picha

Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Dengue

Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa Dengue, ni ugonjwa unaosababishwa na virusi ila unasambazwa na mbu kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine mbu anayasambaza Ugonjwa huu kwa kitaalamu huitwa Aedes mosquito .

Ugonjwa wa Dengue.

1. Kama tulivyoona hapo awali kwamba hawa virusi wanasambazwa na mbu kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine na pia wameweza kuleta madhara makubwa katika ulimwengu kwa sababu kadri ya wataalamu mbalimbali wamefanya uchunguzi na kuona kubwa ni Ugonjwa ambao imeshambulia maeneo mbalimbali kwenye Dunia kama vile kasikazini na kusini mwa Amerika , Afrika, kasikazini na kusini mwa Asia.

 

2. Ugonjwa huu ushambulia kwa vipindi mbalimbali hasa hasa kwa wakati wa mvua ambapo mazalia ya mbu yanakuwa ni mengi na pengine nyasi zinakuwepo za kutosha kwenye mazingira kwa sababu ya kuwepo kwa mvua kwa hiyo mbu wanazaliana kwa urahisi, na kwenye nchi yetu ya Tanzania Ugonjwa huu umetokea tokea sana kwenye sehemu tofauti za nchi kama vile Dar es salaam na kusababisha madhara mbalimbali hata na vifo vilitokea na baadae hali ilitulia.

 

3. Pia ugonjwa huu unaweza kupimwa na kugundulika kulingana na uchumi wa nchi na vifaa vilivyomo, kwa hiyo tunaweza kutumia kipimo cha kuangalia mwili mzima ambapo kwa kitaalamu huitwa full blood picture na pia tunaweza kutumia kipimo ambacho kwa kitaalamu huitwa ELISA for dengue kwa kuangalia protini ya mdudu kama ikikutwa ni Dalili nzuri ya kuonesha kama kuna Dengue, au kuchukua sampuli na kuipeleka kwa mkemia mkuu wa nchi.

 

4. Kwa hiyo baada ya kuwepo kwa mlipuko wa ugonjwa huu wa Dengue ni lazima kuieleza jamii mara moja ili kuweza kujua kuwa kuna Ugonjwa fulani na kuwajulisha watu ili waweze kujua Dalili zake na namna ya kujikinga kwa sababu Ugonjwa huu hauna dawa kwa sababu unasababishwa na virusi, baada ya jamii kujulishwa tahadhari itaweza kuchukuliwa kwa urahisi.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 2497

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉3 Simulizi za Hadithi Audio     👉4 Dua za Mitume na Manabii     👉5 web hosting     👉6 Kitau cha Fiqh    

Post zinazofanana:

Ugonjwa wa Saratani ya ini.

Saratani ya ini ni Saratani inayoanzia kwenye seli za ini lako.

Soma Zaidi...
Dalili za uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo

Post hii inahusu zaidi dalili za uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo, ni dalili ambazo ujitokeza kwa mtu Mwenye tatizo la uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo, ingawa sio watu wote wenye dalili kama hizi Wana uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo Ila zikitokea mtu anapaswa

Soma Zaidi...
Hernia

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu ugonjwa wa hernia

Soma Zaidi...
Kupatwa na ujauzito ukiwa unanyonya: Inawezekana?

Wengi wanaamini kuwa kunyonyesha ni njia tosha ya kuzuia mimba, lakini je, hii ni kweli kisayansi? Makala hii inachambua kwa kina uwezekano wa kupata ujauzito wakati unanyonyesha, jinsi mfumo wa homoni unavyofanya kazi katika kipindi hiki, na mikakati ya uzazi wa mpango inayopendekezwa na wataalamu wa afya. Lengo ni kuwapa akina mama elimu sahihi ya kulinda afya yao na kupanga uzazi kwa ufanisi.

Soma Zaidi...
Matibabu ya VVU na UKIMWI

Somo Hili linakwenda kukuletea matibabu ya VVU/UKIMWI

Soma Zaidi...
Namna ya Kupunguza Stress kwa Njia Asilia

Katika ulimwengu wa sasa wenye kasi kubwa, msongo wa mawazo (stress) umekuwa changamoto ya kawaida kwa wengi. Makala hii inakupa mbinu rahisi, asilia, na zenye ufanisi unazoweza kuzitumia kila siku ili kutuliza akili yako, kuboresha afya yako ya hisia, na kurejesha furaha.

Soma Zaidi...