Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Dengue

Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa Dengue, ni ugonjwa unaosababishwa na virusi ila unasambazwa na mbu kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine mbu anayasambaza Ugonjwa huu kwa kitaalamu huitwa Aedes mosquito .

Ugonjwa wa Dengue.

1. Kama tulivyoona hapo awali kwamba hawa virusi wanasambazwa na mbu kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine na pia wameweza kuleta madhara makubwa katika ulimwengu kwa sababu kadri ya wataalamu mbalimbali wamefanya uchunguzi na kuona kubwa ni Ugonjwa ambao imeshambulia maeneo mbalimbali kwenye Dunia kama vile kasikazini na kusini mwa Amerika , Afrika, kasikazini na kusini mwa Asia.

 

2. Ugonjwa huu ushambulia kwa vipindi mbalimbali hasa hasa kwa wakati wa mvua ambapo mazalia ya mbu yanakuwa ni mengi na pengine nyasi zinakuwepo za kutosha kwenye mazingira kwa sababu ya kuwepo kwa mvua kwa hiyo mbu wanazaliana kwa urahisi, na kwenye nchi yetu ya Tanzania Ugonjwa huu umetokea tokea sana kwenye sehemu tofauti za nchi kama vile Dar es salaam na kusababisha madhara mbalimbali hata na vifo vilitokea na baadae hali ilitulia.

 

3. Pia ugonjwa huu unaweza kupimwa na kugundulika kulingana na uchumi wa nchi na vifaa vilivyomo, kwa hiyo tunaweza kutumia kipimo cha kuangalia mwili mzima ambapo kwa kitaalamu huitwa full blood picture na pia tunaweza kutumia kipimo ambacho kwa kitaalamu huitwa ELISA for dengue kwa kuangalia protini ya mdudu kama ikikutwa ni Dalili nzuri ya kuonesha kama kuna Dengue, au kuchukua sampuli na kuipeleka kwa mkemia mkuu wa nchi.

 

4. Kwa hiyo baada ya kuwepo kwa mlipuko wa ugonjwa huu wa Dengue ni lazima kuieleza jamii mara moja ili kuweza kujua kuwa kuna Ugonjwa fulani na kuwajulisha watu ili waweze kujua Dalili zake na namna ya kujikinga kwa sababu Ugonjwa huu hauna dawa kwa sababu unasababishwa na virusi, baada ya jamii kujulishwa tahadhari itaweza kuchukuliwa kwa urahisi.

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Author Tarehe 2022/04/06/Wednesday - 11:15:11 pm     Share On Facebook or WhatsApp Imesomwa mara 1091

Post zifazofanana:-

Magonjwa ya kuambukiza.
Posti hii inahusu zaidi Magonjwa ya kuambukiza, ni magonjwa ambayo yanaweza kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine na kuweza kusababisha madhara yale yale kwa mtu aliyeambukizwa au anayeambukiza kwa hiyo Maambukizi yanaweza kuwa ya moja kwa moja au yasiwe ya moja kwa moja kama tutakavyoona hapo baadaye. Soma Zaidi...

Upungufu wa vyakula na madhara yake
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu madhara ya upungufu wa vyakula Soma Zaidi...

Njia juu zinazosababisha kuenea kwa ugonjwa wa Ukimwi
Post hii inahusu zaidi njia za kuenea kwa ugonjwa wa Ukimwi. Ukimwi ni upungufu wa kinga mwilini. Soma Zaidi...

Dalili za mawe kwenye kibofu Cha mkono
Mawe ya kibofu ni mkusanyiko mgumu wa madini kwenye kibofu chako. Mawe kwenye kibofu hukua wakati mkojo kwenye kibofu chako unapokolea, na kusababisha madini katika mkojo wako kung'aa. Soma Zaidi...

Sababu za maumivu ya tumbo kitovuni na dalili zake
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu sababu za maumivu ya tumbo kitovuni na dalili zake Soma Zaidi...

Dalili za ugonjwa wa Saratani.
Saratani inahusu ugonjwa wowote kati ya idadi kubwa ya magonjwa ambayo yanaonyeshwa na ukuaji wa seli zisizo za kawaida ambazo hugawanyika bila kudhibitiwa na kuwa na uwezo wa kupenya na kuharibu tishu za kawaida za mwili. Saratani mara nyingi ina uwezo wa kuenea katika mwili wako wote. Soma Zaidi...

Tahadhari za ugonjwa wa UTI
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu tahadhari za kuchukua ili kujikinga na UTI Soma Zaidi...

Maambukizi ya tishu ya Matiti.
Posti hii inazungumzia kuhusiana na maambukizi ya tishu ya matiti ambayo husababisha'maumivu ya matiti, uvimbe, joto na uwekundu. Pia unaweza kuwa na'Homa'na baridi. Ugonjwa huu huwapata zaidi wanawake wanaonyonyesha ingawa wakati mwingine hali hii inaweza kutokea kwa wanawake ambao hawanyonyeshi. Mara nyingi, unyonyeshaji kwenye Ugonjwa huu hutokea ndani ya wiki sita hadi 12 baada ya kujifungua (baada ya kuzaa), lakini inaweza kutokea baadaye wakati wa kunyonyesha. Hali hiyo inaweza kukufanya ujisikie kudhoofika, hivyo kufanya iwe vigumu kumtunza mtoto wako. Soma Zaidi...

Umuhimu wa kupumzika kiafya
Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa kupumzika kiafya, kwa kawaida mwili na viungo vingine vya mwili uweza kufanya kazi zaidi pale mtu akiwa amepumzika. Soma Zaidi...

Vyakula kwa wagonjwa wa sukari na utaratibu wao wa lishe
Post hii inakwenda kukufundisha utaratibu wa lishe kwa wagonjwa wenye kisukari pamoja na vyakula salamakwao. Soma Zaidi...

mambo ambayo utaulizwa mama mjamzito ukifika kituo cha afya unatakiwa utoe majibu sahihi.
Posti hii inahusu zaidi mambo ambayo Mama mjamzito anaweza kuulizwa pindi anapokuja kwenye kliniki ya uzazi ,ni mambo muhimu na ya lazima yanayopaswa kuongea na Mama mjamzito ili kuweza kuona maendeleo yake kama ifuatavyo. Soma Zaidi...

Umuhimu wa kumpeleka mtoto kliniki
Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa kumpeleka mtoto kliniki, kliniki nisehemu ambayo mtoto hupelekwa Ili kujua maendeleo ya mtoto akiwa chini ya umri wa miaka mitano Soma Zaidi...