Menu



Mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme

Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme, tunajua kuwa mama yake na binti alimtorisha yule binti mbali kabisa ila kijana naye aliamua kutoroka na kumfuata binti mfalme na hatimaye akampata alipo.

Mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme.

1. Kama tulivyoishia kwenye sehemu ya kutoroshwa kwa bibi na binti, hali hii ilimuumiza sana mtoto wa kiume wa mfalme, lakini alipoulizwa hakuweza kusema chochote , ila siku Moja mama yake aliandaa chakula kizuri alichokuwa anakipenda yule mtoto wa kiume wa mfalme akawaita na marafiki zake akampatia zawadi nzuri,akawakusanya mabinti wazuri wakawa kwenye Ile tafrija lengo la Mama ni kutaka kumfanya yule kijana asahau yule Binti Ila hayo yote yalikuwa bure, katika sherehe hiyo watu vijana wote waliamka kucheza na wale mabinti wazuri ila mtoto wa kiume wa mfalme hakucheza na Binti yoyote yule.

 

2.ilifika wakati mpaka mabinti wanamsogelea yule kijana aliwaangalia kwa dharau tu, ndipo ilipofika jioni mtoto wa kiume wa mfalme akaandaliwa chumba kizuri kama heshima ya watoto wa mfalme ndani ya chumba aliwekwa msichana mlembo yule kijana alipoingia na kumkuta alitoka chumbani akamfungia yule msichana ndani yeye akatoka nje na kwenda kulala kwa walinzi wa mfalme, mama yake alipoamka asubuhi na mapema kuangalia kwenye chumba kilichoandaliwa alishangaa kuona msichana Yuko mwenyewe kitandani amelala fofofo, mama aliumia sana na akamfungulia msichana akamruhusa aende kwa wenzake..

 

3. Baada ya mtoto wa mfalme kuwa kwenye mawazo mazito aliamuru kumshirikisha rafiki Yake maangaiko aliyo nayo moyoni ila hakumwambia kwamba yule Binti anayemtesa ni ndugu yake Bali alimwambia kuwa amehama na ajui kaenda wapi, basi yule kijana akamwambia wewe ni mtoto pekee wa kiume wa mfalme kwa nini usimwambie mfalme tatizo lako akakupatia watu wakakusaidia kumtafuta huyo Binti? Yule kijana akakubali shingo upanda alipenda Siri hii isijulikane kwa mfalme na aliogopa sana kumwumiza mama yake kwa hiyo hali ikaendelea kuwa mbaya zaidi na maisha yakaendelea kuwa magumu kwa yule kijana kwa sababu hakutaka kumwaibisha mama yake na hakupenda kuoa msichana mwingine tofauti na yule Binti.

 

4. Kadri siku zilivyoenda ndipo na Mama akaingia katika wasi wasi mkubwa na akaamuru kumwita kijana wake na kuongea naye kuhusu Sheria za ufalme ni kwamba mtoto wa kiume wa mfalme anapaswa kuoa Binti ambaye Hana undugu naye na wewe ukipenda kuoa huyu ndugu yako hautaweza kupata ufalme kwa sababu ya kufanya kitendo cha namna hiyo kwa sababu mimi nilikutambulisha kwa mfalme bila kumtambulisha dada Yako lengo ni kwamba wewe urithi ufalme wa baba Yako ila wewe bado unagangania kuoa ndugu yako, yule kijana wa kiume wa mfalme akasema Mama kama yule angekuwa ni ndugu yangu angekuwa anatambulika a kwenye familia na ukoo pia ila kwa kuwa hawamtambui mimi siwezi kukusikiliza kwa hilo kwa hiyo mama tangia mda huu mimi naenda kumtafuta yule binti popote alipo na nitamuoa na sitasikiliza chochote kutoka kwako.

 

5. Baada ya mama kuona msimamo wa kijana ni mkali mno aliwaandaa watu ili kwenda kumuua yule binti na bibi, lakini kijana akapata taarifa ndipo akaenda kwa baba yake akamuomba jeshi akiwa na lengo la kwenda kumwokoa yule binti, alimwambia baba naomba niende kusherehekea na marafiki zangu ila naomba kwenda na jeshi kusudi wanilinde, kwa kuwa baba alikuwa anampenda sana kijana wake akamuandalia chakula, nyama na vitu vyote vinavyofaa kwa sherehe akampatia na jeshi pia akiamuru jeshi limlinde na kumsikiliza kwa kila kitu atakachowaambia baada ya kufika mbele kidogo akawaambia juwa wafuatane na hao wauaji waliotumwa na Mama yake kwa sababu wanajua binti alipo.

