picha

Njia za kuzuia upele

Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali za kuzuia upele, ni njia ambazo utumiwa Ili kupunguza tatizo la upele kwenye jamii, kwa hiyo jamii inapaswa kutumia njia hizi Ili kuweza kupambana na ugonjwa huu ambao unatibika.

Njia za kutibu ugonjwa wa upele.

1. Kwanza kabisa tunapaswa kuoga mara kwa mara walau mara mbili kwa siku kwa wale ambao hawajapata ila kwa waliopata wanapaswa kuoga zaidi ya mara mbili au wakioga hata mara tatu sio mbaya na pia kila wanapooga wanapaswa kubadilisha nguo chafu na kuvaa nguo safi Ili kuweza kuepuka kuendelea kuwepo kwa maambukizi.

 

2. Pia tunapaswa kuwatafuta watu ambao Wana dalili za ugonjwa huu na kuwapatia matibabu muhimu Ili waweze kuwa vizuri Pia kuzunguka kwenye vijiji mbalimbali Ili kuwatafuta wagonjwa wote hasa hasa wale wasiopenda kwenda hospital wapewe elimu Ili waone umuhimu wa kwenda hospital.

 

3. Watu wanapaswa kupewa elimu kuhusu namna ya kufanya usafi kwa sababu kwa wale wanaozingatia usafi ni vigumu sana kupata ugonjwa huu kwa hiyo ni vizuri kuwajulisha njia na namna ugonjwa huu unavyosambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine na jinsi ya kutibu ugonjwa huu.

 

4. Vile vile na mifumo ya maji inapaswa kuboreshwa Ili watu waweze kupata maji ya kutosha kwenye familia na nyumba baada ya nyumba kwa kufanya hivyo watu wataweza kufua na kuoga na maambukizi yataisha au kupunguza kwa kiasi.

 

5. Pia wahudumu wa afya na viongozi wanapaswa kwenda mashuleni kutoa elimu kwa watoto kuhusu namna ya kujikuna kwa sababu watoto wengi wanapata kwa kuambukizana kutoka kwa mtoto mmoja kwenda kwa mwingine na tatizo kama lipo watibiwe kwa wale walioambukizwa Ili kuepuka maambukizi kuendelea.

 

6. Vile vile wahudumu wa afya wanapaswa kuzunguka kutoka kwenye nyumba Moja na nyingine Ili kutibu wale wenye ugonjwa tayari.kwa hiyo jamii inapaswa kuelekezwa kuwa chanzo kikubwa cha ugonjwa huu ni uchafu na dawa kuu ni usafi kwa kujua hivyo hali itaweza kutulia na watu watapona.

 

 

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 2826

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Bongolite - Game zone - Play free game     👉3 web hosting     👉4 kitabu cha Simulizi     👉5 Madrasa kiganjani     👉6 ai web app    

Post zinazofanana:

Dalili za ugonjwa wa Ugumu wa kumeza (dysphagia)

Ugumu wa kumeza (dysphagia) inamaanisha inachukua muda na bidii zaidi kuhamisha chakula kutoka kwa mdomo wako hadi kwenye tumbo lako. Ugumu wa kumeza unaweza pia kuhusishwa na maumivu. Katika baadhi ya matukio, kumeza inaweza kuwa haiwezekani. Ugumu w

Soma Zaidi...
Jinsi ya kupunguza maumivu ya hedhi kwa njia asilia.

Maumivu ya tumbo wakati wa hedhi, kitaalamu kama dysmenorrhea, huwasumbua wanawake wengi kila mwezi. Ingawa mara nyingi hutibika kwa dawa za dukani, njia za asili zinaweza kusaidia sana kupunguza makali ya maumivu hayo bila kuathiri mfumo wa mmeng'enyo wa chakula au figo. Makala hii inaangazia mbinu bora za asili unazoweza kuzitumia nyumbani ili kupata nafuu.

Soma Zaidi...
Matumizi ya chumvi nyingi: Hatari kwa afya ya moyo.

Katika ulimwengu wa kisasa, mtindo wa maisha na vyakula vilivyosindikwa vimesababisha ongezeko kubwa la ulaji wa chumvi kupita kiasi. Makala hii inachunguza uhusiano wa moja kwa moja kati ya ulaji wa sodiamu na magonjwa ya moyo. Tutajadili jinsi chumvi inavyoathiri shinikizo la damu, utaratibu wa uharibifu wa mishipa ya damu, na hatua za kivitendo unazoweza kuchukua ili kupunguza matumizi yake kwa maisha bora na marefu.

Soma Zaidi...
Sababu za Kuvimba kwa kope.

Post hii inazungumzia kuhusiana na Sababu zinazopelekea kuvimba kwa kope, kawaida huhusisha sehemu ya kope ambapo kope hukua na kuathiri kope zote mbili. Pia hutokea wakati tezi ndogo za mafuta ziko karibu na msingi wa kope huziba. Hii inasababisha kuw

Soma Zaidi...
dalili za mwanzo za ukimwi kwa mwanamke

Katika makala hii utakwenda kuzijuwa baadhi ya dalili za ukimwi ama HIV kwa mwanamke

Soma Zaidi...
Dalili za maambukizi kwenye nephroni

Post hii inahusu zaidi maambukizi kwenye nephroni, uweza kutokea kwenye figo Moja au zote mbili.

Soma Zaidi...