picha

Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Dengue

Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa Dengue, ni ugonjwa unaosababishwa na virusi ila unasambazwa na mbu kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine mbu anayasambaza Ugonjwa huu kwa kitaalamu huitwa Aedes mosquito .

Ugonjwa wa Dengue.

1. Kama tulivyoona hapo awali kwamba hawa virusi wanasambazwa na mbu kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine na pia wameweza kuleta madhara makubwa katika ulimwengu kwa sababu kadri ya wataalamu mbalimbali wamefanya uchunguzi na kuona kubwa ni Ugonjwa ambao imeshambulia maeneo mbalimbali kwenye Dunia kama vile kasikazini na kusini mwa Amerika , Afrika, kasikazini na kusini mwa Asia.

 

2. Ugonjwa huu ushambulia kwa vipindi mbalimbali hasa hasa kwa wakati wa mvua ambapo mazalia ya mbu yanakuwa ni mengi na pengine nyasi zinakuwepo za kutosha kwenye mazingira kwa sababu ya kuwepo kwa mvua kwa hiyo mbu wanazaliana kwa urahisi, na kwenye nchi yetu ya Tanzania Ugonjwa huu umetokea tokea sana kwenye sehemu tofauti za nchi kama vile Dar es salaam na kusababisha madhara mbalimbali hata na vifo vilitokea na baadae hali ilitulia.

 

3. Pia ugonjwa huu unaweza kupimwa na kugundulika kulingana na uchumi wa nchi na vifaa vilivyomo, kwa hiyo tunaweza kutumia kipimo cha kuangalia mwili mzima ambapo kwa kitaalamu huitwa full blood picture na pia tunaweza kutumia kipimo ambacho kwa kitaalamu huitwa ELISA for dengue kwa kuangalia protini ya mdudu kama ikikutwa ni Dalili nzuri ya kuonesha kama kuna Dengue, au kuchukua sampuli na kuipeleka kwa mkemia mkuu wa nchi.

 

4. Kwa hiyo baada ya kuwepo kwa mlipuko wa ugonjwa huu wa Dengue ni lazima kuieleza jamii mara moja ili kuweza kujua kuwa kuna Ugonjwa fulani na kuwajulisha watu ili waweze kujua Dalili zake na namna ya kujikinga kwa sababu Ugonjwa huu hauna dawa kwa sababu unasababishwa na virusi, baada ya jamii kujulishwa tahadhari itaweza kuchukuliwa kwa urahisi.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 2523

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Simulizi za Hadithi Audio     👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉6 web hosting    

Post zinazofanana:

Namna ya kuzuia Ugonjwa wa kaswende

Posti hii inahusu zaidi njia za kuzuia Ugonjwa wa kaswende, tunajua wazi kuwa Ugonjwa huu unasambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwa njia ya kufanya ngono zembe na njia nyingine kwa hiyo tunaweza kuzuia kusambaa na kuenea kwa ugonjwa huu kwa n

Soma Zaidi...
Uwepo wa asidi nyingi mwilini

Posti hii inahusu zaidi tatizo la kuwepo kwa asidi nyingi mwilini hali uwasumbua watu wengi na kufikia kiasi cha kusababisha madhara mengine mawilini ikiwamo pamoja na kansa ya koo, ili kujua kama una wingi wa asildi mwilini unapaswa kujua dalili kama ifu

Soma Zaidi...
Ndugu mke Wang viungo vina mlegea miguu inamuaka moto nn tatozo

Je unasumbuliwa na tatizo la kukosa nguvu, kuchoka ama kuhisi viungi vinelegea. Endelea na post hii.

Soma Zaidi...
Dalili za Ukimwi

Makala hii itaeleza dalili za ukimwi, dalili za VVU, magonjwa nyemelezi na matumizi ya ARV

Soma Zaidi...
Tufanyeje ili kuepuka kuaribika kwa figo?

Posti hii inahusu zaidi njia za kuzuia kuaribika kwa figo, hizi ni njia zinazotumika ili kuweza kupunguza tatizo la kuaribika kwa figo na hasa wale ambao hawajapata tatizo hili wazitumie ili tuone kama tutaweza kupunguza tatizo hili.

Soma Zaidi...