Mafunzo ya Database MySQL DATABASE somo la 2

Huu ni mwendelezo wa mafunzo ya DATABASE kwa kutumia MySQL na hili ni somo la pili. Hapa tutakwenda kuona kwa ufupi ni nini DATABASE

SOMO LA PILI:

LENGO LA MAFUNZO HAYA KWA UJUMLA:

Lengo la mafunzo haya ni kukuwezesha kutumia database kwenye bloga ama website yako. Pia uweze kutumia database kwa ajili ya Android App ama web App. Pia utaweza kutumia database kwa ajili ya kudhibiti taarifa zako.

 

 

Ni nini maana ya DATABASE?

Data base ni neno la kiingereza ambalo ukilileta kwa kiswahili ni mkusanyiko wa taarifa zilizopangiliwa na kuhifadhiwa na huweza kupatikana katika mfumo wa kielectronic. Taarifa hizi zinakuwa katika majedwali (table).

 

SQL ni nini?

SQL ni lugha ya kikompyuta ambayo hutumika katika udhibiti wa database. Lugha hii yenyewe hutumiaka kwenye server. Je unajuwa ni nini maana ya server? Pitia somo la kwanza mafunzo ya PHP.

 

SQL ni kifupisho cha maneno ;- Structured Query Language. Hii ndio lugha ya kikompyuta ambayo inahusika katika kuthibiti database kama kufuta taarifa, kuedit na kuongeza ama kupunguza.

 

 

Ni ni Databae management System (DBMS)

Hizi ni software ambazo zimetengenezwa kwa ajili ya kudhibiti taarifa kwenye database. Mifano ya software hizi ni kama:-

  1. Ms
  2. Sql server
  3. IBM DB2
  4. Oracle
  5. MySQL
  6. Microsoft Access

Software hizi ndizo ambazo zinatumia lugha ya SQL kwa ajili ya kutumia database. Chukulia mfano php ni lugha ya kikompyuta lakini haiwezi kufanya kazi mapaka kuwe na server pamoja na software ya php. Hivi ndivyo na SQL inafanya kazi kwenye server na inahitahi software.

 

 

MySQL

Katika masomo yetu haya tutatumia MySQL, kwa kuwa ni free, pa inatumiaka sana kuliko hizo nyingine. Pia ni rahisi kuitumia. Unaweza kuipata kwa kutumia simu ama kompyuta.

 

SQL inaweza kufanya nini?

  1. Kusoma taarifa kwenye database
  2. Kuweka taarifa kwenye database
  3. Kufuta taarifa kwenye database
  4. Kubadili taarifa kwenye database
  5. Kutengeneza jedwali kwenye database
  6. Kufyta majedwali kwenye database

 

 

Mahusiano ya PHP na SQL

  1. PHP inatumika kwenye website kwa ajili ya kutumia SQL ili kufikia database.
  2. Kwa watumiaji wa blog, post na koment zinakuwa kwenye database, hivyo itatumiaka PHP ili kuweza kutumia SQL ili kuzipata post ambazo zipo kwenye database na kufanya watumiaji wa blog waweze kuziona.
  3. PHP pekee haiwezi kutumia database bila ya kuhitaji SQL
  4. Kwa kutumia SQL unaweza kutumia MYSQL ili kuthibiti database bila hata ya kuhitaji PHP.

 

 

SQL na MySQL

Kwa watumiaji wa kawaida MYySQL inatosha kuitumia hata kama hijui SQL lakini ili kuweza kudhibiti vyema database utahitaji kuzungumza kwa lugha hii ya SQL kwenye MySQL ili kudhibiti database. SQL ni lugha ya kikompyuta kama ilivyo PHP lakini MySQL ni software ambayo hutumia SQL kwa ajili ya kudhibiti database.

 

 

Je wajuwa kuwa:

“Katika siku za mwanzoni mwa facebook ilihitaji PHP, SQL na MySQL kwa ajili ya kudhibiti database yote ya facebook”. kwa mchanganyiko wa HTML, JAVASCRIPT, CSS unaweza kufanya makubwa.

 

 

Tukutane somo la Tatu tutakapoanza kujifunza hasa kuhusu hiii SQL na sheria zake. Na vipi utaweza kuitumia. Hakikisha somo la kwanza umelipitia vyema na umeweza kuandaa kifaa chako vyema.

 

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Je umeipenda post hii ?

Ndio            Hapana            Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tehama Main: Jifunze File: Download PDF Views 1182

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

PHP level 1 somo la nane (8)

Hapa utajifunza utofauti kati ya php constant na variable. Na hili ni somo la nane katika mfululizo wa masomo haya ya php level 1.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya HTML level 1 somo la 1 (HTML basic level FOR BEGINNERS)

Haya ni mafunzo ya HTML kwa wanaoanza level ya kwanza, na hili ni somo la kwanza katika masomo 8 yatakayokujia katika mtiririko wa course hii.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya HTML Level 2 somo la 5 (HTML FULL COURSE FOR BEGINNERS LESSON 5)

Karibu tena katika mafunzo haya ya html level 2 na hili ni somo la 5. Katika somo hili utajifunza zaidi kuhusu kuweka style kwenye html file.

Soma Zaidi...
Mafunzo yz database MySQL database somo la 12 (final)

Huu ni muendelezowa mafunzo ya database kwa kutumia MySQl na hili ni somo la 12. katika somo hili tutajifunza namna ya kufanya mahesabu kwa kutumia SQl katika database

Soma Zaidi...
Mafunzo ya DATABASE kwa kutumia MySQL DATABASE kwa kiswahili somo la 4

Huu ni mwendelezo wa mafunzo ya database kwa kutumia MySQL na hili ni somo la nne katika mlolongo wa masomo haya. Katika somo hili utajifuza jinsi ya kubadili jina la database na kufuta database. Pia tutajifunza kutumia SQL kufanya hayo.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya database mySQl database somo la 11

huu ni muendelezo wa mafunzo ya Database klwa kutumia MySQL na hili ni somo la 11. katika somo hili tutaendelea kujifunza mpangilio wa muonekano wa data kwenye database.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya HTML level 1 somo la 7 (HTML basic level FOR BEGINNERS)

Hii ni project ya HTML ambayo imetengenezwa kulingana na mafunzo ya HTML level1. Tunatarajia project hii kuboreshwa kadiri mafunzo yanavyozidi kusonga mbele.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya DATABASE - MySQL database somo la 8

Huuu ni muendeleo wa mafunzo ya database kwa lugha ya kiswahili, na hili ni somo la nane. Katika somo hli utajifunza namna ya kuweka taarifa kwenye database, kuzfuta na kuziediti yaani kuzifanyia marekebisho.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya database MySQL database somo la 9

haya ni mafunzo ya database kwa kutumia MySQl na hili ni somo la 9. katika soo hili utajifunza namna ya kusoma ama kutumia taarifa zilizomo kwenye DATABASE.

Soma Zaidi...
PHP level 11 somo la kumi na moja (11)

Katika somo hilivutajifunza namna ya kutumia HTML form. Namna ya kuookea taarifa kutoka kwenye madodoso ya html form.

Soma Zaidi...