Njia za kuzuia Ugonjwa wa tauni.

Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali ambazo zinaweza kutumika ili kuweza kuepuka Ugonjwa wa raundi.

Njia za kuepuka Ugonjwa wa tauni.

1.Kwanza kabisa tunapaswa kujua kuwa ugonjwa huu utokana na kuwepo kwa panya ambao ubeba wadudu na viroboto ndio wanaofanya kazi ya kusambaza hawa wadudu kwa hiyo jamii inapaswa kujulisha kuwepo kwa Ugonjwa huu maana Ugonjwa huu utokea kwa msimu na kupotea kwa hiyo kuwepo kwa Ugonjwa huu na kujua Dalili zake itakuwa rahisi kuweza kuudhibiti na kuondoa hali ya kunyanyapaa wagonjwa  na watu wakishajua hilo wataweza kuwa na tahadhari.

 

2. Pia jamii inapaswa kuepukana na tabia ya kukubali kuwepo kwa aina yoyote ya panya kwenye mazingira yao na vilevile kama kuna mgonjwa yeyote ametokea ni lazima kutoa taarifa na kuepuka kugusa maji maji yanayotoka kwa mgonjwa ili kuepuka kuambukiza na pia kuwa mbali na mgonjwa pale ambapo mgonjwa amefikia kwenye hatua ya tatu kwa sababu ni ya hatari sana na watu uweza kuambukizwa zaidi hasa kwenye familia na wote wanaowazunguka .

 

3. Elimu ni lazima kutolewa kwa jamii kuhusu jinsi Ugonjwa unavyoambukiza, dalili za ugonjwa , chanzo cha ugonjwa na hatua anazopitia Mgonjwa, kwa kufanya hivyo watu watakuwa makini ili kuweza kuepuka kusambaa kwa ugonjwa wa tauni pia jamii inapaswa kuhakikishiwa juwa huu ni ugonjwa ambao unatibiwa kabisa na watu wanapona na pia wajue hatua za ugonjwa na dalili zake ili waweze kupata matibabu mapema iwezekanavyo.

 

4. Vile vile watu wanapaswa kuacha tabia ya kulala chini kwa sababu chini ndipo kuna viroboto wengi kwa hiyo wanashauriwa kulala kwenye vitanda na pia usafi ni wa lazima hasa katika kipindi cha mavuno kuhakikisha kuwa mazao yamewekwa sehemu nzuri ambapo panya hawawezi kufika na kushambulia mazao na kuleta madhara, au kwa upande mwingine tunapaswa kutumia dawa ili kuua panya na viroboto kwa kufanya hivyo tutaweza kuepuka Ugonjwa huu.

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 2003

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 Bongolite - Game zone - Play free game    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 Simulizi za Hadithi Audio    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Dalili za tezi dume ambayo hazijashuka (cryptorchidism)

Tezi dume ambayo haijashuka si ya kawaida kwa ujumla, lakini ni ya kawaida kwa wavulana waliozaliwa kabla ya wakati.na muda mwingine zikipanda tumboni huwa hazishuki kabisa kwenye korodani.

Soma Zaidi...
NINI CHANZO CHA UGONJWA WA MALARIA? NI YUPI MBU ANAYESAMBAZA MALARIA

Malaria husababishwa na vimelea (parasite) ambavyo husambazwa ama kubebwa na mbu aina ya anopheles.

Soma Zaidi...
Dalili za ugonjwa wa Ugumu wa kumeza (dysphagia)

Ugumu wa kumeza (dysphagia) inamaanisha inachukua muda na bidii zaidi kuhamisha chakula kutoka kwa mdomo wako hadi kwenye tumbo lako. Ugumu wa kumeza unaweza pia kuhusishwa na maumivu. Katika baadhi ya matukio, kumeza inaweza kuwa haiwezekani. Ugumu w

Soma Zaidi...
Namna ya kuzuia virusi vya ukimwi

Posti hii inaelezea kuhusiana na kujikinga au kuzuia virusi vya ukimwi.

Soma Zaidi...
Vipimo vya VVU

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu vipimo mbalimbali vinavyotumika kupima VVU

Soma Zaidi...
Sababu na Chanzo cha vidonda vya tumbo

Zijuwe sababu za kutokea kwa vidonda vya tumbo. Sababu kuu za vidonda vya tumbo hizi hapa

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa ukosefu wa mkojo

Posti hii inaonyesha namna ya kujizuia,Mambo ya Hatari,na na Mambo yanayopelekea Ugonjwa wa ukosefu wa mkojo

Soma Zaidi...
Dalili kuu 7 za vidonda vya tumbo

Zijuwe dalili kuu 7 za vidonda vya tumbo, kama kiungulia, tumbo kujaa, maumivu ya umbo..

Soma Zaidi...
Kuhusu HIV na UKIMWI

Somk hili linakwenda kukueleza kuhusu Mambo mbalimbali yahusuyo HIV na UKIMWI

Soma Zaidi...
Dalilili za polio

Polio ni ugonjwa wa virusi unaoambukiza ambao katika hali mbaya zaidi husababisha kupooza, kupumua kwa shida na wakati mwingine kifo.

Soma Zaidi...