Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa Dengue, ni ugonjwa unaosababishwa na virusi ila unasambazwa na mbu kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine mbu anayasambaza Ugonjwa huu kwa kitaalamu huitwa Aedes mosquito .
1. Kama tulivyoona hapo awali kwamba hawa virusi wanasambazwa na mbu kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine na pia wameweza kuleta madhara makubwa katika ulimwengu kwa sababu kadri ya wataalamu mbalimbali wamefanya uchunguzi na kuona kubwa ni Ugonjwa ambao imeshambulia maeneo mbalimbali kwenye Dunia kama vile kasikazini na kusini mwa Amerika , Afrika, kasikazini na kusini mwa Asia.
2. Ugonjwa huu ushambulia kwa vipindi mbalimbali hasa hasa kwa wakati wa mvua ambapo mazalia ya mbu yanakuwa ni mengi na pengine nyasi zinakuwepo za kutosha kwenye mazingira kwa sababu ya kuwepo kwa mvua kwa hiyo mbu wanazaliana kwa urahisi, na kwenye nchi yetu ya Tanzania Ugonjwa huu umetokea tokea sana kwenye sehemu tofauti za nchi kama vile Dar es salaam na kusababisha madhara mbalimbali hata na vifo vilitokea na baadae hali ilitulia.
3. Pia ugonjwa huu unaweza kupimwa na kugundulika kulingana na uchumi wa nchi na vifaa vilivyomo, kwa hiyo tunaweza kutumia kipimo cha kuangalia mwili mzima ambapo kwa kitaalamu huitwa full blood picture na pia tunaweza kutumia kipimo ambacho kwa kitaalamu huitwa ELISA for dengue kwa kuangalia protini ya mdudu kama ikikutwa ni Dalili nzuri ya kuonesha kama kuna Dengue, au kuchukua sampuli na kuipeleka kwa mkemia mkuu wa nchi.
4. Kwa hiyo baada ya kuwepo kwa mlipuko wa ugonjwa huu wa Dengue ni lazima kuieleza jamii mara moja ili kuweza kujua kuwa kuna Ugonjwa fulani na kuwajulisha watu ili waweze kujua Dalili zake na namna ya kujikinga kwa sababu Ugonjwa huu hauna dawa kwa sababu unasababishwa na virusi, baada ya jamii kujulishwa tahadhari itaweza kuchukuliwa kwa urahisi.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Posti hii inazungumzia kuhusiana na ugonjwa wa Kidole ambao kitaalamu hujulikana Kama Appendicitis. Kidole tumbo husababisha maumivu kwenye tumbo la chini la kulia. Hata hivyo, kwa watu wengi, maumivu huanza karibu na kitovu na kisha kusonga. Kadiri uvi
Soma Zaidi...Watu wengi wamekuwa na mawazo kuwa ili nipate ukimwi ninatakiwa nishiriki ngono zembe na aliyeathirika mara ngapi? Majibu ya swali hili ni mafupi tu, ni kuwa unaweza kuathirika kwa ngono zembe ya siku moja tu ndani ya dakika chache. Lakini jambo la kuzing
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi aina mbili za kifua kikuu, aina ya kwanza ni ile ya kawaida ambayo ushambulia mapafu na aina ya pili ni ile ambayo ushambulia sehemu mbalimbali za mwili kama vile kwenye limfu node, kwenye sehemu za moyo, kwenye uti wa mgongo, kwen
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi makundi ambayo yapo katika hatari ya kupata ugonjwa wa ngiri, ni hatari kwa sababu tunajua kuwa ngiri utokea kwa sababu ya kuta au tishu zinazoshikilia viungo fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwepo kwa uwazi na kufanya viun
Soma Zaidi...Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu presha ya kushuka na matibabu yake
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea ikiwa matibabu kwenye nyonga na kiuno hayatafanyika.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi kuwepo kwa vipele kwenye midomo na sehemu za siri .Ni ugonjwa ambao kwa kitaalamu huitwa herpes zoster
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu presha ya kushuka/ hypotension
Soma Zaidi...Upungufu wa maji mwilini hutokea unapotumia au kupoteza Majimaji mengi zaidi ya unayonywa, na mwili wako hauna maji ya kutosha na Majimaji mengine ya kufanya kazi zake za kawaida. Usipochukua nafasi ya Vimiminika vilivyopotea, utapungukiwa na maji.
Soma Zaidi...Maumivu ya mgongo yanaweza kuwa ni dalili inayoonyesha tatizo fulani la kiafya ikiwemo magonjwa au majeraha.
Soma Zaidi...