Dalili za UTI
Somo hili linakwenda kukuletea dalili za UTI
Dalili za UTI
1.Kukojoa mara kwa mara
2.Kuhisi kuunguwa ama umoto wakati wa kukojoa
3.Kutoa mikojo kwa uchache
4.Mkojo kuwa mchafu, kama mawingu ama mwekundu uliopauka
5.Harufu kali ya mkojo
6.Maumivu ya kwenye njonga kwa wanawake
7.Maumivu ya mkundu na puru kwa wanaume.
Dalili za UTI zinaweza pia kuwa tofauti na hizo hapo juu. Dalili hizi hutofautiana kwa kulingana na aina ya UTI. Kama unataka kuzijuwa dalili zaidi za UTI endelea kusoma makala hii mpaka mwisho.
Aina za UTI na dalili zake.
Ugonjwa wa UTI umegawanyika katika makundi mbalimbali. Makundi hayo ni kama:-
1.UTI ya kwenye figo (acute pyelonephritis). UTI hii huathiri figo, na kusababisha dalili kama:-
1.Maumivu ya mgongo kwa juu
2.Homa kali
3.Kuhisi baridi na kutetemeka
4.Kichefuchefu
5.Kutapika.
2.UTI ya kwenye kibofu (cystitis). hii ni aina ya UTI ambayo huathiri kibofu cha mkojo. Dalili zake ni:-
1.Maumivu ya nyonga
2.Maumivu ya tumbo kwa chini ya kitovu ama mvurugiko wa tumbo kwa chini
3.Kukojoa mara kwa mara huku ukiwa na maumivu.
4.Kukojoa damu, ama mkojo wenye rangi nyekundu ya kupauka.
3.UTI ya kwenye mrija wa mkojo (urethritis). mrija wa mkojo kitaalamu unaitwa urethra. Huu ndio mrija unaotoa mkojo kutoka kwenye kibofu na kuuleta nje. Dalili za UTI hii ni kuhisi kuunguwa wakati wa kukojoa.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 web hosting 👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉4 Madrasa kiganjani 👉5 Simulizi za Hadithi Audio 👉6 Kitau cha Fiqh
Post zinazofanana:
Dalili za jeraha la kawaida kwenye ubongo
Posti hii inahusu zaidi dalili la jeraha la kawaida kwenye ubongo, jeraha la kawaida utokea kwa sababu mbalimbali kama vile kupata ajali na kugongwa na kitu chochote kichwani,
Soma Zaidi...Maumivu ya kiuno na dalili zake
Posti hii inahusu zaidi maumivu ya kiuno na dalili zake, ni maumivu ambayo utokea kwenye kiuno na kusababisha madhara mbalimbali katika mwili,
Soma Zaidi...Tatizo la kutokwa na damu baada ya tendo la ndoa.
Kutokwa na damu baada ya tendo la ndoa (post-coital bleeding) ni hali inayoweza kuleta hofu kwa wanawake wengi. Ingawa mara nyingi sababu zake si za kutisha, ni muhimu kuelewa visababishi mbalimbali vinavyoweza kuashiria matatizo ya kiafya yanayohitaji matibabu. Makala hii inachunguza kwa kina sababu za kibiolojia, maambukizi, na magonjwa yanayoweza kusababisha hali hii, ikitoa mwongozo wa wakati wa kumwona daktari.
Soma Zaidi...Fahamu Ugonjwa wa Saratani ya seli nyeupe.
Posti hii inazungumzia kuhusiana na Saratani ambayo hutokea katika aina ya seli nyeupe ya damu inayoitwa seli ya plasma. Seli za plasma hukusaidia kupambana na maambukizo kwa kutengeneza kingamwili zinazotambua na kushambulia vijidudu. Pia husababish
Soma Zaidi...Kukauka kwa ngozi (Dry skin): Sababu na njia za kuilainisha.
Ngozi kavu ni tatizo la kawaida linaloweza kusababisha ngozi kuvutika, kuwasha, na hata kupata michirizi au magamba. Ingawa mara nyingi sio tatizo kubwa kiafya, inaweza kuwa kero inayoathiri muonekano na raha yako ya kila siku. Makala haya yanakupa mwongozo wa nini kinasababisha ngozi yako kupoteza unyevu na hatua unazoweza kuchukua ili kuirejeshea afya na ulaini wake.
Soma Zaidi...Kwa nini kung’atwa na mbu hakuambukizi UKIMWI?
Ingawa mbu hunyonya damu kwa binadamu, hawana uwezo wa kueneza virusi vya UKIMWI (VVU). Sababu ni kwamba virusi vya VVU haviwezi kuishi wala kuzaliana ndani ya mwili wa mbu, na pia mbu hawaingizi damu ya mtu mmoja kwa mwingine wanapong’ata.
Soma Zaidi...