picha

Njia za kuzuia Ugonjwa wa tauni.

Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali ambazo zinaweza kutumika ili kuweza kuepuka Ugonjwa wa raundi.

Njia za kuepuka Ugonjwa wa tauni.

1.Kwanza kabisa tunapaswa kujua kuwa ugonjwa huu utokana na kuwepo kwa panya ambao ubeba wadudu na viroboto ndio wanaofanya kazi ya kusambaza hawa wadudu kwa hiyo jamii inapaswa kujulisha kuwepo kwa Ugonjwa huu maana Ugonjwa huu utokea kwa msimu na kupotea kwa hiyo kuwepo kwa Ugonjwa huu na kujua Dalili zake itakuwa rahisi kuweza kuudhibiti na kuondoa hali ya kunyanyapaa wagonjwa  na watu wakishajua hilo wataweza kuwa na tahadhari.

 

2. Pia jamii inapaswa kuepukana na tabia ya kukubali kuwepo kwa aina yoyote ya panya kwenye mazingira yao na vilevile kama kuna mgonjwa yeyote ametokea ni lazima kutoa taarifa na kuepuka kugusa maji maji yanayotoka kwa mgonjwa ili kuepuka kuambukiza na pia kuwa mbali na mgonjwa pale ambapo mgonjwa amefikia kwenye hatua ya tatu kwa sababu ni ya hatari sana na watu uweza kuambukizwa zaidi hasa kwenye familia na wote wanaowazunguka .

 

3. Elimu ni lazima kutolewa kwa jamii kuhusu jinsi Ugonjwa unavyoambukiza, dalili za ugonjwa , chanzo cha ugonjwa na hatua anazopitia Mgonjwa, kwa kufanya hivyo watu watakuwa makini ili kuweza kuepuka kusambaa kwa ugonjwa wa tauni pia jamii inapaswa kuhakikishiwa juwa huu ni ugonjwa ambao unatibiwa kabisa na watu wanapona na pia wajue hatua za ugonjwa na dalili zake ili waweze kupata matibabu mapema iwezekanavyo.

 

4. Vile vile watu wanapaswa kuacha tabia ya kulala chini kwa sababu chini ndipo kuna viroboto wengi kwa hiyo wanashauriwa kulala kwenye vitanda na pia usafi ni wa lazima hasa katika kipindi cha mavuno kuhakikisha kuwa mazao yamewekwa sehemu nzuri ambapo panya hawawezi kufika na kushambulia mazao na kuleta madhara, au kwa upande mwingine tunapaswa kutumia dawa ili kuua panya na viroboto kwa kufanya hivyo tutaweza kuepuka Ugonjwa huu.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 3078

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Bongolite - Game zone - Play free game     👉4 web hosting     👉5 Kitau cha Fiqh     👉6 Kitabu cha Afya    

Post zinazofanana:

Zijue sababu za moyo kutanuka.

Posti hii inahusu zaidi sababu za moyo kutanuka, Kuna kipindi ambapo moyo utoka kwenye hali yake ya kawaida na kutanuka hali ambayo usababisha madhara kwa mwenye tatizo hilo, ila Kuna sababu ambazo usababisha moyo kutanuka kama tutakavyoona.

Soma Zaidi...
MALARIA INATOKEAJE? (Namna ambavyo malaria inatokea, inaanza na inavyoathiri afya)

Kama tulivyokwisha kuona kuwa malaria inaweza kuambukizwa kwa kung'atwa na mbu aina ya anophelesi.

Soma Zaidi...
Tahadhari za ugonjwa wa UTI

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu tahadhari za kuchukua ili kujikinga na UTI

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa degedege na dalili zake

Ugonjwa wa degedege ni ugonjwa unaowapata sana watoto chini ya miaka mitano ingawa na watu wazima wanapatwa na ugonjwa huo

Soma Zaidi...
Madhara ya kutotibu ugonjwa wa makende kushindwa kushuka

Posti hii inahusu zaidi madhara ya kutotibu magonjwa ya makende kushindwa t, hiki ni tatizo na huleta madhara

Soma Zaidi...
Mambo yanayosababisha kuharisha

Post hii inahusu zaidi ugonjwa wa kuharisha, kuharisha ni kitendo Cha kupitisha kinyesi Cha maji chenye damu au kisichokuwa na damu

Soma Zaidi...