picha

Njia za kuzuia Ugonjwa wa tauni.

Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali ambazo zinaweza kutumika ili kuweza kuepuka Ugonjwa wa raundi.

Njia za kuepuka Ugonjwa wa tauni.

1.Kwanza kabisa tunapaswa kujua kuwa ugonjwa huu utokana na kuwepo kwa panya ambao ubeba wadudu na viroboto ndio wanaofanya kazi ya kusambaza hawa wadudu kwa hiyo jamii inapaswa kujulisha kuwepo kwa Ugonjwa huu maana Ugonjwa huu utokea kwa msimu na kupotea kwa hiyo kuwepo kwa Ugonjwa huu na kujua Dalili zake itakuwa rahisi kuweza kuudhibiti na kuondoa hali ya kunyanyapaa wagonjwa  na watu wakishajua hilo wataweza kuwa na tahadhari.

 

2. Pia jamii inapaswa kuepukana na tabia ya kukubali kuwepo kwa aina yoyote ya panya kwenye mazingira yao na vilevile kama kuna mgonjwa yeyote ametokea ni lazima kutoa taarifa na kuepuka kugusa maji maji yanayotoka kwa mgonjwa ili kuepuka kuambukiza na pia kuwa mbali na mgonjwa pale ambapo mgonjwa amefikia kwenye hatua ya tatu kwa sababu ni ya hatari sana na watu uweza kuambukizwa zaidi hasa kwenye familia na wote wanaowazunguka .

 

3. Elimu ni lazima kutolewa kwa jamii kuhusu jinsi Ugonjwa unavyoambukiza, dalili za ugonjwa , chanzo cha ugonjwa na hatua anazopitia Mgonjwa, kwa kufanya hivyo watu watakuwa makini ili kuweza kuepuka kusambaa kwa ugonjwa wa tauni pia jamii inapaswa kuhakikishiwa juwa huu ni ugonjwa ambao unatibiwa kabisa na watu wanapona na pia wajue hatua za ugonjwa na dalili zake ili waweze kupata matibabu mapema iwezekanavyo.

 

4. Vile vile watu wanapaswa kuacha tabia ya kulala chini kwa sababu chini ndipo kuna viroboto wengi kwa hiyo wanashauriwa kulala kwenye vitanda na pia usafi ni wa lazima hasa katika kipindi cha mavuno kuhakikisha kuwa mazao yamewekwa sehemu nzuri ambapo panya hawawezi kufika na kushambulia mazao na kuleta madhara, au kwa upande mwingine tunapaswa kutumia dawa ili kuua panya na viroboto kwa kufanya hivyo tutaweza kuepuka Ugonjwa huu.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 3287

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio     👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉5 web hosting     👉6 Dua za Mitume na Manabii    

Post zinazofanana:

Maumivu ya meno na ufizi: Tiba za asili na hospitalini.

Maumivu ya meno na matatizo ya ufizi ni miongoni mwa changamoto za kiafya zinazokumba watu wengi duniani. Hali hizi si tu kwamba huleta maumivu makali, bali pia huathiri uwezo wa kula, kuzungumza, na hata ubora wa maisha kwa ujumla. Makala haya yanatoa mwongozo wa kitaalamu kuhusu sababu za maumivu haya, mbinu za kutuliza maumivu nyumbani, na kwa nini ni muhimu kumuona daktari wa meno (dentist) ili kupata tiba ya kudumu.

Soma Zaidi...
Matatizo ya unene kwa watoto (childhood obesity)

post Ina onyesha madhara na matatizo ya Unene Utoto ni hali mbaya ya kiafya inayoathiri watoto na vijana. Inatokea wakati mtoto yuko juu ya uzito wa kawaida kwa umri na urefu wake

Soma Zaidi...
Fahamu Magonjwa yanayowapata watoto chini ya miaka mitano

Posti hii inaelezea kuhusiana na Magonjwa mbalimbali ambayo watoto chini ya miaka wanaweza kuyapata kiurahi.

Soma Zaidi...
Namna ya kuzuia ugonjwa wa Homa ya inni.

Posti hii inahusu zaidi namna ya kuzuia ugonjwa wa Homa ya inni, ni njia ambazo utumiwa Ili kuepuka kusambaa kwa ugonjwa wa Homa ya inni kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine,

Soma Zaidi...
Dalili za Mgonjwa wa kisukari

Post hii inahusu dalili za mtu Mwenye ugonjwa wa kisukari, dalili hizi zinaweza kujitokeza Moja kwa Moja mtu akagundua kuwa ana Ugonjwa wa kisukari.zifuatazo ni dalili za ugonjwa wa kisukari.

Soma Zaidi...
Dalili kuu za Malaria mwilini

Malaria husababishwa na vijidudu vidogo parasite wanaojulikana kama plasmodium. Vijidudu hivi hubebwa na mbu aina ya anophelesi. Kuna ina nyingi za plasmodium lakini aina 5 tu ndizo husababisha malaria

Soma Zaidi...