Posti hii inahusu zaidi hatua au mbinu za kupambana na ugonjwa wa UTI kwa sababu ugonjwa huu umekuwa tishio kubwa kwa sasa kwa hiyo tunapaswa kutumia njia mbalimbali ili kuweza kupambana na Ugonjwa huu.
1. Hatua ya kwanza ni matumizi ya maji ya kunywa na baada ya kunywa maji nenda haja kubwa mara kwa mara ili kuweza kupunguza uchafu mwilini.
2. Katika matumizi ya vinywaji epuka sana vinywaji ambavyo vinaweza kuhatarisha kibofu cha mkojo kwa sababu kama kuna maambukizo kwenye kibofu cha mkojo kupona ugonjwa wa UTI ni ndoto vinywaji vyenyewe ni kama vile kahawa na matumizi mengi ya vinywaji vyenye wingi wa caffeine.
3. Nenda haja ndogo baada ya kufanya ngono zembe.
Kwa hiyo baada ya kufanya tendo la ndoa nenda haja ndogo ili kama kuna maambukizi yoyote ya ugonjwa wa UTI uweza kuondoka.
4. Kawaida jipanguse kutoka mbele kwenda nyuma.
Kwa sababu kujipangusa kutoka nyuma kwenda mbele unasababisha bakteria walio kwenye kinyesi kuja mpaka kwenye kibofu cha mkojo na kusababisha Maambukizi kwa hiyo siku zote wafundishe watoto kujisafisha kutoka mbele kwenda nyuma sio nyuma kwenda mbele.
5. Hakikisha kila siku sehemu za siri ni safi mda wote ili pia kupunguza Maambukizi unapaswa kuosha sehemu za siri bila kutumia sabuni za manukato tumia sabuni ya kawaida ya kipande.
6. Kila mara jaribu kuoga maji masafi na yanayotiririka kwa sababu maji masafi yanasababisha kuwepo kwa hali ya usafi na kuzuia kuwepo kwa Maambukizi kwenye via vya uzazi.
7. Kwa kawaida ugonjwa huu mwanzoni ilionekana ni ugonjwa unaowapata sana akina dada au wanawake kwa ujumla ila kwa sasa ugonjwa huu uwapata wote yaani wanawake na wanaume kwa hiyo wote tuna haki ya kupigana na ugonjwa huu ili tuweze kuondokana nao na inawezekana.
8. Kwa hiyo usipotibu ugonjwa huu unaweza kupata madhara mengi pamoja na ugumba kwa wanawake, kupata kansa ya kibofu kwa mwanaume na madhara mengine mengi.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Ugonjwa wa degedege ni ugonjwa unaowapata sana watoto chini ya miaka mitano ingawa na watu wazima wanapatwa na ugonjwa huo
Soma Zaidi...Malaria husababishwa na vimelea (parasite) ambavyo husambazwa ama kubebwa na mbu aina ya anopheles.
Soma Zaidi...Huwenda ukawa ni moja kati ya watu wanaotaka kujuwa juu ya dalili za ukimwi. Kama wewe ni katika watu hawa tambuwa kuwa kuna dalili za VVU (hiv) na dalili za ukimwi. Makala hii itakwenda kukuletea dalili kuu za mwanzo za VVU na HIV kuanzia wiki tatu za mw
Soma Zaidi...Hivi umeshawahikujiuliza kuhusu tezi dume. Wacha nikujuze kitu kimoja, ni kuwa tezi dume huwapata watu kuanziamiaka 40 na kuendelea. Na ifahamike kuwa tezi dume sio busha ama ngiri maji. Pia itambulikekuwa rozi dumehutibika.
Soma Zaidi...Makala hii inakwenda kukupa majibu ya maswali mengi kuhusu VVU na UKIMWI. tutakwenda kuona kwa ufupi historian a chanzo cha VVU na UKIMWI. hatuwa za maambukizi ya VVU na ukimwi na dalili zake za kuonekana toka kupata maambukizi. Pia hapa utajifunza namna
Soma Zaidi...Ugonjwa wa kisukari hurejelea kundi la magonjwa yanayoathiri jinsi mwili wako unavyotumia sukari kwenye damu (glucose). Glucose ni muhimu kwa afya yako kwa sababu ni chanzo muhimu cha nishati kwa seli zinazounda misuli na tishu zako. Pia ndio chanzo ki
Soma Zaidi...Zijuwe dalili kuu 7 za vidonda vya tumbo, kama kiungulia, tumbo kujaa, maumivu ya umbo..
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia ambazo VVU huambukizwa
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi aina mbili za kifua kikuu, aina ya kwanza ni ile ya kawaida ambayo ushambulia mapafu na aina ya pili ni ile ambayo ushambulia sehemu mbalimbali za mwili kama vile kwenye limfu node, kwenye sehemu za moyo, kwenye uti wa mgongo, kwen
Soma Zaidi...Katika makala hii utakwenda kuzijuwa baadhi ya dalili za ukimwi ama HIV kwa mwanamke
Soma Zaidi...