Mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme

Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme, tunajua kuwa mama yake na binti alimtorisha yule binti mbali kabisa ila kijana naye aliamua kutoroka na kumfuata binti mfalme na hatimaye akampata alipo.

Mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme.

1. Kama tulivyoishia kwenye sehemu ya kutoroshwa kwa bibi na binti, hali hii ilimuumiza sana mtoto wa kiume wa mfalme, lakini alipoulizwa hakuweza kusema chochote , ila siku Moja mama yake aliandaa chakula kizuri alichokuwa anakipenda yule mtoto wa kiume wa mfalme akawaita na marafiki zake akampatia zawadi nzuri,akawakusanya mabinti wazuri wakawa kwenye Ile tafrija lengo la Mama ni kutaka kumfanya yule kijana asahau yule Binti Ila hayo yote yalikuwa bure, katika sherehe hiyo watu vijana wote waliamka kucheza na wale mabinti wazuri ila mtoto wa kiume wa mfalme hakucheza na Binti yoyote yule.

 

2.ilifika wakati mpaka mabinti wanamsogelea yule kijana aliwaangalia kwa dharau tu, ndipo ilipofika jioni mtoto wa kiume wa mfalme akaandaliwa chumba kizuri kama heshima ya watoto wa mfalme ndani ya chumba aliwekwa msichana mlembo yule kijana alipoingia na kumkuta alitoka chumbani akamfungia yule msichana ndani yeye akatoka nje na kwenda kulala kwa walinzi wa mfalme, mama yake alipoamka asubuhi na mapema kuangalia kwenye chumba kilichoandaliwa alishangaa kuona msichana Yuko mwenyewe kitandani amelala fofofo, mama aliumia sana na akamfungulia msichana akamruhusa aende kwa wenzake..

 

3. Baada ya mtoto wa mfalme kuwa kwenye mawazo mazito aliamuru kumshirikisha rafiki Yake maangaiko aliyo nayo moyoni ila hakumwambia kwamba yule Binti anayemtesa ni ndugu yake Bali alimwambia kuwa amehama na ajui kaenda wapi, basi yule kijana akamwambia wewe ni mtoto pekee wa kiume wa mfalme kwa nini usimwambie mfalme tatizo lako akakupatia watu wakakusaidia kumtafuta huyo Binti? Yule kijana akakubali shingo upanda alipenda Siri hii isijulikane kwa mfalme na aliogopa sana kumwumiza mama yake kwa hiyo hali ikaendelea kuwa mbaya zaidi na maisha yakaendelea kuwa magumu kwa yule kijana kwa sababu hakutaka kumwaibisha mama yake na hakupenda kuoa msichana mwingine tofauti na yule Binti.

 

4. Kadri siku zilivyoenda ndipo na Mama akaingia katika wasi wasi mkubwa na akaamuru kumwita kijana wake na kuongea naye kuhusu Sheria za ufalme ni kwamba mtoto wa kiume wa mfalme anapaswa kuoa Binti ambaye Hana undugu naye na wewe ukipenda kuoa huyu ndugu yako hautaweza kupata ufalme kwa sababu ya kufanya kitendo cha namna hiyo kwa sababu mimi nilikutambulisha kwa mfalme bila kumtambulisha dada Yako lengo ni kwamba wewe urithi ufalme wa baba Yako ila wewe bado unagangania kuoa ndugu yako, yule kijana wa kiume wa mfalme akasema Mama kama yule angekuwa ni ndugu yangu angekuwa anatambulika a kwenye familia na ukoo pia ila kwa kuwa hawamtambui mimi siwezi kukusikiliza kwa hilo kwa hiyo mama tangia mda huu mimi naenda kumtafuta yule binti popote alipo na nitamuoa na sitasikiliza chochote kutoka kwako.

 

5. Baada ya mama kuona msimamo wa kijana ni mkali mno aliwaandaa watu ili kwenda kumuua yule binti na bibi, lakini kijana akapata taarifa ndipo akaenda kwa baba yake akamuomba jeshi akiwa na lengo la kwenda kumwokoa yule binti, alimwambia baba naomba niende kusherehekea na marafiki zangu ila naomba kwenda na jeshi kusudi wanilinde, kwa kuwa baba alikuwa anampenda sana kijana wake akamuandalia chakula, nyama na vitu vyote vinavyofaa kwa sherehe akampatia na jeshi pia akiamuru jeshi limlinde na kumsikiliza kwa kila kitu atakachowaambia baada ya kufika mbele kidogo akawaambia juwa wafuatane na hao wauaji waliotumwa na Mama yake kwa sababu wanajua binti alipo.

