image

Mafunzo ya DATABASE kwa kutumia MySQL DATABASE kwa kiswahili somo la 4

Huu ni mwendelezo wa mafunzo ya database kwa kutumia MySQL na hili ni somo la nne katika mlolongo wa masomo haya. Katika somo hili utajifuza jinsi ya kubadili jina la database na kufuta database. Pia tutajifunza kutumia SQL kufanya hayo.

Katika somo hili la nne tutakwenda kujifunza mambo makuu matatu ambayo ni:-

  1. Kubadili jina la database
  2. Kufuta database
  3. Kutumia SQL kufanya mabo hayo yaliyotajwa juu na mengineyo.

 

Kama ulishiriki mafunzo katika somo la tatu ulijifunza namna ya kutengeneza database kwa kutumia MySQL na kwa mutumia SAL command. Sasa katika somo hili tutakwenda kutumia database zetu mbili ambazo tulizitengeneza katika somo la tatu.

 

1. Kuona orodha ya database:

Hili ni jambo rahisi tu, baada ya kuingia kwenye MySQL, angalia menu yako, kisha bofya databases hapo utaona orodha ya database zote ambazo umetengeneza.

 

Sasa tunataka kufanya kitu kama hicho cha kuona orodha ta database kwa kutumia SQL language. Kufanya hivi fuata hatuwa hiz:-

  1. Kwenye menu bofya SQL
  2. Utakuja uwanja wa kuandika SQL hapo tumia command hii
  3. SHOW DATABASES;
  4. Baada ya hapo bofya neno GO lipo kwa chini pande wa kulia
  5. Kumbuka kuwa katika kuandika SQL mwisho tunamalizia na hizo semicolon (;) kama ilivyo hapo juu.
  6. Baada ya hapo utaona orodha ya database zote ulizotengeneza.

 

2. Kutumia database

Baada ya kuona orodha ya database zote hatuwa inayofata ni kuitumia hiyo database ama hizo database. Kutumia database maana yake ni kufanya hicho ambacho ulikusudia kwenye hiyo database kwa mfano kufuta, kubadili jiana ama kuweka data ama kuondoa na kubadili.

 

Kufanya hivi kwenye MySQL pia ni rahisi sana, unachotakiwa kufanya ni kubofya hiyo database yako. Ukishaubofya utaona umefunguka na kama kuna taarifa utaanza kuona majedwali yaliyopo.

 

Kufanya hivi kwa kutumia SQL pia ni rahisi, fuata hatuwa zifuatazo:-

  1. Ingia kwenye uwanja wa SQL
  2. Andika command hii
  3. USE post;
  4. Baada ya hapo bofya neno GO
  5. Command yetu hapo ni USE na hiyo post ni database ambayo tayari ipo hivyo tunataka kuitumia. Command hiyo ni maneno ya kiingereza yanayoweza kufahamika kuwa ni kuiambai MySQL kutumia database inayoitwa post.
  6. Mpaka kufika hapo utakuwa tayari kutumia database hiyo na unaweza kuifanya unachotaka.

 

3. Kubadili jina la database

Kwa kutumia MySQL baada ya kubofya hiyo database angalia kwenye menu tafuta neno oprrations, bofya hapo. Kisha tafuta palipoandikwa rename database to chini ya maneno hayo utaona kuna kabox. Kwenye hako kabox utaweka jina ambalo unataka kubadili. Kwa mfano database yetu inaitwa post sasa tunataka kuibadili jina kuiita makala.

 

Hivyo ingiza kwenye hicho kibox jina makala kisha bofya neno GO lipo upande wa kulia.kuna ujumbe utakuja unasema CREATE DATABASE makala / DROP DATABASE post hapo  utabofya OK kukubali. Mpaka kufikia hapo utakuwa umemaliza kubadili jina na hapo database yako itakuwa imebadilika.

 

Kufanya hivi kwa kutumia SQL utatumia RENAME ila kwa sasa hatutajifunza kufanya hivi ni kwa sababu command hii iliondolewa kwenye MySQl kwa sababu za kiusalama. Hivyo utaendelea kutumia MySQL interface kubadili jina.

 

4. kufuta database

Kufuta database kwenye MySQL utakwenda kwenye operations kama ulivyofanya hapo juu. Kisha tafuta palipoandikwa Remove database chini ya hayo maneno utaona kuna maneno yanasomeka Drop the database (DROP) bofya hayo maneno kisha kuna ujumbe utakuja You are about to DESTROY a complete database! Do you really want to execute "DROP DATABASE `makala`"? hapo bofya OK kukubali. Kufikia hapo utakuwa umeifuta database yako na hutoweza kuirudisha tena lamda iwe umeshaifanyia backup.

