picha

Njia za kuzuia upele

Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali za kuzuia upele, ni njia ambazo utumiwa Ili kupunguza tatizo la upele kwenye jamii, kwa hiyo jamii inapaswa kutumia njia hizi Ili kuweza kupambana na ugonjwa huu ambao unatibika.

Njia za kutibu ugonjwa wa upele.

1. Kwanza kabisa tunapaswa kuoga mara kwa mara walau mara mbili kwa siku kwa wale ambao hawajapata ila kwa waliopata wanapaswa kuoga zaidi ya mara mbili au wakioga hata mara tatu sio mbaya na pia kila wanapooga wanapaswa kubadilisha nguo chafu na kuvaa nguo safi Ili kuweza kuepuka kuendelea kuwepo kwa maambukizi.

 

2. Pia tunapaswa kuwatafuta watu ambao Wana dalili za ugonjwa huu na kuwapatia matibabu muhimu Ili waweze kuwa vizuri Pia kuzunguka kwenye vijiji mbalimbali Ili kuwatafuta wagonjwa wote hasa hasa wale wasiopenda kwenda hospital wapewe elimu Ili waone umuhimu wa kwenda hospital.

 

3. Watu wanapaswa kupewa elimu kuhusu namna ya kufanya usafi kwa sababu kwa wale wanaozingatia usafi ni vigumu sana kupata ugonjwa huu kwa hiyo ni vizuri kuwajulisha njia na namna ugonjwa huu unavyosambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine na jinsi ya kutibu ugonjwa huu.

 

4. Vile vile na mifumo ya maji inapaswa kuboreshwa Ili watu waweze kupata maji ya kutosha kwenye familia na nyumba baada ya nyumba kwa kufanya hivyo watu wataweza kufua na kuoga na maambukizi yataisha au kupunguza kwa kiasi.

 

5. Pia wahudumu wa afya na viongozi wanapaswa kwenda mashuleni kutoa elimu kwa watoto kuhusu namna ya kujikuna kwa sababu watoto wengi wanapata kwa kuambukizana kutoka kwa mtoto mmoja kwenda kwa mwingine na tatizo kama lipo watibiwe kwa wale walioambukizwa Ili kuepuka maambukizi kuendelea.

 

6. Vile vile wahudumu wa afya wanapaswa kuzunguka kutoka kwenye nyumba Moja na nyingine Ili kutibu wale wenye ugonjwa tayari.kwa hiyo jamii inapaswa kuelekezwa kuwa chanzo kikubwa cha ugonjwa huu ni uchafu na dawa kuu ni usafi kwa kujua hivyo hali itaweza kutulia na watu watapona.

 

 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 2673

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉5 Kitabu cha Afya     👉6 Kitau cha Fiqh    

Post zinazofanana:

vidonda vya tumbo

Kupata kitabu hiki download faili la PDF hapo chini na usome bila ya internet.

Soma Zaidi...
Njia za kupunguza makali ya pressure au shinikizo la damu

Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali za kupunguza ugonjwa wa pressure au shinikizo la damu kwa waliokwisha kupata wanaweza kupunguza na kwa wake ambao hawajapata ni nzuri inawasaidia kuepuka hatari ya kupata ppresha.

Soma Zaidi...
Dalili za maambukizi ya sikio kwa watu wazima

Posti hii inazungumzia kuhusiana na Maambukizi ya sikio mara nyingi ni maambukizi ya bakteria au virusi ambayo huathiri sikio la kati, nafasi iliyojaa hewa nyuma ya ngoma ya sikio ambayo ina mifupa midogo ya sikio inayotetemeka. Maambukizi ya si

Soma Zaidi...
Sababu za maumivu ya tumbo

hapa utajifunza maradhi mbalimbali yanatopelekea kuwepo kwa maumivu ya tumbo

Soma Zaidi...
Kivimba kwa utando wa pua

post hii inazungumzia kuhusiana na kuvimba kwa utando wa pua unaoonyeshwa na mchanganyiko wa dalili zifuatazo: Kupiga chafya Msongamano wa pua Muwasho wa kiwambo cha sikio Kuwasha kwa pua na koromeo Uvimbe huu hutokea ikiwa mashambulizi ya kupiga chafya,

Soma Zaidi...