 

6. Yule kijana akamwambia mkuu wa jeshi kwamba kabla hatujaenda kwenye sherehe tunapaswa kumwokoa mchumba wangu kutokana na wauaji na tupambane nao mpaka tumwokoe , basi mkuu wa majeshi anawapanga watu wake na wakaanza mashambulizi mpaka wakamwokoa yule binti na bibi, baada ya hapo bibi alipopata taarifa za kutaka kuuawa kwa sababu ya yule binti alisikitika sana na akaamuru kuvujisha siri hiyo kwa wake wengine wa mfalme, basi mtoto wa kiume wa mfalme akamchukua yule binti akaenda kusherehekea naye na baadae akaja naye kwa mfalme akamtambulisha kama mke wake mfalme akafurahi kwa kuona kijana wake kapata mke ila mama alikoswa amani.

 

7. Basi ikafika siku ya maandalizi ya kumsimika kijana kurithi ufalme wa baba yake kwa sababu alikuwa ni mzee, kufuatia na sheria ya kwamba mtu anayerithi ufalme ni lazima mke wake wasiwe na undugu hata kidogo na kumbuka habari imo mikononi mwa wake wenza, je unafikili watanyamaza? 

 

itaendelea

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2022/07/11/Monday - 10:41:44 pm     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 817

Post zifazofanana:-

Madhara ya kunywa pombe kiafya
Posti hii inahusu zaidi madhara ya kunywa pombe kiafya, ni madhara ambayo utokea kwa watu wanaokumywa pombe kwa kupita kiasi kwa hiyo wanapaswa kupunguza kunywa pombe baada ya kujua madhara yake. Soma Zaidi...

je ute wa uzazi uanza kuonekana siku ya 14 tu au kabla ? Na je mimba ya siku tatu inaweza kucheza?
Miongoni mwa dalili zamwanzo za ujauzito ni maumivu ya tumbo ama kupatwa na damu kidogo. Mabadiliko ya ute ute sehemu za siri ni katika baadhi ya dalili. Endelea na makala hii utajifunza zaidi. Soma Zaidi...

Tango (cucumber)
Somo hili linakwenda kukuletea faida za kiafya za kula tango Soma Zaidi...

Faida za kitunguu thaumu mwilini
Makala hii itakuletea faida za kitunguu thaumu katika afyabyako. Soma Zaidi...

Mtihani penzini
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani Soma Zaidi...

Sababu zinazopelekea tumbo kujaa gesi
Kiufipi posti hii inaelezea kuhusiana na dalili na sababu zinazopelekea tumbo kujaa gesi Soma Zaidi...

Dalili za maumivu ya uti wa Mgongo
Posti hii inahusu zaidi dalili za uti wa mgongo ni dalili ambazo ujitokeza kwa mtu Mwenye tatizo la uti wa Mgongo. Soma Zaidi...

Jifunze jinsi ya kumsaidia mwenye kifafa
Kifafa hakiambukizi na ugonjwa wa ubongo lakini kifafa pia hakiathiri akili au ubongo Ila kikiwa kifafa Cha kudumu na Cha nguvu ndio huweza kuadhiri. Pia Kuna kifafa Cha mimba na kifafa Cha kawaida.kifafa Cha mimba ndio kinahatari Sana kuliko Cha Kawaid Soma Zaidi...

Zijue hatua za kufata ili kuepuka maradhi ya tumbo
Posti hii inaelezea kuhusiana na hatua za kufata ili kujikinga au kuepuka maradhi ya tumbo.kuna vitu vikikosekana husababisha maumivu ya tumbo. Soma Zaidi...

Sababu za kuvimba na maumivu kwenye korodani moja au zote mbili
Post yetu ya Leo inaenda kutufundisha kuhusiana na uvimbe wa korodani moja au ambayo kitaalamu huitwa EPIDIDYMITIS. EPIDIDYMITIS ni ugonjwa unaoathiri mfumo wa kiume wa uzazi. Epididymis ni mrija (tube) uliyoko nyuma ya korodani ambayo mbegu za kiume Soma Zaidi...

Namna za kujilinda na fangasi ukeni
Posti hii inahusu zaidi namna ya kuepuka fangasi za ukeni, ni njia ambazo usaidia kuepuka madhara ya fangasi za ukeni. Soma Zaidi...

Mgawanyo wa matibabu ya kifua kikuu.
Posti hii inahusu zaidi mgawanyo wa matibabu ya kifua kikuu, tunajua kubwa kifua kikuu ni Ugonjwa ambao utumia mda mrefu kidogo katika matibabu kwa hiyo mgawanyiko wake uko kwenye sehemu mbili muhimu kama tutajavyoona Soma Zaidi...