picha

Dalili za UTI

Somo hili linakwenda kukuletea dalili za UTI

Dalili za UTI

1.Kukojoa mara kwa mara

2.Kuhisi kuunguwa ama umoto wakati wa kukojoa

3.Kutoa mikojo kwa uchache

4.Mkojo kuwa mchafu, kama mawingu ama mwekundu uliopauka

5.Harufu kali ya mkojo

6.Maumivu ya kwenye njonga kwa wanawake

7.Maumivu ya mkundu na puru kwa wanaume.

 

Dalili za UTI zinaweza pia kuwa tofauti na hizo hapo juu. Dalili hizi hutofautiana kwa kulingana na aina ya UTI. Kama unataka kuzijuwa dalili zaidi za UTI endelea kusoma makala hii mpaka mwisho.

 

Aina za UTI na dalili zake.

Ugonjwa wa UTI umegawanyika katika makundi mbalimbali. Makundi hayo ni kama:-

1.UTI ya kwenye figo (acute pyelonephritis). UTI hii huathiri figo, na kusababisha dalili kama:-

1.Maumivu ya mgongo kwa juu

2.Homa kali

3.Kuhisi baridi na kutetemeka

4.Kichefuchefu

5.Kutapika.

 

2.UTI ya kwenye kibofu (cystitis). hii ni aina ya UTI ambayo huathiri kibofu cha mkojo. Dalili zake ni:-

1.Maumivu ya nyonga

2.Maumivu ya tumbo kwa chini ya kitovu ama mvurugiko wa tumbo kwa chini

3.Kukojoa mara kwa mara huku ukiwa na maumivu.

4.Kukojoa damu, ama mkojo wenye rangi nyekundu ya kupauka.

 

3.UTI ya kwenye mrija wa mkojo (urethritis). mrija wa mkojo kitaalamu unaitwa urethra. Huu ndio mrija unaotoa mkojo kutoka kwenye kibofu na kuuleta nje. Dalili za UTI hii ni kuhisi kuunguwa wakati wa kukojoa.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 3122

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 Simulizi za Hadithi Audio     ๐Ÿ‘‰2 Madrasa kiganjani     ๐Ÿ‘‰3 Kitabu cha Afya     ๐Ÿ‘‰4 ai web app     ๐Ÿ‘‰5 Dua za Mitume na Manabii     ๐Ÿ‘‰6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    

Post zinazofanana:

Maajabu ya damu na mzunguuko wake mwilini.

Ukistaajabu ya Musa utastaajabu ya Firauni. Haya ni maneno ya wahenga. Sasa hebu njoo u staajabu ya damu

Soma Zaidi...
Fangasi wanaojulikana kama Blastomyces

Fangasi wanaojulikana kama Blastomyces, hawa ni fangasi wanaosababisha maradhi yajulikanayo kama blastomycosis.

Soma Zaidi...
Dalili na ishara za jipu la Jino

Jipu la jino ni mfuko wa usaha unaosababishwa na maambukizi ya bakteria.

Soma Zaidi...
Maradhi ya macho

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu maradhi ya macho,dalili na matibabu yake

Soma Zaidi...
Mapigo ya moyo kwenda mbio, mwili kuchoka,kichefuchefu, kizungungu, joto kiasi.

Je, mtu mwenye dalili zifuatazo Kama, Mapigo ya moyo kwenda mbio, mwili kuchoka,kichefuchefu, kizungungu, joto kiasi.

Soma Zaidi...
Je na kwa upande wa mwanaume kuumwa upande wa kushoto wa tumbo kuna shida gani?

Maumivu ya tumbo upande wa kushoti, kwa mwanamke huwenda ikawa ni ujauzito ama shida nyingine za kiafya kama tumbo kujaa gesi, kukosa choo na kadhalika. Sasa vipi kwa wanaume ni ipi hasa sababuรขยโ€

Soma Zaidi...