image

PHP level 1 somo la tano (5)

Haya ni mafunzo ya php na hili ni somo la tano. Katika somovhili utajifunza namna ya kutengeneza functions.

SOMO LA TANO:
PHP FUNCTIONS:
Katika programming language, php imepata ubora wake kwa kuwa na hiki kipengele cha functions. Katika php kuna functions zaidi ya 1000. pia php inakupa uwezo wa wewe kuandika function yako mwenyewe kulingana na matarajio yako. Hivyo basi zipo funtion ambazo tayari zipo. Hizi zinaitwa built-in PHP functions. Na kuna hizo ambazo unaweka mwenyewe, hizi huitwa user defined functions.


 

Sasa function ni nini hasa?
Function ya kikundi cha maelekezo (block of statement) katika code za php ambazyo huweza kutumika zaidi na zaidi katika program. Tofauti na statement nyingine kama echo na print, ambazo huleta matokea punde tu ukiran code ama ukurasa ukufunguliwa au kurefresh. Function zenyewe mpaka zitu ziitajwe kwenye code yaani (by calling the functions).

Katika somo hili tutaona baadhi ya mifano ya built-in-function na jinsi zinavyofanya kazi kwa mifano. Hapa tutaangalia hasa kwenye string. Kama tulivyojifunzakatika somo lililopita.


 

KANUNI ZA FUNCTION (built-in-php functions)
1.Kwanza ni jina la function ila lisianze na namba mfano salamu
2.Kisha linafatiwa na mabano () mfano salamu()
3.Ndani ya mabano kunawekwa ujumbe ama maudhui ya hiyo function mfano salami(hujamb)
4.Kisha coloni ; mfano salamu salami(hujamb);

Tutajifunza kanuni nyingine za function kwenye somo linalofata kuhusu user defined functions.


 

FUNCTIONS KWENYE STRING:
1.Kujuwa idadi ya character kwenye string
. Kama unataka kujuwa je katika string kuna herufi ngapi ama namba ngapi ama character ngapi, basi tunatumia strlen() function. Neno hili ni ufupisho wa maneno string length.
Mfano:
<?php
echo strlen (“bongoclass”);
?>
Hii itakupa matokeo 10 kumaanisha kuwa kuna character 10.


 

2.Kwa kutumia php functions unaweza kubadili ama ku replace baadhi ya maandishi ndani ya string. Function inayotumika ni str_replace (). Kwa mfano katika mfano ufuatao nita replace neno bongoclass na kwa google.
<?php
echo str_replace ('karibu', 'bongoclass', 'welcome google');
?>
Hii itakupa matokeo welcome google maneno ya kwanza utaona yamebadilishwa kwa maneno ya pili.


 

3.Kuhesabu idadi ya maneno kwenye string
Katika hali ya kawaida unaweza kusema kuwa hii haina haja.lakini chukulia mfano data zipo kwenye database, na huwezi kuhesabu idadi ya maneno, na kwa mfano unatakiwa umlipe mtu kulingana na maneno aliyoandik, hapa utahitaji function ya kuweza kukuhiabia idadi ya maneno kwenye database.

Hivyo kwa namna hii function inayotumika hi hii str_word_count() mfano:-
<?php
echo str_word_count("welcome at bongoclass");
?>
Hii itakupa jibu la 3 yaani katika string iliyotumika kuna maneno matatu.


 

4.Pia unaweza kugeuza maneno, yamomeke mbelenyuma nyuma mbele. Kwa mfabo “welcome at bongoclass “ ukiligeuza litasomeka “ssalcognob ta emoclew”. ili kufanya hivi function inayotumika ni strrev yaani string revise. Mfano

<?php
echo strrev("welcome at bongoclass");
?>


 

5.Pia kwa kutumia strpos() unaweza kutafuta neno fulani kama lipo, kisha kama lipo matokeo utaambiwa position lilipo kwenye string. Yaani kama lipo la tatu kutoka mwanzo ama la nne. Kwa mfano katika string ifuatayo tutaangalia position ya neno bongoclass.

<?php
echo strpos('welcome google,welcome bongoclass,welcome facebook', 'bongoclass');
?>
Hapa utapata jibu 23 yaani neno bongoclass linapatikana kuanzia kwenye string ya 23 kutoka mwanzo. Na katika kuhesabu huku huanzia 0 na sio kwenye 1.