 

Kufanya hivi kwa kutumia SQL fuata taratibu zifuatazo. Kwa kuwa database ya makala tumeifuta basi sasa tunakwenda kufuta ile ya mafunzo.

  1. Ingia kwenye uwanja wa SQL
  2. Andika command hii
  3. DROP DATABASE mafunzo;
  4. Kisha bofya GO
  5. Hapo database ya mafunzo itakuwa imesha futika.

 

Kwa ufupi command ambazo zimetumika kwenye somo hili ni

  1. Show databases hii ni kwa ajili ya kuona orodha ya databases
  2. Use hii umetumika kutumia database
  3. Drop database hii imetumika kufuta database
  4. Create database hii imetumika kutengeneza database

 

Tukutane somo la tano tutakapojifunza Type of data in MySQL somo hili litakuwa ni muhimu sana na ni msingi hasa wa somo la sita. Pia kwa wale abao wanahitaji kujatumia database zao vilivyo wanatakiwa walifahamu vyema somo la tano.

 

Mafunzo haya yanakujia kwa ihsani ya

Bongoclass

Web: www.bongoclass.com

Email: mafunzo@bongoclass.com





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1253


Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

PHP level 11 somo la kumi na moja (11)
Katika somo hilivutajifunza namna ya kutumia HTML form. Namna ya kuookea taarifa kutoka kwenye madodoso ya html form. Soma Zaidi...

Mafunzo ya database MySQL database somo la 9
haya ni mafunzo ya database kwa kutumia MySQl na hili ni somo la 9. katika soo hili utajifunza namna ya kusoma ama kutumia taarifa zilizomo kwenye DATABASE. Soma Zaidi...

Mafunzo ya HTML Level 2 somo la 3 (HTML FULL COURSE FOR BEGINNERS LESSON 3)
Hili n somo la tatu katka muendelezo wa mafunzo ya HTML LEVEL 2 kwa lugha ya kiswahili. Mafunzo haya yanakujia kwa Ihsani ya bongoclass Soma Zaidi...

Mafunzo ya Database MySQL DATABASE somo la 2
Huu ni mwendelezo wa mafunzo ya DATABASE kwa kutumia MySQL na hili ni somo la pili. Hapa tutakwenda kuona kwa ufupi ni nini DATABASE Soma Zaidi...

Mafunzo ya HTML Level 1 somo la 2 for beginner (html full course for beginners)
Somo la pili katika mafunzo ya HTML level 2. Katika somo hili utajifunza maana ya HTML pamoja na historia yake fupi. Soma Zaidi...

Mafunzo ya HTML level 1 somo la 5 (HTML basic level FOR BEGINNERS)
katika somo hili la tano kwenye mafunzo ya HTML level 1 utajifunza jinsi ya 1.Kuweka picha 2.Kuweka rangi 3.Kuweka linki 4.Kupangilia position na alignment ya maandishi 5.Kuongeza ukubwa wa herufi 6.Kukoment Soma Zaidi...

Mafunzo ya HTML kwa wenye kuanza (basic level)
Huu ni utangalizi wa mafunzo ya HTML kwa wenye kuanza level ya kwanza kwa lugha ya kiswahili. Haapa utapata msingi wa kuweza kutengeneza tovuti na blog. Soma Zaidi...

Mafunzo ya HTML level 1 somo la 8 (HTML basic level FOR BEGINNERS)
Katika somo hili la 8 mafunzo ya html level 8 utajifunza jinsi ya kuhost project ya html na kuwa live, watu wakaipitia na kusoma maudhui yake. Soma Zaidi...

Php level 1 somo la saba (7)
Hili ni somo la saba, mafunzo ya php level 1. Katika somo hili utajifunza jinsi ya kuandika function yako mwenyewe. Soma Zaidi...

Mafunzo ya HTML level 1 somo la 2 (HTML basic level FOR BEGINNERS)
Hili ni somo la pili katika mfululizo wa mafunzo ya html level ya 1 na hapa tutakwenda sasa kunanza somo letu rasmi, kwani katika somo la kwanza umejifunza jinsi ya kuandaa kifaa chako kwa ajili ya mafunzo. Soma Zaidi...

Mafunzo ya HTML level 1 somo la 4 (HTML basic level FOR BEGINNERS)
Hili ni somo la nne katika mafunzo ya html basic level. Hapa tutakwenda kuona jinsi ya kuzifanyia kazi tag ambazo umejifunza katika somo lililotangulia. Soma Zaidi...

Mafunzo ya php level 1 somo la nne (4)
somo hili la 4 katika mafunzo ya PHP level 1 utajifunza aina za data mabazo php inakwenda kuzitumia. Soma Zaidi...