AINA ZA MINYOO: tapeworm, livefluke, roundworm, hookworm, flatworm

AINA ZA MINYOO: tapeworm, livefluke, roundworm, hookworm, flatworm

AINA ZA MINYOO Minyoo ambao wanaweza kuishi ndani ya mwili wa binadamu wapo aina nying, lakini hapa nitakueleza aina kuu tatu za minyoo hawa.

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

AINA ZA MINYOO: tapeworm, livefluke, roundworm, hookworm, flatworm

AINA ZA MINYOO

AINA ZA MINYOO
Minyoo ambao wanaweza kuishi ndani ya mwili wa binadamu wapo aina nying, lakini hapa nitakueleza aina kuu tatu za minyoo hawa. Aina hizi ni Minyoo wanaotambulika kama flatworm, roundworm na thory-headed worm. Majina ya minyoo hawa yanafanana na maumbile yako kama tutakavyoona hapo chini. Wengi katika hawa minyoo wanaweza kuonekana kwa macho



1.Minyoo inayotambulika kama Tapeworm
Hawa ni katika aina za flatworm, minyoo hawa wanaumbo lililo bataa yaani flati. Unaweza kuwapata minyoo hawa kwa kunywa maji ambayo yana mayai ya minyoo hawa au lava. Pia unaweza kuwapata. Minyoo hawa kwenye chakula ambacho hakikupikwa ama hakikuiva vizuri.kama nyama hasa ya ngurue. Karibia nyama za wanyama wote zina wadudu hawa.

Minyoo hawa wanaonekana kama pingili zilizoungana na kutengeneza cheni ndefu. Minyoo hawa wanaweza kuwa warefu mpaka kufikia futi 80 na wanaweza kuishi ndani ya mwili wa mwanadamu mpaka miaka 30.



2.minyoo inayotambulika kama flukes
Hawa pia ni katika aina za minyoo waitwao flatworm. Mwanadamu anaweza kuwapata minyoo hawa kupitia maji yasiyo salama,kupitia mboga ambazo hukuwa ndani ya maji.pia kwa kula samaki ambaye ana minyoo hawa. Pia inatokea ukaosha mboga, tunda kwa kutumia maji ambayo yana minyoo hawa.

Minyoo hawa wanapoingia mwilini wanaelekea kwanye utumbo mdogo na huko ndipo huishi, pia maeneo mengine wanapoishi ni kwenye damu, na tishu za mwili kama ini. Kuna aina nyingi za aina hii ya minyoo, lakini ukubwa wao hawazidi nchi kadhaa.



3.minyoo wanaotambulika kama Hookworm
Hawa ni minyoo aina ya roundworm. Minyoo hawa wanaweza kusambazwa kwa kupitia kinyesina udongo. Hasa kwa wale wanaokula udongo ni rahisi sana kupata aina hii ya minyoo. Njia nyingine nyepesi kwa kupata minyoo hawa ni kwa kutembea miguu peku kwenye udongo ambao una mayai au lava wa aina hii ya minyoo. Malava haya yanaweza kuingia kwenye ngozi yako.

Minyoo hawa wanaishi kwenye utumbo mwembamba, na kwa kuwa kichwani kwao kuna kama miimba ilofanana na ndiwano, wanaitumia kujitundika kwenye utumbo mdogo. Ukubwa wao hauzidi nusu nchi.



4.minyoo wanaotambulika kama pinworms (threadworms)
Hawa ni katika minyoo wadogo sana na maranyingi hawana madhara. Minyoo hawa ni maarufu sana kwa watoto, walezi wa watoto wadogo na maeneo yeye watoto wadogo wengi unweza kuwapata sana hawa. Wana rangi nyeupe na ukubwa wao hauzindi nusu nchi.



Minyoo hawa unawapata kwa kuyala mayai yao kutoka kwa mtu mwenye minyoo hii. Mayai ya minyoo hawa hayawezi kuonekana kwa macho. Pindi unapokula mayai haya yanakwenda kukaa kwenye utumbo mdogo mpaka kutotolewa. Wakati wa usiku minyoo wanawake wanakwenye chini kwenye puru na kutaga mayai kwenye mikunjo ya puru. Kama mtu atajikuna sehemu ya puru mayai yale yanabakia mkononi zaidi ya masaa kadhaa.



Ikitokea mtu huyu ameshika kitu bila ya kunawa mayai yele yanabaki pale. Kama mtu mwingine akapashika pale na akala kitu bila ya kunawa anaweza akayala mayai yale na kupata minyoo. Pia minyoo hii unaweza kuipata kwa kuvuta hewa yenye mayai ya minyoo hii.