 

6.Kujiwa aina ya data iliyotumika
Ili uweze kujuwa aina ya data iliyotumika huwa tunatumia var_dump(). hii ni function ambayo hutumika katika kuonyesha aina ya data iliyotumika kwenye php. Angalia mifano hapo chini:-


Mfano 1:
<?php
$a = "hello piga *112#";
Var_dump ($a);
?>

Hapa iakuletea: string(16) "hello piga *112#" hii inamaana kuwa data nilizotumia kwenye mfano huu ni string, ambazo ni mkusanyiko wa herufi, namba na alama kama * na #. hiyo 16 hapo ina maanisha kuwa string iliyotumika ina character 16.


Katika somo lijalo tutaona function kwenye tarehe na kalenda na baadhi ya built-in-functions kwenye php. Hakikisha somo hili umelimudu vyema kwa kulifanyia mazoezi kabla ya kuingia somo linalofata.


Mafunzo haya yanakujia kwa ihsani ya bongoclass
Web: www.bongoclass.com
Email:mafunzo@bongoclass.com
Phone: 0774069753 unaweza kunicheki wasap kwa link hii https://wa.me/message/7CTQP5BSWBR5I1

 





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 722


Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

Mafunzo ya Database MySQL database somo la 10
Huu ni muendelezo wa mafunzo ya Database kwa kutumia MySQL na hili ni somo la 10. katika somo hili tutakwenda kuendelea namna ya kupangilia muonekano wa data zako kwenye database. Soma Zaidi...

Mafunzo ya HTML Level 2 somo la 5 (HTML FULL COURSE FOR BEGINNERS LESSON 5)
Karibu tena katika mafunzo haya ya html level 2 na hili ni somo la 5. Katika somo hili utajifunza zaidi kuhusu kuweka style kwenye html file. Soma Zaidi...

Mafunzo ya HTML level 1 somo la 3 (HTML basic level FOR BEGINNERS)
Hili ni somo la Tatu katika mfululizo wetu wa mafunzo ya HTML kwa basic level kwa wanaoanza kujifunza. Hapa tutakwenda kujifunza tag za html ambazo huwa zinatumika katika uandishi. Soma Zaidi...

Mafunzo ya html level 2 (html full course for beginners)
haya ni mafunzo ya HTML level 2 kwa wenye kuanza. Mafunzo haya ni muendelezo wa level 1 html. Katika course hii utajifunza mengi zaidi lu;iko level1 pia tutazidi kuboresha project yetu. Soma Zaidi...

Mafunzo ya HTML level 1 somo la 1 (HTML basic level FOR BEGINNERS)
Haya ni mafunzo ya HTML kwa wanaoanza level ya kwanza, na hili ni somo la kwanza katika masomo 8 yatakayokujia katika mtiririko wa course hii. Soma Zaidi...

Utangulizi wa Android App Development
Haya ni mafunzo ya muda mfupi katika kujifunza hasa ujuzi wa kutengeneza Android App hata kama haujui kitu kuhusiana na Android Development Soma Zaidi...

Mafunzo ya php level 1 somo la pili (2)
hili ni somo la pili katika mfululizo wa mafunzo haya ya php level 1 na hapa utajifunza namna ya kuandika faili klako la kwanza la php. Soma Zaidi...

Mafunzo ya DATABASE - MySQL database somo la 8
Huuu ni muendeleo wa mafunzo ya database kwa lugha ya kiswahili, na hili ni somo la nane. Katika somo hli utajifunza namna ya kuweka taarifa kwenye database, kuzfuta na kuziediti yaani kuzifanyia marekebisho. Soma Zaidi...

Mafunzo ya php level 1 somo la tatu (3)
hili ni somo la tatu katika masomo ya php level 1. Hapa utajifunza zaidi kuhusu variable na namna ya kuitengeneza. Soma Zaidi...

Mafunzo ya HTML level 1 somo la 8 (HTML basic level FOR BEGINNERS)
Katika somo hili la 8 mafunzo ya html level 8 utajifunza jinsi ya kuhost project ya html na kuwa live, watu wakaipitia na kusoma maudhui yake. Soma Zaidi...

Mafunzo ya HTML level 1 somo la 5 (HTML basic level FOR BEGINNERS)
katika somo hili la tano kwenye mafunzo ya HTML level 1 utajifunza jinsi ya 1.Kuweka picha 2.Kuweka rangi 3.Kuweka linki 4.Kupangilia position na alignment ya maandishi 5.Kuongeza ukubwa wa herufi 6.Kukoment Soma Zaidi...

Mafunzo ya database MySQL somo la 3
Huu ni mwendelezo wa mafunzo ya database na jinsi ya kutengeneza bloga na website na hili ni somo la tatu. hapa utajifunza jinsiya kutengeneza database yako kwa mara ya kwanza. Soma Zaidi...