picha

Hatua za kupambana na ugonjwa wa UTI

Posti hii inahusu zaidi hatua au mbinu za kupambana na ugonjwa wa UTI kwa sababu ugonjwa huu umekuwa tishio kubwa kwa sasa kwa hiyo tunapaswa kutumia njia mbalimbali ili kuweza kupambana na Ugonjwa huu.

Hatua za kupambana na ugonjwa huu wa UTI.

1. Hatua ya kwanza ni matumizi ya maji ya kunywa na baada ya kunywa maji nenda haja kubwa mara kwa mara ili kuweza kupunguza uchafu mwilini.

 

 

 

2. Katika matumizi ya vinywaji epuka sana vinywaji ambavyo vinaweza kuhatarisha kibofu cha mkojo kwa sababu kama kuna maambukizo kwenye kibofu cha mkojo kupona ugonjwa wa UTI ni ndoto vinywaji vyenyewe ni kama vile kahawa na matumizi mengi ya vinywaji vyenye wingi wa caffeine.

 

 

 

 

 

3. Nenda haja ndogo baada ya kufanya ngono zembe.

Kwa hiyo baada ya kufanya tendo la ndoa nenda haja ndogo ili kama kuna maambukizi yoyote ya ugonjwa wa UTI uweza kuondoka.

 

 

 

 

4. Kawaida jipanguse kutoka mbele kwenda nyuma.

Kwa sababu kujipangusa kutoka nyuma kwenda mbele unasababisha bakteria walio kwenye kinyesi kuja mpaka kwenye kibofu cha mkojo na kusababisha Maambukizi kwa hiyo siku zote wafundishe watoto kujisafisha kutoka mbele kwenda nyuma sio nyuma kwenda mbele.

 

 

 

5. Hakikisha kila siku sehemu za siri ni safi mda wote ili pia kupunguza Maambukizi unapaswa kuosha sehemu za siri bila kutumia sabuni za manukato tumia sabuni ya kawaida ya kipande.

 

 

 

6. Kila mara jaribu kuoga maji masafi na yanayotiririka kwa sababu maji masafi yanasababisha kuwepo kwa hali ya usafi na kuzuia kuwepo kwa Maambukizi kwenye via vya uzazi.

 

 

 

 

7. Kwa kawaida ugonjwa huu mwanzoni ilionekana ni ugonjwa unaowapata sana akina dada au wanawake kwa ujumla ila kwa sasa ugonjwa huu uwapata wote yaani wanawake na wanaume kwa hiyo wote tuna haki ya kupigana na ugonjwa huu ili tuweze kuondokana nao na inawezekana.

 

 

 

 

 

8. Kwa hiyo usipotibu ugonjwa huu unaweza kupata madhara mengi pamoja na ugumba kwa wanawake, kupata kansa ya kibofu kwa mwanaume na madhara mengine mengi.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 2131

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Simulizi za Hadithi Audio     👉4 web hosting     👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉6 Bongolite - Game zone - Play free game    

Post zinazofanana:

Dalili za fangasi wa kucha.

Posti hii inazungumzia kuhusiana na dalili,sababu za Hatari,na namna ya kujizuia na fangasi wa kucha.

Soma Zaidi...
Je, unaweza kupata mimba siku chache baada ya hedhi kuisha?

Jibu fupi ni ndiyo, inawezekana. Ingawa watu wengi huamini kuwa huwezi kupata ujauzito mara tu baada ya hedhi, uhalisia wa kibiolojia unaonyesha kuwa dirisha la uzazi linaweza kufunguka mapema kuliko unavyotarajia. Makala hii inaelezea jinsi mzunguko wa hedhi unavyofanya kazi na kwa nini ni muhimu kuwa makini wakati wote.

Soma Zaidi...
Dalili za Mimba Changa Wiki ya Kwanza

​Wiki ya kwanza ya ujauzito mara nyingi ni kipindi ambacho mwili huanza mabadiliko ya siri ya homoni. Post hii inatoa mwongozo kuhusu dalili ambazo mwanamke anaweza kuzihisi, ikizingatia ukweli wa kibaolojia na umuhimu wa utambuzi sahihi katika hatua hii ya awali.

Soma Zaidi...
Dalili za UKIMWI kwa Mtu Aliyeambukizwa Karibuni

Makala hii inaelezea hatua ya awali ya maambukizi ya virusi vya UKIMWI (VVU), inayojulikana kama hatua ya maambukizi makali (acute HIV infection). Inafafanua dalili za kawaida zinazoweza kujitokeza wiki chache baada ya mtu kupata maambukizi, umuhimu wa kupima mapema, na kuondoa dhana potofu kuhusu dalili hizi.

Soma Zaidi...
Je vvu inaweza sababisha mate kujaa mdomoni

Je kujaa kwa mate mdomoni ni dalili ya kuwa na VVU, na je ni zipi dalili za Virusi Vya Ukimwi (VVU) mdomoni?

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa pepopunda kwa watoto

Pepopunda ni ugonjwa hatari wa kutishia maisha unaosababishwa na sumu inayojulikana Kama tetanospasmin inayotolewa kwenye majeraha yaliyoambukizwa. Bakteria ya pepopunda huingia kwenye mwili wa mtoto mchanga kupitia kisiki cha kitovu ambacho kimekatwa na

Soma Zaidi...