 

6. Yule kijana akamwambia mkuu wa jeshi kwamba kabla hatujaenda kwenye sherehe tunapaswa kumwokoa mchumba wangu kutokana na wauaji na tupambane nao mpaka tumwokoe , basi mkuu wa majeshi anawapanga watu wake na wakaanza mashambulizi mpaka wakamwokoa yule binti na bibi, baada ya hapo bibi alipopata taarifa za kutaka kuuawa kwa sababu ya yule binti alisikitika sana na akaamuru kuvujisha siri hiyo kwa wake wengine wa mfalme, basi mtoto wa kiume wa mfalme akamchukua yule binti akaenda kusherehekea naye na baadae akaja naye kwa mfalme akamtambulisha kama mke wake mfalme akafurahi kwa kuona kijana wake kapata mke ila mama alikoswa amani.

 

7. Basi ikafika siku ya maandalizi ya kumsimika kijana kurithi ufalme wa baba yake kwa sababu alikuwa ni mzee, kufuatia na sheria ya kwamba mtu anayerithi ufalme ni lazima mke wake wasiwe na undugu hata kidogo na kumbuka habari imo mikononi mwa wake wenza, je unafikili watanyamaza? 

 

itaendelea

Download app yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download

Download Now Bongoclass

           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu image Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Jamvini Main: Post File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Views 1259


Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Simulizi za Hadithi Audio     👉5 kitabu cha Simulizi     👉6 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

WAKATI WA KUFUMBUKA SEHEMU YA 1
Post hii inahusu zaidi hadithi mpya na nzuri inayoitwa wakati wa Kufumbuka, ni hadithi inayohusu maisha ya kawaida ambapo watu ushindwa kudhamini watu wa karibu nao na kuona watu wa mbali ndio wenye maana ila shida zikifika ndipo wanaona umuhimu wao. Soma Zaidi...

Mwendelezo wa hadithi ya vijana wawili
Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya vijana wawili, kuhusu hadithi hii ni pale Jackie anaandikiwa barua na Julius ili apotezwe akili na wavulana wengine kwa sababu Jackie aliwapita darasani. Soma Zaidi...

Hasara za wivu na kutokuwa wazi ( sehemu ya 2)
Posti hii inahusu zaidi hasara za wivu na kutokuwa wazi sehemu ya pili, sehemu hii inahusu mama Lisa anaenda kwa mama lina ili kuuliza kinachoendelea kwa mtoto wake , kwa hiyo tuona atapata jibu gani. Soma Zaidi...

Usichofahamu kuhusu mazoezi
Posti hii inahusu zaidi mambo muhimu ambayo hufahamu kuhusu mazoezi,ni mambo ambayo utokea au no matokeo mazuri kwa watu wanaofanya sana mazoezi. Soma Zaidi...

Mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme sehemu ya tano
Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme sehemu ya tano, baada ya bibi kuachana na mke mdogo wa mfalme alienda kwa kijana wa kiume wa mfalme na kuona udhaifu wake kwamba anapenda sana mali. Soma Zaidi...

SAFARI YA MUUJIZA ( SEHEMU YA PILI)
Post hii ni mwendelezo wa hadithi ya safari yenye muujiza ,ni pale mtoto ya Mungu mengi anafika kwenye kituo Cha ntonga na kuona yake mazingira na kufahamu njia ya kwenda kule. Soma Zaidi...

Mwendelezo wa hadithi ya Mama mchoyo na mwehu
Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya Mama mchoyo na mwehu, kwa sababu mwehu alikuwa mkarimu alichukua ule mkate akawapstia watoto wa yule mama wakiwa wanatoka shule kwa hiyo tutaona kilichotokea kwa wale watoto. Soma Zaidi...

NIMLAUM NANI? (Sehemu ya pili)
Post hii ni mwendelezo wa hadithi iliyopita ambapo Frank aliwakuta Amina ambaye ni mpenzi wake ameumbatiana na James ambaye ni rafiki yake ,kwa hiyo tuendelee kusikia yaliyotokea baada ya Amina na James kukutwa na Franki. Soma Zaidi...

Hasara za wivu na kutokuwa wazi (sehemu ya 3)
Posti hii inahusu zaidi hasara za kuwa na wivu na kutokuwa wazi, sehemu hii inahusu zaidi maendeleo ya Lisa shuleni yanakuwa mabaya zaidi na lina anaendelea kumtunzia siri lengo lake lina ni kuendelea kuwa wa kwanza darasani. Soma Zaidi...

USALITI (sehemu ya kwanza)
Post hii inahusu zaidi vijana wawili ambao ni msichana na mvulana walioingia kwenye mahusiano wakiwa sekondari na wakahaidiana kuoana ila kwa sababu mbalimbali walizokutana nazo kwenye safari yao ya mahusiano mmoja akamsaliti mwingine na kusababisha kupo Soma Zaidi...