Minyoo hii haina athari zaidi kwa afya lakini mwenye minyoo hii atahisi kuwashwa kwenye puru, ama kuzungukia sehemu ya haja kuwa, wakati mwingine maumivu yatumbo. Wakati mwingine ngozi inawasha sana. Minyoo hawa pia kwa wanawake wanaweza kuhama kutoka kwenye puru na kuelekea kwenye uke wa mwanamke na kuingia ndani. Huenda hali hii ikapelekea kupata UTI na matatizo mengine ya kiaya.



Kupambana na minyoo hawa hakikisha unaosha mikono unapoamka, unapotaka kula chochote, kuingia kwenye choo safi na usipende kushikshika vitu hasa maeneo ya vyoo vya watu wengi. Minyoo hawa ni rahisi kutibika tofauti na minyoo wengine.



5.minyoo wanaotambulika kama trichinosis worm
Minyoo hawa ni katika minyoo ambao wanapatikana kutoka kwa wanyama. Mtu anaweza kuwapata minyoo hawa kwa kula nyama ambayo haukuiva vyema, ama kwa kula nyama mbichi. Malava ya minyoo hawa yanakwenda kwenye utumbo mdogo, na huko huweza kuingia kwenye mirija ya damu na kuenda maeneo mengine ya mwili, kwenye misuli na tishu za mwili.


                   

Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 1542

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Bongolite - Game zone - Play free game    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

ATHARI ZA KIAFYA ZA KUTOTIBU MALARIA AU KUCHELEWA KUTIBU MALARIA
ATHARI ZA KIAFYA ZA KUTOTIBU MALARIA AU KUCHELEWA KUTIBU MALARIA

Pindi malaria isipotibiwa inaweza kufanya dalili ziendelee na hatimaye kusababisha kifo.

Soma Zaidi...
Madhara ya gonorrhea endapo haitotibiwa
Madhara ya gonorrhea endapo haitotibiwa

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu madhara ya gonorrhea endapo haitotibiwa

Soma Zaidi...
nahis miguu pamoja na mikono kuishiwa nguvu ni mgongo kuuma ni dalili za ugonjwa gan ?
nahis miguu pamoja na mikono kuishiwa nguvu ni mgongo kuuma ni dalili za ugonjwa gan ?

mm nahis miguu pamoja na mikono kuishiwa nguvu ni mgongo kuuma ni dalili za ugonjwa gan ?

Soma Zaidi...
Fahamu matatizo ya ini kuwa na kovu
Fahamu matatizo ya ini kuwa na kovu

kovu (Fibrosis) ya ini inayosababishwa na aina nyingi za magonjwa na hali ya ini, kama vile Homa ya Ini na unywaji pombe kupita kiasi. Ini hufanya kazi kadhaa muhimu, ikiwa ni pamoja na kuondoa vitu vyenye madhara katika mwili wako, kusafisha damu yako

Soma Zaidi...
Dalili za Ugonjwa wa kula kupindukia
Dalili za Ugonjwa wa kula kupindukia

Ugonjwa wa kula kupindukia ni ugonjwa mbaya wa ulaji ambapo mara kwa mara unatumia kiasi kikubwa cha chakula na kuhisi huwezi kuacha kula.

Soma Zaidi...
Mtoto Kutokwa na matongo tongo tiba ake nin sababu
Mtoto Kutokwa na matongo tongo tiba ake nin sababu

Hili ni swali lililowahi kuulizwa na moja ya wasomaji wetu

Soma Zaidi...
Njia za kutibu saratani
Njia za kutibu saratani

Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali za matibabu ya ugonjwa wa saratani,ni ugonjwa ambao unaweza kupona ikiwa umegundulika mapema katika hatua za mwanzo na kama ugonjwa huu umefikia hatua za mwisho Tiba yake huwa ni kupunguza makali ya ugonjwa.

Soma Zaidi...
Dalili za minyoo
Dalili za minyoo

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za minyoo

Soma Zaidi...
Dalili za kwanza za HIV na UKIMWI kuanzia wiki ya kwanza toka kuathirika
Dalili za kwanza za HIV na UKIMWI kuanzia wiki ya kwanza toka kuathirika

DALILI ZA HIV ZA MWANZO NA DALILI ZA UKIMWI ZA MWANZO Kama ilivyo magonjwa mengi hupitia hatua kadha kadha na kuonyesha dalili kadha katika hatua hizo.

Soma Zaidi...