picha

Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Dengue

Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa Dengue, ni ugonjwa unaosababishwa na virusi ila unasambazwa na mbu kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine mbu anayasambaza Ugonjwa huu kwa kitaalamu huitwa Aedes mosquito .

Ugonjwa wa Dengue.

1. Kama tulivyoona hapo awali kwamba hawa virusi wanasambazwa na mbu kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine na pia wameweza kuleta madhara makubwa katika ulimwengu kwa sababu kadri ya wataalamu mbalimbali wamefanya uchunguzi na kuona kubwa ni Ugonjwa ambao imeshambulia maeneo mbalimbali kwenye Dunia kama vile kasikazini na kusini mwa Amerika , Afrika, kasikazini na kusini mwa Asia.

 

2. Ugonjwa huu ushambulia kwa vipindi mbalimbali hasa hasa kwa wakati wa mvua ambapo mazalia ya mbu yanakuwa ni mengi na pengine nyasi zinakuwepo za kutosha kwenye mazingira kwa sababu ya kuwepo kwa mvua kwa hiyo mbu wanazaliana kwa urahisi, na kwenye nchi yetu ya Tanzania Ugonjwa huu umetokea tokea sana kwenye sehemu tofauti za nchi kama vile Dar es salaam na kusababisha madhara mbalimbali hata na vifo vilitokea na baadae hali ilitulia.

 

3. Pia ugonjwa huu unaweza kupimwa na kugundulika kulingana na uchumi wa nchi na vifaa vilivyomo, kwa hiyo tunaweza kutumia kipimo cha kuangalia mwili mzima ambapo kwa kitaalamu huitwa full blood picture na pia tunaweza kutumia kipimo ambacho kwa kitaalamu huitwa ELISA for dengue kwa kuangalia protini ya mdudu kama ikikutwa ni Dalili nzuri ya kuonesha kama kuna Dengue, au kuchukua sampuli na kuipeleka kwa mkemia mkuu wa nchi.

 

4. Kwa hiyo baada ya kuwepo kwa mlipuko wa ugonjwa huu wa Dengue ni lazima kuieleza jamii mara moja ili kuweza kujua kuwa kuna Ugonjwa fulani na kuwajulisha watu ili waweze kujua Dalili zake na namna ya kujikinga kwa sababu Ugonjwa huu hauna dawa kwa sababu unasababishwa na virusi, baada ya jamii kujulishwa tahadhari itaweza kuchukuliwa kwa urahisi.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 2457

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio     👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉3 Dua za Mitume na Manabii     👉4 Kitabu cha Afya     👉5 ai web app     👉6 web hosting    

Post zinazofanana:

Maambukizi ya ngozi (Cellulitis): Dalili na tiba ya hospitalini.

Ufafanuzi: Ugonjwa wa dharura wa maambukizi ya bakteria kwenye tabaka za ndani za ngozi.Maeneo Yanayoathiriwa Zaidi: Mara nyingi hutokea kwenye miguu, ingawa unaweza kuathiri sehemu yoyote ya mwili ikiwemo uso na mikono.Dalili Kuu: Ngozi kuwa nyekundu, kuvimba, kuhisi joto kali, maumivu makali, na kutoa malengelenge au michirizi myekundu.Tiba ya Hospitalini: Matumizi ya viuavijasumu (antibiotics) vya kumeza au vya kuwekewa kwenye mishipa ya damu (Intravenous) kulingana na ukali wa maambukizi.Matatizo: Isipotibiwa, inaweza kusababisha maambukizi kwenye damu (sepsis), uharibifu wa tishu (necrotizing fasciitis), au maambukizi kwenye mifupa (osteomyelitis).

Soma Zaidi...
Maambukizi ya VVU: Dalili za mwanzo na jinsi ya kuishi nayo.

​Makala hii inachunguza kwa kina virusi vya VVU (Virusi vya Upungufu wa Kinga Mwilini), ikianzia na utambuzi wa dalili za mwanzo (acute HIV infection), umuhimu wa upimaji wa mapema, na mikakati ya kisayansi ya kuishi maisha marefu na yenye tija kwa kutumia tiba ya kufubaza virusi (ART). Lengo ni kuondoa unyanyapaa na kutoa mwongozo wa kitaalamu kwa watu wanaoishi na VVU.

Soma Zaidi...
Namna ya kuangalia Maambukizi kwenye mifupa.

Posti hii inahusu zaidi njia zinazotumika ili kuangalia Maambukizi kwenye mifupa.

