l humaanisha siku katka wiki
5.h humaanisha saa yaani hour
6.m humaanisha dakika yaani minute
7.S humaanisha sekunde yaani second
8.a humaanisha Ante meridiem (Am) na Post meridiem (Pm)
wacha tuone mifano hapo chini:-
1.Mfano wa kwanza
<?php
echo "today is", "<br><br>",
date("Y/m/d/l");
?>
Hii itakupa mwaka, mwezi, tarehe na siku katika wiki.
Kama unataka kuonyesha mwaka pekee, utaweka Y tu kwenye function
2.Mfano 2
<?php
echo "today is", "<br><br>",
date("Y");
?>
Hii itakupa mwaka tu
3.Mfano
<?php
echo "today is", "<br><br>",
date("m");
?>
Hii itakupa mwez tu
4.Mfano
<?php
echo "today is", "<br><br>",
date("d");
?>
Hii itakupa tarehe ya leo
5.Mfano
<?php
echo "today is", "<br><br>",
date("l");
?>
Hii itakupa jila la siku ya wiki ya leo kama ni juma tatu, ama jumanne ama vinginevyo
6.Mfano
<?php
echo "the time is " .
date("h:i:sa");
?>
Hii itakupa saa, dakika, sekunde na kama Am ama Pm.
Ukitaka kuonyesha saa tupu utaweza kufanya kama ilivyofanywa juu kwenye tarehe.
7.Mfano
<?php
echo "the time is " .
date("h");
?>
Hii itaonyesha saa tu.
SAA KWA ZONE
Changamoto utakayoipata kwenye php function iliyotumika hapo juu utaona kuwa masaa hayaposawa na ilvyo saa yako. Hii ni kutokana na kuwa time zone iliyotumika ni tofauti. Hivyo basi itakupasa kujuwa time zote yako ili uweze kupata saa sahihi. Kufanya hivi tutatumia function hii date_default_timezone_set()
Ili kuweka timezone, kwanza uweke region au bara kwa mfano tanzania ipo Africa kisha weka alama / kisha weka time zone. Kwa mfano Tanzania ipo kwenye timezone ya Nairobi hivyo utaandika Africa/Nairobi
8.Mfano
<?php
date_default_timezone_set("Africa/Nairobi");
echo "the time is " . date("h:i:sa");
?>
Hii itaonyesha saa kulingana na timezone ya East Africa, ambayo inachukuliwa nairobi.
COPYRIGHT KWENYE TOVUTI
Hivi umesha tembelea tovuti na blog, halafu chini utaona mwaka ilipoanzishwa mpaka mwaka wa sasa. Nikijuze kuwa ule mwaka wa sasa hubadilika automatiki, na hakuna haja ya kubadili, haya utayafanya kwa kutumia php. Mfano
9.Mfano
©: 2018 - <?php echo date("Y");
?>
Hii itakupa matokeo ©: 2018 - 2021
Tutajifunza zaidi kuhusu kalenda katika masomo yatakayofata.
Mafunzo haya yanakujia kwa ihsani ya bongoclass
Web: www.bongoclass.com
Email:mafunzo@bongoclass.com
Phone: 0774069753 unaweza kunicheki wasap kwa link hii https://wa.me/message/7CTQP5BSWBR5I1
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
haya ni mafunzo ya database kwa kutumia MySQl na hili ni somo la 9. katika soo hili utajifunza namna ya kusoma ama kutumia taarifa zilizomo kwenye DATABASE.
Soma Zaidi...Hii ni project ya HTML ambayo imetengenezwa kulingana na mafunzo ya HTML level1. Tunatarajia project hii kuboreshwa kadiri mafunzo yanavyozidi kusonga mbele.
Soma Zaidi...Huu ni utangalizi wa mafunzo ya HTML kwa wenye kuanza level ya kwanza kwa lugha ya kiswahili. Haapa utapata msingi wa kuweza kutengeneza tovuti na blog.
Soma Zaidi...Mafunzo ya php level 1 somo ka 12 mwisho wa mafunzo. Hapa utaona project ambazo unaweza kufanya kutokana na mafunzo haya.
Soma Zaidi...Haya ni mafunzo ya muda mfupi katika kujifunza hasa ujuzi wa kutengeneza Android App hata kama haujui kitu kuhusiana na Android Development
Soma Zaidi...Katika somo hili la 6 mafunzo ya HTML level 2, tutajfunza namna ya kugawa ukurasa wa wavuti wa html.
Soma Zaidi...Karibu kwenye mafunzo ya PHP level 1 na hili ni somo la kwanza. Hapa utajifunza maana ya php, inavyofanya kazi pamoja na historia yake kwa ufupi
Soma Zaidi...Katika somo hili la 8 mafunzo ya html level 8 utajifunza jinsi ya kuhost project ya html na kuwa live, watu wakaipitia na kusoma maudhui yake.
Soma Zaidi...Hapa utajifunza utofauti kati ya php constant na variable. Na hili ni somo la nane katika mfululizo wa masomo haya ya php level 1.
Soma Zaidi...Karibu tena katika somo la nne la mafunzo ya HTML level2 html full course for beginners. Katika somo hili utajifunza kuhusu attributes na namna zinavyofanya kazi
Soma Zaidi...