Navigation Menu



Mafunzo ya HTML Level 2 somo la 7 (HTML FULL COURSE FOR BEGINNERS LESSON 7)

Ktika somo hili la 7 utajifunza namna ya kuandaa na kujiandaa kutengeneza website ama blog. Pia utajifunza maandalizi ya kuhost

HATUWA ZA KUTENGENEZA WEBSITE AMA BLOG
Unapotaka kutengeneza website ama blog kuna mambo mengi unatakiwa uyawaze hata kabla ya kuanza. Blog ama website ni kitambulisho cha biashara ama kampuni ama taasisi husika. Ni kitambulisho ambacho kitawafikia watu dunia nzima, watu wa jinsia zote kwa malengo tofauti tofauti. Hivyo basi unatakiwa ufikiri kwa makini.



Haya ni mawazo unatakiwa ujiulize kabla ya kudizaidi tovuti yako:
1.Itahusu nini
2.Kina nani watakuwa wateja wako
3.Ni aina gani tovuti yako
4.Kwa nini watu watembelee tovuti yako na si nyinginezo
5.Nini wanufaika kwako ambacho kwa wengine hawatakipata.
6.Kwa nini unahitaji tovuti
7.Je ni gharama kiasi gani itahitajika



Kisha baada ya kuyapata majibu ya maswali hayo unatakiwa uwaze kabisa jinsi watu watakavyokupata kwenye hito tovuti yako. Tambuwa kuwa kuna zaidi ya tovuti bilioni tatau. Na karibia tovuti milioni 400 zipo active. Hivyo unatakiwa ufikiri vyema vipi watu watakupata.

1.Tafuta jina la tofuti yako liendane na malengo yako
2.Jina liwe fupi na lennye maana
3.Jinaliwe lenye kukaririka vyema
4.Lisiwe lipo wazi
5.Jina liwe la kipekee
6.Lugha yako iendane na watu uliowatageti



Baada ya kuwaza namna ambavyo watu watakavyokupata sasa ni wakati wa wewe kuanza kunihusisha moja kwa moja katika utengenezaji. Haijalishi uwe unatengenezewa ama unatengeneza wewe mwenyewe, kuna mambo unatakiwa uyafanye:-
1.Gharama kiasi gani nitatumia
2.Muda gani utahitajika
3.Chanzo cha maudhui ya tovuti yako.
4.Je web yako itakuwa static ama dynamic
5.Nani anatengeneza ni wewe ama unatengenezewa.



Kuna aina kuu mbili za tovutii ambzo ni static ana dynamic. Static ni ile ambayo inatumia html, css na javascript. Yaani static inakuwa haibadiliki. Dynamic ni zile ambazo taarifa zake hubadilika badilika. Yaani admin anaweza kuedit makala hata kamakuna mtu anaisoma. Dynamic ni kama ambazo zimetengenezwa na php na database. Blog zote zinaingia kwenye kundi hili.



Kwa ufupi static ni tovuti ambazo zenyewe taarifa zake hazina mabadilikobadiliko. Na inachukuwa muda mrefu kubadili taarifa moja, mpaka uingie kwenye system nzima.ststic website zenyewe zinahitaji html na css . Lakini dynamic zenyewe muda wowote unaweza kuongeza taarifa na kutoa ama kuediti ama kukoment.



Hatua inayofata ni kuingia kazini sasa kuitengeneza tovuti yako. Hapa ndipo panahitaji umakini, kwani ukiharibu kwenye muonekano unaweza kukosa watu. Kumbuka uzuri we muonekano wa tovuti kwenye kompyuta sio sawa na kwenye simu. Katika hatuwa hii fanya haya:-
1.Chora mchoro wa kuonyesha tovuti yako itakavyofanya kazi
2.Chaguwa text editor kulingana na level ya ujuzi wako unaweza piakutumia WYSIWYG
3.CODE tovvuti yako kwakufuata mchoro wako
4.Zingatia mabadiliko ya screen, kuna wengine watatembelea tovuti yako kwa kompyuta na wengine simu, hivyo uzingatie na ubora
5.Fanya iwe simple, usitumie sana rangi



