Dalili za UTI
Somo hili linakwenda kukuletea dalili za UTI
Dalili za UTI
1.Kukojoa mara kwa mara
2.Kuhisi kuunguwa ama umoto wakati wa kukojoa
3.Kutoa mikojo kwa uchache
4.Mkojo kuwa mchafu, kama mawingu ama mwekundu uliopauka
5.Harufu kali ya mkojo
6.Maumivu ya kwenye njonga kwa wanawake
7.Maumivu ya mkundu na puru kwa wanaume.
Dalili za UTI zinaweza pia kuwa tofauti na hizo hapo juu. Dalili hizi hutofautiana kwa kulingana na aina ya UTI. Kama unataka kuzijuwa dalili zaidi za UTI endelea kusoma makala hii mpaka mwisho.
Aina za UTI na dalili zake.
Ugonjwa wa UTI umegawanyika katika makundi mbalimbali. Makundi hayo ni kama:-
1.UTI ya kwenye figo (acute pyelonephritis). UTI hii huathiri figo, na kusababisha dalili kama:-
1.Maumivu ya mgongo kwa juu
2.Homa kali
3.Kuhisi baridi na kutetemeka
4.Kichefuchefu
5.Kutapika.
2.UTI ya kwenye kibofu (cystitis). hii ni aina ya UTI ambayo huathiri kibofu cha mkojo. Dalili zake ni:-
1.Maumivu ya nyonga
2.Maumivu ya tumbo kwa chini ya kitovu ama mvurugiko wa tumbo kwa chini
3.Kukojoa mara kwa mara huku ukiwa na maumivu.
4.Kukojoa damu, ama mkojo wenye rangi nyekundu ya kupauka.
3.UTI ya kwenye mrija wa mkojo (urethritis). mrija wa mkojo kitaalamu unaitwa urethra. Huu ndio mrija unaotoa mkojo kutoka kwenye kibofu na kuuleta nje. Dalili za UTI hii ni kuhisi kuunguwa wakati wa kukojoa.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 kitabu cha Simulizi 👉2 Bongolite - Game zone - Play free game 👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉4 Dua za Mitume na Manabii 👉5 Simulizi za Hadithi Audio 👉6 Madrasa kiganjani
Post zinazofanana:
nahis miguu pamoja na mikono kuishiwa nguvu ni mgongo kuuma ni dalili za ugonjwa gan ?
mm nahis miguu pamoja na mikono kuishiwa nguvu ni mgongo kuuma ni dalili za ugonjwa gan ?
Soma Zaidi...DALILI ZA HOMA YA BONDE LA UFA (RVFD) NA INAVYOSAMBAZWA.
Homa hii inapatikana katika maeneo ya bonde la ufa barani Afrika na na Mashariki ya kati.
Soma Zaidi...Je minyoo inaweza kusababisha mmeng'enyo wa chakula kuwa dhaifu?
Mfumo wa chakula unaweza kuwa dhaifu kwa sababu nyingi ikiwepo vyakula vyenyewe, vinywaji ama maradhi. Vipi kuhusu minyoo? Endelea na makala hii utajifunza zaidi.
Soma Zaidi...Njia za kupunguza ugonjwa wa zinaa
Posti hii inahusu zaidi njia ambazo zinaweza kutumika Ili kuweza kupunguza kuwepo kwa magonjwa ya zinaa
Soma Zaidi...Sababu za Kutokwa na Damu Mwanzoni mwa Mimba:
Kutokwa na damu katika miezi mitatu ya kwanza ya ujauzito ni hali inayoweza kuleta hofu kubwa kwa mama mjamzito. Makala hii inachambua sababu za kawaida za hali hii, inapopaswa kuwa na wasiwasi, na hatua muhimu za kuchukua ili kulinda afya yako na ya kiumbe kilichopo tumboni.
Soma Zaidi...