Mafunzo ya HTML Level 2 somo la 4 (HTML FULL COURSE FOR BEGINNERS LESSON 4)

Karibu tena katika somo la nne la mafunzo ya HTML level2 html full course for beginners. Katika somo hili utajifunza kuhusu attributes na namna zinavyofanya kazi

ATTRIBUTES NA NAMNA AMBAVYO ZINAFANYA KAZI:
Kama tulivyoona katika somo lililopita tulijifunzakuwa Attributes zina kazi ya kuongeza taarifa nyinginezo kwenye tag. Katika somo hili tutakwenda kujifunza zaidi kluhusu attributes, sifa zake, kanuni zake na zinavyofanya kazi. Kwa ufupi attributes zinawza:-

 

 

1.Kuwa katika element yoyote ya HTML
2.ATTRIBUE HUPATIKANA KWENYE TAG YA KUANZIA NA SI YA KUFUNGIA
3.HUONGEZA TAARIFA ZA ZIADA KWENYE ELEMENT
4.Attributes zinakuwa katika kanuni hii jina=”” naani unaanza kutaja jina la attribute kisha unaweka alama ya sawasawa kisha thamani ya attribute inawekwa ndani ya alama za funga semi.

 

 

 

 

MIFANO YA ATTRIBUTES
1.Attribute wakati wa kuweka link. Hii hukaa kwenye tag ya <a> pale unapotaka kuweka link ya ukurasa mwingine wa wavuti.

 

 

Kwanza utaweka tag ya <a kisha itafatiwa na jina la attribute href (hhypertext referrence) kisha itafatiwa na alama ya = na thamani ya attribute itawekwa kwenye alama za “”.
Mfano
<a href=”www.bongoclass.com”>weka jina la link hapa</a> katika mfano huu <a ndio tag na href ni jina la attribute na “www.bongoclass.com” ndio thamani ya attribute.

 

 

2.ATTRIBUTE ZINAZOTUMIKA KUWEKA PICHA
Attribute hizi hukaa kwenye tag ya <img lengo la attribute hii ni kuweka chanzo cha picha na jina la picha. Chanzo cha picha huwekwa kwa src=” ” na jina la picha huwekwa kwa alt=” ”

 

 

Mfano:
<img src=”bongo.png” alt=”picha”> katika mfano huu <img ndio tag na src ndio jina la attribute na “bongo.png” ndio thamani ya attribute. Pia katika mfano huu una attribute mbili. Attribute nyingine jina lake ni alt na thamani yake ni “picha”. attribute hii hutumika kuonyesha jina la picha hiyo. Endapo picha haita onekana kwa mfano mtandao ukawa low basi jina ndio huonekana.

3.Attribute zinazotumika kuonyesha ukubwa kama urefu na upana. Attribute hii ni height kuonyesha urefuwa kimo na width kuonyesha upana wa kitu.

Mfano
<img src=”picha.png” width=”100%” alt=”picha”> katika mfano huu attribute nyingine hapo ni width kuonyesha upana wa picha na thamani yake ni 100%.

4.Attribute ya kuweka style
Atribute hii hutumika katika shughuli nyingi. Kwa mfano ukitaka kuweka rangi kwenye maandishi, ama kubadili muelekeo, na mpangilio wa herufi atribute hii hutumika. Kwa mfano:-

<p style=”color:yellow”>maandishi haya yatakuwa na rangi ya njano</p> katika mfano huu attribute ni style na thamani yake ni color:red yaani rangi nyekundu.

5.Attribute ya title yaani ya kuwekea kicha cha habari cha faili. Mfano <h1 title=”HTML”> SOMO LA HTML</title> katika mfano huu tumeweka jina kwenye tag ya <h1> hivyo attribute ni title na thamani yake ni “HTML”.

 

 

Attribute nyingine kama ile ya lang tuliotumia kuweka lugha inayotumika katika faili la html.pia atribute za metadata na nyinginezo tutaziona katika masomo yajayo. Katika kutumia attribute unashauriwa kutumia herufi ndogo na funga na funguwa semi mbilimbili yaani “ kama ilivyo kwenye mifano hapo juu.

 

 

 

 

Hivyo katika mifano hiyo tumetumia attributes zifuatazo:-
1.href
2.src
3.width
4.alt
5.style
6.Title

 

 

 

 

Tukutane somo lijalo tutakapokuja kujuwa zaidi jinsi ya kuweka stayle mbalimbali katika uandishi katika html. Somo hili litaanza kutumia tag na attributes kwa pamoja katika ufanisi wa kufanikisha uandishi.

 

 

 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tehama Main: Jifunze File: Download PDF Views 934

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game    👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 Madrasa kiganjani    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Mafunzo ya HTML Level 2 somo la 7 (HTML FULL COURSE FOR BEGINNERS LESSON 7)

Ktika somo hili la 7 utajifunza namna ya kuandaa na kujiandaa kutengeneza website ama blog. Pia utajifunza maandalizi ya kuhost

Soma Zaidi...
Mafunzo ya HTML level 1 somo la 3 (HTML basic level FOR BEGINNERS)

Hili ni somo la Tatu katika mfululizo wetu wa mafunzo ya HTML kwa basic level kwa wanaoanza kujifunza. Hapa tutakwenda kujifunza tag za html ambazo huwa zinatumika katika uandishi.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya html level 2 (html full course for beginners)

haya ni mafunzo ya HTML level 2 kwa wenye kuanza. Mafunzo haya ni muendelezo wa level 1 html. Katika course hii utajifunza mengi zaidi lu;iko level1 pia tutazidi kuboresha project yetu.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya HTML Level 2 somo la 3 (HTML FULL COURSE FOR BEGINNERS LESSON 3)

Hili n somo la tatu katka muendelezo wa mafunzo ya HTML LEVEL 2 kwa lugha ya kiswahili. Mafunzo haya yanakujia kwa Ihsani ya bongoclass

Soma Zaidi...
Mafunzo ya HTML Level 2 somo la 6 (HTML FULL COURSE FOR BEGINNERS LESSON 6)

Katika somo hili la 6 mafunzo ya HTML level 2, tutajfunza namna ya kugawa ukurasa wa wavuti wa html.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya php level 1 somo la nne (4)

somo hili la 4 katika mafunzo ya PHP level 1 utajifunza aina za data mabazo php inakwenda kuzitumia.

Soma Zaidi...
Php level 1 somo la saba (7)

Hili ni somo la saba, mafunzo ya php level 1. Katika somo hili utajifunza jinsi ya kuandika function yako mwenyewe.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya HTML Level 2 somo la 5 (HTML FULL COURSE FOR BEGINNERS LESSON 5)

Karibu tena katika mafunzo haya ya html level 2 na hili ni somo la 5. Katika somo hili utajifunza zaidi kuhusu kuweka style kwenye html file.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya HTML level 1 somo la 7 (HTML basic level FOR BEGINNERS)

Hii ni project ya HTML ambayo imetengenezwa kulingana na mafunzo ya HTML level1. Tunatarajia project hii kuboreshwa kadiri mafunzo yanavyozidi kusonga mbele.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya HTML kwa wenye kuanza (basic level)

Huu ni utangalizi wa mafunzo ya HTML kwa wenye kuanza level ya kwanza kwa lugha ya kiswahili. Haapa utapata msingi wa kuweza kutengeneza tovuti na blog.

Soma Zaidi...