Post hii inahusu mwendelezo wa hadithi ya Nimlaumu nani ambapo juma anapanga na madaktari wanaopima DNA ili kuweza kutambua kwamba mtu mimba ni ya kwake na sio ya Frank kwa hiyo tuendelee kusikiliza mpaka tutakapoona mimba itakuwa ya Frank au juma.
1. Kama tulivyoona kwamba juma anaenda hospitalini na kuwapatia hela nyingi wale wanaopima DNA ili kuweza kutangaza kwamba mimba sio ya Frank ni ya juma, kwa sababu juma alikuwa anazomewa na marafiki zake pamoja na ndugu kwa kufikia umri alio nao bila kuwa na mtoto hali hiyo umepata kwa sababu ya kutembea na wanawake wengi na pia mara nyingi huwa anadhulumia watoto na waume wengine, kwa hiyo alipobahatisha kwa Amisa na akakuta Frank hana hili wala lile akaamua kutaka kuchukua watoto wasio wa kwake.kwa hiyo siku zikaenda na frank akawa anajiandwa na watu wengi ndipo Amisa akaamua kumpeleka Frank chuo ili kukamilisha masomo yake aliyoachia njiani kwa sababu ya kukosa mtu wa kumlipia karo.
2. Basi Frank akaamua kwenda kusoma nchi za nje kwa kuwa alikuwa amefaulu vizuri masomo ya sayansi akaamua kuchukua udaktari wa kupima genetic kwa sababu ya tatizo aliloliacha nyumbani, kwa hiyo akaanza kusoma ila mawazo yake ni juu ya mimba yake aliyoacha inagombaniwa , Frank alipoondoka nyumbani Amisa mimba yake ilikuwa na miezi sita tu, kwa hiyo alipofika chuoni akatengeneza urafiki na balozi wa nchi yake aliyekuwa kule nje alikoenda kusomea na akamwambia inshu yote na jinsi hongo ilivyotumika ili kuweza kuwachukua watoto wake, kwa hiyo huyo balozi akawa bega kwa bega na Frank.
3. Basi siku za kujifungua zinafika na Amisa alikuwa na rafiki yake aliyekuwa anaitwa Rhoda akimsindikiza mpaka hospitali na hatimaye akajifungua mapacha wawili watoto wa kike, baada tu ya Mama kujifungua tayari madaktari wa kupima DNA wakajitokeza tayari na Amisa akawa na wasiwasi sana na akaamua kumpigia Frank simu , Frank akasema kadri ya sheria watoto upimwa DNA wakiwa na miaka mitano ila madaktari baada ya kuambiwa na Amisa hawakukubali wakajifanya ujuaji na Amisa akampigia simu Frank na baadae Frank akawasiliana na balozi na balozi akawasiliana na wizara ya afya nchini na mda mfupi polisi wakawa weka chini ya ulinzi madaktari pamoja na Juma na hatimaye wakawa weka sero na madaktari wakanyanganywa leseni kila mtu akaanza kusema NIMLAUMU NANI? Basi wakatumikia kifungo kwa mda na baadae mda ulipofika wakatolewa kifungoni na maadui wa Frank wakaongezeka mara James, Amina, Baba Amina na Juma.
4. Basi Frank akamaliza masomo na wakati ule baba Amina alifungua hospitali kubwa ya kupima genetic na hakuwa na daktari wa kusimamia hospital yake alipoangalia mtandaoni akaona kuna daktari mmoja ndiye aliye na ujuzi wa kufanya kazi ya genetic kwa hiyo akatafuta number zake akampigia simu akisema Mheshimiwa dactor Frank naomba unipe mda nije kuongea nawe basi akamwambia aje, alipofika ofisini kwa Frank alipiga magoti na kumsalimia Frank na Frank hakumtambua mara moja kama alikuwa baba Amina na baba Amina hakumtambua frank.
5. Basi wakaelewana na Frank akakubali kuwepo pale kama mkuu wa hospitali kwa hiyo baba Amina akasema inabidi wafanye mkataba wakapanga siku ya mkataba na siku hiyo baba Amina alimletea Amina Ili aweze kushuhudia basi Frank anajitambulisha na history yake kwa ufupi na katika kujitambulisha na kusema magumu aliyoyapitia akiwasihi vijana waliokuwapo pale kupambana na kutokata tamaa na kuendelea kupambana Amina alikuwa na uchungu mkubwa kwa sababu aligundua kwamba ni Frank na ukizingatia alikuwa ameolewa na James na maisha yakawa magumu na akarudi nyumbani kwao kwa hiyo kabla ya Frank kumaliza kuongea Amina aliangua kilio kikubwa na watu wakakimbia kumsaidia ili watake kujua chanzo ni nini hapo Amina akaanza kuita akisema Frank nisamehe.
itaendelea.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya hapa chini kuipakua sasa!
Umeionaje Makala hii.. ?
Nani kama mama? Hadithi hii itakufunza umuhimu wa kuwa muwazi kuhusu familia yako.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya vijana wawili, hapa tunaona Jackie anajibu barua ya Julius kwa kusema yafuatayo.
Soma Zaidi...Post hii inahusu hadithi fupi tu kuhusu mtoto wa tajiri na maskini, palikuwepo na watoto wawili mmoja akiwa mtoto wa tajiri na mwingine wa maskini.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya Mama mchoyo na mwehu, kwa sababu mwehu alikuwa mkarimu alichukua ule mkate akawapstia watoto wa yule mama wakiwa wanatoka shule kwa hiyo tutaona kilichotokea kwa wale watoto.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi hadithi ya vijana wawili ambapo mitihani inaisha na wanaanza kuhukumiwa mmoja baada ya mwingine.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi mahusiano yaliyotokea kati ya vijana wawili ila yanafika baadae mmoja akamsaliti mwenzake.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme sehemu ya nne ni pale bibi anawachanganya kwa maneno yake yaani mke wa kwanza anaambiwa aandae malkia na mke mdogo atafute njia za kufanya kijana wake kuwa mfalme.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya mahusiano ya vijana wawili baada ya kuhamia shule mpya.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi mtoto wa tajiri na mtoto wa maskini wakipanda gari kuelekea shule kuanza maisha mapya.
Soma Zaidi...Post inahusu zaidi hadithi ya NIMLAUMU NANI ambayo ni sehemu ya sita, katika kipengele hiki tunaenda kumwona msichana Amina anapambana na hatimaye anafunga ndoa ya kiserikali na Frank
Soma Zaidi...