Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Dengue
Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa Dengue, ni ugonjwa unaosababishwa na virusi ila unasambazwa na mbu kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine mbu anayasambaza Ugonjwa huu kwa kitaalamu huitwa Aedes mosquito .
Ugonjwa wa Dengue.
1. Kama tulivyoona hapo awali kwamba hawa virusi wanasambazwa na mbu kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine na pia wameweza kuleta madhara makubwa katika ulimwengu kwa sababu kadri ya wataalamu mbalimbali wamefanya uchunguzi na kuona kubwa ni Ugonjwa ambao imeshambulia maeneo mbalimbali kwenye Dunia kama vile kasikazini na kusini mwa Amerika , Afrika, kasikazini na kusini mwa Asia.
2. Ugonjwa huu ushambulia kwa vipindi mbalimbali hasa hasa kwa wakati wa mvua ambapo mazalia ya mbu yanakuwa ni mengi na pengine nyasi zinakuwepo za kutosha kwenye mazingira kwa sababu ya kuwepo kwa mvua kwa hiyo mbu wanazaliana kwa urahisi, na kwenye nchi yetu ya Tanzania Ugonjwa huu umetokea tokea sana kwenye sehemu tofauti za nchi kama vile Dar es salaam na kusababisha madhara mbalimbali hata na vifo vilitokea na baadae hali ilitulia.
3. Pia ugonjwa huu unaweza kupimwa na kugundulika kulingana na uchumi wa nchi na vifaa vilivyomo, kwa hiyo tunaweza kutumia kipimo cha kuangalia mwili mzima ambapo kwa kitaalamu huitwa full blood picture na pia tunaweza kutumia kipimo ambacho kwa kitaalamu huitwa ELISA for dengue kwa kuangalia protini ya mdudu kama ikikutwa ni Dalili nzuri ya kuonesha kama kuna Dengue, au kuchukua sampuli na kuipeleka kwa mkemia mkuu wa nchi.
4. Kwa hiyo baada ya kuwepo kwa mlipuko wa ugonjwa huu wa Dengue ni lazima kuieleza jamii mara moja ili kuweza kujua kuwa kuna Ugonjwa fulani na kuwajulisha watu ili waweze kujua Dalili zake na namna ya kujikinga kwa sababu Ugonjwa huu hauna dawa kwa sababu unasababishwa na virusi, baada ya jamii kujulishwa tahadhari itaweza kuchukuliwa kwa urahisi.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitabu cha Afya 👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉3 kitabu cha Simulizi 👉4 Madrasa kiganjani 👉5 web hosting 👉6 Kitau cha Fiqh
Post zinazofanana:
Njia za kuondokana na fangasi
Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali za kuweza kupambana na fangasi za ukeni ili kuweza kujiepusha na madhara mbalimbali kwenye maisha ambayo ni pamoja na ugumba na Maambukizi kwenye via vya uzazi.
Soma Zaidi...Jifunze kuhusu ugonjwa wa bawasiri na dalili zake
Katika somo hili utakwenda kujifunz akuhusu ugonjwa wa Bawasiri na dalili zake. Pia utajifunza njia za kujilinda nao.
Soma Zaidi...Aina mbalimbali za michubuko
Post hii inahusu zaidi aina mbalimbali za michubuko,kwa Sababu michubuko utokea sehemu tofauti tofauti na pia Kuna aina mbalimbali kama tutakavyoona hapo mbeleni.
Soma Zaidi...IJUE HOMA YA CHIKUNGUNYA (CHIKV) DALILI ZAKE, TIBA YAKE, CHANJO YAKE, NA MBU ANAYESAMBAZA HOMA HII
Haya ni maradhi ambayo husambazwa kutoka kwa mtu kwenda kwa mtu kwa kupitia mbu.
Soma Zaidi...AFYA NA MAGONJWA
Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote
Soma Zaidi...Dalili zake mtoto mwenye Ugonjwa wa Maambukizi kwenye koo
Pisti hii inahusu zaidi dalili za mtoto mwenye Maambukizi ya ugonjwa wa Dondakoo, tunajua wazi kuwa ugonjwa huu uwashambulia hasa watoto wadogo ambao wako chini ya miaka mitano, kwa hiyo zifuatazo ni baadhi ya Dalili zinazoweza kujitokeza kwa watoto hawa.
Soma Zaidi...