Baada ya kuikamilisha website yako utahitaji kuihost. Kuihost ni kuifanya ipatikane kwenye internet. Cheki somo la nane katika course iliyopita tumetoa maelekezo ya video jinsi a kuhost kwa free. Kuna mitandao mingi inatoa huduma ya kuhost code zako free. Hapa ntakuorodheshea tovuti chake
1.Google cloud
2.Google firebase
3.00webhosting
4.Infinityfree
5.Digitalocean



Zipo kampuni nyingine nyingi tuu zitakupa huduma hii ure. Nimetaja hizo chache kwa sababu nina uzoefu nazo. Kama utakuwa na code za php nakusauri tumia 00webhosting ama infinityfree. Ila kama ni html css na javascript google firebase ni nzuri japo ni ngumu kuielewa mwanzo, hivyo vyema kutumia hizo mbili nilizozitaja hapo juu.

Download app yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download

Download Now Bongoclass

           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu image Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Tehama Main: Post File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Views 989


Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Simulizi za Hadithi Audio     👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉6 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Mafunzo ya HTML level 1 somo la 6 (HTML basic level FOR BEGINNERS)
hili ni somo la sita katika mfululizo wa mafunzo ya HTML level 1. Katika somo hili tutajifunza mambo makuu matatu ambayo ni kuweka menyu, kuweka background color na kufanya faili lako liwe responsive. Soma Zaidi...

Mafunzo ya HTML Level 2 somo la 3 (HTML FULL COURSE FOR BEGINNERS LESSON 3)
Hili n somo la tatu katka muendelezo wa mafunzo ya HTML LEVEL 2 kwa lugha ya kiswahili. Mafunzo haya yanakujia kwa Ihsani ya bongoclass Soma Zaidi...

Mafunzo ya HTML Level 2 somo la 8 (HTML FULL COURSE FOR BEGINNERS LESSON 8)
Hili ni somo la mwisho mafunzo ya HTML level 2 (html full course for beginners) Soma Zaidi...

Mafunzo ya php level 1 somo la kwanza (1)
Karibu kwenye mafunzo ya PHP level 1 na hili ni somo la kwanza. Hapa utajifunza maana ya php, inavyofanya kazi pamoja na historia yake kwa ufupi Soma Zaidi...

Php level 1 somo la saba (7)
Hili ni somo la saba, mafunzo ya php level 1. Katika somo hili utajifunza jinsi ya kuandika function yako mwenyewe. Soma Zaidi...

Mafunzo ya php level 1 somo la pili (2)
hili ni somo la pili katika mfululizo wa mafunzo haya ya php level 1 na hapa utajifunza namna ya kuandika faili klako la kwanza la php. Soma Zaidi...

Mafunzo ya HTML Level 1 somo la 2 for beginner (html full course for beginners)
Somo la pili katika mafunzo ya HTML level 2. Katika somo hili utajifunza maana ya HTML pamoja na historia yake fupi. Soma Zaidi...

Mafunzo ya HTML level 1 somo la 1 (HTML basic level FOR BEGINNERS)
Haya ni mafunzo ya HTML kwa wanaoanza level ya kwanza, na hili ni somo la kwanza katika masomo 8 yatakayokujia katika mtiririko wa course hii. Soma Zaidi...

Mafunzo ya database mySQl database somo la 11
huu ni muendelezo wa mafunzo ya Database klwa kutumia MySQL na hili ni somo la 11. katika somo hili tutaendelea kujifunza mpangilio wa muonekano wa data kwenye database. Soma Zaidi...

Mafunzo ya database MySQL - DATABASE somo la 6
Huu ni muendelezo wa mafunzo ya database kwa kutumia MySQL na hili ni somo la 6. Katika somo hili tutakwenda kuona jinsi ya kutengeneza table kwa kutumia MySQL na kwa kutuma SQL. Soma Zaidi...