picha

Mafunzo ya Database MySQL DATABASE somo la 2

Huu ni mwendelezo wa mafunzo ya DATABASE kwa kutumia MySQL na hili ni somo la pili. Hapa tutakwenda kuona kwa ufupi ni nini DATABASE

SOMO LA PILI:

LENGO LA MAFUNZO HAYA KWA UJUMLA:

Lengo la mafunzo haya ni kukuwezesha kutumia database kwenye bloga ama website yako. Pia uweze kutumia database kwa ajili ya Android App ama web App. Pia utaweza kutumia database kwa ajili ya kudhibiti taarifa zako.

 

 

Ni nini maana ya DATABASE?

Data base ni neno la kiingereza ambalo ukilileta kwa kiswahili ni mkusanyiko wa taarifa zilizopangiliwa na kuhifadhiwa na huweza kupatikana katika mfumo wa kielectronic. Taarifa hizi zinakuwa katika majedwali (table).

 

SQL ni nini?

SQL ni lugha ya kikompyuta ambayo hutumika katika udhibiti wa database. Lugha hii yenyewe hutumiaka kwenye server. Je unajuwa ni nini maana ya server? Pitia somo la kwanza mafunzo ya PHP.

 

SQL ni kifupisho cha maneno ;- Structured Query Language. Hii ndio lugha ya kikompyuta ambayo inahusika katika kuthibiti database kama kufuta taarifa, kuedit na kuongeza ama kupunguza.

 

 

Ni ni Databae management System (DBMS)

Hizi ni software ambazo zimetengenezwa kwa ajili ya kudhibiti taarifa kwenye database. Mifano ya software hizi ni kama:-

  1. Ms
  2. Sql server
  3. IBM DB2
  4. Oracle
  5. MySQL
  6. Microsoft Access

Software hizi ndizo ambazo zinatumia lugha ya SQL kwa ajili ya kutumia database. Chukulia mfano php ni lugha ya kikompyuta lakini haiwezi kufanya kazi mapaka kuwe na server pamoja na software ya php. Hivi ndivyo na SQL inafanya kazi kwenye server na inahitahi software.

 

 

MySQL

Katika masomo yetu haya tutatumia MySQL, kwa kuwa ni free, pa inatumiaka sana kuliko hizo nyingine. Pia ni rahisi kuitumia. Unaweza kuipata kwa kutumia simu ama kompyuta.

 

SQL inaweza kufanya nini?

  1. Kusoma taarifa kwenye database
  2. Kuweka taarifa kwenye database
  3. Kufuta taarifa kwenye database
  4. Kubadili taarifa kwenye database
  5. Kutengeneza jedwali kwenye database
  6. Kufyta majedwali kwenye database

 

 

Mahusiano ya PHP na SQL

  1. PHP inatumika kwenye website kwa ajili ya kutumia SQL ili kufikia database.
  2. Kwa watumiaji wa blog, post na koment zinakuwa kwenye database, hivyo itatumiaka PHP ili kuweza kutumia SQL ili kuzipata post ambazo zipo kwenye database na kufanya watumiaji wa blog waweze kuziona.
  3. PHP pekee haiwezi kutumia database bila ya kuhitaji SQL
  4. Kwa kutumia SQL unaweza kutumia MYSQL ili kuthibiti database bila hata ya kuhitaji PHP.

 

 

SQL na MySQL

Kwa watumiaji wa kawaida MYySQL inatosha kuitumia hata kama hijui SQL lakini ili kuweza kudhibiti vyema database utahitaji kuzungumza kwa lugha hii ya SQL kwenye MySQL ili kudhibiti database. SQL ni lugha ya kikompyuta kama ilivyo PHP lakini MySQL ni software ambayo hutumia SQL kwa ajili ya kudhibiti database.

 

 

Je wajuwa kuwa:

“Katika siku za mwanzoni mwa facebook ilihitaji PHP, SQL na MySQL kwa ajili ya kudhibiti database yote ya facebook”. kwa mchanganyiko wa HTML, JAVASCRIPT, CSS unaweza kufanya makubwa.

 

 

Tukutane somo la Tatu tutakapoanza kujifunza hasa kuhusu hiii SQL na sheria zake. Na vipi utaweza kuitumia. Hakikisha somo la kwanza umelipitia vyema na umeweza kuandaa kifaa chako vyema.

 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2021/11/15/Monday - 03:17:05 pm Topic: Tehama Main: Jifunze File: Download PDF Views 1658

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game    👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉4 Madrasa kiganjani    👉5 ai web app    👉6 web hosting   

Post zinazofanana:

Mafunzo ya php level 1 somo la tatu (3)

hili ni somo la tatu katika masomo ya php level 1. Hapa utajifunza zaidi kuhusu variable na namna ya kuitengeneza.

Soma Zaidi...
PHP level 1 somo la tisa (9).

Somo la nane mafunzo ya php, katika somo hili utajifunza kuhusu array na jinsi ya kutengeneza array.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya php level 1 somo la nne (4)

somo hili la 4 katika mafunzo ya PHP level 1 utajifunza aina za data mabazo php inakwenda kuzitumia.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya HTML Level 1 somo la 2 for beginner (html full course for beginners)

Somo la pili katika mafunzo ya HTML level 2. Katika somo hili utajifunza maana ya HTML pamoja na historia yake fupi.

Soma Zaidi...
PHP level 1 somo la kumi (10)

Somo la 10 mafunzo ya php level 1. Katika somo hili utajifunza kuhusu condition statement.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya HTML Level 2 somo la 3 (HTML FULL COURSE FOR BEGINNERS LESSON 3)

Hili n somo la tatu katka muendelezo wa mafunzo ya HTML LEVEL 2 kwa lugha ya kiswahili. Mafunzo haya yanakujia kwa Ihsani ya bongoclass

Soma Zaidi...
Mafunzo ya HTML Level 2 somo la 5 (HTML FULL COURSE FOR BEGINNERS LESSON 5)

Karibu tena katika mafunzo haya ya html level 2 na hili ni somo la 5. Katika somo hili utajifunza zaidi kuhusu kuweka style kwenye html file.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya HTML Level 2 somo la 4 (HTML FULL COURSE FOR BEGINNERS LESSON 4)

Karibu tena katika somo la nne la mafunzo ya HTML level2 html full course for beginners. Katika somo hili utajifunza kuhusu attributes na namna zinavyofanya kazi

Soma Zaidi...
Mafunzo ya HTML level 1 somo la 6 (HTML basic level FOR BEGINNERS)

hili ni somo la sita katika mfululizo wa mafunzo ya HTML level 1. Katika somo hili tutajifunza mambo makuu matatu ambayo ni kuweka menyu, kuweka background color na kufanya faili lako liwe responsive.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya HTML Level 2 somo la 7 (HTML FULL COURSE FOR BEGINNERS LESSON 7)

Ktika somo hili la 7 utajifunza namna ya kuandaa na kujiandaa kutengeneza website ama blog. Pia utajifunza maandalizi ya kuhost

Soma Zaidi...