Huu ni mwendelezo wa mafunzo ya database kwa kutumia MySQL na hili ni somo la nne katika mlolongo wa masomo haya. Katika somo hili utajifuza jinsi ya kubadili jina la database na kufuta database. Pia tutajifunza kutumia SQL kufanya hayo.
Katika somo hili la nne tutakwenda kujifunza mambo makuu matatu ambayo ni:-
Kama ulishiriki mafunzo katika somo la tatu ulijifunza namna ya kutengeneza database kwa kutumia MySQL na kwa mutumia SAL command. Sasa katika somo hili tutakwenda kutumia database zetu mbili ambazo tulizitengeneza katika somo la tatu.
1. Kuona orodha ya database:
Hili ni jambo rahisi tu, baada ya kuingia kwenye MySQL, angalia menu yako, kisha bofya databases hapo utaona orodha ya database zote ambazo umetengeneza.
Sasa tunataka kufanya kitu kama hicho cha kuona orodha ta database kwa kutumia SQL language. Kufanya hivi fuata hatuwa hiz:-
2. Kutumia database
Baada ya kuona orodha ya database zote hatuwa inayofata ni kuitumia hiyo database ama hizo database. Kutumia database maana yake ni kufanya hicho ambacho ulikusudia kwenye hiyo database kwa mfano kufuta, kubadili jiana ama kuweka data ama kuondoa na kubadili.
Kufanya hivi kwenye MySQL pia ni rahisi sana, unachotakiwa kufanya ni kubofya hiyo database yako. Ukishaubofya utaona umefunguka na kama kuna taarifa utaanza kuona majedwali yaliyopo.
Kufanya hivi kwa kutumia SQL pia ni rahisi, fuata hatuwa zifuatazo:-
3. Kubadili jina la database
Kwa kutumia MySQL baada ya kubofya hiyo database angalia kwenye menu tafuta neno oprrations, bofya hapo. Kisha tafuta palipoandikwa rename database to chini ya maneno hayo utaona kuna kabox. Kwenye hako kabox utaweka jina ambalo unataka kubadili. Kwa mfano database yetu inaitwa post sasa tunataka kuibadili jina kuiita makala.
Hivyo ingiza kwenye hicho kibox jina makala kisha bofya neno GO lipo upande wa kulia.kuna ujumbe utakuja unasema CREATE DATABASE makala / DROP DATABASE post hapo utabofya OK kukubali. Mpaka kufikia hapo utakuwa umemaliza kubadili jina na hapo database yako itakuwa imebadilika.
Kufanya hivi kwa kutumia SQL utatumia RENAME ila kwa sasa hatutajifunza kufanya hivi ni kwa sababu command hii iliondolewa kwenye MySQl kwa sababu za kiusalama. Hivyo utaendelea kutumia MySQL interface kubadili jina.
4. kufuta database
Kufuta database kwenye MySQL utakwenda kwenye operations kama ulivyofanya hapo juu. Kisha tafuta palipoandikwa Remove database chini ya hayo maneno utaona kuna maneno yanasomeka Drop the database (DROP) bofya hayo maneno kisha kuna ujumbe utakuja You are about to DESTROY a complete database! Do you really want to execute "DROP DATABASE `makala`"? hapo bofya OK kukubali. Kufikia hapo utakuwa umeifuta database yako na hutoweza kuirudisha tena lamda iwe umeshaifanyia backup.
Kufanya hivi kwa kutumia SQL fuata taratibu zifuatazo. Kwa kuwa database ya makala tumeifuta basi sasa tunakwenda kufuta ile ya mafunzo.
Kwa ufupi command ambazo zimetumika kwenye somo hili ni
Tukutane somo la tano tutakapojifunza Type of data in MySQL somo hili litakuwa ni muhimu sana na ni msingi hasa wa somo la sita. Pia kwa wale abao wanahitaji kujatumia database zao vilivyo wanatakiwa walifahamu vyema somo la tano.
Mafunzo haya yanakujia kwa ihsani ya
Bongoclass
Web: www.bongoclass.com
Email: mafunzo@bongoclass.com
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Katika somo hilivutajifunza namna ya kutumia HTML form. Namna ya kuookea taarifa kutoka kwenye madodoso ya html form.
Soma Zaidi...Huu ni muendelezo wa mafunzo ya DATABASE kwa kutumia software ya MySQL na hili ni somo la tano. katika somo hili utajifunza type of data yaani aina ya taarifa ambazo unaweza kuzihifadhi kwenye database yako.
Soma Zaidi...Haya ni mafunzo ya muda mfupi katika kujifunza hasa ujuzi wa kutengeneza Android App hata kama haujui kitu kuhusiana na Android Development
Soma Zaidi...hili ni somo la tatu katika masomo ya php level 1. Hapa utajifunza zaidi kuhusu variable na namna ya kuitengeneza.
Soma Zaidi...Karibu kwenye mafunzo ya PHP level 1 na hili ni somo la kwanza. Hapa utajifunza maana ya php, inavyofanya kazi pamoja na historia yake kwa ufupi
Soma Zaidi...Hili n somo la tatu katka muendelezo wa mafunzo ya HTML LEVEL 2 kwa lugha ya kiswahili. Mafunzo haya yanakujia kwa Ihsani ya bongoclass
Soma Zaidi...Katika somo hili la 6 mafunzo ya HTML level 2, tutajfunza namna ya kugawa ukurasa wa wavuti wa html.
Soma Zaidi...Haya ni mafunzo ya php na hili ni somo la tano. Katika somovhili utajifunza namna ya kutengeneza functions.
Soma Zaidi...Huu ni mwendelezo wa mafunzo ya DATABASE kwa kutumia MySQL na hili ni somo la pili. Hapa tutakwenda kuona kwa ufupi ni nini DATABASE
Soma Zaidi...somo hili la 4 katika mafunzo ya PHP level 1 utajifunza aina za data mabazo php inakwenda kuzitumia.
Soma Zaidi...