Hatua za kupambana na ugonjwa wa UTI
Posti hii inahusu zaidi hatua au mbinu za kupambana na ugonjwa wa UTI kwa sababu ugonjwa huu umekuwa tishio kubwa kwa sasa kwa hiyo tunapaswa kutumia njia mbalimbali ili kuweza kupambana na Ugonjwa huu.
Hatua za kupambana na ugonjwa huu wa UTI.
1. Hatua ya kwanza ni matumizi ya maji ya kunywa na baada ya kunywa maji nenda haja kubwa mara kwa mara ili kuweza kupunguza uchafu mwilini.
2. Katika matumizi ya vinywaji epuka sana vinywaji ambavyo vinaweza kuhatarisha kibofu cha mkojo kwa sababu kama kuna maambukizo kwenye kibofu cha mkojo kupona ugonjwa wa UTI ni ndoto vinywaji vyenyewe ni kama vile kahawa na matumizi mengi ya vinywaji vyenye wingi wa caffeine.
3. Nenda haja ndogo baada ya kufanya ngono zembe.
Kwa hiyo baada ya kufanya tendo la ndoa nenda haja ndogo ili kama kuna maambukizi yoyote ya ugonjwa wa UTI uweza kuondoka.
4. Kawaida jipanguse kutoka mbele kwenda nyuma.
Kwa sababu kujipangusa kutoka nyuma kwenda mbele unasababisha bakteria walio kwenye kinyesi kuja mpaka kwenye kibofu cha mkojo na kusababisha Maambukizi kwa hiyo siku zote wafundishe watoto kujisafisha kutoka mbele kwenda nyuma sio nyuma kwenda mbele.
5. Hakikisha kila siku sehemu za siri ni safi mda wote ili pia kupunguza Maambukizi unapaswa kuosha sehemu za siri bila kutumia sabuni za manukato tumia sabuni ya kawaida ya kipande.
6. Kila mara jaribu kuoga maji masafi na yanayotiririka kwa sababu maji masafi yanasababisha kuwepo kwa hali ya usafi na kuzuia kuwepo kwa Maambukizi kwenye via vya uzazi.
7. Kwa kawaida ugonjwa huu mwanzoni ilionekana ni ugonjwa unaowapata sana akina dada au wanawake kwa ujumla ila kwa sasa ugonjwa huu uwapata wote yaani wanawake na wanaume kwa hiyo wote tuna haki ya kupigana na ugonjwa huu ili tuweze kuondokana nao na inawezekana.
8. Kwa hiyo usipotibu ugonjwa huu unaweza kupata madhara mengi pamoja na ugumba kwa wanawake, kupata kansa ya kibofu kwa mwanaume na madhara mengine mengi.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Dua za Mitume na Manabii 👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉3 Bongolite - Game zone - Play free game 👉4 Kitau cha Fiqh 👉5 web hosting 👉6 ai web app
Post zinazofanana:
Sababu za Maambukizi kwenye mifupa.
Post hii inahusu zaidi Maambukizi kwenye mifupa ambayo kwa kitaalamu huitwa Osteomyelitis, ni Maambukizi ambayo hutokea kwenye mifupa kwa sababu mbalimbali ambazo usababisha ugonjwa huu.
Soma Zaidi...Dalili na ishara za Ugonjwa wa kuambukiza.
Magonjwa ya kuambukiza ni maradhi yanayosababishwa na vijidudu kama vile bakteria, virusi, fangasi au vimelea. Viumbe vingi vinaishi ndani na kwenye miili yetu. Kwa kawaida hazina madhara au hata kusaidia, lakini chini ya hali fulani, baadhi ya viumbe
Soma Zaidi...Sababu za Uvimbe wa tishu za Matiti kwa wavulana au wanaume
posti hii inazungumzia kuhusiana na uvimbe wa tishu za matiti kwa wavulana au wanaume, unaosababishwa na kutofautiana kwa homoni za estrojeni na testosterone. Pia unaweza kuathiri matiti moja au zote mbili, wakati mwingine bila usawa. Watoto wachanga,
Soma Zaidi...Matatizo yanayosababisha saratani ya mapafu
Posti hii inaonyesha matatizo yanayosababisha saratani ya mapafu .
Soma Zaidi...Dalili na ishara za anemia ya minyoo
Posti hii inshusiana na dalili za anemia ya minyoo
Soma Zaidi...Je, UKIMWI Unaweza Kukaa Bila Dalili?
Jibu fupi ni ndiyo. VVU (Virusi vya Upungufu wa Kingamwili) vinaweza kuwepo mwilini kwa miaka mingi bila kuonyesha dalili zozote dhahiri za ugonjwa. Hali hii ya kutokuwa na dalili ndiyo inayochangia kwa kiasi kikubwa kusambaa kwa virusi hivi, kwani mtu anaweza kuwa anaambukiza wengine bila yeye mwenyewe au wengine kujua.
Soma Zaidi...