Mafunzo ya HTML level 1 somo la 1 (HTML basic level FOR BEGINNERS)

Mafunzo ya HTML level 1 somo la 1 (HTML basic level FOR BEGINNERS)

Haya ni mafunzo ya HTML kwa wanaoanza level ya kwanza, na hili ni somo la kwanza katika masomo 8 yatakayokujia katika mtiririko wa course hii.

HTML SOMO LA KWANZA

HTML ni ufupisho wa maneno yanayosomeka kama:-

Hypertext

Markup

Language

 

 

Ni lugha ya komputa inayotumika katika kutengenezea kurasa za tovuti (website) ama blog.Inaungana na lugha nyingine katika kuboresha kurrasa za tovuti ama blog na kuzifanya ziweze kufanya kazi iliyokusudiwa vyema. Unaweza kutumia HTML tu ukatengeneza website yako bila ya lugha nyingine. Hata hivyo muonekano wake hautakuwa vyema sana kama hutatumia nyinggine.

 

 

Je na wewe una ndoto za kuwa na blog ama website uliyoitengeneza wewe mwenyewe. Mafunzo haya ni kwa ajili yako. Katika mafunzo haya utajifunza namna ya kutengeneza website yako kupitia kiganja chako yaani simu yako ya mkononi. Kama utakuwa na kompyuta hatutakuacha pia.

 

Somo hili la kwanza utajifunza namna ya kuandaa simu yako ama kompyuta yako kwa ajili ya kutengeneza website, ama kwa ajili ya kutumia HTML. Kama tutaenda vyema na mafunzo haya hadi mwisho nakuhakikishia kama Mwenyezi Mungu akitujaalia nguvu, uwezo na uhai, utaweza kutengeneza website yako na kuiweka live.

 

Muda wa masomo haya kwa hatuwa za Awali (Basics) itakuwa na wiki moja. Kisha baada ya hapo hatuwa ya pili ya mafunzo itaendelea. Tafadhali kuwa tayari kujifunza, kuwa muulizaji na mchangiaji:

 

 

VIGEZO VYA KUJIFUNZA:

1.Kuwa na simu ya smartphone au kompyuta

2.Uwe unajuwa kusoma na kuandika

3.Kuwa tayari kujifunza

4.Kuwa mjanja

5.Uwe mwenye kufanyi akazi (fanya mazoezi)

 

 

 

NAMNA YA KUANDAA SIMU YAKO:

1.Download App inayoitwa TrebEdit. Tumia link hii https://play.google.com/store/apps/details?id=com.teejay.trebedit

2.Funguwa App yako kisha bofya Menu

3.Bofya palipoandikwa Workplace

4.Bofya kitufe chenye alama ya kujumlisha chini

5.Kisha bofya palipandikwa New Project

6.Andika jina la Project (mimi natumia HTML) kisha bofya save.

7.Ingia kwenye project uliotengeneza kwa kubofya jina lake, ukurasa mpya utafunguka

8.Bofya tena kitufe cha alama ya kujumlisha

9.Bofya palipoandikwa new folder (hapa tunatengeneza folda la kuweka picha tutakazokuja kuzitumia kwenye tovutu tutakayotengeneza)

10.Andika jina la folda tumia image kisha bofya save.

11.Baada ya hapo rudi nyuma hatuwa moja kwenye project yako.

12.Bofya tena jina la project yako

13.Bofya kitufe cha alama ya kujumlisha

14.Bofya palipandika New file (hapa ndipo tutakapoanzia kuweka code za kutengeneza tovuti yetu)

15.Utatkiwa kuandika jina la file hapo andika index.html (hili ndio faili letu la kwanza la tovuti yetu.

16.Bofya faili hilo ulilolitengeneza, utaona limeandika index.html

17.Baada ya kufunguka kuna maneno chini yameandika html snippet, bofya hayo maneno

18.Ukursa wako sasa utaona una code HONGERA SANA KWA KUFIKA HATUWA HII

19.Juu ya ukurasa kuna kibatani cha kusave, kimefanana na kile cha kwenye microsoft office. Bofya hicho kibatani, hapo utakuwa umesave code zilizopo hapo.

20.Kuna kibatani kingni cha kuplay kimefana na kile tunachotumia kwenye media player. Bofya hicho kupreview code zako.

