picha

Njia za kuzuia Ugonjwa wa tauni.

Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali ambazo zinaweza kutumika ili kuweza kuepuka Ugonjwa wa raundi.

Njia za kuepuka Ugonjwa wa tauni.

1.Kwanza kabisa tunapaswa kujua kuwa ugonjwa huu utokana na kuwepo kwa panya ambao ubeba wadudu na viroboto ndio wanaofanya kazi ya kusambaza hawa wadudu kwa hiyo jamii inapaswa kujulisha kuwepo kwa Ugonjwa huu maana Ugonjwa huu utokea kwa msimu na kupotea kwa hiyo kuwepo kwa Ugonjwa huu na kujua Dalili zake itakuwa rahisi kuweza kuudhibiti na kuondoa hali ya kunyanyapaa wagonjwa  na watu wakishajua hilo wataweza kuwa na tahadhari.

 

2. Pia jamii inapaswa kuepukana na tabia ya kukubali kuwepo kwa aina yoyote ya panya kwenye mazingira yao na vilevile kama kuna mgonjwa yeyote ametokea ni lazima kutoa taarifa na kuepuka kugusa maji maji yanayotoka kwa mgonjwa ili kuepuka kuambukiza na pia kuwa mbali na mgonjwa pale ambapo mgonjwa amefikia kwenye hatua ya tatu kwa sababu ni ya hatari sana na watu uweza kuambukizwa zaidi hasa kwenye familia na wote wanaowazunguka .

 

3. Elimu ni lazima kutolewa kwa jamii kuhusu jinsi Ugonjwa unavyoambukiza, dalili za ugonjwa , chanzo cha ugonjwa na hatua anazopitia Mgonjwa, kwa kufanya hivyo watu watakuwa makini ili kuweza kuepuka kusambaa kwa ugonjwa wa tauni pia jamii inapaswa kuhakikishiwa juwa huu ni ugonjwa ambao unatibiwa kabisa na watu wanapona na pia wajue hatua za ugonjwa na dalili zake ili waweze kupata matibabu mapema iwezekanavyo.

 

4. Vile vile watu wanapaswa kuacha tabia ya kulala chini kwa sababu chini ndipo kuna viroboto wengi kwa hiyo wanashauriwa kulala kwenye vitanda na pia usafi ni wa lazima hasa katika kipindi cha mavuno kuhakikisha kuwa mazao yamewekwa sehemu nzuri ambapo panya hawawezi kufika na kushambulia mazao na kuleta madhara, au kwa upande mwingine tunapaswa kutumia dawa ili kuua panya na viroboto kwa kufanya hivyo tutaweza kuepuka Ugonjwa huu.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 3280

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
πŸ‘‰1 Madrasa kiganjani     πŸ‘‰2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     πŸ‘‰3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     πŸ‘‰4 ai web app     πŸ‘‰5 kitabu cha Simulizi     πŸ‘‰6 web hosting    

Post zinazofanana:

Ugonjwa wa kisukari ambao husababisha kupoteza fahamu ( coma ya kisukari)..

Posti hii inazungumzia kuhusiana na Ugonjwa wa kisukari unaopelekea kukosa fahamu ni tatizo linalohatarisha maisha kisukari ambalo husababisha kupoteza fahamu. Ikiwa una kisukari, sukari ya juu ya damu (hyperglycemia) au sukari iliyopungua sana (hypoglyc

Soma Zaidi...
Dalili za mimba changa kutoka

Post hii inaenda kuzungumzia zaidi kuhusiana na mimba zinazoharibika . mimba huweza kuaribika au kutoka anzia miezi 3 na kuendelea .

Soma Zaidi...
Namna madonda koo yanavyotokea

Posti hii inahusu namna madonda koo yanavyotokea, ni jinsi na namna Magonjwa haya au Maambukizi yanavyotokea na kuweza kusababisha madhara kwa watu.

Soma Zaidi...
Ukweli Kuhusu Punyeto kwa Wanaume

​Punyeto ni suala linalozungumziwa sana katika jamii, na mara nyingi limegubikwa na dhana potofu. Makala haya yanalenga kuweka sawa ukweli wa kisayansi kuhusu mazoea haya, athari zake zinazowezekana, na wakati ambapo inakuwa ni tatizo linalohitaji uangalizi.

Soma Zaidi...
Ujuwe ugonjwa wa ebola, dalili zake na jinsi unavyoweza kusambazwa.

Posti hii inahusu sana kuhusu ugonjwa wa ebora. Ugonjwa huu usababishwa na virusi.Virusi hivyo husababisha kutokwa na damu nyingi mwilini kutokana na kupasuka kwa mishipa ya damu

Soma Zaidi...
Mimba ya Uongo ni Nini?

Makala hii inaangazia hali ya kisaikolojia na kimwili inayojulikana kama "Mimba ya Uongo" (Pseudocyesis). Tutaelezea maana yake, dalili kuu ambazo mwanamke anaweza kuzihisi, sababu za kitaalamu zinazosababisha hali hii, na umuhimu wa kupata msaada wa kitabibu na kisaikolojia

Soma Zaidi...