Soma Zaidi...
Mabadiliko ya mwili katika wiki za mwanzo za mimba

​Wiki za kwanza za ujauzito ni kipindi cha mabadiliko makubwa ya ndani na nje ya mwili wa mwanamke. Makala hii inafafanua mabadiliko hayo ili kumsaidia mama kuelewa kinachoendelea na jinsi ya kukabiliana na hali hiyo kwa usalama.Utangulizi​Wakati mwingine, mabadiliko ya mwili huanza kujitokeza hata kabla hujapima na kupata majibu chanya ya mimba. Hii inatokana na msukosuko wa homoni unaolenga kutengeneza mazingira rafiki kwa ukuaji wa kiumbe kilichotungwa. Kuelewa dalili hizi ni muhimu ili uweze kujijali na kumpa mtoto wako nafasi nzuri zaidi ya ukuaji kuanzia siku ya kwanza.​Maudhui: Mabadiliko ya Mwili katika Wiki za Mwanzo​Katika kipindi hiki, mwili wako unafanya kazi kubwa kurekebisha mfumo wake:​Mabadiliko ya Homoni: Kiwango cha homoni za estrogen na progesterone hupanda kwa kasi ili kusaidia ujauzito, hali inayoweza kubadili hisia zako (mood swings).​Mabadiliko katika Matiti: Matiti yanaweza kuwa makubwa, mazito, na yenye maumivu mepesi kutokana na kuongezeka kwa mtiririko wa damu na kujiandaa kwa ajili ya uzalishaji wa maziwa.​Mabadiliko ya Mfumo wa Chakula: Unaweza kuhisi kichefuchefu, hasa asubuhi, au kupata mabadiliko ya ladha (kuchukia vyakula fulani ulivyokuwa unapenda awali).​Uchovu: Mwili hutumia nishati nyingi katika wiki za mwanzo kuunda mfumo wa kondo la nyuma (placenta), hali inayokufanya uhisi uchovu na usingizi wa mara kwa mara.​Kukojoa Mara kwa Mara: Uterasi inapoanza kukua na shinikizo la damu kuongezeka, kibofu cha mkojo hupata shinikizo zaidi, jambo linalokufanya utake kwenda chooni mara kwa mara.​Fact Check: Je, mabadiliko haya ni hatari?​Ukweli: Mabadiliko mengi unayoyahisi ni ya kawaida kabisa na ni ishara kuwa mwili wako unakubali ujauzito. Hata hivyo, si kila mwanamke anapata dalili hizi zote.​Tahadhari: Ikiwa utapata dalili hizi, unapaswa kuonana na daktari mara moja:​Maumivu makali ya tumbo (upande mmoja au sehemu ya chini).​Kutokwa na damu nyingi ukeni (vaginal bleeding).​Homa kali au maumivu wakati wa kukojoa.​Kutapika sana kiasi cha kushindwa kuhifadhi maji mwilini.​Hitimisho​Mabadiliko ya mwili katika wiki za mwanzo ni ishara ya maajabu ya kimaumbile yanayotokea ndani yako. Ingawa baadhi ya hali hizi zinaweza kuwa kero, kumbuka kuwa ni za muda mfupi. Kula mlo kamili, kunywa maji ya kutosha, na kupumzika ipasavyo kutakusaidia kupitia kipindi hiki kwa urahisi zaidi. Usisahau kuhudhuria kliniki mapema ili kupata ushauri wa kitaalamu na ufuatiliaji wa ukuaji wa mtoto wako

Soma Zaidi...
HPV (Human Papillomavirus): Chanjo na saratani ya shingo ya kizazi.

​Virusi vya Human Papillomavirus (HPV) ni kundi la virusi vinavyoambukiza ngozi na utando wa ndani wa mwili. Ingawa maambukizi mengi ya HPV hupona yenyewe, aina fulani za virusi hivi zinaweza kusababisha mabadiliko ya seli yanayoendelea na kuwa saratani, hasa saratani ya shingo ya kizazi. Makala hii inachambua uhusiano kati ya HPV na saratani, umuhimu wa chanjo, na hatua za kinga ambazo kila jamii inapaswa kuzichukua.

Soma Zaidi...
Kifuwa kinaniuma katikati kinaambatana nakichwa

Maumivu ya kifuwa yanaweza kutokea baada ya kubeba kitu kizito, ama kupata mashambulizi ya vijidudu vya maradhi. maumivu ya viungo na hata vidonda vya tumbo. Lakini sasa umesha wahi fikiria maumivu ya kifuwa kwa katikati?

Soma Zaidi...