21.Utaona ukurasa mtupu. Vyema sasa fanya hivi rudi nyuma kisha:-

22.Tafuta haya maneno

Page title

kisha yabadilishe yasomeka

Home Page

 


23.Chini ya maneno haya

 

weka maneno haya

 

 

 

Mafunzo ya HTML

 

Jifunze bure

 

Haya ni mafunzo ya HTML kwa kutumia simu








From
Bongoclass


24.Save

25.Bofya kitufe cha kuplyay ili kuangalia kilichotokea baada ya kuweka hizo code

26. Hongera sana ukurasa wako wa HTML umekamilika. Unaweza kubadili maneno kwenye hizo code hapo juu kweka yako.

 

 

NAMNA YA KUANDAA KOMPYUTA YAKO

 

Kwa watumiaji wa kompyuta funguwa notepad, ama notepadplus ama sublimetext3. unaweza kudowload bure ila kwa notepad haina haja ya kudownload ipo kwenye kompyuta yako. Kwanza tengeneza folder lipe jina website.kisha ndani ya folder hilo tengeneza folda jingine lipe jina imae. Rudi kwenye folda la website Tengeneza faili jipya kisha pest code hizo hapo chini kwenye faili lako.save as andika jina index.html. Lifunguwe faili lako la index.html kwakutumia browser kama chrome litafungukakama website. Angalia video itakusaidia. Unaweza kudownload notepadplus hapa https://notepad-plus-plus.org/downloads/v8.1.4/


 

 

 

 

 

My First Webpage

 

 

 

 

 

Welcome to my webpage

 

 

Welcome to my brand new website.

 

Google

 

 


Somo la pili tutaanza kujifunza hizo code ulizoziweka kazi yake na vipi zinafanya kazi. Kama umefanikiwa hatuwa zote hizo tupe maoni yako, ama tutumie screenshot yako.

 

Bongoclass
Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya hapa chini kuipakua sasa!

Zoezi la Maswali

Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tehama Main: Jifunze File: Download PDF Views 3063

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Mafunzo ya HTML Level 2 somo la 7  (HTML FULL COURSE FOR BEGINNERS LESSON 7)
Mafunzo ya HTML Level 2 somo la 7 (HTML FULL COURSE FOR BEGINNERS LESSON 7)

Ktika somo hili la 7 utajifunza namna ya kuandaa na kujiandaa kutengeneza website ama blog. Pia utajifunza maandalizi ya kuhost

Soma Zaidi...
Mafunzo ya DATABASE - MySQL somo la 7
Mafunzo ya DATABASE - MySQL somo la 7

Mafunzo ya database kwa utumia software ya MySQL kwa lugha ya kiswahili na hili ni somo la 7.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya HTML Level 2 somo la 8  (HTML FULL COURSE FOR BEGINNERS LESSON 8)
Mafunzo ya HTML Level 2 somo la 8 (HTML FULL COURSE FOR BEGINNERS LESSON 8)

Hili ni somo la mwisho mafunzo ya HTML level 2 (html full course for beginners)

Soma Zaidi...
Mafunzo ya database MySQL -  DATABASE somo la 6
Mafunzo ya database MySQL - DATABASE somo la 6

Huu ni muendelezo wa mafunzo ya database kwa kutumia MySQL na hili ni somo la 6. Katika somo hili tutakwenda kuona jinsi ya kutengeneza table kwa kutumia MySQL na kwa kutuma SQL.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya DATABASE - MySQL database somo la 8
Mafunzo ya DATABASE - MySQL database somo la 8

Huuu ni muendeleo wa mafunzo ya database kwa lugha ya kiswahili, na hili ni somo la nane. Katika somo hli utajifunza namna ya kuweka taarifa kwenye database, kuzfuta na kuziediti yaani kuzifanyia marekebisho.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya database mySQl database somo la 11
Mafunzo ya database mySQl database somo la 11

huu ni muendelezo wa mafunzo ya Database klwa kutumia MySQL na hili ni somo la 11. katika somo hili tutaendelea kujifunza mpangilio wa muonekano wa data kwenye database.

Soma Zaidi...
PHP level 1 somo la sita (6)
PHP level 1 somo la sita (6)

Katika somo hili la php level 1 somo la 6 utajifunza namna ya kutumia tarehe yaani function date() kwenye PHP

Soma Zaidi...
Mafunzo ya HTML Level 2 somo la 1  (HTML FULL COURSE FOR BEGINNERS LESSON 1)
Mafunzo ya HTML Level 2 somo la 1 (HTML FULL COURSE FOR BEGINNERS LESSON 1)

hili ni somo la pili katika mafunzo ya HTML level 2 html full course for beginners. Katika somo hili tutaangalia utangulizi juu ya HTML na pia utajifunza faida za HTML.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya Database MySQL DATABASE somo la 2
Mafunzo ya Database MySQL DATABASE somo la 2

Huu ni mwendelezo wa mafunzo ya DATABASE kwa kutumia MySQL na hili ni somo la pili. Hapa tutakwenda kuona kwa ufupi ni nini DATABASE

Soma Zaidi...
Mafunzo yz database MySQL database somo la 12 (final)
Mafunzo yz database MySQL database somo la 12 (final)

Huu ni muendelezowa mafunzo ya database kwa kutumia MySQl na hili ni somo la 12. katika somo hili tutajifunza namna ya kufanya mahesabu kwa kutumia SQl katika database

Soma Zaidi...